Niulize chochote kuhusu injini za magari madogo na pickup zinazotumia Petroli

Niulize chochote kuhusu injini za magari madogo na pickup zinazotumia Petroli

Mkuu nadhani ungebenchmark in terms of milage ikaeleweka vizuri engine iwe imetembea kuanzia km ngapi ndo haswa tatizo huwa maarufu kuliko kiumri. kwasababu kuna Lililotembea km elfu 10 kwa miaka nane na lililotembea km laki na 20 kwa miaka nane tangu litoke kiwandani. Kwa scenario ya umri sidhani kama inaapply vizuri hapa.

Ni sawa kuwa milage ni muhimu kuhusu ubora wa injini; lakini catalytic converter ndani yake mna madawa (catalyst) ambayo yana life span; baada ya muda yana-expire. Miaka minane nimechukulia umri wa chini, nyingine zinadumu mpaka miaka 15 kabla hayachoka
 
Mkuu na gari dogo la 1.5L, kwa kawaida likiwa idle mshale wa rpm unakua chini kidogo ya moja.
Leo nikiwa kwenye nimesimama kwenye foleni limenizimikia.
Nikaliwasha likawak na kuweza kuondoka bila shida yoyote.
Gari halikua lime overheat, sikua nimewasha AC, tank lilikua chini kidogo tu ya nusu.
Level ya coolant, oil zote zipo sahihi na sehemu liliponizimikia ni tambarare.
Tatizo linaweza kuwa nini? Maana kitu pekee nilichobadili hivi recently ni redio na nimenotice saa ya kwenye redio ilireset baada ya kutokea hivyo.
Kuna sababu kadhaa zinazoweza kusababisha hali hiyo; nitakujibu kwa kina nikirudi nyumbani.
 
Asante saaana kwa nafas hiyo,,mimi naomba unishauri nitumie oil gan ya engine na gearbox ambapo gar ni toyota premio yenye cc 1490 ya mwaka 2005 na mpaka sasa imetembea jumla ya km 71,179 na hiyo oil nibadili kila baada ya km ngap kwan wapo wanaoshaur km 3000 na km5000!!
Pia naomba unijuze ipi oil nzur kati ya Total na Castrol ambapo mm ni mkaazi wa mkoani mbeya ambapo hali ya hewa huku n barid.
Asante Boss

(1) Nafikiri nilishakujibu katika thread nyingine. Engine oil kwa nchi za joto tumia full Synthetic 5W-30 au 10W-30 ingawa. Nakushauri zaidi utumia 10W-30. Uchaguzi wa brand gani ya oil, sisi kiufundi hatuoni tofauti yoyote kabisa labda kampuni iandike 10W-30 kumbe siyo oil hiyo, lakini kama TBS inafanya kazi zake sawasawa, zote Castrol, Total, na oil zote zenye namba hizo zitakuwa ni sawa tu. Kuna watu wanakuwa washabiki wa brand fulani lakini kiufundi hakuna tofauti kabisa.

(2) Kuhusu ubadilishaji wa oil, usifuate urefu wa safari au urefu wa muda tangu umeweka oil tu. Ingawa magari mengi ya kijapani wanashauri kila baada km 8,000 au baada ya miezi 6, usiamani sana hizo namba. Fanya mambo mawili, kila wiki uwe unapima ile dipstick, na kuangalia rangi ya oil imebadiliakaje. Kwa vile wewe siyo fundi, swala la rangi ya oil labda halitakusaidia sana, lakini upime dipstick kila wiki na ukiona oil imeshapungua chini ya kiwango, basi mwaga oil yote ya zamani uweke mpya wala usiongezee tu; unapobadilisha oil ubadilishe pia oil filter. Ukifikisha miezi 6 au km 8,000 wakati oil iko level ile ile basi ubadilishe oil hiyo wakati huo. Wakati mwingine muungurumo wa injini unapobadilika basi ujue pia kuwa ni muda wa kubadili oili. Sijui kama maelezo hayo yamesaidia.

(3) Kuhusu mafuta ya Transmission (ATF) pia nilikueleza kuwa tumia mafuta halisi ya kulingana na ilivyoelezwa na mtengenezaji, sijui ilikuwa Type T-IV kama ninakumbuka. Acha gari lipoe, mwaga mafuta yote ya zamani, badilisha transmission oil filter, halafu weka mafuta mapya; usiongezee tu. Kuna magari mengine hayana plug ya kumwagia mafuta ya transmission, kwa hiyo utalazimika uonde transmission fluid sump na utatakiwa uweke na gasket mpya. Uzuri ni kuwa ukibadilisha transmission fluid, unarefusha maisha ya gearbox yako umbali wa km150,000 tena bila matatizo yoyote.
 
Suzuki Swift inawaka taa ya EPS kwenye dashboard halafu usukani unakuwa mgumu, mafundi wangu wameshindwa kutengeneza utansaidiaje kwa hilo mkuu.

