Niulize chochote kuhusu injini za magari madogo na pickup zinazotumia Petroli

Niulize chochote kuhusu injini za magari madogo na pickup zinazotumia Petroli

Gari yangu ina tatizo kama hili la oil kupungua,
Haina changamoto yoyote kwenye speed au nguvu.
Tatizo wakati wa kuiwasha asubh kama itakuwa imekaa siku bila kuiwasha inatoa moshi na pop sound.
Inavujisha oil kwenye combustion chamber pole pole sana; inabidi ikaguliwe. Kwa dalili hizo, mshukiwa mkubwa anweza kuwa ni valve seats
 
Wakuu na mafundi wa magari naombeni msaada wenu wa kina, nina gari yangu Premio Old model NZT240 gari ya 2007 engine ya 1NZfe imekutana na tatizo ambalo sielewi, Ina tetemeka na kuzima ikiwa kwenye mwendo, tumeshabadili Plug, fuel pump, Airflow sensor lakini tatizo liko pale pale, Nini kifanyike ili kuweza kutatua tatizo Hilo? gari ipo dodoma na Kama Kuna fundi mzr zaidi kwa dodoma mnisaidie niweze kumfikia na kutatua tatizo Hilo Ahsanteni sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu na mafundi wa magari naombeni msaada wenu wa kina, nina gari yangu Premio Old model NZT240 gari ya 2007 engine ya 1NZfe imekutana na tatizo ambalo sielewi, Ina tetemeka na kuzima ikiwa kwenye mwendo, tumeshabadili Plug, fuel pump, Airflow sensor lakini tatizo liko pale pale, Nini kifanyike ili kuweza kutatua tatizo Hilo? gari ipo dodoma na Kama Kuna fundi mzr zaidi kwa dodoma mnisaidie niweze kumfikia na kutatua tatizo Hilo Ahsanteni sana

Sent using Jamii Forums mobile app
Nadhani hizo old models zinatumia timing belt na hilo linaweza kuwa ndiyo tatizo lako; hizi models za siku hizi zinatumia timing chain. Kagua kama ina timing belt, basi ndiyo inayolalamika inataka kwenda kulala.
 
Nadhani hizo old models zinatumia timing belt na hilo linaweza kuwa ndiyo tatizo lako; hizi models za siku hizi zinatumia timing chain. Kagua kama ina timing belt, basi ndiyo inayolalamika inataka kwenda kulala.
Ahsante sana mkuu ngoja niipeleke kwa fundi waikague nitaleta mrejesho hapa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nadhani hizo old models zinatumia timing belt na hilo linaweza kuwa ndiyo tatizo lako; hizi models za siku hizi zinatumia timing chain. Kagua kama ina timing belt, basi ndiyo inayolalamika inataka kwenda kulala.
Timing belt zipo sawa, machine imesoma code upande wa hewa ila bahati mbaya fundi aliepelekewa gari bado hakuweza kufahamu zaidi atengeneze Nini, gari inaandaliwa utaratibu wa kuja dar pengine tunaweza kutatua hilo tatizo kwa huku

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Timing belt zipo sawa, machine imesoma code upande wa hewa ila bahati mbaya fundi aliepelekewa gari bado hakuweza kufahamu zaidi atengeneze Nini, gari inaandaliwa utaratibu wa kuja dar pengine tunaweza kutatua hilo tatizo kwa huku

Sent using Jamii Forums mobile app

Imesoma code namba gani?

Kama Airflow Sensor ni mpya, Fuel Pump nimMpya, na nina imani Alternator inafanya kazi sawasawa ama sivyo baada ya muda gari lisingekuwa lina start, basi jaribu kuangalia Manifold Absolute Pressure (MAP) Sensor. Mara nyingi MAP sensor inapokufa utakutana na tatizo kama lako pia.
 
Imesoma code namba gani?

Kama Airflow Sensor ni mpya, Fuel Pump nimMpya, na nina imani Alternator inafanya kazi sawasawa ama sivyo baada ya muda gari lisingekuwa lina start, basi jaribu kuangalia Manifold Absolute Pressure (MAP) Sensor. Mara nyingi MAP sensor inapokufa utakutana na tatizo kama lako pia.
Mtaalam naomba contacts zako za whatsapp
 
Imesoma code namba gani?

