Nini tafsiri ya mabinti kuzaa wakiwa bado wapo kwa wazazi?

Nini tafsiri ya mabinti kuzaa wakiwa bado wapo kwa wazazi?

Hili tatizo halitakwisha mpaka pale wanawake watakapo badilika.......wanawake wengi wanaishi katika ulimwengu wa kufikirika ambao upo vichwani mwao pekee....wana ndoto za kuolewa na mtu ambaye hayupo katika ulimwengu halisi...wengi wao wana machaguo mengi mno wanapotafuta wenza huku fedha na mali vikiwa ndio dira yao kuu.....lakini bahati mbaya hawajiandai kuishi maisha ya ndoa....wanayalinganisha maisha ya ndoa na yale wanayoyaona kwenye tamthilia....kwa kuthaminisha pendo na kiasi cha fedha na mali ndio unakuta wengi wanatumika kama chombo cha starehe na mwisho wake huwa ni mimba na hatimaye maradhi.....hapo watoto wa mitaani hawawezi kuisha kwa kuwa wazazi wa aina huwa wanakuwa hawapo tayari kulea wala kupambana na majukumu kama mzazi........Vile vile kina dada waache kujirahisi kwa kuwa bidhaa rahisi huwa ina watumiaji wengi lakini haithaminiwi....wakati umefika umefika kwa wanawake kutambua thamani yao na kujua kwanini muumba aliona si vyema adamu abaki pekee yake bila ya msaidizi.....waondoe maisha ya kufikirika vichwani mwao na waishi katika ulimwengu halisi.....wapunguze machaguo yasiyo ya msingi mume bora ni yule anayeweza kukabiliana na majukumu yake na kuihakikishia mahitaji yote ya msingi kwenye kaya yake na si kwa uzuri wa sura au mwili uliojengeka kwa mazoezi au mrefu kuliko wote...........wasilinganishe penzi kwa kiwango cha fedha kwa kuwa true love is priceless..........
 
hili halikuwepo miaka ya 90s kurudi nyuma, sisemi kwamba haikuwa ikitokea, la hasha! Bali hata kama ilikuwa inatokea basi ni kwa asilimia ndogo sana tofauti na ilivyo sasa.

Katika maeneo ninayokuwa hasa kwa watu mbalimbali ninawafahamu, jambo hili linaonekana kukuwa zaidi ya mara dufu na inavyoonekana hali ikazidi huko mbele ya safari.

Mabinti wengi wanaozaa wakiwa bado hata hawajaposwa wamekuwa wakiwaacha watoto wao wakilelewa na babu&bibi huku wakiendelea masuala yao ikiwemo kuendeleza uhusiano na wanaume ambao unapelekea kuongeza idadi ya watoto kwa wazazi bila kujua ugumu wa kulea watoto.

Wanaume wamekuwa wakiwazalisha mabinti bila kuwaoa wamekuwa hawatoi ushirikiano wa kulea badala yake mwanamke ndio anaachiwa jukumu la uangalizi wa mtoto ambaye naye anakabidhi majukumu kwa wazazi wake! Kimsingi wazazi hawawezi kuwakataa watoto wa watoto wao.

Suala linaonekana kuwa mzigo hata kama mtoto atapewa mahitaji mengine kama kulishwa na kuvishwa kwa gharama za nje ya wazazi wa binti lakini suala la kuwaangalia watoto ni zito na linachosha maana linaonekana kuwasumbua wazee tu ambao jukumu lao la kuangalia watoto lilishapita tangu siku nyingi nyuma.

ulitaka wakazalie wapi??? Gesti au kwako??
 
hapo ndio ujiulize ww kwann mwanaume akukatae kama kweli yeye ndio mhusika?
Unatakiwa ujitathmin mwenendo wa mahusiano kipind upo naye,, nakuona kabisa unachombezwa na wanaume zaidi ya wawili utafikir mm ntakukubali kirahisi?

Upuuuzi wanaoufanya iweje ukubali kubeba mimba wakat unajijua upo kwa wazaz wako?
Hujatambulishwa hajatambulishwa wala mahar hujatolewa how come?

Mabint kiukweli hawajitambui, hawatambui thaman yao, hawaitambui heshima ya familia yao...

