Pre GE2025 Nini kitatokea ikiwa chama kimojawapo cha Upinzani kitakuwa na fedha za kampeni sawa na walizonazo CCM?

Pre GE2025 Nini kitatokea ikiwa chama kimojawapo cha Upinzani kitakuwa na fedha za kampeni sawa na walizonazo CCM?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Sijui kama wachambuzi wa siasa na chaguzi zetu wameangazia vya kutosha suala la FEDHA na RASILIMALI wanazokuwa nazo CCM wakati wa kampeni.

Vyama vya Upinzani siku zote vimekuwa vikifanya kampeni kwa kuunga-unga na kuzidiwa kwa kiwango kikubwa na CCM.

Sasa sijui mazingira hayo yanachangia kwa kiwango gani[ asilimia ngapi] kushindwa kwa vyama vya upinzani ktk mapambano yao dhidi ya CCM.

Hivyo basi nimewaza kuhusu uchaguzi wa 2025. Nini kitatokea ikiwa chama kimojawapo cha upinzani kitakuwa na kiwango sawa cha fedha walizonazo CCM? Je, mazingira hayo yatachangia kwa kiwango gani kupata matokeo mazuri zaidi ya tuliyoyazoea?
Ukiweza kuwalipa wale jamaa basi Ikulu ni Asubuhi tu. Ila hutakuwa umepata viongozi wazuri bali CCM B
 
makamu mwenyekiti wa chama chenu cha wachaga anachangisha upatu kununua gari pesa ya uchaguzi mtoe wapi? M/kiti wa maisha mboye pesa aliyohongwa kishaimalizia kwenye konyagi
Wafrika na fikra za kikabila mmelaaniwa.

You can not think beyond Tribalism.
 
..hapo nime-cover the basics.

..wapinzani wawe na wakala lila kituo, na wamlipe.

..kama Ccm watamhonga uwezekano ni wakala wa upinzani kuwa na maokoto kuliko wakala wa Ccm.

..wakala wa upinzani aliyelipwa na akaongezewa cha juu na Ccm, kwangu mimi ana afadhali kuliko wakala ambaye wapinzani hawajamlipa kabisa.
Kumlipa wakala ni mwanzo mzuri ukishirikisha na umakini mkubwa wa kuwapata wakala hao tokea sasa. Hawa siyo watu wa kuokotwa tu dakika za mwisho mwisho katikati ya shughuli za uchaguzi.

Mkuu 'JokaKuu', ni hivi: Wakati huu CHADEMA wanapopita huko kwenye Kanda zao na kufanya mikutano ya hadhara, CCM wapo tayari kwenye mikakati ya mipango ya chaguzi toka mashinani/mitaani. Kazi inaendelea huko sasa hivi kimya kimya.
Kama huamini, hapo ulipo (?); jaribu kumtafuta kiongozi wako wa mtaa na wenzake wote katika ngazi hizo za huko chini akutatulie shida yako.
Soma vizuri alama za nyakati. Hawa watu wapo katikati ya kujiandaa na hizi chaguzi tayari.
Kuhusu vyama vya upinzani, na hasa CHADEMA wanafanya nini katika ngazi hizo wakati huu, hilo silijui

Mikutano ya Mwenyekiti na viongozi wenzake huko kwenye kanda ni muhimu sana, lakini umuhimu huo hauwezi kuwa mbadala wa mikakati mizuri ya chama kwenye hizi ngazi za chini kabisa walipo wananchi.

Ni kama nimetoka kwenye mstari kidogo, lakini nadhani ni njia inayohusiana na kudhibiti utaratibu wa kura pia wakati wa uchaguzi.
 
Wafrika na fikra za kikabila mmelaaniwa.

You can not think beyond Tribalism.
hebu tuone uongozi wa hicho mnachoita chama kuanzia umiliki, viongozi wa mbele ya pazia na nyuma ya pazia tujue kama nasema ukweli au mimi ni mkabila
 
..Wapinzani wakiweza kusimamisha wagombea kila sehemu.

..Wapinzani wakifanya mikutano ya kampeni mingi kupita Ccm.

..Wapinzani wakiweza kuweka mawakala kila kituo nchi nzima na kuwalipa.

