Nissan Dualis yawaka moto. Hizi gari zina shida gani?

Nilichojifunza wengi wetu hatuna hata muda wa kufanya kusoma na kujua gari hii inahitaji nini na haihitaji nini...ila tunaruka na upepo w mafundi ....fundi kasema fundi kasema....na mafundi wetu sasa hawashauliki kabisa maana kuna fundi mkuu huko zamani alishamuaminisha kitu flani...kwa uzoefu wangu kumiliki chombo cha moto sio ghalama....lakini mafundi wamefanya iwe ghalama na anasa ....kwa sababu ya ujinga wao.
 
Mimi naona chanzo ni watu wengi kuanza kuvamia kutumia gari bila ya kusoma user manual,kuna maelekezo mengi sana juu ya kuendesha gari ukiwa unafuata maelekezo yao,ila kinyume cha hapo usitegemee miujiza.Kuna gari kama Range rover zina vitu vingi sana vinavyotumia umeme,sasa ukisema umeivamia tu na kuanza kuindesha kuna uwezekano mkubwa sana likakuletea shida.Sijafanya research yoyote juu ya hizi Dualis lakini sidhani kama zinauzwa Tanzania tu,na kama shida ingekuwa ni kubwa kihivyo zingeshatolewa sokoni.Kingine tujitahidi kwenda driving school,kuna wimbi kubwa sana la madereva hasa wa gari ndogo kujifunzia magari nyumbani na kununua leseni kisha kuingia barabarani,hili nalo ni tatizo lingine.....
 
Nissan Dualis chuma moja tamu sana [emoji3059] wala haina hayo makandokando wanayoisingizia!

Matatizo ni ya madereva wenyewe!

Wengine ni haters tu! [emoji817]
 
ni kweli spea zake hazipo TZ na hakuna fundi wa kuzijulia??
 
Nakubaliana nawe mkuu.
1. Changamoto iko sana kwenye services kwa wakati gari linaendeshwa tu.
2. Kuongeza vitu vya ziada kwenye magari. Kuna siku nilipita sehemu nikakuta mtu anafunga radio kwenye IST akaweka spika kubwa sana kwenye buti yaan nikabaki nashangaa tu. Hili pia nahisi linaweza kuleta shida kwenye mifumo ya umeme.
3. Kama ulivyosema upo uwezakano wa baadhi ya madereva hawakwenda kusoma udereva au walisoma lakini kwa juujuu au walisoma lakini wanapuuza ile elimu. Mfano mtu anawasha gari asubuhi bila kulikagua na kuacha kwa muda angalau dakika kadhaa.
4. PIa baadhi ya watu wananunua magari ambayo yako juu ya uwezo wao wa kiuchumi. Hii nadhani pia huleta tatizo kwenye kulitunza.
5. Pia kuna manual user kwenye magari nadhani pia inasaidia. Sijajua kwa magari ya kununua mkononi lakini ya kununua japan inakuja na kitabu chake kuna vitu ukivisoma vinasaidia. Pa unaweza ku google kwenye mitandao ukalisoma gari lako vizuri na ukajua jinsi ya kuishi nalo.
 

Mkuu sorry naomba nieleweshe hapa

umesema DSG oil inatumika kwa vw na audi, sikujua hili, siku zote nilikua naweka castrol ATF

Na je DSG oil inapatikana wapi maana sijawahi kuiskia. Na je nitapata madhara gani maana nimekua nikiweka ATF ya castrol
 
Mkuu sorry naomba nieleweshe hapa

umesema DSG oil inatumika kwa vw na audi, sikujua hili, siku zote nilikua naweka castrol ATF

Na je DSG oil inapatikana wapi maana sijawahi kuiskia. Na je nitapata madhara gani maana nimekua nikiweka ATF ya castrol
Gari yako ina gearbox ya DSG?
 
Mshaanza mafundi maiko.
Teknolojia muwezi mnaaishia Kubahatisha tu. Kuna fundi kakorofisha Alphad mpaka ijitambui nikiwasha inafungua vioo.
Kesho namdamkia tumalizane hajui uchungu wa kununua gari
Daaaaah [emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
 
Technolojia ya magari imebadilika na kubireshwa ila mafundi wa bongo weng bado technolojia yao ni zaman na hawataki kuboresha utaalamu wao apo ndo ttzo huanzia
 
Sasa tabu zote hizo Hadi saa ngapi na mafundi wengi hawajui?
 
Bro umesema safi sanaa.
Watu kama nyie ndo tuna wahitaji humu.

Mi ndo gari yangu,Sijalala mpaka sasa hivi hapa tangu niione ile ilio waka moto.
Maana nimenunua na week 2 tu.
Na mkopo wenyewe una riba ndefu.

Yaani ni stupid things.
Sorry Mkuu ,, gari sio kitu cha mhimu sana mpaka ukajiingize kwenye madeni yenye mariba
 
Bora nimeipata hii taarifa mapema. Nilikuwa naifikiria NISSAN DUALIS, lakini kwa taarifa hii, nimehitimisha kuwa NISSAN DUALIS hainifai.
Anakutisha tu.

Nilileta uzi humu kuomba ushauri kuhusu hii gari, kila mmoja alisema lake!

Mimi nikainunua!

Huwezi amini nilichogundua... wabongo wana negativity sana!

Wengi wanaondika humu kukandia, hawamiliki magari!

Nissan Dualis ni gari nzuri sana! Yaani sana!!

Maneno mengi kuihusu ni ya vijiweni tu!

Kuhusu kuwaka moto sababu na suluhisho lake ni hili hapa [emoji116]

View attachment 2788591
 
Safi kiongozi umeongea vyema.
Naomba kujua hili for more Clarification eg. Toyota Ractis ukitaka kufunga Mziki pamoja na Android yake hizo waya utachukua moto sehem gan bila kuathiri utendaji kazi wa injini pamoja na betri ya gari.
 
Mkuu nilichogundua mafundi ndio wanaua hizi gari mkuu. Transmission fluid yake OG lita 4 inauzwa kati ya 160000 hadi 180000 ikitegemea umeinunua wapi na gari inakula 7.5 lita sasa mafundi wengi hawajui anaweka lita 4 na mwenye nalo anaona kutoa 320000 kununua transmission fluid parefu.
Pili mafundi wanabahatisha.
Mimi wamela pesa yangu wakisingizia gearbox wakabadilisha TCM module ikawa kama imepoa bado tatizo likabadilika likaja lingine.
Solution nimekuja kuisolve mwenyewe na kwa njia rahisi.
Niliwaona wanagoogle nami nikagoogle. Waliweka TCM used so tayari ilikuwa na errors zake na Contorl module pia nayo ilikuwa na errors zake. Dawa na kufuta errors zote ianze jifunza upya uendeshaji wako.
Nilichofanya nikuchomoa terminal za betry unasubr dakika kumi then unaunga positive terminal na negative terminal unasubr dakika 10 ili zidrain umeme wote kwenye capacitors isahau kila kitu ikowemo na errors.
Baada ya hapo rudisha kila kitu.
Gari tatizo lilipotea gearvox haina shida kabsa.
Ila cvt inahitaj uendeshaji wa heshima si kukanyaga bati hovyo hovyo si nzuri kwa vijama wapenda ligi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…