Rakims
JF-Expert Member
- Jun 4, 2014
- 5,002
- 4,571
- Thread starter
- #381
Habari mkuu pole kwa changamoto unayopitia maelekezo na mtizamo unaonyesha kuwa wewe unaonyesha ni mtu mwenye asili ya upepo wa juu na pia yeye anaonekana ni mtu mwenye asili ya udongo mwekundu ni mtu ambaye mnashare nae sayari lakini ni mtu ambaye hamuendani sana kwa kuwa ni mtu ambaye upo nae kwenye ndoa nitakupa maelekezo mengi hapa lakini mngekuwa kwenye mahusiano tu ningekwambia achana nae atakuharibia maisha kama ninavyowajibu wengine lakini ndoa ina uzito wake hivyo nitazidisha hekima katika kukujibu na ukizingatia maelezo uliyoyatoa kwenye PM na hapa sawa kwanza kabisa elewa mtizamo unaonyesha kama kuendana wewe na yeye ni kuwa;-Habari Rakims
[emoji419] Kwanza nikupongeze kwa elimu nzuri unayoitoa kwa watu wengi,naam mimi nimekuwa mfaidika kwa kiasi kikubwa; Lakini pia ni kama vile mimi ndio naishikilia hii ndoa kwa kiasi kikubwa,nikimaanisha mwenzangu alishajitoa muda mrefu kuipigania ndoa hii_Je,hapa hatima ya ndoa hii ni vipi? Inawezekana nilioa mtu ambaye sikupaswa kumwoa? Nakutajia details za tarehe zetu|miezi|na miaka tuliyozaliwa ili UNISAIDIE KUNIFUNULIA HATMA na SIRI NYINGINE KATIKA MAHUSIANO HAYA[emoji120]ili kama kuna MAAMUZI MAGUMU YA KUFANYA BASI NIYAFANYE MAPEMA.
Mimi mwanaume jina langu herufi ya kwanza:I
Nimezaliwa tarehe:04/10/84
Mwezi wangu jina lake herufi ya kwanza: J
Kazaliwa tarehe:16/5/86
NB: NATANGULIZA SHUKRANI ZANGU[emoji120][emoji120]
Sent using Jamii Forums mobile app
Mnaendana kwa asilimia 25% tu ambapo tukianzia kwenye upande wa sayari kwa kuwa tu mnashare sayari moja na siku moja mtizamo unakuwa ;-
Nyote wawili mnashare mapenzi katika kupenda mziki na sanaa ndicho kitu mnachofanana, zaidi ya hapo yeye ni mtu wa kupenda kuwa nyumbani yaani kujiweka weka ndani mfano chumbani sio mtu wa kutoka toka na ndio kitu cha kwanza huanza kuwa kero kwako kwa maana wewe ni mtu unapenda kujichanganya na jamii na mambo ya kijamii.
Mwenye kupenda kutumia pesa katika mambo ya starehe na anasa, wakati yeye ni mtu wa kujibana bana na mwenye asili ya ubahili. Unakuwa ni mtu mwenye kukosa subira kwa tabia yake ya kuopenda kukutawala na mfano wa kauli yake ya you have to deal with it no matter what, yeye akisema ndio anataka awe kasema na mjuaji zaidi kwenye mahusiano. Tabia zake za misimamo mikali mfano wa mfia dini akilitaka lake kwa njia lake ni lake ndicho kitu kingine ambacho hakikuvutii.
Ni mtu mwenye wivu kwako kwa kila kitu hata kwa vitu vyako mwenyewe na zaidi mnavutia kwenye tendo la ndoa sasa pale inapofikia kukinaiana ndio balaa huanza kwa maana kati yenu hakuna mapenzi zaidi ya tendo la ndoa ndio kitu pekee kinachowaonyesha mnamapenzi ziada kama kuzungumza vizuri kuelewana kupenda zaidi ya tendo hakuna. Kama unahitaji sex partiner sawa zaidi ya hapo hamna maisha.
nikiamua kuwaweka kwenye asilimia inakuwa hivi;
TENDO LA NDOA - 30UAMINIFU - 20
MAELEWANO - 5
HISIA -25
THAMANI - 40
USHIRIKIANO - 65
Sasa unapokuwa na ndoa na mtu ambaye yote hayo yanakuwa hayapo zaidi ya thamani tu ambayo unaweza kuipata kwa mtu yoyote na ushirikiano ambao unaweza kuupata hata kwa mtu usiyemjua yoyote tu hizo sifa 2 hazibebi ndoa. ndoa kitu cha kwanza kabisa kinachoibeba ni maelewano ambapo hapo hakuna.
Look somewhere else utapasuka roho hapo.
Rakims