Nini story au kisa nyuma ya username yako na avatar yako hapa JF

Nini story au kisa nyuma ya username yako na avatar yako hapa JF

Kuna mkaka mmoja alikuwa king'ang'anizi kama kupe.
Alikuwa ananipenda halafu simpendi,
Sikuwahi kumwambia jina langu basi zake ikawa ni kuniita cute wangu.
Hadi marafiki zangu wakawa wanambeza wakimwona wananiambia B our cutie anakuja.
Basi siku najiunga humu nikatumia cute then B ni herufi ya kwanza ya jina langu.
Cute B
za masiku mrembo?
 
Nimemaliza kupitia zooote tokea mwanzo, imenichukua masaa mawili, kwa kweli hongera mleta uzi Na wachangiaji pia!, kwani sijawahi kutumia muda mrefu hivi kwa social media!. Sasa zamu yangu:
Nilihangaika Sana kutumia majina yenye msisimko flani hivi, yote yakawa tayari yana wamiliki wake, nikaona shida yote ya nini, nikatupia jina la mtaa wangu wa nyumbani kabisa( nilipojifunzia mema na mabaya) likakubali!.
Kuhusu avatar:- Mimi jinsia yangu ndizi , pia ndio tunda ninalolipenda, hulikosi mezani pangu nikiwa na sahani ya ubwabwa maharagwe!, na tena ndizi kwa samaki ni chakula bora kabisa kwangu hasa nikila siku ambayo niko happy Sana!, Mwisho warembo wachache Tu waliobahatika kupatiwa huduma Yangu huwa wanahoji nimepaka nini?, mbona tamu?, nimekuwa nikipenda kuwajibu, ndizi mbivu haihitaji kusaidiwa kunoga!. Ni hayo tu! Samahani kwa usumbufu!.
Kama unahitaji ndizi ni-PM ( ladies only).
duuuuh lipia tangazo
 
Kweli JF ni raha Mimi kinumi ni jina la kiaya namaanisha dume nilipewa na babu yangu kila nilipokwenda kumtembelea enzi hizo na hiyo picha namkubali huyo jamaa kwa misimamo yake hasa kwa Africa kutawaliwa tena
 
Mkuu nakushukuru kwa kutumia MASAA MAWILI kuusoma uzi huu, its real an honour. Nashukuru sana. Uzi huu umekuwa na baraka kwa JF members, kila mmoja kwa nafasi yake.

Kuhusu jina lako na ndizi story mie nakutakia ugawaji mwema wa ndizi kwa wadada ambao watakuwa interested!! Sharing is caring, kwann uwanyime ndizi kama wanataka ndizi😀
Halafu ndizi yenyewe hawana uwezo Kula wakaimaliza.
 
Mzee=jina la ukoo tu mimi ni kijana bado..
23=tarehe ya kuzaliwa
Avatar=nilijikuta naipenda sana nchi yangu wakati wa kampeni za uchaguzi wa oct.2015..huenda ni kwa jinsi ulivokuwa na mshikemshike nkahisi hatutavuka salama..Mungu mkubwa tumevuka salama na sasa ni 'kazi tu'
 
Aisee angaau leo nimepata pa kusemea

Aaah unajua mimi ni mpenzi wa mpira na fan wa ligi ya EPL especialy Club ya Man U. Sasa hii Id niliipata kwenye mechi ya fainali ya Champions League kati yetu sisi na Chelsea. Pele wanaingia wachezaji wamevaa jezi zilizoandikwa RESPECT mikononi huku wakisindikizwa na mabango yaliyotapakaa uwanja mzima yakiwa na maandishi kama hayo. Mwisho wa mechi tunamgonga Chelsea na kuchukua bakuli letu.

So kuanzia siku hiyo nikawa nawatania mashabiki wa chelsea kwa kuwaambia RESPECT kila ninapowaona. Kama hiyo haitoshi na kibanda changu nikaandika Bango kuubwa lenye Maandishi Respect..! Hii WA BODA inawakilisha nitokako (Mpakani Tunduma)

So siku najiunga Jf nikawa nabahatisha kama naweza kujiunga... Nikaandika Id hiyo alhandulilah nikafanikiwa. Kunabaadhi ya watu wanadhani najikweza kwa kujiita RESPECT nadhani ufafanuzi huu unawafaa.

BACK TANGANYIKA
 
Aisee angaau leo nimepata pa kusemea

Aaah unajua mimi ni mpenzi wa mpira na fan wa ligi ya EPL especialy Club ya Man U. Sasa hii Id niliipata kwenye mechi ya fainali ya Champions League kati yetu sisi na Chelsea. Pele wanaingia wachezaji wamevaa jezi zilizoandikwa RESPECT mikononi huku wakisindikizwa na mabango yaliyotapakaa uwanja mzima yakiwa na maandishi kama hayo. Mwisho wa mechi tunamgonga Chelsea na kuchukua bakuli letu.

So kuanzia siku hiyo nikawa nawatania mashabiki wa chelsea kwa kuwaambia RESPECT kila ninapowaona. Kama hiyo haitoshi na kibanda changu nikaandika Bango kuubwa lenye Maandishi Respect..! Hii WA BODA inawakilisha nitokako (Mpakani Tunduma)

So siku najiunga Jf nikawa nabahatisha kama naweza kujiunga... Nikaandika Id hiyo alhandulilah nikafanikiwa. Kunabaadhi ya watu wanadhani najikweza kwa kujiita RESPECT nadhani ufafanuzi huu unawafaa.

BACK TANGANYIKA

Respect sana mkuu, mie pia nilikuwa najuwa unajipa promo tu, kumbe chanzo ni mlivyotunyuka chelsea kwenye fainali ya UEFA😱😱
 
Aisee angaau leo nimepata pa kusemea

Aaah unajua mimi ni mpenzi wa mpira na fan wa ligi ya EPL especialy Club ya Man U. Sasa hii Id niliipata kwenye mechi ya fainali ya Champions League kati yetu sisi na Chelsea. Pele wanaingia wachezaji wamevaa jezi zilizoandikwa RESPECT mikononi huku wakisindikizwa na mabango yaliyotapakaa uwanja mzima yakiwa na maandishi kama hayo. Mwisho wa mechi tunamgonga Chelsea na kuchukua bakuli letu.

So kuanzia siku hiyo nikawa nawatania mashabiki wa chelsea kwa kuwaambia RESPECT kila ninapowaona. Kama hiyo haitoshi na kibanda changu nikaandika Bango kuubwa lenye Maandishi Respect..! Hii WA BODA inawakilisha nitokako (Mpakani Tunduma)

So siku najiunga Jf nikawa nabahatisha kama naweza kujiunga... Nikaandika Id hiyo alhandulilah nikafanikiwa. Kunabaadhi ya watu wanadhani najikweza kwa kujiita RESPECT nadhani ufafanuzi huu unawafaa.

BACK TANGANYIKA
mkuu nikiangalia Man u ya leo na nikikmbuka hzo zama nabaki na stress
 
Back
Top Bottom