..Wapinzani wakiweza kugawa t-shirt na kofia nyingi kuliko Ccm.

..Je, matokeo yatakuwa tofauti na tulivyozoea?
Jibu ni HAPANA.
Dondoo zako zinahitaji kujibiwa moja baada ya nyingine kwa nini jibu ni HAPANA.
Nitatafuta nafasi kujibu.
 
Hivi kwa nini CCM inapokea pesa kutoka CCCP China, matajiri wa kiarabu Loliondo na DPW nk hela hizo haziitwi za kuuza nchi wakati ni wazi wanauza kwa hao. Lakini mfano Chadema ikipokea msaada toka kwa chama chochote cha upinzani toka Ujerumani au uingereza maneno ni mengi?
 
Upinzani ukiwa imara inabidi uwe na watu kwenye serikali. Tena watu wazito ambao waidhoofishe ccm kimkakati kabisa. Ila kwa type ya upinzani wa bongo wakina Mwami na Mbowe ni ntu za dili tu
 
Mm siaminigi kama CCM wanaiba kura. Wananchi hawapigi kura, vijana mihemko mingi ila kwenye kura hawatokei. Hivi tuongee ukweli robo tatu ya wapiga kura muikate CCM kweli watajitangazia ushindi. Shida watu hampigi kura mwishowe wanaenda vibibi na vibabu kuipigia CCM.
 
Sijui kama wachambuzi wa siasa na chaguzi zetu wameangazia vya kutosha suala la FEDHA na RASILIMALI wanazokuwa nazo CCM wakati wa kampeni.

Vyama vya Upinzani siku zote vimekuwa vikifanya kampeni kwa kuunga-unga na kuzidiwa kwa kiwango kikubwa na CCM.

Sasa sijui mazingira hayo yanachangia kwa kiwango gani[ asilimia ngapi] kushindwa kwa vyama vya upinzani ktk mapambano yao dhidi ya CCM.

Hivyo basi nimewaza kuhusu uchaguzi wa 2025. Nini kitatokea ikiwa chama kimojawapo cha upinzani kitakuwa na kiwango sawa cha fedha walizonazo CCM? Je, mazingira hayo yatachangia kwa kiwango gani kupata matokeo mazuri zaidi ya tuliyoyazoea?
CCM inategemea wizi wa kura unaoratibiwa na kutekelezwa na vyombo vya dola hivyo hata wapinzani wawe na matrilioni ya kumwaga bado wagombea wa CCM watatangazwa kuwa wameshinda at gun point.
 
CCM inategemea wizi wa kura unaoratibiwa na kutekelezwa na vyombo vya dola hivyo hata wapinzani wawe na matrilioni ya kumwaga bado wagombea wa CCM watatangazwa kuwa wameshinda at gun point.

..usicheze na fedha.
 
Sijui kama wachambuzi wa siasa na chaguzi zetu wameangazia vya kutosha suala la FEDHA na RASILIMALI wanazokuwa nazo CCM wakati wa kampeni.

Vyama vya Upinzani siku zote vimekuwa vikifanya kampeni kwa kuunga-unga na kuzidiwa kwa kiwango kikubwa na CCM.

Sasa sijui mazingira hayo yanachangia kwa kiwango gani[ asilimia ngapi] kushindwa kwa vyama vya upinzani ktk mapambano yao dhidi ya CCM.

Hivyo basi nimewaza kuhusu uchaguzi wa 2025. Nini kitatokea ikiwa chama kimojawapo cha upinzani kitakuwa na kiwango sawa cha fedha walizonazo CCM? Je, mazingira hayo yatachangia kwa kiwango gani kupata matokeo mazuri zaidi ya tuliyoyazoea?
Kikubwa waoneshe source ya hela zao,Kuna sheria ya money loundering na nakumbuka Magufuli aliwaoiga Pini Wanaojiita watetezi wa Haki za binadamu walipokea ma hela kibao ya uchaguzi 2020 akazipiga Pini.
 
JokaKuu ishu kuu hapa sio fedha.....

Kusema hivi haina maana kuwa fedha si nyenzo muhimu katika uchaguzi...

