Nisaidieni mbinu za kupambana na huyu jirani 'mwizi wa umeme'

Nisaidieni mbinu za kupambana na huyu jirani 'mwizi wa umeme'

Kama ni usiku na amewasha taa na unahisi atakua anatumia umeme wako, nenda kwenye main switch zima kisha cheki kama jirani kuna giza
 
Kama wiring ya nyumba ni ile inakua shared na wall sockets za chumba zaidi ya kimoja basi inawezekana kachomeka extension na friji lake, tv na subwoofer la Sea Piano vyote vinafadhiliwa na wewe.

Yaani yeye units zake zinasoma kwenye taa tu.
 
Nafatilia nasubiria mrejesho. Mtu kuiba umeme waziwazi hizo Ni dharau Kama ni kweli
 
Kwahiyo jirani ndo umekuja kunitisha na huku ili nisikudhibiti?

Sasa kwa taarifa yako, lazima nilete fundi akague. Kama ulikuwa huna bajeti ya umeme anza mapema kuitafuta.

Naenda kukata mirija ya umeme wa kitonga
Huna lolote mkuu.. huo umeme unaotumia ni wakwako kabisa we lipa bili. Kwanza unamavitu mengi ya umeme unashangaa nini bili kua kubwa? Jikaze kiume 🤣🤣
 
Hii nyumba ninayoishi tupo wapangaji watatu kwenye compound moja. Nimehamia hapo huu ni mwezi wa pili unaenda kuisha.

Ndani ya hizi wiki chache, nimeona mabadiliko makubwa ya matumizi ya umeme. Mwanzoni ilikuwa natumia wastani wa unit 2.4 kwa siku, ila kwa sasa imepanda mpaka 3.6 kwa siku.

Nimeona sio kawaida, mpaka nimehisi kwamba inawezekana kuna jirani ananipiga umeme wangu, na ushahidi nilionao ni kwamba, mahali ilipo mita yangu ipo pamoja na jirani yangu mmoja, ila sasa maajabu nashangaa hii siku ya pili nimechunguza, hiyo mita ni kama unit za umeme za jana ndo zipo leo. Nikimaanisha kwamba, ni kama vile huyu jirani atakuwa anatumie umeme kwenye source ingine ambayo possibly ameconnect umeme wangu.

Nnachokifikiria kwa haraka haraka ni kumleta fundi wiring ili akague system nzima ya umeme wangu.

Naombeni mnipe mbinu zaidi wakuu, nimekereka sana kuligundua hili, kitendo cha mtu kuniibia huwa nakichukulia kama kuniona sina akili na kunitusi.

Nahisi kama nimuadabishe bila kumuambia chochote. Haiwezekani mtu ufikiria kupambana na maisha halafu ufikirie tena kupambana na majirani wezi.

Mbinu safi na chafu nazipokea ahsante
Anayekuibia umeme siyo lazima readings za mita yake zibaki constant.
Inawezekana huyo mwizi mita yake akaibebesha mzigo wa vifaa visivyokula umeme. Hivyo mita yake itasoma units kidogo na mita ya Mushi akaipiga mzigo kisawa sawa na ikasoma units nyingi.
 
NJIA sahihi ni kukagua system.

Inawezekana huyu jirani yake ka connect waya wa kwenda kutumia device moja au mbili wenda jiko au friji huku system nyingine iki fanya kazi sawa..

Kama kafanya hivi basi jamaa kwa kutumia mbinu ya kuzima, au kusubiri uneme uishe bado hato pata jawabu ikiwa jamaa ame connect na friji au jiko la kupikia.
 
Anayekuibia umeme siyo lazima readings za mita yake zibaki constant.
Inawezekana huyo mwizi mita yake akaibebesha mzigo wa vifaa visivyokula umeme. Hivyo mita yake itasoma units kidogo na mita ya Mushi akaipiga mzigo kisawa sawa na ikasoma units nyingi.
Hapo sawa sawa..sasa nishauri hapo.. itakuwa wizi umefanyika kwenye waya huo mkubwa?
 
Kama wiring ya nyumba ni ile inakua shared na wall sockets za chumba zaidi ya kimoja basi inawezekana kachomeka extension na friji lake, tv na subwoofer la Sea Piano vyote vinafadhiliwa na wewe.

Yaani yeye units zake zinasoma kwenye taa tu.
Hii ndo nahisi imefanyika, yaani wizi umefanyika kwenye socket ambazo tunashare kuta.. nataka nilete fundi ikibidi nikate nyaya zote za socket ambazo zinaenda upande wa nyumba yake ilipo
 
Back
Top Bottom