Mimi ni mwanamke ila wanawake wenzangu wengine sio...wana apply PMU (Pata Mimba Uolewe).....wanategesha kusudI...matokeo yake ndio hayo...unabwagwaa anaenda olewa mwingine...mwanaume hajakwambia umzalie...kwanini usiwe makini na siku zako...au ndo utamu unakolea..hell no....wanaume sometym tunawaona wabaya vingine twajitakia..kwanini akubali sex bila condom
 
Hili halikuwepo miaka ya 90s kurudi nyuma, sisemi kwamba haikuwa ikitokea, la hasha! bali hata kama ilikuwa inatokea basi ni kwa asilimia ndogo sana tofauti na ilivyo sasa.

Katika maeneo ninayokuwa hasa kwa watu mbalimbali ninawafahamu, jambo hili linaonekana kukuwa zaidi ya mara dufu na inavyoonekana hali ikazidi huko mbele ya safari.

Mabinti wengi wanaozaa wakiwa bado hata hawajaposwa wamekuwa wakiwaacha watoto wao wakilelewa na babu&bibi huku wakiendelea masuala yao ikiwemo kuendeleza uhusiano na wanaume ambao unapelekea kuongeza idadi ya watoto kwa wazazi bila kujua ugumu wa kulea watoto.

Wanaume wamekuwa wakiwazalisha mabinti bila kuwaoa wamekuwa hawatoi ushirikiano wa kulea badala yake mwanamke ndio anaachiwa jukumu la uangalizi wa mtoto ambaye naye anakabidhi majukumu kwa wazazi wake! kimsingi wazazi hawawezi kuwakataa watoto wa watoto wao.

Suala linaonekana kuwa mzigo hata kama mtoto atapewa mahitaji mengine kama kulishwa na kuvishwa kwa gharama za nje ya wazazi wa binti lakini suala la kuwaangalia watoto ni zito na linachosha maana linaonekana kuwasumbua wazee tu ambao jukumu lao la kuangalia watoto lilishapita tangu siku nyingi nyuma.

Utandawazi unahusika sana
 
kwa upande wangu wazazi wanachangia kwa kiasi kikubwa sanaaaaa. nina uthibitisho kwa mabinti kadhaa ambao nawajua, mmoja wapo akiwa sister wangu. sister wangu wakati yupo chuo kuna watu wenye heshima zao walikuwa walikuwa wanakuja nyumbani kutaka kumuoa lakini kikwazo kikubwa kilikuwa kinatoka kwa wazazi!! nakumbuka wazazi walikuwa wanasema "mtoto wetu bado mdogo, anasoma na visingizio vingine kama hivyo ambavyo walikuwa hawaviweki wazi (mfano jamaa anaetaka kumuoa akiwa hana pesa za maana) wazazi hao hao waliokuwa wanakataa asiolewe walikuwa hawajui binti yao ambao wao wanamuona mdogo kuingia kwenye ndoa, kumbe binti yao alianza mambo ya ngono tokea zamani. wamekuja kustuka mwaka wa tatu chuoni sister ana mimba!! akazalia nyumbani na jamaa aliyemtia mimba aliikataa mimba. mtoto mpaka leo hii yupo home analelewa na wazee.

na mi huwa nawachana live wazee kuwa wao ndio waliosababisha binti yao kuzalia nyumbani kwa kumuona ni mdogo kuwa hawezi kuingia kwenye ndoa. kumbuka wazee wetu walikuwa anaolewa bado wadogo sana (mfano bi mkubwa wangu anasimulia yeye aliolewa na miaka 18) sasa hapa ndio nashagaa kwanini walishindwa kumuozesha binti yao kwa kipindi kile ambapo alikuwa na miaka 22!!

wazazi inabidi muwe makini sana kama mtu anakuja kutaka kumuoa mwanao kwa nini ukatae na unaweaza kuta mtu ana vigezo vyote vya kuoa lakini wazazi wanasigizia binti mdogo na mambo mengine!! matokeo yake aibu mtoto anazalia nyumbani. AIBU SANA!!!

Umesema vizuri mkuu
 
Back
Top Bottom