CCM hutumia fedha nyingi kama hadaa tu lakini hawa hata kama watumie bajeti yote ya 2024/2025 hawana ushawishi wowote wa kisera na mipango kwa wananchi...

Fedha zao zote hutumika kuandaa matamasha wanayoyaita "kampeni za uchaguzi" huku ukweli ukiwa kuwa hayo huwa ni matamasha ya burudani tu kwa sababu CCM wanajua kuwa kwa ujinga wa watanzania hicho ndicho wanachokihitaji...!
=============================================

Hebu cheki hii..

Kampeni za mwaka 2015 zilikuwa za fedha nyingi sana kwa CCM lakini CHADEMA hawakuwa na fedha kufikia hata robo tu kulinganisha na za CCM lakini bado CCM hii hii ilipigwa kwenye sanduku la kura na mgombea wa CHADEMA ndugu Edward Lowassa.. HAKUTANGAZWA MSHINDI, AKATANGAZWA ALIYESHINDWA John P. Magufuli....!!

Ndivyo ilivyokuwa kule Zanzibar mpaka...

HUKO ZANZIBAR, jamaa kwa makusudi kabisa wakafuta matokeo yote ya uchaguzi baada ya kugundua kuwa Dokta Mohammed Shein (CCM) kapigwa na hayati Maalim Seif Shariff Hamad (CUF)....!!

HIYO IKAPITA. Ukaja uchaguzi wa 2019 na 2020. Kama kawa, CCM wanajua fedha sio kigezo cha kushinda uchaguzi kwa Tanzania. CCM walikuwa na fedha zote kwa kadiri ya mahitaji yao. Wakatajirika kupitia fedha hizo...

CHADEMA na Tundu Lissu hawakuwa hata na robo ya fedha za CCM. Angalia kampeni zao. Watu walikuwa wanakuja wenyewe kwa maelfu na wakampa Tundu Lissu kura kama zote.

TUNDU LISSU HAKUTANGAZWA...!!

Jamaa Magufuli na CCM yake kuona hivyo kuwa ameshalizwa kwenye sanduku la kura, wakapora uchaguzi wote. Akajitangaza kwa nguvu kuwa ndiye mshindi na sasa yuko kaburini, anatawala walio makaburini....!

Kuna Chawa anaitwa Etwege najua anachukia kweli ukimtaja Magufuli kwa mtazamo huu[emoji1318][emoji1318]. Shauri lake. Akitaka amfuate huko aliko, lakini ukweli juu ya historia ya Magufuli wake ndivyo ilivyo na ulivyo...

Mpaka leo hakuna kura za u - Rais ambazo ziko gazzeted kuonesha Magufuli na CCM walipata ngapi kwa kila jimbo kama sheria inavyotaka kutangazwa kwa kura hizo...

Why?

The anaswer is very simple........... Ni kwa sababu walivuruga vuruga kila kitu hata wakapoteana wao kwa wao kiasi cha hesabu kugoma hata kughushika...!!

Hata zile za ubunge na udiwani zote ni utopolo tu. Hakuna aliyeshinda na leo hii kila mtu na kila Mtazanzania analipia uovu na ujinga wa CCM na Magufuli wao.....

The issue here is not about money. Hata bila fedha nyingi kama za CCM CHADEMA watafanya kampeni all over the country kama ilivyofanyika miaka yote ya nyuma....

Kwa sababu CHADEMA kila mwananchi ni wakala wake ktk kampeni. Wananchi tutafanya kampeni kuanzia kwenye familia zetu, mtaani kwetu na tutaeleweka kirahisi....

TANU ya Nyerere haikufanikiwa kupambania uhuru wa Tanganyika kwa sababu ilikuwa na fedha. They had nothing in their pockets lakini mioyo ya watu ilielewa malengo ya TANU. Mkoloni akaondoka....

NDIVYO ILIVYO LEO KWA CHADEMA. Watu wakishaelewa madhara ya kukumbatia mkoloni mweusi CCM, hakuna fedha ya kuzuia mabadiliko na uhuru wa wananchi...!

