Mkuu huyo jamaa alikufanya nini? Ni kutofautiana tu mitazamo au kuna kitu chengine zaidi?Shujaa yupi? Yule aliyemuachia Vice president wa Acacia na kumpa ubunge ilihali alituaminisha wametusababishia hasara ya Trillion 300?
Hakuna mnafiki kama yule shujaa feki, hata aliwahi waambia watu wamtegemee Mungu sio dawa za wazungu ilihali yeye alikua anatumia pacemaker ya mzungu kwa ajili ya kusukuma moyo wake!!
Nasikia jamaa anapitia sana Hotuba za Mwamba Jiwe Magufuli.Wanasubiri tufungue accounts za benki kwao (Ulaya) ili siku moja watwambie fanyeni hiki, fanyeni kile, vinginevyo tunawafungia. Sisi hatujali… Hatuna accounts huko na hatuhitaji kuwa na accounts… Hatuna chochote huko na haitokaa itokee tukamiliki chochote huko.
Kila tunachokifanya ni kwa ajili ya Burkina Faso. Sisi hatuhitaji hata kutoka nje ya Burkina Faso yetu. Tuna amani hapa… Tukihitaji kwenda kutalii nje ya nchi, tutakwenda Bamako (Mali), Niamey (Niger) au miji mingine… Hatuna sababu ya kwenda huko kwao… Tupo vizuri hapa kwetu.
Kuhusu uoga, hatuna uoga… Tunafahamu athari zinazotuzunguka… Tumeamua kulitumikia taifa letu, tume-sacrifice maisha yetu kwa taifa hili Kwa nini tuwe waoga? Tumeweka kando ujana wetu, kwa lengo la kulitumikia taifa, kwa hiyo hatuna uoga wowote, ondoeni shaka!… Uoga sifuri.
Kuna mfanano naouna Kati yake na mmoja wa Marais waliowahi kuiongoza nchi yetu. Kudos!Wanasubiri tufungue accounts za benki kwao (Ulaya) ili siku moja watwambie fanyeni hiki, fanyeni kile, vinginevyo tunawafungia. Sisi hatujali… Hatuna accounts huko na hatuhitaji kuwa na accounts… Hatuna chochote huko na haitokaa itokee tukamiliki chochote huko.
Kila tunachokifanya ni kwa ajili ya Burkina Faso. Sisi hatuhitaji hata kutoka nje ya Burkina Faso yetu. Tuna amani hapa… Tukihitaji kwenda kutalii nje ya nchi, tutakwenda Bamako (Mali), Niamey (Niger) au miji mingine… Hatuna sababu ya kwenda huko kwao… Tupo vizuri hapa kwetu.
Kuhusu uoga, hatuna uoga… Tunafahamu athari zinazotuzunguka… Tumeamua kulitumikia taifa letu, tume-sacrifice maisha yetu kwa taifa hili Kwa nini tuwe waoga? Tumeweka kando ujana wetu, kwa lengo la kulitumikia taifa, kwa hiyo hatuna uoga wowote, ondoeni shaka!… Uoga sifuri.
Media gani hapo, hiyo ni website ya wanaharakati Transparency InternationalTaarifa ya rushwa unaipata kutoka kwa wakoloni,(western media), hahaha,kalaghabaho
Toka lini transparency International ni ya diasporaSi ajabu hiyo taarifa hapo ameiotoa huko kwenye viwebsite uchwara ambavyo ukichunguza zaidi zimeandikwa na diaspora wale ambao wameikimbia nchi baada ya Traore kuingia madarakani..... na siku zote habari za kuwachafua hawa viongozi wanaonesha kuwa ni Pan-Africanist huwa zinaenea kwa kasi sana.
Usitegemee huyo mpenda demokrasia uchwara(afrika hatuna demokrasia bali tuna mwamvuli tu wa demokrasia) aone kama kuna jema kutoka kwa Traore.
Ukishasema tu transparency halafu "International" tayari moja kwa moja tunajua ni nani yuko nyuma ya hicho chanzo.... tangu lini hizo International media outlets zikawa na jema kuhusu viongozi wazalendo wa kiafrika wanaokinzana na matakwa yao zaidi ya kueneza propaganda chafu tu dhidi yao?Media gani hapo, hiyo ni website ya wanaharakati Transparency International
Toka lini transparency International ni ya diaspora
Kuna kutofautiana katika uelewa wa yaliyosemwa. Matokeo yake ikatolewa tafsiri tofauti, hilo silo jambo la ajabu kutokea.Aliyoyasema ni yapi, maana inaonekana unayajua yote na haya niliyoandika hapa sio maneno yake.