Kama Airflow Sensor ni mpya, Fuel Pump nimMpya, na nina imani Alternator inafanya kazi sawasawa ama sivyo baada ya muda gari lisingekuwa lina start, basi jaribu kuangalia Manifold Absolute Pressure (MAP) Sensor. Mara nyingi MAP sensor inapokufa utakutana na tatizo kama lako pia.
System turin

Sent using Jamii Forums mobile app
 
IST Ukiwasha AC gari ikiwa imesimama inatetemeka sana ila ikiwa kwenye mwendo au ukiweka handbrake husikii mitetemo...!! je tatizo ni nini??
 
IST Ukiwasha AC gari ikiwa imesimama inatetemeka sana ila ikiwa kwenye mwendo au ukiweka handbrake husikii mitetemo...!! je tatizo ni nini??

Nanukuu “ In most cases, if your car shakes at idle, but runs fine otherwise, you have problems with idle air control. Older cars use an idle air control valve to send air around the throttle when it’s closed. Over time, it can clog or stop moving, so your engine doesn’t get the air it needs. Newer cars with a throttle-by-wire system open the throttle enough to keep the engine running. If the throttle position sensor is bad, the ECU can’t adjust the throttle to keep up with air demand.

If the car shakes when AC is on or shakes more, it’s due to the load the air conditioner compressor puts on the engine. This makes issues with idle air control more noticeable, since the engine needs more air to keep running.”
 
Nikumbushe tena baada ya mwaka mpya kwa vile sasa hivi niko kwenye mithani, na nikimaliza mitahani sitakwenda kwenye karakaraka yetu kwani itakuwa imefungwa kwa ajili ya Krismas hadi tarehe 3 January.
Sawa boss!
 
Usishangae kuhusu utambulisho huu. Mimi sasa ni ASE Certified Service Consultant wa magari madogo yanayotumia petroli hasa ya Ford, GM, na Chrysler.

Nimepata license yangu hivi majuzi tu mwaka huu baada ya kuitafuta kwa muda kidogo through part-time activities kwani hiyo siyo kazi yangu kuu.

Certification hiyo inahitaji siyo tu kufaulu mtihani wake, lakini pia uwe na uzoefu wa kutosha kwenye auto-repair shop.

Nimekamilisha experience hiyo inayotakiwa mwaka huu na kupata license yangu.

Kwa vile injini nyingi za petroli zinafanana katika utendaji, jisikie free kuniuliza swali lolote kuhusu matatizo ya injini ya gari yako model yoyote inayotumia mafuta ya petroli.

Siahidi kuwa majibu yangu yote yatakuwa ni sahihi, lakini sehemu kubwa itakuwa ni sahihi, na hata yale ambayo hayatakuwa sahihi yanaweza kukusadia kujua wapi pa kuanzia.
Peugeot 504 pick up
Kila usubuhi inasumbua kuwaka
Baada ya kusumwa itakuwa vyema siku nzima
 
Habari mkuu
Nataka kubadili ATF kwenye 2NZ, dukani nimekuta galoni za lita nne na naona hapo mtandaoni wanasema zinawekwa 5.6 je, nini cha kufanya au kipi sahihi?
Screenshot_20231219-164026.jpg
 
IST Ukiwasha AC gari ikiwa imesimama inatetemeka sana ila ikiwa kwenye mwendo au ukiweka handbrake husikii mitetemo...!! je tatizo ni nini??
Niliwahi kupata changamoto kama hii hasa nikiwa kwenye foleni na nimewasha AC. Tulikuja kugundua kuwa engine mounts kama mbili zilikuwa zimechoka na kukatika. Baada ya kufunga mpya, tatizo likapotea.
 
Mimi yangu ni Toyota Succeed.
Model code: NCP59G-FWPLK
Vin: NCP590003329
Product date: 2002/10

Nitafutie hiyo manual ya kiingereza. Halafu niambie niandae kiasi gani?
Habari bwana Kichuguu. Uliniahidi baada ya sikukuu za mwisho wa mwaka nikukumbushe juu ya manual ya kiingereza ya gari tajwa hapo juu. Nadhani huu ndo muda mwafaka. Ahsante.
 
Habari bwana Kichuguu. Uliniahidi baada ya sikukuu za mwisho wa mwaka nikukumbushe juu ya manual ya kiingereza ya gari tajwa hapo juu. Nadhani huu ndo muda mwafaka. Ahsante.
Habari bwana Kichuguu. Mimi nakumbushia tu ahadi uloniahidi. Uliniahidi baada ya sikukuu za mwisho wa mwaka nikukumbushe juu ya manual ya kiingereza ya gari tajwa hapo juu. Nadhani huu ndo muda mwafaka. Ahsante.
 
Back
Top Bottom