Nini kitatokea baada ya Magufuli kustaafu Urais?

Mkuu vingozi wazuri wapo ila Magufuli kawafunika. Pia wanaogopa kuonyesha uwezo wao kazini kwani wanaweza kugeukwa na Magufuli kwa kuonekana mjuaji, mwenye kiburi, kuonekana kujipanga kuelekea 2025 na mwisho kabisa kuogopa hujuma kutoka kwa viongozi wenzie ukizingatia siasa imejaa wivu na uchonganishi.
 
Yule Mbunge anayetaka Rais Magufuli aongezewe mhula akiiona hii comment yako, atamwambia Rais usikubali kabisa kuachia madaraka.
 
sikubaliani na wewe kuwa viongozi wazuri wapo ila wana muogopa Magufuli?!! hapana hiyo si kweli kwa sababu

1. Magufuli mwenyewe ameonyesha na kuthibitisha anawapenda sana wachapa kazi wasio na uoga wenye kujiamini, mifano ipo mingi tu.

2. yeye mwenye Rais Magufuli akiwa waziri alionyesha uwezo wake wa utendaji bora na kufuatilia na kila kiongozi na wananchi walimkubali kwa uhodari wake wa kuchapa kazi na kufuatilia, alikuwa ni kiongozi mwenye kujiamini kwa kusimamia maamuzi yake na haswa anapo jua kuwa sheria imeelekeza ni mtu mwenye msimamo mpaka leo matokeo yake ndio maana leo hii ni Rais.

hayo maneno mengine ni porojo za kwenye vijiwe vya kahawa, yeye anapenda wachapa kazi wenye kujiamini kinyume chake kama hujiamini huwezi kufanya kazi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unalivuka daraja unapo lifikia. Unawaza kufika ukomo wa rais ambaye alisha kwambia akiondoka nani atafanya au kukamilisha haya yote aliyo yaanzisha?
 

Atawaachia screen lakini remote atakaa nayo yeye
 
Lazima wakitafute kitu smart kikae pale ikulu wala sio kijana wataweka mtu ambaye ni smart na amewahi shika nyadhifa nyeti ili waweze fanya kazi. Maana kutakuwa na kazi nzito sana kuiweka serikali kwenye mstari na kuhakikisha hapatatokea tena Rais ataongoza kama alivyo ongoza Mh Rais wa sasa. Last watendaji wakuu waliokuwa ktk serikal yake wengi watakuwa na safari za mahakaman kujibu hoja za utaratibu. Sijuwi itakuwaje bado makesi mengine ya wafanya bihashara na watu wengine..
 
Unalivuka daraja unapo lifikia. Unawaza kufika ukomo wa rais ambaye alisha kwambia akiondoka nani atafanya au kukamilisha haya yote aliyo yaanzisha?
Kwamba hakuna Mtanzania wa kuvaa viatu vyake?
 
Tunaacha kujadili changamoto zilizopo na kupendekeza suluhisho na kukimbilia kutabiri itakavyokuwa miaka mitano ijayo!.
 
Aliekuambia anastaafu nani,kashapanga mbuzi wake waongeze muda wa kukaa madarakani,covid ipige hilo bunge wapukutike tu hawana faida
 
Hivi tulikuwa wajinga? Sasa je?
Tulikuwa wajinga sana kuchagua kiongozi huyu huku tukijua uwezo wake ni mdogo kama alivyoonyesha akiwa Waziri, sasa ni wajinga wa kupindukia kwa kurudia kosa hata baada ya kuona wazi udhaifu wake kama Rais ndani ya miaka 5 lakini tukamrudisha madarakani tukijua hata kisomo chake wasiwasi tukidanganyika na PhD. Miaka 5 ya kwanza alitumia kubomoa na kuvuruga taratibu na mifumo ya Utawala Bora aliyoikuta na kuleta ya kwake ambayo sasa ameishiwa hana jipya anafanya kazi ambazo zingefanywa na MaDC. Katika kubomoa mifumo aliyoikuta, alianza na kutumbua wasomi aliowakuta na kuanzisha uteuzi wa kiupendeleo na kuleta watumishi wasiyo na taaluma kama yeye na wakutoka maeneo teule. Akawabana wananchi kutoa maoni yao waziwazi na kuminya vyombo vya Habari kutoa habari asizopenda na hii ikafanya hata taarifa zake nzuri zisiwafikie wananchi na matatizo yao yasimfikie yeye kwa utatuzi. Tumerogwa!
 
WE kijana huoni kinachoendelea bungeni au!? Wadhaanza mikakati ya kutaka aongezewe muda na vyama vya upinzani vifutwe!!!
 
Usisikilize maneno tuu, angalia matendo. Mtu utamjua kwa matendo yake Na dalili ya mvua ni mawingu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…