Nini tafsiri ya ndoto hii ?

Nini tafsiri ya ndoto hii ?

naishukuru jf na nakushukuru na wewe pia,kwajinsi ulivyolichambua hili jambo hakika ni dhahiri,ni kweli nina ambition ya mafanikio kupita kiwango cha kawaida,ila tangu nazaliwa sijawahi kufikiria kupata mali kwa njia isiyo halali,nimeshawahi kujitoa kwenye mradi tulioanzisha na wenzangu ambao ulikuwa wa hela nyingi sababu kubwa ikiwa niliona kuna njia za udanganyifu wenzangu wanataka kuzitumia,sijawahi kuiba hata cent wala kufikiria kufanya hivyo,nina uamnifu wa hali ya juu,lakini naheshimu hapo uliposema sijawahi kutangaza,hakuna anayejua ambition zangu,ni mimi mwenyewe tu

wewe ni mtu mwaminifu. nauona uaminifu wako katika maneno yako. ila kufafanua kauli yangu labda niseme hivi. sijakuita mwizi. ila nimesema kwenye ngazi yako ya hurka ya ubinadamu ambayo imejificha, ambayo inaitwa sub-conscious, kunaweza kuwapo mambo nje ya utashi wako katika hali halisi. Na wewe hautakuwa wa kwanza kuwa na mgongano kati ya kilichopo kwenye hali halisi, nipaite concious level, na hurka iliyojificha (sub-conscious level). Binadamu wengi wanakuwa na tatizo hilo la vita kati ya conscious na sub-conscious.

Na pale vita hiyo inapokuwa kali sana kati ya hali halisi kupingana na hurka iliyojificha, binadamu wengine hupatwa na ugonjwa wa akili unaoitwa Neurosis kutokana na vita hiyo ya ndani kwa ndani. Unaweza kukuta mtu analewa kupindukia. Mwili upo katika vita hapo; inawezekana kabisa pombe inatumika kufunika hitaji katika hurka iliyojificha ambalo limekatazwa ha hali halisi. Au mwanamke, au hata mwanamume anaweza kuwa kitandani kavua nguo zote lakini mashine ikawa imegoma kabisaa.... Hapo uwezekano mkubwa ni kwamba kuna vita kati ya sub-conscious na hali halisi. Hizo ngazi mbili hazijakubaliana kuhusu kitu.

Now back to the topic: kwa maelezo uliyoweka awali, na haya ya sasa, napata picha kwamba conscious level yako, yaani hali halisi inayo upper hand katika maamuzi yako. Lugha ya kawaida wanasema umeweza kujitawala. Hilo ni jema. Lakini ndoto zako zinaonesha kuna kitu unataka. Ni vizuri kwamba umeweza kujitawala, ingawa hilo halina maana kwamba unaweza kujitawala kila wakati, ndiyo maana kunakuja hitaji la kuwa na kitu kinachokuwezesha kuwa na kipato ili kishawishi hiki kibaya kilichopo kwenye sub-conscious kisifike mahale kikapata upper hand. Ni wakati mzuri pia kuwaza habari za msaada kutoka kwa Mungu, kwani mafundisho mengi yaliyopo katika dini nyingi yanaelekeza kuzishinda hurka zetu za kibinadamu za ulafi. Katika Ukristo wanasisitiza sana neno 'kiasi'; kwamba uwe mtu wa kiasi, na uendelee hivyo. Maelezo yako ya pili yameonesha kuwa wewe umejitahidi sana kuwa mtu wa kiasi. Naomba Mungu akutie nguvu ili uendelee kuwa hivyo uishinde hii hurka ya ulafi wa utajiri kama wanayoonesha wabunge wetu kule Dodoma
 
Utajiri huo mama, unakujia lakin lazima uende kwanza kwa mganga wa kienyeji
 
Naunga mkono hoja,umesema ukweli, tena itakuwa katika biashara afanyayo anapata fursa nzuri za kujikuza kiuchumi lakini anazipuuzia,kama ulivyosema inabidi ajitahidi kujiepusha na makundi yasiyofaa yafanyayo biashara isiyo halali ambayo itampelekea kny matatizo
nimepata msaada, nimeanza kujisogeza karibu zaidi na muumba,nayaishi maneno yenu kwa maana nimeamini ni kweli ni nisipokuwa makini nitapotea
 
Nimeota mimi mwenyewe na niliwahi kuiota pia, hii ni kama mara ya 2 au 3,iko hivi; natokea magari wawili ya kubebea pesa yanapinduka(ni katika mji ambao sijawa kuuona ila mazingira na matukio kati ya ndoto hii na zilizopita yanafanana), watu wengi wanaenda kuokota pesa ambazo ni dollar lakini mimi siendi naendaelea kutembea, baadae wenzangu wawili niliokuwa nao lakini walienda kuokota dollar wanarudi nazo na wananipa nyingine niwashikie wao wananipa dollar 250 zote walizokuwa nazo na wanabaki na dollar ambazo ni dollar 20, 10 na nyingine lakini hakuna kubwa kufikia note za dollar 250 aliyenipa hela nishike ni mtu niliyesoma nae chuo kikuuna huyu mwingine ni ndugu yangu na inaoneka walikubaliana wagawane baadae, mtende inaonekana anataka kama baadadhi ya note za dollar 250 anataka kumdhulumu ndugu yangu,natambua hilo kwa kumwangalia machoni na mm nakuwa kama nimekubaliana nae.

