Nitajie tarehe yako na ya mwenza wako nikwambie mpo vipi na hatima yenu, siri yake n.k

Nitajie tarehe yako na ya mwenza wako nikwambie mpo vipi na hatima yenu, siri yake n.k

Habari Rakims
[emoji419] Kwanza nikupongeze kwa elimu nzuri unayoitoa kwa watu wengi,naam mimi nimekuwa mfaidika kwa kiasi kikubwa; Lakini pia ni kama vile mimi ndio naishikilia hii ndoa kwa kiasi kikubwa,nikimaanisha mwenzangu alishajitoa muda mrefu kuipigania ndoa hii_Je,hapa hatima ya ndoa hii ni vipi? Inawezekana nilioa mtu ambaye sikupaswa kumwoa? Nakutajia details za tarehe zetu|miezi|na miaka tuliyozaliwa ili UNISAIDIE KUNIFUNULIA HATMA na SIRI NYINGINE KATIKA MAHUSIANO HAYA[emoji120]ili kama kuna MAAMUZI MAGUMU YA KUFANYA BASI NIYAFANYE MAPEMA.

Mimi mwanaume jina langu herufi ya kwanza:I
Nimezaliwa tarehe:04/10/84
Mwezi wangu jina lake herufi ya kwanza: J
Kazaliwa tarehe:16/5/86

NB: NATANGULIZA SHUKRANI ZANGU[emoji120][emoji120]

Sent using Jamii Forums mobile app
Habari mkuu pole kwa changamoto unayopitia maelekezo na mtizamo unaonyesha kuwa wewe unaonyesha ni mtu mwenye asili ya upepo wa juu na pia yeye anaonekana ni mtu mwenye asili ya udongo mwekundu ni mtu ambaye mnashare nae sayari lakini ni mtu ambaye hamuendani sana kwa kuwa ni mtu ambaye upo nae kwenye ndoa nitakupa maelekezo mengi hapa lakini mngekuwa kwenye mahusiano tu ningekwambia achana nae atakuharibia maisha kama ninavyowajibu wengine lakini ndoa ina uzito wake hivyo nitazidisha hekima katika kukujibu na ukizingatia maelezo uliyoyatoa kwenye PM na hapa sawa kwanza kabisa elewa mtizamo unaonyesha kama kuendana wewe na yeye ni kuwa;-
Mnaendana kwa asilimia 25% tu ambapo tukianzia kwenye upande wa sayari kwa kuwa tu mnashare sayari moja na siku moja mtizamo unakuwa ;-
Nyote wawili mnashare mapenzi katika kupenda mziki na sanaa ndicho kitu mnachofanana, zaidi ya hapo yeye ni mtu wa kupenda kuwa nyumbani yaani kujiweka weka ndani mfano chumbani sio mtu wa kutoka toka na ndio kitu cha kwanza huanza kuwa kero kwako kwa maana wewe ni mtu unapenda kujichanganya na jamii na mambo ya kijamii.
Mwenye kupenda kutumia pesa katika mambo ya starehe na anasa, wakati yeye ni mtu wa kujibana bana na mwenye asili ya ubahili. Unakuwa ni mtu mwenye kukosa subira kwa tabia yake ya kuopenda kukutawala na mfano wa kauli yake ya you have to deal with it no matter what, yeye akisema ndio anataka awe kasema na mjuaji zaidi kwenye mahusiano. Tabia zake za misimamo mikali mfano wa mfia dini akilitaka lake kwa njia lake ni lake ndicho kitu kingine ambacho hakikuvutii.
Ni mtu mwenye wivu kwako kwa kila kitu hata kwa vitu vyako mwenyewe na zaidi mnavutia kwenye tendo la ndoa sasa pale inapofikia kukinaiana ndio balaa huanza kwa maana kati yenu hakuna mapenzi zaidi ya tendo la ndoa ndio kitu pekee kinachowaonyesha mnamapenzi ziada kama kuzungumza vizuri kuelewana kupenda zaidi ya tendo hakuna. Kama unahitaji sex partiner sawa zaidi ya hapo hamna maisha.

nikiamua kuwaweka kwenye asilimia inakuwa hivi;​

TENDO LA NDOA - 30
UAMINIFU - 20
MAELEWANO - 5
HISIA -25
THAMANI - 40
USHIRIKIANO - 65

Sasa unapokuwa na ndoa na mtu ambaye yote hayo yanakuwa hayapo zaidi ya thamani tu ambayo unaweza kuipata kwa mtu yoyote na ushirikiano ambao unaweza kuupata hata kwa mtu usiyemjua yoyote tu hizo sifa 2 hazibebi ndoa. ndoa kitu cha kwanza kabisa kinachoibeba ni maelewano ambapo hapo hakuna.
Look somewhere else utapasuka roho hapo.