Electronic Power Steering (EPS) failure inapotokea maana yake ni kuwa ile motor inayokusaidia kuzungusha steering wakati wa kupiga kona inakuwa haifanyi kazi sawasawa, kwa hiyo hupeleka data kwenye computer ya injini (ECU) ambayo hukata umeme usiende kwenye motor hiyo kabisa, ndiyo maana steering yako inakuwa ngumu sana.

Hii motor hufanya kazi kwa kusoma nguvu inayotakiwa na steering kwenye kupiga kona fulani wakati wewe unazungusa hiyo steering, halafu huamua kiasi cha umeme wa kuepelea kwenye motor hiyo kusudi ibebe mzigo huo badala yako. Sasa basi, wakati mwingine hutokea kwa bahati mbaya tu kwamba computer ilipata spike ya data mbaya lakini hakuna tatizo; ukizima injini na kuondoa waya mmoja wa betri kwa robo saa na kustart gari tena itafanya kazi tu. Ila kama haifanyi kabisa hata ukishazima injini na kuondoa waya mmoja wa betri, basi kwa kisi kikubwa itakuwa ni steering torque sensors zinahitaji kubadilishwa, au kwa kiasi kidogo sana labda ni motor yenyewe imechoka.

Kiwango kidogo zaidi na ambacho ndicho serious sana ni pale ile gearbox inayoendesha steering yako itakuwa ndiyo imekufa. Hayo ndiyo maeneo makubwa matatu ya kuangalia.

Kupata jibu halisi, ipeleke gari yako ikafanyiwe coomputer scanning kujua tatizo halisi linatoka wapi. Kama sehemu zote hizo ni sawa kabisa, basi inawezekana alternator yako ndiyo imechoka haipeleki umeme wa kutosha unaohitajiwa kuendesha motor hiyo.
 
Mwenye uzi yupo lunch....
Me nakushauri tumia Total Quartz 9000 5w 30 au 10W 30 au 5W 40 kwa mqzingira ya Mbeya na umri wa gari siyo mbaya...
Ila zaidi tumia 5W 30... Hii kama umefunga oil filter genuine unaweza kwenda mpaka km 8000.
Castro ni nzuri sema zina soko sana hivyo kuna feki...kuwa makini..

Huyu niliwahi kumjibu katika thread nyingine; in fact swali lake hilo ndilo lilinishawishi nianzishe uzi huu.
 
Mkuu kuna uwezekano wa kupata Manual book ya gari la kijapani iliyoandikwa kwa kiingereza?
Ndiyo zipo. Sisi tunalipia kwa mwaka kuweza kusoma service manual ya gari yoyote online. Niambie model ya gari lako na mwaka wake kama nitaipata nitadownload na kukuwekea hapa
 
Mkuu namiliki paso, na safari zangu ni mwanza dar huwa naenda mara kwa mara na paso yangu na huwa siipumnzishi njiani kwa imani kwamba huwa natembea naangalia gauge ya heat.. Naweza kuwa naiumiza gati
Kwa kawaida hakuna tatizo lolote kwa gari kwenda umbali mrefu bila kusimama iwapo ina maji ya kutosha na oil haijachoka. Ule muda unaosimama kwenda uwani, kula na kuongeza mafuta hutosha sana kupumzisha injini ya gari lako, siyo lazima ipoe.
 
Mkuu Kichuguu, naomba unishauri kuhusu Nissan X trail, Hi ni gari ambayo navutiwa nayo sanaa hasa Nissan X trail Axis. Je, unaweza kunishauri chochote kabla sijanunua hii gari maana napenda sana magari ya SUV.

Ntashukuru kama utanijibu kwa nafasi yako.
 
Mkuu na gari dogo la 1.5L, kwa kawaida likiwa idle mshale wa rpm unakua chini kidogo ya moja.
Leo nikiwa kwenye nimesimama kwenye foleni limenizimikia.
Nikaliwasha likawak na kuweza kuondoka bila shida yoyote.
Gari halikua lime overheat, sikua nimewasha AC, tank lilikua chini kidogo tu ya nusu.

Level ya coolant, oil zote zipo sahihi na sehemu liliponizimikia ni tambarare.
Tatizo linaweza kuwa nini? Maana kitu pekee nilichobadili hivi recently ni redio na nimenotice saa ya kwenye redio ilireset baada ya kutokea hivyo.

Injini kuzimika wakati wa idling kunasababishwa na sababu nyingi sana ndogo ndogo ambazo hazina madhara kabisa kwenye injini yako. Ngoja nitaje ambazo ni za kawaida sana.

(1) Inawezekana air filter yako imeshajaa uchafu; iangalie na ukiweza uibadilishe.
(2) Inawezekan air flow sensor imeshachafuka au imekufa. Air flow sensor ni kiwaya chembamba sana kinachoweza kukatika hasa iwapo air filter ni chafu. Kama imechafuka, kuna mafuta ya kuisafishia, na kama imekufa unaweza kubadilisha na kuweka nyingine. Zinagharimu kati ya dola mbili hadi kumi na tano tu.

