Nitajie tarehe yako na ya mwenza wako nikwambie mpo vipi na hatima yenu, siri yake n.k

Nitajie tarehe yako na ya mwenza wako nikwambie mpo vipi na hatima yenu, siri yake n.k

November 30th Me
18th August Ke

Majina J (me)
F (ke)
Katika mahusiano yenu wewe unaonekana ni mwenye asili ya moto wa nyasi na yeye ni moto wa mkaa mnaendana vema kila mmoja kati yenu anamuona mwenzie anamfaa zaidi.

Kuna mambo mengi ya kusisimua yatakayo kuja kuwatokea kwenye mahusiano yenu, yeye mwenye kujiamini inatoa uhakika kabisa kwamba atafungua hisia zako zote za tamaa ulizonazo katika mapenzi, na mapenzi yenu ni ya maajabu sana, nyote mnafurahia kusafiri pamoja, kukutana na watu wapya, na kila mmoja kati yenu anafurahika kuwa karibu na mwenzie yeye ni mwenye kupenda uhuru sana ikiwa ni pamoja na wewe,

Hivyo katika mahusiano yenu kutakuwa hakuna matatizo ya wivu ikiwa ni pamoja na kutawaliana ni couple moja nzuri sana mkipatana.

Wewe una mwanga mzuri wa kuendana nae kimazungumzo na vile vile ni mwenye uwezo mkubwa wa kukabiliana na Gubu lake.

Hakuna maelezo mengi kuhusu mausiano yenu isipokuwa jambo kubwa moja ni kwamba nyie ni Grand mating.

Ukimpoteza huyo kumpata wa hivyo huwa kazi.

Rakims
 
Kiume
30/01

Kike
07/04
wacha nikujibu kifupi kama ulivyoandika.

Wawili kati yenu kwenye haya mahusiano mnaonekana kufurahika na utani wa kila mmoja kwa mwenzie na michezo michezo ya utani nyote mnapenda,

Jinsi unavyokuwa unamfikiria na kumtengeneza katika fikra zako basi mara nyingi ndivyo yeye huenda na katika tendo la ndoa yeye ni mwenye shauku/hamu ambayo hukuvutia zaidi ambaye hupenda tendo la kweli lisilokuwa na maigizo,

nyote wawili mnaelewana matakwa ya kila mtu katika kuwa huru, na wala hamtakuwa ni wenye kubanana banana katika uhuru wa kila mtu, na vile vile ni watu wa kupenda adventure na interest za nje zaidi,

na sio wenye kupenda kutawaliwa au kusikia la mtu kwenye mahusiano yenu, ingawa yeye mara nyingi hupenda kuwa mwenye kauli ya mwisho kwenye mahusiano yenu.

Ikiwa utakubaliana nae awe ndio kiongozi kwenye mahusiano yenu basi utafurahia mapenzi lakini kama wewe ni mwanaume basi wanaume wote wana asili ya kupenda kutawala inapofikia hatua anampa mwanamke madaraka huona kama anatawaliwa ni wachache hukubali hilo. Future yenu ni nzuri ikiwa kila mtu atacheza vema part yake.

Rakims
 
Mimi wa kiume
Herufu E na 19/06.

Mke wangu ni
Herufu L na 23/05

Imee kaaje
Kwa mtizamo mnaonekana nyote wawili ni wenye asili ya upepo wa pumzi hivyo katika vitu vyenu vingi nyie ni kama pacha wa kiroho lakini hiyo haimaanishi kuwa mmekamilika kwa sababu mnaendana kwa asilimia 83% ingawa mna thamani kubwa ya muendano mtizamo wenu unakuwa
Hakuna mfano wa mahusiano kama yanapokuwa yamejengwa na watu wawili wenye mtizamo huu wa upepo ulio wa kuendana vizuri kwenye haiba, wenye msisimko na furaha kama wa wewe na mwenzio mnaonekana ni watu ambao hamtawahi kuchoshana au kuchokana kirahisi kwa maana nyie ni kama mapacha na ni wenye nia moja kwa kila jambo ;- kasi yenu katika mahusiano inashika namba za juu mkiwa pamoja na mnakuwa ni sawa na mfano wa kuigwa kwa mahusiano ya wengine ndio hawa mkikutana utasikia ndoa zingine zinawapigia mfano kuwa unawaona fulani na fulani.

Nyote ndoto zenu kila mmoja kwa mwenzie ni kubwa na hakuna kati yenu anaweza kumkatia tamaa mwingine. Pia ni wenye mazungumzo ya kuvutia hata chat zenu mtu mwingine akitizama anaweza kutamani jinsi mnavyojibizana na jinsi mnavyoweza kuelewana katika maongezi

pia mahusiano yenu yanaonekana kuwa na marafiki wengi na pamoja mnaweza kuwa mnafanya makaribisho ya chakula au sherehe mkiwakaribisha watu wanakuwa wanawatamani sana. Sex ni mchezo mzuri na uliojaa matani mengi kwenu lakini ndio mahusiano yenu kuna kipindi yanaweza kuwa kama ya juu juu, yasio imara, na msiokuwa na utulivu hasa mkiondoka mazingira ya nyumbani /chumbani na mkikaa muda mrefu bila kukutana na kucheza cheza kimwili basi kila kitu kinakuwa machafuko mkikosa tendo kwa muda ikiwa mnajua au hamjui basi huzuka chokochoko za ugomvi wa maneno.