Rakims
 
mkuu

mkuu Rakims umeniruka post namba 386 ujanichambulia details mimi mwanaume sijaoa
mimi me:tareh 10/1 herufi J
mpenz ke:tareh 29/7 heruf A
uhusiano ni wapenzi
nahitaji kumuoa je imekaaje na vp hisia zake kwangu na yote kumuhusu
Nimetembea hadi post mia 400 hakuna hata mtu aliyetuma ya soda.
🙂
Kwa mtizamo mnaonekana wewe ni moto wa mkaa na yeye ni mchanga wa pwani hivyo kwa mtizamo huu tu kuendana kwenu ni mtihani na itafikia sehemu kila mmoja ataangalia pengine kwa maana kinachowabeba ni maongezi tu yaani mnaongea vizuri lakini kwa kuendana ni asilimia 20 tu.
Hivyo wewe mapenzi yako yanaonekana ni ya hali ya juu yaani ni mtu mwenye kutapa mapenzi ya gharama na kujitanua ambapo yeye utakuta ni mtu wa kujibana bana na tahadhari na atakuwa anakunyima uhuru mwingine. unakuwa wewe ni mtu huru lakini yeye anataka kujibana na kukuambukiza kujibana na kujinyima kitu ambacho kwa asili zote za moto huwa zinapingana nacho.
Nyote wawili mnakuwa na mvuto kingono lakini mkiwa na tofauti za kimsingi.
Wewe unakuta ni mtu mwenye kusambasa upendo lakini yeye anakuwa hataki na pia hata katika tendo unaweza kukuta unajinsi unavyotaka na yeye hataki itafikia sehemu utaanza kumfikiria ni mchoyo wa mapenzi labda ukifanya kitu atabadirika lakini usijidanganye. Yeye ni bahiri wa mapenzi kuyatoa na kugawa kwako vile unavyotaka.
Asili yako kwenye mapenzi ni mtu wa kutaka kutukuzwa na kusifiwa kwa huyu ni mtihani kwako na hakuna kati yenu atakae kuja kukubali kuwa chini labda tu ni maigizo ya awali kisha baadae atageuka tu.
Mahusiano yenu mtatia nanga kabla hata ya meli kuanza safari.

SEHEMU ZAKE ZA HISIA;

Hisia zake zipo miguuni pamoja na hisia zake za kimapenzi na wewe hisia zako zipo moyoni na kwenye kifua chako sasa hapa utaumia tu.
 
mkuu Rakims naomba usiniruke please Mimi ni Mwanaume sijaoa
mimi me: heruf J tarh 10/january
mpenz ke:heruf A tarh 29/july.
mahusiano yetu ni wapenzi na pia vp atanifaa kumuoa na vp hisia zake kwangu
Nimekujibu hapa

Kwa mtizamo mnaonekana wewe ni moto wa mkaa na yeye ni mchanga wa pwani hivyo kwa mtizamo huu tu kuendana kwenu ni mtihani na itafikia sehemu kila mmoja ataangalia pengine kwa maana kinachowabeba ni maongezi tu yaani mnaongea vizuri lakini kwa kuendana ni asilimia 20 tu.
Hivyo wewe mapenzi yako yanaonekana ni ya hali ya juu yaani ni mtu mwenye kutapa mapenzi ya gharama na kujitanua ambapo yeye utakuta ni mtu wa kujibana bana na tahadhari na atakuwa anakunyima uhuru mwingine. unakuwa wewe ni mtu huru lakini yeye anataka kujibana na kukuambukiza kujibana na kujinyima kitu ambacho kwa asili zote za moto huwa zinapingana nacho.
Nyote wawili mnakuwa na mvuto kingono lakini mkiwa na tofauti za kimsingi.
Wewe unakuta ni mtu mwenye kusambasa upendo lakini yeye anakuwa hataki na pia hata katika tendo unaweza kukuta unajinsi unavyotaka na yeye hataki itafikia sehemu utaanza kumfikiria ni mchoyo wa mapenzi labda ukifanya kitu atabadirika lakini usijidanganye. Yeye ni bahiri wa mapenzi kuyatoa na kugawa kwako vile unavyotaka.
Asili yako kwenye mapenzi ni mtu wa kutaka kutukuzwa na kusifiwa kwa huyu ni mtihani kwako na hakuna kati yenu atakae kuja kukubali kuwa chini labda tu ni maigizo ya awali kisha baadae atageuka tu.
Mahusiano yenu mtatia nanga kabla hata ya meli kuanza safari.