Dah!Unaonaje ukaacha kutumia teknojia za hao unaoita mashoga ili kuungana kauli na Traore na uungane na Urusi ambao sio mashoga na sio mabeberu.
Uanze kutumia gari za Lada ambazo hata ukute hujawahi kuziona, uondoke JF maana haina teknolojia ya Mrusi hii ni ya Mmarekani ambaye kwako ni shoga. Uachane na internet, uachane na banking system, uachane na kupanda ndege Tanzania hij hakuna ndege ya Mrusi kuna za unaoita mashoga.
haya maneno ndiyo unayomlisha wewe, kwa tafsiri unayoitaka wewe. Kukataa kukubali masharti ya nchi za Magharibi haina maana ya kujitenga na kila nchi duniani. Sijui tafsiri hii mnaitoa wapi? Nchi za Magharibi siyo DUNIA.Ili umaanishe Traore yuko sahihi inabidi tusikuone humu, uanze kujitenga kama anavyotaka kuitenga nchi yake. Ama ukubali wewe ni shoga ndio maana umeweza access huduma za unaoita mashoga.
hicho kichura kwenye avatar yako kinawajibika kwa nani?Huyu naye hamna kitu, mbona anarudia ya dikteta mwenzie. Kwanza kaongeza miaka 5 ya utawala ambao hautambuliki kikatiba, na rushwa ndio imeongezeka maana hawawajibiki kwa yoyote, sio bunge wala mahakama.
He'll be worst, na nabashiri hapa atapinduliwa kabla ya hiyo miaka 5 aliyojipa. Kiburi cha madaraka kimemjaa
Utawaweza wajuaji wa JF hawa.. hata kuongoza nyumba yake tu mtihan, weka mbali hajawah hata kubeba jukum la kuongoza nyumba 10 kama baloziUnajua jamaa amekuzidi maono kwa mbali sana
T14 Armata kuna time huwa anakuruouka kwa hojabza kipumbavu pumbavuuuu. Sema ndio hivyo tena kuna watu mtu unawaheshim tu kwakua kwenye uoande mwingine wana madini mazuri kama huyu jamaa. Ila kukukuruoa huwa anakurupuka muda mwingine . Nafikiri ana amhaba yaliopitiliza kwa WestDah!
Mkuu 'T14 Armata', umekuja na hoja ambayo sikuitegemea kabisa kuwa inaweza kuwa sehemu ya kutishia watu!
Teknolojia mbona ipo kila mahala siku hizi. Wewe unadhani hao jamaa wa magharibi bado ndio wanao miliki teknologia yote? Maswala ya magari, hujui Joe analia sana kuhusu mchina anavyoteka soko la magari ya umeme duniani? Wewe unadhani bado kuna nchi au kundi la nchi linalohodhi teknolojia tena, kwamba waitumie kama silaha ya kuwatwanga wengine? Kwani hiyo teknolojia kwani ni ya nini, si ni biashara? Wewe unadhani watakubali kupoteza biashara kizembe?
Sitaeleza hili kwa kirefu, lakini nakupa tu mfano uufikirie na kupata jibu la hoja yako hii.
Mfano wenyewe ni huu: usifikiri nchi za Magharibi ziliwapenda sana waChina wakati nchi hiyo ilipo amua kufunguka na kufanya biashara na mataifa hayo. Na usidhani hata kwa mara moja kuwa waChina waligeuka kuwa watu wazuri sana kwa mataifa hayo kiasi kwamba makampuni ya nchi hizo yakimbilie huko, tena kwa masharti magumu sana ya uwekezaji.
Kama wewe ni mfuatiliaji wa maswala ya namna hii utaelewa ninacho lenga hapa kujibu hoja yako.
haya maneno ndiyo unayomlisha wewe, kwa tafsiri unayoitaka wewe. Kukataa kukubali masharti ya nchi za Magharibi haina maana ya kujitenga na kila nchi duniani. Sijui tafsiri hii mnaitoa wapi? Nchi za Magharibi siyo DUNIA.
Wewe sasa umezungumza kitu chenye akili kubwa.Alishafeli huyo kiuchumi, Kuna vitu kama kiongozi wa nchi hutakiwi kuviongea hata kama una chuki na mabepari Kwa kiasi gani. wewe tekeleza kimya kimya maono yako bila kumnanga mtu Kwa sababu katika njia ya kuliinua taifa na watu wake utawahitaji wote hata wale waliokuumiza hapo mwanzo ili mradi tu unawatumia Kwa manufaa ya watu wako.
