Nini tafsiri ya mabinti kuzaa wakiwa bado wapo kwa wazazi?

Nini tafsiri ya mabinti kuzaa wakiwa bado wapo kwa wazazi?

Kawaida tu sema inaonekana jambo la ajabu kwasababu ya mazoea na tamaduni lakin ni jambo la kawaida sana. Mbona wanaume nao wapo wanaonazalisha wanawake kisha wanaume hao wanaachiwa watoto wadogo ambao wanakuja kuwa mzigo kwa wazee vilevile ila hawasemwi?

Mila na desturi zikikataza kitu hakiwezi kuwa kawaida tena...
Ila nakubali kwa baadhi ya makabila hii inachukuliwa powa...na kweli ni kawaida kama unavyosema...
 
Da Pretty kwa mtoto wa kiume tukubali tukatae ni tofauti kabisa...
Thamani yake haishuki kwa kuzaa kabla ya ndoa...
wahanga ni watoto wa kike...
Hapo hakuna usawa aisee...
Mimi nina watoto wa kiume tu...wakizaa huko watajiju...
Na hata sioni shida kulea mjukuu..
Lakini mjukuu wa mtoto wa kike ni tofauti...
Nimelelewa kwenye familia strict siwezi futa aikilini kuwa ni aibu mtoto wa kike kuzalia home...

Wangekuwa wa kike nadhani ningekuwa na kazi ya ziada ya kuwapa somo la mimba za nje ya ndoa au za utotoni...

Usidhani kila mwanamke yupo kwenye hatari ya hilo janga.
Sio wote humu ni mabinti wadogo. Nilishavuka huko kitambo, wewe upo upande wa vijana wadogo wakati mimi nipo upande wa wazazi/ walezi.
Siwezi kunyamaza kwa mtoto wangu wa kiume eti kwa vile yeye hashuki thamani au haimuathiri.
Na lazima ujue kua hatuwezi kufanana mtazamo, kwangu hata mtoto wa kiume kuwa baba kwenye umri mdogo itanigusa.
Usilazimishe niwe na mtazamo wako wala kupinga mawazo yangu haibadilishi kitu.
 
Jamani comment ziwe fupi mwaka mpya ukute tumeifunga mada
 
Tafsiri yake ni mmomonyoko wa maadili uliochangiwa kwa kiasi kikubwa na utandawazi, watoto wa siku hizi wanajua mambo mengi na makubwa yanayoendelea duniani ambayo mengine hayaendani na umri wao. Na kibaya zaidi wazazi, jamii na hata taifa kwa ujumla hawajui/wanapuuza bila kujali kama mambo hayo yanaathari kwa mtoto na matokeo yake mojawapo ndo hilo la mtoto kubeba mimba. Suala la msingi kuna baadhi ya mambo ambayo hayaendani na maadili yetu yangefungiwayasiwepo kwenye mitandao ya kijamii na baadhi ya huduma zingekuwa zinatolewa kwa kuzingalia umri na kuwekwe vituo maalumu vya kufanya usajili na sio mtu kuamua tu kujiunga mwenyewe na kugushi nyaraka. Mfano mzuri fb watu wanajisajili kiholela tu hadi watoto wa shule za msingi wapo fb siku hizi! Na ukitaka kuingia kwenye website za ngono wala hawaulizi suala la umri wenyewe wanasubiri tu udownload wapate pesa je kwa kijana ambaye yupo kwenye kipindi cha foolish age hajaenda kujarib na yeye! So utandawazi unasababisha matatizo mengi likiwemo hilo
 
Msichana kama msichana swala lakujilinda nakujchnga nilako mwenyewe haswa unapofkisha umri wa miaka 18 unatakiwa ujitambue nakujiona wathamani hakuna mwanaume atakuchezea jitambue msichana.
 
Hili halikuwepo miaka ya 90s kurudi nyuma, sisemi kwamba haikuwa ikitokea, la hasha! bali hata kama ilikuwa inatokea basi ni kwa asilimia ndogo sana tofauti na ilivyo sasa.

Katika maeneo ninayokuwa hasa kwa watu mbalimbali ninawafahamu, jambo hili linaonekana kukuwa zaidi ya mara dufu na inavyoonekana hali ikazidi huko mbele ya safari.

Mabinti wengi wanaozaa wakiwa bado hata hawajaposwa wamekuwa wakiwaacha watoto wao wakilelewa na babu&bibi huku wakiendelea masuala yao ikiwemo kuendeleza uhusiano na wanaume ambao unapelekea kuongeza idadi ya watoto kwa wazazi bila kujua ugumu wa kulea watoto.

Wanaume wamekuwa wakiwazalisha mabinti bila kuwaoa wamekuwa hawatoi ushirikiano wa kulea badala yake mwanamke ndio anaachiwa jukumu la uangalizi wa mtoto ambaye naye anakabidhi majukumu kwa wazazi wake! kimsingi wazazi hawawezi kuwakataa watoto wa watoto wao.

Suala linaonekana kuwa mzigo hata kama mtoto atapewa mahitaji mengine kama kulishwa na kuvishwa kwa gharama za nje ya wazazi wa binti lakini suala la kuwaangalia watoto ni zito na linachosha maana linaonekana kuwasumbua wazee tu ambao jukumu lao la kuangalia watoto lilishapita tangu siku nyingi nyuma.
Singo mazaz
 
Back
Top Bottom