SEHEMU ZAKE ZA HISIA;

Hisia zake zipo miguuni pamoja na hisia zake za kimapenzi na wewe hisia zako zipo moyoni na kwenye kifua chako sasa hapa utaumia tu.
 
Mwanaume nimezaliwa 17-05 jina I
Mwanamke amezaliwa 21-05 jina H
Tupo kwenye mahusiano tuu wapenzi.
Mkuu usiniruke tena aisee.

Mim mwanaume Rakims
 
Mahusiano bado ni uchumba
Mimi ME, 27/03, G
Yeye KE, 19/01, C

Naomba msaada wako Mkuu...

Sent from my Nokia 5.1 using JamiiForums mobile app
Unaonekana ni mwenye asili ya moto wa jaha na yeye ni mchanga wa bahari kwa mtizamo huo hamuendani na mtaishia njia unaonekna ni mtu mwenye vionjo vya uvumbuzi na mwenye nguvu ya kutambua jambo au kuhisi kitu kinachoendelea na ikawa kweli kuhusu yeye hayo ni majaribio yanaweza yasifurahishe yeye ambaye ni conservative.
Wewe ni mwenye kufanya vitu kupindukia na usiye na subira wakati yeye ni mtaratibu na mwenye kupenda usalama wa mapenzi.
Kama ni mtu una malengo ya kuwa nae kwa muda mfupi sawa lakini kwenye ndoa itageuka ndoana ndio utasikia watu tunakwambia mmekaa kwenye uhawara miaka 5 ndoa miezi mitatu imewashinda.
Hakuna maelezo mengi kwenye couple yenu zaidi ni heri uangalie pengine kwa maana nie ni mataifa mawili ambayo hayaingiliani

Rakims
 
Mwanaume nimezaliwa 17-05 jina I
Mwanamke amezaliwa 21-05 jina H
Tupo kwenye mahusiano tuu wapenzi.
Mkuu usiniruke tena aisee.

Mim mwanaume Rakims
Wewe ni mwenye asili ya upepo na yeye ni mchanga hamuendani hata kidogo mtaachana mkuu,
Ingawa unaonyesha mwanzoni utaweza kwenda nae vizuri lakini yeye mkizidi kusogea utaanza kuona kama anakuhisi huna msimamo nae hiyo ni kutokana na yeye kutizama zaidi maisha yenye msimamo na ndoa kwake ni jambo la msingi sana na kuu katika maisha yake sasa ya wewe ambaye ni mwepesi kusimama katika serious relationship itakushinda kwa maana ni mtu wa kupenda mambo mapya katika maisha yako ya kila siku yeye ni mtu wa kutaka ndoa na wewe unaonekana ni mtu wa kutaka mahusiano wewe ni mtu unaweza kupata upendo kidogo kwake na pia yeye ni mtu hupenda mtu anaeweza kumdhibiti jinsi anavyotaka sasa kwa wewe mwenye kupenda vitu vya nje kiasi kikubwa hamtaendana na ataanza kukuomba muachane the moment kahisi usaliti.
 
Mkuu nisaidie kuangalia haya mahusiano make inaonekana bila Mimi hayapo

Mwanamke jina S
20/ November

Mwanaume jina J

20/ October
 
Mkuu Rakims hii hukuiona?
Sikuiona mkuu,

Mimi ME 02/9 (J)
Mwenzangu KE 15/12 (J)

Mahusiano

Hamuendani mkuu japo ni watu mahusiano yenu yamejaa raha utani na maelewano ya hapo hapo kisha mkipeana nafasi imeisha hiyo wewe ni msaliti na yeye ni msaliti mzuri tu no matter how hidden you both will be.

Jambo la kwanza kuu sex kwenu litakuja kuwa tatizo kubwa
wewe ni mtu makini katika mipangilio ya maisha yako na yeye ni mtu tunakuita ponda mali yaani ni aina ya watu wenye matumizi ya fujo kwenye pesa katika kununua vitu ni mtu unataka kujenga na kuweka sawa maisha yako ya baadae haijarishi ni maskini au tajiri lakini yeye utaona ni mtu wa kutokujali hilo ni wa leo ya leo na hata ukimletea habari za kuwekeza for future atakupigia hesabu za hali ya juu na mwenye kukatisha tamaa.
Wote nyie ni wenye akili nzuri lakini katika mitizamo miwili tofauti yeye ni mwenye kujitanua na mwenye maisha ya fujo na wewe ni mwenye kupendelea urahisi wa mambo na mipangilio na kutokujitesa.
Yeye kuna muda anakudhania wewe ni mjinga huelewi vitu au hujajua mambo hivyo hamna maisha marefu ya kulala shuka moja.
 
Back
Top Bottom