Niulize chochote kuhusu Subwoofer na Sounds system

kelphin

JF-Expert Member
Joined
Dec 24, 2019
Posts
9,872
Reaction score
16,319
Ikiwa inakusumbua,ikiwa unataka kufahamu chochote kinachokutatiza.

Karibu

Nieleze kidogo kuhusu subwoofer
Je, unataka kununua, basi zingatia haya.

Zipo za aina mbili old model na digital. Siyo majina hapana ,yaani inaweza kua rising,seapiano,codjec,aborder au vyovyote Ila itakua digital au old model.

Hizo digital ni Aina ya subwoofer ambayo inamuundo wakisasa ,mala nyingi utakuta Ina (nob) kivingilisho Cha sauti kimoja tu.

Ila kinafanya multipurpose, ukibonyeza hyo hiyo nob unaweza ongeza sauti ,kuongeza bass, na mid.
kifupi mambo yote ni in one button.

Faida yake ni kuwa, aina ya power supply yake Ni ilitaka ifanane na ya home theater(Ila haijawahi[emoji2][emoji2inakua na umeme mnyoofu kidogo.

Zinakua na music mkubwa na mdundo zaidi ni digital,yaani yakisasa,
lakini pia display yake ni LCD haitumii umeme mwingi.

Je utaijuaje?
Nob ya kuongezea sauti ni moja tu na zaidi utakuta button za menu na input inategemeana). Ukiigeuza nyuma ina kiplastic kidogo kilichozungushwa nati, yaani ikiwa italeta shida fundi huku nyuma hafungui mfuniko wote wa nyuma, hufungua ki plastic tu hapo nyuma ndio kimebeba card zoote na subwoofer.

Hasara zake
  1. Ikitokea imeharibu card yake hauwez kubadilisha ,sababu ndani Ina circuit Kama ya phone mafundi weeengi hawana(hatuna) technology yakuitengeneza kwahyo unaenda dukani unanunua Tena kard na si chini ya 40000.
  2. Ila ukifika unaipachika tu huangaiki.
  3. Inahitaji utulie ili uioperate maana inatumia single nob.
  4. Speaker yake ya bass huwekwa ohms ndogo ili idunde sana kwahiyo usipende kuweka sauti kubwa Sana kwa muda mrefu.

Aina ya pili ndio zile old model
Hizo zinaitwa dunda udundavyo ni nzuri kwenye uzuri wake. Yenyewe ukiingalia utakuta Ina nob yaani vile vyakuongezea sauti zaidi ya kimoja. Yaani cha master volume, bass, tweeter na mic, na ukivizungusha vinafika mwisho.

Yenyewe ndani power supply yake ni ya kawaida, inatumia mtransformer wake na diodes za kawaida. kisha umeme huingia kwenye capacitor ndio unaanza kusambazwa ndani. Yaweza kuwa Seapiano, Codjec Aborder au vyovyote. Ukiigeuza nyuma mfuniko wote unafunguka wa nyuma.

Faida yake
  1. ikizingua unaiweza kuirekebisha kiurahisi tu
  2. Zinavumilia sana
  3. Hata muziki upo pia
  4. Rahisi kuitumia
Hasara zake
  1. Display yake ni VFD kama ni seapiano hapa mbele inakioo,inavyoimba Kuna vitu vinacheza cheza kwenye kioo(hii ni kwa baadhi ya subwoofer)
  2. Muonekano wake ni wakizamani ikilinganishwa na hizi mpya

Soma hi pia [emoji1427]
Ndani ya subwoofer panya hupenda kuishi humo, huzaliana na kuleta hitilafu kwa kukata nyaya na kula speaker.
Waya wa speaker una chumvi chumvi hivyo akiingia hauachi.