Ukifika wakati wa CCM kutoweka ktk uso wa nchi ya Tanganyika, na wakati huo tayari umeshafika, basi hakuna kiwango cha fedha kinachoweza kusaidia uwepo wao kuendelea ku - exist ....!!
lets be honest,
Lowassa hakushinda 2015, magufuli alishinda kihalali (may be uniambie kura za magu ziliongezwa, lkn kushinda alishinda kihalali),

2020 hata kusingekua na mazongwe still jiwe angeshinda, ila kwa % ndogo kuliko 80+ aliyojipa!

kwenye ngazi ya uraisi wapinzani bado hawajawa na wagombea wa kuaminiwa na umma,....
 
Kampeni ile ya Lowasa na JPM nadhani Ukawa walikuwa na Nguvu sawa na Ccm ila Serikali ikaingilia kati
Lowassa angekua na afya imara, kisha hajapakwa uchafu (ofcoz cdm ndio walimpaka) basi 15 angeshinda, lkn kwa scenario iliyokuwepo ni hakushinda fair&square!
 
1. wakala wa upinzani ktk kila kituo, na alipwe.

2. Mfumo independent wa wapinzani kukusanya, na kujumlisha, matokeo.

3. waangalizi huru wa uchaguzi, kwa mfano taasisi za kidini, NGOs, ktk kila kituo.

Tatizo ninaloliona ni kukosekana kwa UWAZI ktk kuhesabu kura, na kutangaza matokeo.
namba 1&2 inaondoa hilo 'tatizo' ulilotaja hapo mwishoni automatically,

hizo 1&2 zikifanywa, basi kufika saa 4 usiku mnakua na matokeo ya nchi nzima, na kufika asubuhi mnajua nani mshindi, kitu ambacho upinzani hawajawahi kufanya, hata 2015 hawakufanya!
 
Kikubwa waoneshe source ya hela zao,Kuna sheria ya money loundering na nakumbuka Magufuli aliwaoiga Pini Wanaojiita watetezi wa Haki za binadamu walipokea ma hela kibao ya uchaguzi 2020 akazipiga Pini.

..wapinzani peke yao, au hata Ccm?

..uchaguzi wa 2005 au 2010 Ccm walipewa fedha na Waarabu.
 
Mambo matatu yanaweza kukikuta:
(1) Kitaundiwa zengwe la aina yake
(2) Kitapingwa hata na vyama vingine vya upinzani.
(3) Kitakufa
 
lets be honest,
Lowassa hakushinda 2015, magufuli alishinda kihalali (may be uniambie kura za magu ziliongezwa, lkn kushinda alishinda kihalali),

2020 hata kusingekua na mazongwe still jiwe angeshinda, ila kwa % ndogo kuliko 80+ aliyojipa!

kwenye ngazi ya uraisi wapinzani bado hawajawa na wagombea wa kuaminiwa na umma,....

You said, we have to be honest....

But I am very surprised because you're not being honest to yourself ndugu dong yi....!!

John Pombe Magufuli na CCM at large, hawakushinda mwaka 2015 kote Tanganyika na Zanzibar. Upende, usipende ama utake usitake lakini huu ni ukweli ulio wazi na usiopingika...

Wewe unaweza kuwa mbali na ukweli huu kwa sababu ni mtu unayeishi kwa kulishwa propaganda na uongo wa CCM badala ya kuishi ktk facts za kutafuta mwenyewe...!

Mimi nakupa za ndani kabisa maana sisi wengine ni ma - unanimous ambao tumo ndani ya "mtungi", tunajua na tunaelewa...

Ushahidi kuwa CCM iligaragazwa mapema sana tena kwa tofauti ya kura nyingi ni huu👇🏻

CCM walikuwa na tallying center yao somewhere pale Upanga na kikosi hicho by then kiliongozwa na January Makamba. CHADEMA/UKAWA nao walikuwa na tallying centre zao maeneo tofauti mawili....

January Makamba akiwa anaongoza kikosi cha kupokea matokeo, mapema tu waliona mgombea wa CHADEMA ndugu Edward Lowassa akimpiga kwa mbali sana mgombea wao John P. Magufuli....

Kuona hivi, ilitoka amri kuvamia tallying centers zote za CHADEMA, ku - confiscate zana zao zote za kukusanyia na kujumlishia matokeo na wahusika wote wakakamatwa...