(3) Inawezekana injector zako zina uchafu, kwa hiyo hazipitishi mafuta wakati pressure ni ndogo. Kama tatizo ni hili, kuna injector cleaners ambazo unaweza kuongeza kichupa kimoja kwe tanki la mafuta likiwa full tank kukusafishia injector hizo.

(4) Inawezekana throttle position sensors kwa upande wa chini haifanyi kazi, kwa hiyo ukiachia accelerator basi computer inakuwa haipati taarifa za position ya accelerator yako kwa hiyo inashindwa kujua ni kiasi gani cha mafuta kinahitajiwa na hivyo inaamua kukata mafuta kabisa. TPS zinazuwa kati ya dola tatu hadi 15 tu.

(5) Inawezekan fuel pressure regulator imeshachoka kwa hiyo inavujisha mafuta kurudi kwenye tank wakati pressure ni ndogo na kuiacha injini na ukame wa mafuta. Hii ikitokea, gari inaaza kupungukiwa na spidi hata ikiwa katika mwendo wa barabarani wa kawaida, kwa hiyo iwapo ukiwa barabarani hunaoni tatizo lolote basi ni wazi hili siyo tatizo ulilo nalo.

Sababu namba (2) hadi namba (4) zikitokea, ni lazima zitaregister kwenye computer ya gari na utapata checki engine light. Kama inakuonesha check engine light, ipeleke kwenye computer scan ujue ni sensor gani. Kama hakuna check engine light, basi kwa asilimia kubwa ni kwa air filter yako imechoka sana.
 
Thanks kaka
Mwenye uzi yupo lunch....
Me nakushauri tumia Total Quartz 9000 5w 30 au 10W 30 au 5W 40 kwa mqzingira ya Mbeya na umri wa gari siyo mbaya...
Ila zaidi tumia 5W 30... Hii kama umefunga oil filter genuine unaweza kwenda mpaka km 8000.
Castro ni nzuri sema zina soko sana hivyo kuna feki...kuwa makini..
 
ENGINE YA BEAM 2000 (1G Fe) ILIKAPA T.BELT IKAPASUA PISTON NAMBA MOJA. NIMEBADILISHA CYLINDER HEAD NA HIYO PISTON GARI HAIJARUDIA MLIO WA MWANZO SASA NAFIKIRIA KUBADILISHA MSWAKI UNANISHAURI NINI MKUU
 
Naomba kujua hili swala la kuwasha gari asubuhi au likiwa limekaa muda mrefu bila ya kutembea,kuna wanaosema inabidi usubiri kama dkk 2 ndio uondoke na wengine wanasema unaweza tu kuondoa gari,tupe ufafanuzi hapa lipi hasa ni kweli na sababu ni nini...?
 
Naomba kujua hili swala la kuwasha gari asubuhi au likiwa limekaa muda mrefu bila ya kutembea,kuna wanaosema inabidi usubiri kama dkk 2 ndio uondoke na wengine wanasema unaweza tu kuondoa gari,tupe ufafanuzi hapa lipi hasa ni kweli na sababu ni nini...?
Najibu hivi..akija ataongezea...
Magari ya siku hizi yenye mifumo ya umeme mwingi, EFI au VVTi, Automatic transmission, kitaalamu hayana haja ya kusubiri sana endapo umeliwasha asubuhi..

Narejea User manual ya Nissan yangu...inasema ukiwasha gari asubuhi subiri sekunde 10 oil ipande sehemu za juu...kisha weka gia ondoka na injini ikiwa ya baridi sana asubuhi, usiendeshe zaidi ya 80kph kwa km 2 za mwanzo....Hii ni user manual Nissan ndivyo inavyosema....nadhani inaweza ikafanana kwa magari mengi ya kijapani...
 
Najibu hivi..akija ataongezea...
Magari ya siku hizi yenye mifumo ya umeme mwingi, EFI au VVTi, Automatic transmission, kitaalamu hayana haja ya kusubiri sana endapo umeliwasha asubuhi..
Narejea User manual ya Nissan yangu...inasema ukiwasha gari asubuhi subiri sekunde 10 oil ipande sehemu za juu...kisha weka gia ondoka na injini ikiwa ya baridi sana asubuhi, usiendeshe zaidi ya 80kph kwa km 2 za mwanzo....Hii ni user manual Nissan ndivyo inavyosema....nadhani inaweza ikafanana kwa magari mengi ya kijapani...
Huwa nafuata huu utaratibu mara zote kutokana na jinsi nilivyofundishwa,ingawa logic nilikuwa siijui...
 
Ndiyo zipo. Sisi tunalipia kwa mwaka kuweza kusoma service manual ya gari yoyote online. Niambie model ya gari lako na mwaka wake kama nitaipata nitadownload na kukuwekea hapa
Toyot succeed UB-NCP55V-FXPGK mwaka 2002.
 
Back
Top Bottom