Nini tafsiri ya ndoto hii ?

duh me sipo deep kiivyo ila First what does your heart tells you. .go with it..thats God's voice. sikiliza sauti inayokupa amani ndani yako. go with it.

Best answer so far.
Kudos!
 
Shalom! Ingawa mimi sio mtumishi lakini tambua Mungu ameweka kusudi katika kila mwanadamu, hivyo nawe kwanza muombe Mungu akuonyeshe kusudi lake na usimame ktk hilo. Pili ktk kila jambo kuna muda na mahali maalumu Mhubiri 3:1-11. Tatu tambua kanisa ni mwili wa Kristo una nguzo zake kuu kama huduma mbalimbali, lakini pia karama tofauti ili kuujenga mwili wa Kristo kwa kufaidiana.
Kutokana na hayo hapo juu ninafikiri uliitwa kutumika kweli, lakini ktk kanisa la mwanzo, tatizo hukuwa na subira wala kumuuliza Mungu ukaenda kusoma? Na umeanza kutumika hapo. Lakini kwavile si kusudi la Mungu wewe kuwa hapo ndio unakutana na maono hayo unaitwa kule ulikokusudiwa na hivyo kujikuta huna amani na ufanyacho hapo. Kwamba unapofika kanisa la mwanzo unakuta mtu anahudumu hiyo sio kikwazo ni kuwa wakati wako utafika unaitwa ukakae miguuni kwa Mungu, ukakae chini ya mtu uikulie huduma yako ukiwa tayari utaitwa kutumika. Nakupa mfano wa Biblia watu ambao waliitwa, walipakwa mafuta na kuzijua kusudi zao lakini walikaa miguuni mwa Mungu chini ya watumishi wakijifunza ndipo wakaanza kutumika: mfalme Daudi chini ya Sauli, nabii Samuel chini ya Elli, Paulo na kanisa la Antiokia, Timotheo kwa Paulo. Nakushauri kaa chini muulize Mungu kusudi lako kusoma Theology sio kuijua karama yako. Kama mtumishi omba ujue kuisikia na kuijua sauti ya Mungu. Zaburi 27, uwe na ------. Blessings
 
Wewe unatamani kwenda huko, Hayo unayoyaongea ni reflection ya mawazo yako. Cdhani kama hiyo ni ndoto kama ulivyoandika . Pia ninahofu na imani yako mwalimu, sababu kama kweli ni ndoto ungeomba Mungu akuongoze kuitafusiri kuliko kuja kutuandikia hapa.
 
It sounds mwenyewe unapenda tu huko ACT kiasi hata mawazo yako yako huko kwa kiasi kikubwa na ndo maana unaota ota the same thing. Jiulize kwanza ni kitu gani unataka?, project faida na hasara za hapo ulipo na huko ACT, angalia future. Ila la msingi SIKILIZA SAUTI YA MUNGU
 
Act umechemka...chama cha waha,rudi kule kule kwa awali
 
Kuna saa huwa sielewagi kabisa. Wee sema kule kwa zamani unaona kuna neema zaidi.

Na unapaota sana sababu unapawaza sana. Kumbuka uliondoka kule kwa maslahi ya kidunia (ajira ya uchungaji), nahisi uchungaji wako.ni kikazi zaidi kuliko wito zaidi.
 
unashindwa kuelewa labda pia hata na kwa mifano ya majina ya hayo makanisa, mengine hayana baraka za Mungu, jaribu kubadirisha halafu pioga goti Mungu akufunulie maana ya hiyo ndoto, mwambie Mungu kama ulivyompa kipawa cha kutafsiri ndoto yusufu kwa farao akupe na wewe, ila muhimu badilisha hayo majina nuliyotoa.
 
Mungu hana dhehebu, akikuita ni amekuita kwa ajili ya Watu wake, utakuwa umefanya kosa kubwa sana la usaliti kwa hao waliokusomesha kama ukiamua kurud kule bila ya kutumika kwao, (walau kurudisha faida ya investment yao kwao )

After chukulia kama Mungu ni mjenz mkuu, kanisa lake ndo linalojengwa, hao ACT ni mafundi mchundo, Na KT ni wapauaji, wewe ukatoka ACT ukaenda KT haulet hasara yeyote kwa fundi mkuu, ila kwa kikundi cha wale wapauaji.

Amani ya kristo ikuongoze katika maamuzi yako. Amen
 
Aisee.Sijui nisemeje!?!Lakn hukupaswa kuleta hili hapa Jf.Mtafute Mungu unayemtumikia akujibu..
 
Mimi huwa naota napaa...yaani ikitokea ishu na nataka kuondoka then nashtukia napaa juu kama ndege na naenda popote na eti watu wanakua wananishangaa...na hii ndoto imeshajirudia kama kumi hivi na sijui maana yake....hadi nimeizoea
 
Mkabizi mwajiri wako(Mungu) Kwa njia ya maombi na kufunga atakupa majibu sahihi siyo hapa JF
 
Itafute kweli nayo itakuweka huru.

Na kweli hiyo hutaipata kwenye MISA wala JF.

Roho mtakatifu yupo kwa mambo mengi.
Mfano hutuelekeza wa kumwomba ushauri.
 

Inategemea KANISA GANI. Streamline Churches zina utaratibu wake. Huwezi tu kwenda kuhudumu bila utaratibu kuna taratibu za kutambulika na labda halmashauri kuu, Tume ya Askofu n.k. Ila najua pia kuna makanisa ambayo utaratibu huo haupo kama uko huko, usiende kuharibu kazi za watu simply moyo wako au ndoto imekuonyesha hivyo, we fuata Utaratibu kama unawiwa kurudi ulikotoka mara ya kwanza, Mfuate Kiongozi wako kama ni Askofu au Mkuu wa Jimbo au Mchungaji Kiongozi mweleze na mzungumze. Lakini ukumbuke pia kuwa waliokusomesha pia walikuwa na lengo la kupata watumishi, hivyo ni vema kuwekana nao sawa. Nje ya hapo kule ulikotoka ACT unaweza kwenda kuwasalimia na kuhudumu mara upatapo nafasi, kwa suala la ajira mhh sijui! Pamoja na kwamba ni ndoto hayo mambo yanahitaji taratibu za kibinadamu pia, achana na kwamba ndoto zinaweza kuwa zinacommunicate spiritual things. All the Best.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…