Nini story au kisa nyuma ya username yako na avatar yako hapa JF

Nini story au kisa nyuma ya username yako na avatar yako hapa JF

Nilikuwa nataka kujua maana ya ID yako
haina story kubwa..Kaboom ni sauti ya mlipuko mkubwa..Unaweza kuitumia kuashiria hatari lakini pia unaweza kuitwist na kuitumia kusifia,kushangaa nk ..Kuna artist anapenda kulitumia..Ndo nililichukua kwake..Sijui kama nimejibu swali lako
 
Aroon

Mm ni mshabiki wa arsenal , nikiwa form 1 baada ya ubatizo nilipewa hilo jina , na nilikuwa nampenda Aaron Ramsey , baada ya kupoteza password ,kwa ac ya awali, nikaamua kutumia aroon ,

Kwenye avatar ni mtunzi maarufu wa nyimbo za tenz za rohoni, na nyimbo za kristo
 
haina story kubwa..Kaboom ni sauti ya mlipuko mkubwa..Unaweza kuitumia kuashiria hatari lakini pia unaweza kuitwist na kuitumia kusifia,kushangaa nk ..Kuna artist anapenda kulitumia..Ndo nililichukua kwake..Sijui kama nimejibu swali lako
Umejibu ila hujaniambia kuhusu avatar
 
Wanaume wa Dar hakuna kitu wanaweza kufanya zaidi ya kupaka mikorogo na umbeya.
Lakini demu wako unayemzimia Sana anakaa huku state house na hao unaowatukana ni mashemeji zako wanaokulindia usingizi wako na muda mwingine ndo wanaokusaidia kazi unapokuwa huko mkoani[emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125]
 
Nimpenzi mkubwa wa novels....Jina nalotumia limetoka kwa Mario Puzo author wa The Godfather ikiwa ni jina la moja ya novel zake (The Last Don).......napenda miziki ya latin amerika na Avatar ni ya jamaa anayeitwa Don Omar ambaye ni mmoja wa wanamuzik wa kilatino.

The Last Don, umenikumbusha hii Novel mkuu.

Characters kama Don Clurecuzio, Cross (mtoto wa Pippi aliyeuwawa na Dante, Dante ambaye alikuja kudedishwa na Cross mwenyewe).

Kulikuwa na dada mkali sana ambaye nilishindwa ku-imagine uzuri wake, Athena Aquitane.

Moja ya sentence maarufu niliyotoka nayo ni "The most important thing in life is to earn your bread."
 
Huyo ni J.Cole..Moja ya wasanii wa hip hop ninaowakubali..Haya turudi kwako basi
Linamo ni ufupisho wa majina yangu mawili.
LINA lilitokana na rafiki yangu kushindwa kuita jina langu kwa urefu wake hivyo akawa ananiita LINA.
MO ni herufi za mwanzo za jina la ukoo wangu.
Wakati najiunga JF rafiki yangu huyo ndo alinichagulia jina hivyo akaniambia andika Linamo. Hivyo ikawa hivyo mpaka sasa ananiita Linamo.
 
Linamo ni ufupisho wa majina yangu mawili.
LINA lilitokana na rafiki yangu kushindwa kuita jina langu kwa urefu wake hivyo akawa ananiita LINA.
MO ni herufi za mwanzo za jina la ukoo wangu.
Wakati najiunga JF rafiki yangu huyo ndo alinichagulia jina hivyo akaniambia andika Linamo. Hivyo ikawa hivyo mpaka sasa ananiita Linamo.
Ok..Avatar?
 
Sina undugu na Membe ila ni home boy wangu tu na namkubali kwa kazi zake na harakati zake simjui hanijui ila nilitamani awe Rais kwa sababu ya kazi zake huwa nazikubali sana jamaa ni jembe la KIMWERA ila now kamuachia MAJALIWA harakati za kwenda MAGOGONI akishindwa basi mimi nitakuwa nimeshakomaa tayari kwa kukabidhiwa nchi ili kuwavusha Watanzania kuwafikisha katika nchi ya ahadi.
unaleta za kikanda?.....ooh sorry, i shouldn't bring politics to this
 
Back
Top Bottom