Kule Zanzibar ndiyo ilikuwa hatari zaidi maana CCM na Dr Mohamed Shein waligaragazwa vibaya na CUF ya Maalim Seif Sharff Hamad. Na hitimisho ilikuwa, futa matokeo yote na uchaguzi urudiwe upya...!!

Bado huamini tu kuwa CCM walishindwa vibaya? Na in fact hawajawahi kushinda tangu mwaka 1995 baada ya chaguzi za mfumo wa vyama vingi zilipoanza kufanyika..!

Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, huu nao umenishangaza kweli kwa kusema eti CCM na Magufuli walishinda...

You're too naive my friend. And that's why I see you as not being a honest human being...!

Najiuliza kama ni mtu mwenye fikra huru, kwanini ushindwe kuelewa kirahisi tu kuwa CCM na Magufuli hawakupata hata 30% ya kura zote za u-Rais mwaka 2020..????

Ushahidi mkuu ni kuwa, John P. Magufuli wa CCM alijitangaza mwenyewe "MSHINDI WA KITI CHA URAIS" kwa nguvu kwa kuitumia tu NEC na kwa mlango wa nyuma....!

Kama unataka justification ya ukweli huu waulize NEC matokeo ya kura za u-Rais jimbo kwa jimbo Tanzania nzima yako wapi maana sheria inataka kuchapishwa ktk gazeti la serikali na kwenye tovuti ya tume ya uchaguzi kwa matokeo hayo yote jimbo kwa jimbo ndani miezi 6 mara baada zoezi la kupiga kura, kuhesabiwa na kutangazwa mshindi kuwa limekamilika...

Cha ya ajabu mpaka leo miaka karibu minne sasa NEC - Tume ya Uchaguzi haijafanya hivyo halafu wewe eti bado uanaamini kuwa Magufuli na CCM walishinda with what you said "slightest difference!!".... Really?

Wewe kwa akili na ufahamu wako unadhani NEC wana sababu gani ya kutoyaweka matokeo hayo wazi mpaka sasa....?

The answer is very simple....

Kwamba hawana matokeo ya kweli. Walichonacho ni matokeo ya kughushi na hayarekebishiki. Wakiya display wazi, kutakuwa na chaos ya kutosha maana hayata reflect reality...!!

Tundu Lissu na CHADEMA walimgaragaza John P. Magufuli na CCM yake na mapesa yao yote mwaka 2020 kwa tofauti ya kura nyingi mno na ni aibu hata ukizitaja hapa...!

John P. Magufuli huko aliko anajua na CCM yote wanajua na kuutambua ukweli. Ndiyo maana utawala wao na maisha yao yametawaliwa na kile wanasaikolojia wanakiita kwa kiingereza "The fear of rejection...!" mpaka sasa..!
 
Sijui kama wachambuzi wa siasa na chaguzi zetu wameangazia vya kutosha suala la FEDHA na RASILIMALI wanazokuwa nazo CCM wakati wa kampeni.

Vyama vya Upinzani siku zote vimekuwa vikifanya kampeni kwa kuunga-unga na kuzidiwa kwa kiwango kikubwa na CCM.

Sasa sijui mazingira hayo yanachangia kwa kiwango gani[ asilimia ngapi] kushindwa kwa vyama vya upinzani ktk mapambano yao dhidi ya CCM.

Hivyo basi nimewaza kuhusu uchaguzi wa 2025. Nini kitatokea ikiwa chama kimojawapo cha upinzani kitakuwa na kiwango sawa cha fedha walizonazo CCM? Je, mazingira hayo yatachangia kwa kiwango gani kupata matokeo mazuri zaidi ya tuliyoyazoea?
CCM HAWANA HIZO FEDHA, WANACHOTA FEDHA ZA SERIKALI KAMA ALIVYOFANYA MAGUFULI WAKATI ULE KULIPS MISHAHARA YA WATUMISHI CCM NA NYINGINE WALICHOTA KWA AJILI YA KUKARABATI VIWANJA WALIVYOPORA, MATUMIZI YA CCM NDANI YA BUNGE LA CHAMA KIMOJA NI KUFURU.
 
Back
Top Bottom