Nini maana ya ndoto hii?

Nini maana ya ndoto hii?

Mama Mwana

JF-Expert Member
Joined
Jun 6, 2023
Posts
2,435
Reaction score
7,784
Nimeota nipo sehemu nisioijua ni kama mji hivi, umechangamka kiasi nikajikuta na mtu nisiemjua, tukaenda kwenye mwembe uliokua umemwaga maembe mengi lakini hayana muokotaji.

Basi tukaanza kuyaokota lakini mengi yalikua mabichi nikasema niokote mabichi ndio makubwa na la kuiva lilikua dogo nililiokota hivohivo, kwa pembeni kulikua na nyasi nikahisi uwepo wa nyoka mweusi mdogo, nikarusha jiwe sikujua kama lilimpata au la, nikajikuta kwenye mfuko nina embe moja tu lililoiva dogo.

Nikawa najiuliza inawezekanaje wakati nimeokota mengi sana na yule mtu alinipotea tu sikumuona, nikajikuta nipo mjini kwenye huo mji, kilichonifanya nijue hapa ni mjini ni wingi wa magari ajabu kila gari ninayotaka kuipanda imejaa na haisimami, mwisho ikaja gar haikua na watu wengi nikaingia lakini lile gari likakwama kuondoka.

Nikashtuka, inaweza kuwa kuna kitu gani kinaendelea? naomba kutafsiriwa kwa anejua.
 
Acha kusikiliza maneno ya watu (mji wenye watu wengi usio wajua)na usipokee kila ushauri unaopewa( maembe mabichi), Una melengo uliojiwekea japo hujui namna ya kuyageuza kuwa mafankio(embe dogo mfukoni) ,Jipange uongeze elim ujitofautishe na watu wengi (watu kwenye gari lilojaa) ,Wenye mafanikio (gari ulilopanda) siku zote huwa ni wachache acha kufuata mkumbu.
 
Acha kusikiliza maneno ya watu (mji wenye watu wengi usio wajua)na usipokee kila ushauri unaopewa( maembe mabichi), Una melengo uliojiwekea japo hujui namna ya kuyageuza kuwa mafankio(embe dogo mfukoni) ,Jipange uongeze elim ujitofautishe na watu wengi (watu kwenye gari lilojaa) ,Wenye mafanikio (gari ulilopanda) siku zote huwa ni wachache acha kufuata mkumbu.
hell no, mimi sio mtu wa kufuata ushaur wa watu, ukweli hua naamini sana katika kuifuata akili yangu kwanza, halaf hua s mwingi wa kutaka ushaur kwa watu kwajambo lolote lile nikishaamua nafanya nitafanya nikisema niache hua naacha, circle ya watu wanaonizunguka wakaribu ni ndogo mno mkumbo upi ndugu??
 
hell no, mimi sio mtu wa kufuata ushaur wa watu, ukweli hua naamini sana katika kuifuata akili yangu kwanza, halaf hua s mwingi wa kutaka ushaur kwa watu kwajambo lolote lile nikishaamua nafanya nitafanya nikisema niache hua naacha, circle ya watu wanaonizunguka wakaribu ni ndogo mno mkumbo upi ndugu??
Mimi sikuzungumzii ww natafsiri ndoto ulioota namtafsiri wa ndotoni sio wewe.unapaswa kujua sio kila ndoto ina ukweli kwenye maisha, unavyojichukulia ww haimaanishi ndivyo ulivyo kwenye macho y watu.Hapo sijakwambia kuhusu ushahihi wa ndoto yako.
 
Mimi sikuzungumzii ww natafsiri ndoto ulioota namtafsiri wa ndotoni sio wewe.unapaswa kujua sio kila ndoto ina ukweli kwenye maisha, unavyojichukulia ww haimaanishi ndivyo ulivyo kwenye macho y watu.Hapo sijakwambia kuhusu ushahihi wa ndoto yako.
Allah! Allah! naona unanichanganya kabisa, so there is me behind this keyboard and there is another one kwenye ndoto who is she?? unamaanisha nn? so huyo wa kwenye ndoto anaishi maisha gan? come slowly nielewe
 
Ndoto yako inakutaka ule matunda kwa wingi chelea chelea utakufa kwa utapiamlo! Yaonyesha wewe sio mlaji wa matunda ndio maana yameamua yakufate ndotoni.. ifike mahali uone aibu unakula matunda ukiumwa tu huo ni mwili na sio pagala la manyimio!..
Tena upunguze kunywa pombe unakunywa mpk unaanguka kwenye mashimo ya nyoka ipo siku yatakulalua na mwisho ununue gari unauwezo wa kununua gari uache kuomba lift Hadi ndotoni..

Hiyo ndo tafsiri
 
Ndoto yako inakutaka ule matunda kwa wingi chelea chelea utakufa kwa utapiamlo! Yaonyesha wewe sio mlaji wa matunda ndio maana yameamua yakufate ndotoni.. ifike mahali uone aibu unakula matunda ukiumwa tu huo ni mwili na sio pagala la manyimio!..
Tena upunguze kunywa pombe unakunywa mpk unaanguka kwenye mashimo ya nyoka ipo siku yatakulalua na mwisho ununue gari unauwezo wa kununua gari uache kuomba lift Hadi ndotoni..

Hiyo ndo tafsiri
Pia inaelekea ana unyafunzi hapati mlo kamili oyaaa kula matunda wewe utakufa unyafunzi
 
Back
Top Bottom