Nipo chuo kikuu ( MZUMBE ) Morogoro; Naombeni msaada kwa moyo mmoja

Nipo chuo kikuu ( MZUMBE ) Morogoro; Naombeni msaada kwa moyo mmoja

Hiyo huwa ipo na wala Tatizo sio Lugha, nakumbuka nikiwa wakati nikifanya Field ya Masomo yangu nilipata NGO moja inayo fanya kazi na vikundi so tukawa tunaenda Vijijini kufanya Mikutano ya Uhamasishaji, ilikuwa kazi sana kuongea mbele ya Wanakijiji, Ila taratibu nilianza kuzoea na sasa hata kama ni watu wengi namna gani kama wale wa Mikutano ya CDM naweza ongea kabisa,

Ishu si Lugha bali huwa ni uoga uliopo miongoni mwa watu, na hii vilevile kwa Chuoni husababishwa na my be kujiona utakosea na kama mdau mmoja alivyo sema kama kuna Demu unamzimikia hapo ndo tatizo kabisa
 
kipindi niko chuo jamaa alilewa ili apresent lililomkuta ni alizimika katikati ya presentation. moja ya siri za presentation nikuto kuwaangalia unaowapa presentation unatakiwa wao waone unawaangalia while wewe waangalia kwingine.
 
Darasa lenu lina ukubwa kiasi gani? Jaribu kuongea wakati mkiwa kwenye discussion kabla ya kua mbele ya mkufunzi uone kama utaweza.watu wengi kuongea mbele ya umati ni ngumu sana hasa siku za mwanzoni.Yawezekana hata lugha nayo ni tatizo make English ni wito.Jaribu na husikate tamaa misho wa siku utaweza.
 
Mimi ni mwanachuo mwaka wa kwanza Mzumbe, kama mjuavyo chuoni kuna presentation za hapa na pale. Tatizo linalonikabili ni kushindwa kabisa kuongea ninapofika pale mbele ya darasa, nasika kutetemeka, roho inakwenda mbio sana,midomo inakauka kabisa yaani naskia kuanguka.

Nimejaribu kufata jinsi wenzangu wanavyonishauri ili niweze kushinda hali hiyo ila nimeshindwa kabisa hivyo naongea kidogo tu nashindwa kabisa kuendelea kwani sauti inatoweka kabisa nashindwa kuongea. Naskia uchungu kuona wenzangu wanavyoongea vizuri mbele ya darasa lakini mi nashindwa kabisa.Kwa mwanafunzi yeyote atakayekuwa yuko na mimi kozi moja na darasa moja hope atakuwa amenijua hivyo naomba pia anipe ushauri kama bado hajawahi kunipa tukiwa group discussion.

Mwisho wanaJF wote natumai mtanipa ushauri utakaoweza kunisaidia.
kijana hilo ni jambo la kwaida kuwa na fear what byou have to do is to think of your role model like obama or oprah and then it is done. utakuwa na confidence ya kufa mtu lakini ucisahau what you are talking about!!
 
zaidi pia tangu niko shule chekechea hadi hapa nilipofika sijawahi kabisa kufanya presentation sababu mi nimesoma msingi kijijini na secondary pia kijijini,,,,,,,,,,,,ila five na sx kidogo ndio ilikuwa mjini sababu shule ilikuwa wilayani.....huko kusini huko,,,,,, sasa hivi ndio niko morogoro yaani nimekutana na presentation nashindwa kabisa kuongea,,,,,,,ila moyoni naumia sana ninaposhindwa sababu najitahidi lakini wapi,,,kuna rafiki yangu kaninunulia vitabu viwili nimevisoma lakini wapi,,,,,,vyote ni vya public speaking, pia nimesoma sana kupitia internet jinsi yakuweza kuongea mbele za watu lakin badi haijanisaidia,,,,,,, yaani siku ya presentation naiwaza,,,,,,yaani km ni kesho usiku silali,nakuwa nawaza na kushtuka jinsi ya kwenda kuongea pale mbele,,,,,,,yaani jamani mwenzenu napata tabu si siri,,,,,nisaidieni jamani
Just relax amini wale wanafunzi wenzako mpo pale kwa ajili ya kujifunza,dakika ya kwanza nay pili lazima utetemeke laikini baada ya hapo unaagain control.Wakati mwengine kabla hujaenda kupresent wachukue marafiki zako kadhaa muende sehemu yenye uwazi mkubwa au kidarasa fulani halafu ufanye maazoezi ya kupresent baada ya siku kadhaa ukuwa nondo
 
mmm hii wakati naanza chuo nilikuwa nayo

mimi sikuamini nilichofanya siku ya presentation ya DS nilijiona siwezi but kumbe mm ni bonge la presenter

funika vibayavibaya, hope ni kujiamini kama unawezaaa
 
mimi sikuamini nilichofanya siku ya presentation ya DS nilijiona siwezi but kumbe mm ni bonge la presenter

funika vibayavibaya, hope ni kujiamini kama unawezaaa
mkuu mimi pia mara ya kwanza advance nilikuwa nakoseakosea nikazoea.kufika chuo kupewa microfoni ambayo cjawah tumia ilinitia kiwewe but now nina macomfidence mbaya
 
usizoeane na ma she kupita mpaka dats my advice.fanya hivyo den ipo siku utaniPM mwenyeww
 
Wakati wa presentation macho yako angalia nyuz 90, geuka pembe zote za drs, usiangalie mtu na USIWE NA HOFU. 0788325376
 
Ushauri mwingi sana umepewa sasa chukua ule mzuri sana halafu nenda kaufanyie kazi ili baadaye utuletee kilichojiri maana hata JK Mrisho alikuwa hivyohivyo akashauri hapa jf vunja baraza la mawaziri akavunja,epa watu wameiba akafuatlia ni kweli
Tatizo lake hadi kesho ni finishing ya mambo anayoambiwa hapa jf,zaidi inakuwa bhalaa bhalaa hadi sasa anamaliza miaka yake ya urais.
 
Back
Top Bottom