Dada, Asante sana kwa majibu yako. Ni kweli una tatizo na, kwa maoni yangu, tatizo hili si la mwenzio bali ni la kwako.
Kabla sijakupa ushauri napenda kukufahamisha kuwa asilimia kubwa ya wanawake duniani hawafikii kilele (orgasm) katika tendo la ndoa kwa hiyo huko peke yako. Mara nyingi hili ni tatizo la papara za sisi wanaume na sio la wanawake. Wakati mwingi sisi wanaume kama dushelele letu likisimama tu basi hujali kama mwenzio yuko tayari au la - tunaparamia tu na baada ya dakika moja au mbili (at most) tunachemsha - hoi. Wanawake wengi inabidi wajitosheleze wenyewe (masturbation). Pengine itabidi tutafute muda hapa sisi wanaume (kwa msaada wa wakina mama) tujuzane the art of love making and not just jerking-off.
TATIZO LAKO:
Mimi naona hili tatizo ni la kwako. Nitajaribu kueleza tatizo liko wapi lakini NASISITIZA umuone daktari wako (obstetrics/gynecology doctor) ili aweze kukupima na kukupa ushauri mzuri.
Tatizo lako nadhani ni lile wataalam wanaloliita FOD (Female orgasmic disorder) au taahira ya nyege kwa wanawake. Hili tatizo linaweza kuletwa na sababu kuu mbili. Sababu za kumaumbile (physiological factors) au sababu za kisaikolojia (psychological factors).
TATIZO LA KIMAUMBILE:
Nyege (sexual arousal) hutokea wakati mishipa ya damu kwenye kinena (uke ) ikipanuka na kuruhusu damu nyingi kupita kwenye uke. Hii inafuatiwa na ute kuenea kwenye uke wote na kutoa utelezi (lubrication). Hali hii inaendelea mpaka utakapofikia kilele (orgasm). Wanawake wana bahati kuwa wanaweza kufikia vilele zaidi ya kimoja kwenye tendo moja la ndoa kutegemea alihanjamishwa (excited) kiasi gani mwanzoni.
Hii nyege inaweza kuwa tabu kuipata kama:
· Mishipa ya damu kwenye kinena imeathirika hivyo haileti damu ya kutosha.
· Matatizo ya mishipa ya fahamu (nerves or spinal cord) inayokuja kwenye kinena.
· Side effects ya madawa (kama antidepressants, narcotics, nk.)
· Kukeketwa (ambako umesema hukufanyiwa)
TATIZO LA KISAIKOLOGIA:
Hili kwa kweli ni tatizo gumu sana kulijua au kulitibu kwa sababu kuna vitu vingi sana vinavyoweza kukufanya usipende tendo la ndoa. Vitu vinavyoweza kufanya hali hii ni:
· Matatizo ya maisha (fedha, ajira, shinikizo toka kwa ndugu, shule, nk.)
· Mambo yanayokufanya uone tendo la ndoa kuwa ni uchafu kufuatia KUBAKWA ulipokuwa mtoto au mafundisho ya kidini/kimila uliopata wakati ulipokuwa unakuwa.
· Mental health disorder au depression kubwa.
TIBA:
Kwa sababu si rahisi kujua tatizo lako liko wapi, ushauri wangu ni umuone daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake akupe ushauri mzuri.
Samahani sikuweza kukupa tiba ya uhakika. Naomba jumuia inisahihishe ipasavyo kama nimekosea mahala. Lengo ni kupata njia ya kumsaidia mwenzetu.
Nawakilisha.