rakims
 
Me:- 12/04
Mwenzangu:- 15/12
Wewe ni moto wa jaha na yeye ni moto wa nyasi;
ni watu mnaendana vizuri tu ya kuzingatia ni kwamba yeye na wewe nyote mna moto wenye kufanana kwa maana moto wa nyasi huwezi kuanza wenyewe na pia moto wa jaha huzuka tu na kuwaka wenyewe hivyo couple yenu ni nzuri ila ina vichekesho vingi.

Yeye kwako ni mwenye joto la kukutosheleza,
Nyote wawili ni wenye kujituma, kujishughulisha na wenye kupenda kuwa pamoja vile vile kutoka pamoja.
Pia nyote wawili ni wenye kupenda raha au maisha mazuri,
vile vile kutakuwa kati yenu kuna migogoro;
hii ni kwa sababu nyote ni wakali na wenye kupenda ukweli,
Mabishano yatakuwepo na yakianza nyumba inakuwa kama kunawaka moto;-

Pia linapokuja suala la muingiliano yaani ufanyaji wako wa tendo kwa pupa sio kila mara yeye atavumilia

Pia hata hivyo kati yenu mna hisia za ajabu mkiwa pamoja,
hali ya ucheshi na kufurahia ushirika wa kila mmoja.
ni watu ambao hamuoni tabu kufanya mapenzi popote hisia zikiwakamata.

SEHEMU ZAKE ZA HISIA:
Sehemu zake kuu za hisia ni kwenye miguu na mapacha yake unaweza kurudi kwenye quotes za nyuma ukaona kuna mtu nimeshamuelezea

Rakims
 
Mimi ni Me 5/6 E
Yeye ni Ke 26/6 G
Mapacha na Kaa

Mahusiano haya yanaonyesha kwa yeye mwenye mapenzi ya hamu na shauku huweza kukutimizia wewe mwenye mahitaji ya kimwili zaidi

Furaha yako yako katika tendo huangaza tabia yake yeye ingawa mapenzi yenu huwa matamu mwanzoni lakini huwa hayana maisha marefu tabia yako ya michepuko/ kuchezea mapenzi humtia kovu yeye mwenye hisia kali sana za mapenzi zilizojificha,

Tabia yako na style yako ya kutongoza humfanya awe ni mwenye kujihisi kuwa huwezi kumlindia mapenzi yake nae kuliko kuumia atataka ajiengue taratibu. Wawili nyie hamna maisha marefu ya mahusiano kila mtu atashika njia yake.

Maana yeye ni mwenye kuhitaji mtu mwenye kulinda mapenzi na tegemezi, wakati wewe ni mwenye kupenda kuchangamshana na hupendi kufungwa fungwa na vile vile wewe ni mtu usiye na subira kwake kwa maana utafikia sehemu umuone kama drama queen na vile vile ulimi wako wenye maneno makali ni mchachu sana kwa yeye kuvumilia ambaye yeye ni mwenye Gubu la mara kwa mara.

Nyie mahusiano yenu mnahangaika kupandisha maji mlima.

Rakims
 
ME; 27.12 E
KE ; 14.10 A

Rakim
Mahusiano haya nilishayajibu ni sawa na huyu
Kwa jinsi ulivyoomba mkuu nilitamani majibu yawe tofauti lakini kwa uwezo ambao niliojaliwa kwa kifupi naweza tu kukujibu kwamba hapo umekosea uelekeo,
Wewe ni mchanga wa bahari na yeye ni upepo wa juu licha ya kutokuendana hata kukaribiana hakaribiani na hili utajionea maana ya ile kauli kwamba unaweza kukaa kwenye uhawara miaka 10 lakini mwaka mmoja wa ndoa ukakushinda.
Wewe ni mtu mwenye kuvutiwa na yeye kwa sababu anamvuto ambao wewe unajikuta ni mtu wa kumbembeleza na na kubembelezea mapenzi upendo mlionao unaweza kukuokoa kwa kipindi fulani lakini hizi ndio ndoa ambazo wenza huwa wanarushiana ngumi maana ni uvumilivu hadi una give up japo mtafanikiwa kupata watoto kirahisi na mtazaa watoto wazuri kwa kuwa tu mnaingia mlango wa 5 kwenye ndoa yaani kizazi na mali lakini mateso ni makubwa kuliko mapenzi.