Simple way jinsi ya kudhibiti
Pale kwenye tobo kuna ki corn cha duara huwa wanakipachika unaweza kukitoa kwa kufuata mpangilio ufuatao:

  1. Chukua maji ya moto kidogo na kitambaa, kichovye kitambaa kwenye maji kisha kikande kuzunguka mduara kwa dakika tano.
  2. Kisha chukua kisu, tumia ncha yake kuingiza pembezoni mwa mduara bila kuikwajua. Huku ukiinua kidogo kidogo kuzunguka corn nzima,ukisha kitoa kitoboe vitundu vidogo kukizunguka upande wa ndani(sio Huku uliko Kanda kwa maji).
  3. Ukisha kitoa chukua waya mgumu usuke upande wa ndani kuzunguka uwazi wa duara wote mule ulimotoboa, kisuke hakikisha unaacha vyumba vidogovidogo kiasi kwamba kinaweza kupita kidore kidogo tu.
  4. Paka gundi upande wa ndani, huku ulikokua unakanda na maji kisha kibandike tena kama kilivyokuwa.

NB: Hii ni kwazile subwoofer kama pichani hapo juu, ambazo hutolea upepo pembeni kwenye kiduara. Wale zinazotolea mbele chini ni habari nyingine.

***
Kiasi chake mtanielewaView attachment 1560194View attachment 1560195

Some updates,
Je, music system yako haina bluetooth na unataka kuongezea? Easy sana na inawezekana pia, kwa mafundi ninaweza kuwaelekeza.

Lakini pia music system yako ulipenda itoe mp5, yaani picture, video inawezekana pia[emoji3][emoji3].
Hususani wale wenye TV za kizamani yaani unachomeka flash disk yako kwenye subwoofer, unapata mdundo alafu kuna cable itatoka kwenye subwoofer hadi kwenye TV yako.

Stay here.
More good things are here.
Welcome.

View attachment 1921368
View attachment 1921369
 
Nimekupata mkuu ngoja nihakikishe hayo kwanza

Sent from my 502SO using JamiiForums mobile app
 
Kati ya kampuni ya Rising, Sea Piano, A border na VOI ipi nzuri zaidi?
 
Anha ,
Hizo subwoofer zinaitwa digital
Inaweza kua panya aliingia amekata waya
Au power supply imeungua ,au kunakifaa kimeleta hitilafu
Pia huenda card yake inatatizo
NDIO MATATIZO YAKE
Nina subwoofer ya aina hio...iliburst capacitor kipindi Tanesco wanafanya mchezo wa kuzima na kuwasha umeme.
Nilibadili Capacitor ila ita has never been the same, sauti ya aux imepungua kidogo compared na ya Bluetooth. Pia Led display imekata zile namba au maneno zinazodenote functions unapozibonyeza.
 
Kati ya kampuni ya Rising, Sea Piano, A border na VOI ipi nzuri zaidi?

Mkuu hili nmesha lijibu huko juu
By the way hayo ni majina tu
Hata wewe unaweza enda pale zontech china unasema nataka pic million 20 za subwoofer ila ziitwe @Azarel wanakutengenezea
Kwahyo majina hayana nguvu ki hivyo
Ukikutana na subwoofer imeandika lg au Samsung basi jipange sana bei zake

Kwahyo hapo niseme nzuri seapiano kwa wingi wake kua ikitokea imeharibika basi unaweza kutengeneza
Ila aboda pia nzuri japo wanaweka current nying mno ili zipige sana nazo sio mbaya sana
 

Inaweza kua ili iletea shida processor ya channel mkuu
Inaitwa pt2313 ipo nyuma pale
 
Aux na Bluetooth zinafanya kazi vizuri tu

Sent from my 502SO using JamiiForums mobile app

Basi inawezekana ile sehemu ya kuchomeka flash imetanuka
Ndani pale pana terminar4 na zote lazima zikutane na termn za flashi yako
Ikiwa moja wapo ita fel bas ndicho kinachokutokea wew
Sina uhakika kama processor ya hyo sehem itakua imesumbua kwasabab ikiungua ile vyote havitafanya kazi hapo
Kwahyo mtafute fundi akuangalizie hapo
 
Kwanini subwoofer ya gari ina mziki mzuri sana kushinda subwoofer za kichina.

@Extrovert vipi kwenye hyo ndinga yako umetia la watts ngap mkuu[emoji23][emoji23]

By the way zile za kwenye gari zinaingiza had volts40 kwenye circuit yake tofaut na subwoofer
Ndio maana mkiyo zinapishana
Lakin pia kwenye gari kuna vitu kama crossover zenye uwezo mzuri
Ndio maana kule inakua real kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…