Nini msimamo wa TLS kwa wanachama wake kuwatetea wabakaji na walawiti ambao jamii nzima imeona unyama wao?

Wanaccm kama kawaida ya wanaisakama tls kwa kutetea Haki za wahanga eti kwa sababu
Uovu umetendwa na watumishi wa serekali

Ccm bana wamechoka sana
 
Unafahamu maana ya haki ya kusikilizwa. Hata ufanye kosa la namna gani lazima upewe haki ya kusikilizwa kabla ya kuhukumiwa. Haki ya kusikilizwa inakwenda sambamba na kuwa na mawakili mahakamani.

Kazi ya wakili ni kuisaidia mahakama kufikia hukumu ya haki.

Kwa mfano wakati wa tukio lile la ubakaji kulikuwa kuna chupa za bia kuna mwingine alikuwa akivuta bangi.

Sasa kisheria ili tufikie maamuzi ya haki matendo yako /actus reus lazima yaendane na nia yako ya kufanya kosa mens rea.

Hivyo vitu visipokwenda sambamba havi-tally impact yake ni kubwa
 
"Nini msimamo wa TLS kwa wanachama wake kuwatetea wabakaji na walawiti"!
kwanini hawa watetewe badala ya kuwatetea WABAKWAJI na WANAOLAWITIWA.
 
Hii lugha huwa mnaongea wapi? Au mnaishia kuandika tu?
Imebaki lugha ya kitaalamu, inatumika na wanasheria na madaktari. Inasadikika ndio Lugha ambayo Mungu anaongea ndio maana iliondolewa kwenye matumizi ya kawaida. Hivyo ukitaka Maombi yako Mungu ayajibu haraka jifunze kusali Kilatini. In nómine Patris, et Fílii, et Spírutus sacti . Amen 🙏
 
Ni haki ya kila mtu kutetewa mahakamani. Nia ni kuifanya mahakama kufikia uamuzi sahihi.
 
Kila mtu ana haki, hivyo ni halali kwao kutetewa, mtu hana hatia mpaka atiwe hatiani
 
Umepigaje hapa? Finita Causa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…