Kwa Sasa njia ya kujichomoa kutoka umaskini Kwa nchi zetu ambazo ni masoko ya wakubwa ni ngumu na haihitaji watu kama yeye bali ni wanafiki huku unajua wapi unataka kuwafikisha watu wako ama sivyo ataishi Kwa hofu kama digidigi
Hapa unafanya juhudi za kujisahaulisha tu, kwamba watu hawakulazimika kushika silaha na kumwaga damu kutafuta uhuru wao toka kwa watu hao hao ambao wao ndio wamekubuhu katika hayo unayotaka Traore ayafanye, ya unafiki.Nimeamini sisi waafrika wengi wanapenda watu maarufu, wajinga wajinga, wenye mihemko katika vyeo vikubwa.
Kwenye kuongoza nchi unapaswa uwe mjanja sana na mtu makini huyu bwana kwa mfano ukamtoa Burkina Faso kwa nafasi aliyonayo ukampeleka China na ukamtoa Xi Jinping ukamuweka yeye ndani ya mwezi China inaenda mlama.
Kwenye kuongoza unahitaji watu wali calm, wasio na mihemko, wasio na macho mafupi yanayo tazama leo na kesho tu bali macho yatakayo tazama taifa lilikuwa wapi, lipo wapi( katika hali gani hapa siasa za ndani na za nje ) na linapaswa kuwa wapi miaka ijayo( hapa ndipo penye ugumu mkubwa)
Huyu bwana mdogo anapaswa ajifunze kwa mabwana zake warusi sasa( katika kupambana na mifumo iliyo kita mizizi tena Urusi ni taifa kubwa lenye uchumi mkubwa na rasimali nyingi linapitia hali gani ? halafu achanganye na akili zake na za washauri wake je, Burkina Faso inaweza pambana ? Au ina hitaji ushirikiano na mataifa yote ya pande zote )
asiishie tu hapo ajifunze na kwa Kim wa NK je kujifungia kama panya kumeiimarisha NK au ndio kutwa kuwa lilia China wawape misaada
Kingine cha mwisho ajifunze kwa wachina namna wanavyo pambana na mifumo ya kimagharibi huku wakati huo huo akinufaika na mifumo hiyo hiyo ya kimagharibi( nacho maanisha kumshinda adui kwa mchezo wake huo huo anao cheza unakuwa smart kuliko yeye )
Huyu bwana mdogo anapaswa kuwa smart sana tu tena sana ningekuwa mtu wake wa karibu ningemshauri apeleke wataalam Singapore wakajifunze iliwezekana vipi Singapore wakati wa Cold war na sasa kuweza kuwa neutral kwa powers mbili.
Lee aliweza vipi kuifanya Singapore kutoegemea upande mmoja bali kujali maslahi yake na kushirikiana na pande zote licha ya kutokuwa rasimali nyingi kama walizonazo Burkina Faso.
Singapore mpaka leo siasa zao za ndani na za kimataifa ni bora sana kwa sababu wao ni smart.
Shida kazi kunwa aloifanya itakuja kuharibiwa na mpuuzi mmoja, ndo maana viongozi wengi wa kimapinduzi hutaman kutawala milele. Ningekuwa Traore sitokuja kuachia madaraka mpaka kifoSafi akifanikiwa kujenga system nzuri ya uongozi atakuwa amepiga bao kweli kweli.
Upo sawa.Hapa unafanya juhudi za kujisahaulisha tu, kwamba watu hawakulazimika kushika silaha na kumwaga damu kutafuta uhuru wao toka kwa watu hao hao ambao wao ndio wamekubuhu katika hayo unayotaka Traore ayafanye, ya unafiki.
Unatoa mifano ya Urusi na Korea kaskazini. Kwa akili yako unadhani hivyo vikwazo walivyo wawekea nchi hizo na nyinginezo, kama Iran, zimekomesha maisha ya wananchi wa nchi hizo kuishi, unataka wakajitweze kwa hao wakubwa!
Katika jamii yoyote, watu wa aina yako hawakosekani. Hata enzi za utumwa watu wa misimamo kama huu wako walikuwepo, na kama wao ndio wangesikilizwa, siyo ajabu utumwa hadi leo hii ungekuwa unaendelea.
China hajitwezi kwa nchi hizo kama unavyo fikiri wewe.
Traore hajasema hatashirikiana na mataifa mengine; bali katika akili yako unadhani kushirikiana na mataifa hayo ndiyo njia pekee ya nchi kupata mafanikio.
Lakini hata katika nchi hizo za Magharibi, siyo kila nchi inafuata mwongozo wa mkubwa wao, kwa hiyo ushirikiano na nchi hizo utakuwepo.