Mimi naelekea mahali pengine na wao pengine kwa miadi ya kukutana baadae, mimi naangaika na kutafuta bar hili nile ghafla rafiki yangu ananipigia simu kuwa niende kuongea na simu kwenye jengo alimokuwa ambalo ni kama benki kuu hivi ananitajia jina la mtu anayetaka kuongea na mimi, ni mtu ambaye nimemfaham kupitia ndoto niliyoota before ndoto hii kwa maana ndoto zilipandana na siikumbuki hiyo ndoto ila nakumbuka kuwa namfahamu huyo jamaa, namwambia rafiki yangu a-transfer call kwenye simu yangu ya kiganjani lakini anakataa na mimi namuona kwa kuwa jengo lilikuwa mbele yangu,

Wakati naenda kuwaona nilitereza nikaingia kwenye dimbwi dogo la matope machafu sana na kunauwezekano tope likawa limechanyika na kinyesi.

Sandles zangu zinapotelea humo, natoka humo nafika ili kuongea na simu kumbe ni mtego wale wenzangu walikuwa wameshikwa na walitumika ili na mimi nishikwe,wakati nashuka na watu wa benki kwenda ukaguzi na dollar ninazo mfuko nafkria nifanye nn mara ndugu yangu ananipa 12,000 ni niwape wakaguzi wasinifunge, wakati nafikiria udogo wa 12,000 huku nazipokea nikawa najaribu kutoa hizo dollar nimpe ndugu yangu ili nisikutwe nazo ikawa inaniwia viggumu na ndoto ikaisha.

Naombeni tafsiri wana jamvi,si mara ya kwanza kuiota, si kila mtu ana kipawa cha kutafsiri ndoto na ipo mpaka kwenye vitabu vitakatifu, mimi nimeshindwa kuielewa naomba mwenye kuielewa anisaidie

Maana yake tunza mzigo wako kwani kuna njama za kuibiwa...mzigo ni pamoja na mama watoto wako, mali zako
 
tayta tuwekee picha

hahahaaaa sijui ataweka ya madola yaliyomwagika au kudumbukia kwenye kinyesi au, au...au?

hahaha ngoja tumsubirie mkuu

Tyta hebu tafsiri hii ndoto kwa picha.... Rural Swagga anataka aione kwa picha!
DreamingOfMoney.jpg
Dreaming_of_Money.gif
 
Jana nmeota kua watu wamejazana ikulu nje kuzunguka fensi ni wengi hadi posta na wana mapanga, mawe, marungu na silaha zingne za jadi...pia kuna polisi 100 na magari 20 ya washawasha......
 
Uliwezaje kuwahesabu polisi na ukapata idadi yake?
Au kwasababu ni ndoto?
 
Subiri tutaanzisha category JF kwa ajili ya ndoto za watu muweke post zenu zote kule.
 
Oh nilimsikia mkulu jana akisema si tz hatukopesheki kwani tuna virungu, magari ya maji ya kuwasha, pingu na mabomu ya machozi...we unadhani nani atarisk ela yake atukopeshe? Hiyondo tafasiri
 
Inaelekea una kawaida ya kuwaza mara kwa mara kuhusiana na kilichokutokea ndotoni ndio maana umejiwa na hiyo ndoto
 
Hilo ni suala la katiba kaka katiba wananchi wanayotaka viongozi wakilazimisha huenda Magogoni pasikalike pakawa kama Tunisia!!Hili jambo ni la kuombea lisitokee.Lazima tutafakari kwa nini umeota wakati huu?kwa nini umeota Ikulu ya Dar?Kwanini hujaota chama fulani?kwanini wana silaha za jadi na sio za moto?Hapa kuna jambo kubwa tuweke siada pembeni huo ni ulimwengu wa roho unaobeba ulimwengu wa mwili wa baadae.all the best
 
Hii ndoto ilikuwa inamaana mbili:
1. Uliumia sana sanana maneno ya jk bungeni
2. Kikwete yuko Safe mpaka anatoka madarakani na hao watu uliowaona hapo nje. I wale waliochukizwa na hotuba yake
 
Habari wana MMU,
Nimekuwa nikiota ndoto, nashindwa kupita kwenye daraja nyembamba ya miti au njia za milimani au ngazi. mfano leo nimeota ngazi, ilikuwa mchana na watu wengi tu wanapita mimi nikiwa na mr. tulipofika sehemu ya kushuka hizo ngazi sasa ni nyembamba imesimama wima na anapita mtu mmoja mmoja, na akiwa anashuka mtu zinakuwa kama zinacheza cheza. ilipofika zamu yangu nilipojaribu kushuka nikawa naona kizunguzungu nikashindwa nikaa pembembeni wakati huo Mr. alishashuka yupo chini anagomba kwa nini nashindwa kushuka wakati wengine wanashuka.

Msaada tafadhali.
 
Pole that's means utakwama/kushindwa kwy jambo muhimu maishani mwako!kama ni unayeamini uwepo wa bwana na mwokozi Yesu Kristu,sali na kemea maana hizo uwa ni hila za shetani!
 
Hivi kuna wafasiri wa ndoto humu?
hebu jiamini bwana! Wanavuka tembo na nyati kwenye vidaraja msituni seuze wewe?
 
Back
Top Bottom