Yeye ni mtu mwenye tamaa na wewe kwenye mahusiano kwa muda huu. Elewa ya kwamba mahitaji yake katika mapenzi kuna jinsi na hali atakazo kuwa anataka uwe na wewe hutakuwa na uwezo wa kumpatia kikubwa wapo ni hisia haijarishi utafanya nini kwake hataona ukweli wa hisia zako kumpenda na ataona ni maneno pia kutoshelezana kwenu ni kwa uchache sana yeye anapenda sana mauno na wewe magoti kidogo itafikia sehemu itakuwa ni mtihani kipindi hiki kwanza utakua huelewi elewi utakuwa unaona kama ni mtu asiyesomeka baadae mwezi wa 9 hadi wa 10 kama hujamuoa anaweza kukwambia anaona uelekeo wa maisha hauoni na kuna uweze kano mkubwa mwezi huo wa mwaka huu akaanza kujihusisha na mtu mwingine na pia utapata habari kupitia mawasiliano yake kwa hivi sasa.
Atapenda mambo ambayo hutaweza kumtimizia kwa wakati anaoutaka sio kwamba huna uwezo wa kutimiza na akiwa tofauti na mtu mwingine utaona hiyo tabia hana atakuwa nayo kwako.
Na katika hali za kujionyesha na kuwaonyesha watu kuwa anajambo fulani ni tabia ambayo wewe huna kitu ambacho yeye hupenda mtu aliyenae awe hivyo
Na utakuwa ukimuheshimu kwenye mahusiano na yeye atakuwa anakuchukulia kama ni mpuuzi,atakuona mbinafsi na unakosea na mapenzi hayapohivyo na utatolewa kasoro

Baada ya hapo kwenye mahusiano hukugeuka na kuanza
kuangalia mahali pengine. Na kukuweka uwe na wivu nae kwake ni starehe japo ni jambo litakalo kuwa linakutesa.
Japo kuwa ni mtu mzuri kwa watu wengine kwako wewe mahusiano haya ni Kichocheo cha maafa (Sijataka kwenda deep sana kwenye case ya wazazi ambayo ndio inanifanya nikwambie ni mtu asiyekufaa.

SEHEMU YA HISIA:
Kiuno chake ndio sehemu inapotawala hisia yake utaona analalama kiuno kinasumbua ili tu kupata kupapaswa na kukandwa eneo hilo.
 
Wewe ni moto wa jaha na yeye ni moto wa nyasi;
ni watu mnaendana vizuri tu ya kuzingatia ni kwamba yeye na wewe nyote mna moto wenye kufanana kwa maana moto wa nyasi huwezi kuanza wenyewe na pia moto wa jaha huzuka tu na kuwaka wenyewe hivyo couple yenu ni nzuri ila ina vichekesho vingi.

Yeye kwako ni mwenye joto la kukutosheleza,
Nyote wawili ni wenye kujituma, kujishughulisha na wenye kupenda kuwa pamoja vile vile kutoka pamoja.
Pia nyote wawili ni wenye kupenda raha au maisha mazuri,
vile vile kutakuwa kati yenu kuna migogoro;
hii ni kwa sababu nyote ni wakali na wenye kupenda ukweli,
Mabishano yatakuwepo na yakianza nyumba inakuwa kama kunawaka moto;-

Pia linapokuja suala la muingiliano yaani ufanyaji wako wa tendo kwa pupa sio kila mara yeye atavumilia

Pia hata hivyo kati yenu mna hisia za ajabu mkiwa pamoja,
hali ya ucheshi na kufurahia ushirika wa kila mmoja.
ni watu ambao hamuoni tabu kufanya mapenzi popote hisia zikiwakamata.

SEHEMU ZAKE ZA HISIA:
Sehemu zake kuu za hisia ni kwenye miguu na mapacha yake unaweza kurudi kwenye quotes za nyuma ukaona kuna mtu nimeshamuelezea

Rakims
Msaada kidogo

ni kwann yanapotokea magomvi hasa ninamkosea mimi mkewang huw nakutan na badluck , Niliwah pat ajar tukiw kwenye ugomv kuibiw pkpk, juz nimebamiz gar nyuma ?
 
Mapacha na Kaa

Mahusiano haya yanaonyesha kwa yeye mwenye mapenzi ya hamu na shauku huweza kukutimizia wewe mwenye mahitaji ya kimwili zaidi

Furaha yako yako katika tendo huangaza tabia yake yeye ingawa mapenzi yenu huwa matamu mwanzoni lakini huwa hayana maisha marefu tabia yako ya michepuko/ kuchezea mapenzi humtia kovu yeye mwenye hisia kali sana za mapenzi zilizojificha,

Tabia yako na style yako ya kutongoza humfanya awe ni mwenye kujihisi kuwa huwezi kumlindia mapenzi yake nae kuliko kuumia atataka ajiengue taratibu. Wawili nyie hamna maisha marefu ya mahusiano kila mtu atashika njia yake.

Maana yeye ni mwenye kuhitaji mtu mwenye kulinda mapenzi na tegemezi, wakati wewe ni mwenye kupenda kuchangamshana na hupendi kufungwa fungwa na vile vile wewe ni mtu usiye na subira kwake kwa maana utafikia sehemu umuone kama drama queen na vile vile ulimi wako wenye maneno makali ni mchachu sana kwa yeye kuvumilia ambaye yeye ni mwenye Gubu la mara kwa mara.

Nyie mahusiano yenu mnahangaika kupandisha maji mlima.

Rakims
True aisee ila mm sio mchepukaji km yy
 
Back
Top Bottom