Niulize chochote kuhusu Wilaya ya Sikonge Tabora

Niulize chochote kuhusu Wilaya ya Sikonge Tabora

ha ha ha

Iwensato ilikuwa ni kijiji kikubwa mno kabla ya operration vijiji miaka ya 70. Kwa sasa ni mapori matupu - tukiwa wadogo tulikuwa tunakwenda kule kuchuma Mapera, Maembe na matunda mwitu kama nsungwi, ntarali na zambarao nk
Nsungwi matunda haya matam sana.
 
Wilaya ya Sikonge kwa muda mrefu haikuwa na barabara ya kukatisha kuingia na kutoka kwenye mikoa mingine - kifupi Wilaya ilikuwa kama kisiwa hivi. Kwa sasa ndiyo kuna barabara inajengwa toka Tabora mjini kupitia Sikonge hadi Katavi.

Barabara hii sasa ndiyo itahuisha biashara kati ya wilaya ya Sikonge na Katavi hadi Kigoma.

Ardhi ipo ya kumwaga, lakini kilimo chochote kinahitaji Mbolea, Mzunguko wa pesa hakuna - maisha ni magumu mno hasa wa vijana na kina mama.

Chakula kikuu ni Ugali wa Mahindi - Mboga ni Mlenda, Swalu, nsansa, kisanvu ma msusa - Mboga zote hizi zikiungwa kwa tui la karanga!! Uhodari wa wanawake wa Kinyawezi ni ile sifa yao katika mapishi - ni hatari.
Wanasifa gani hasa wanawake wa kinyamwezi ?
 
Kwa mazinge tupo pana Hospital ya Wilaya na watu wanajenga na Barabara kuu ya rami inayotoka Tabora imekuja tokezea hapo imepita nyuma ya Sikonge madukani
Vipi maeneo ya Mwanambuya, nasikia hata Mazinge watu wameanza kujenga. Nasiku nyingi sijafika Sikonge
 
Malazi zipo hotel 2 na guests za kutosha kwa upande wa chakula wanyamwezi chakula chao kikuu ni ugali mzunguko wa umeanza kuwa mzuri baada ya barabara ya kuelekea mkoa wa Katavi kupitika kwa misimu yot
Kwanini wanaume wa sikonge ni mboga mboga yaani laini laini?
Wilaya ya skonge ina wastani wa watu wa ngapi?
 
ha ha ha

Iwensato ilikuwa ni kijiji kikubwa mno kabla ya operration vijiji miaka ya 70. Kwa sasa ni mapori matupu - tukiwa wadogo tulikuwa tunakwenda kule kuchuma Mapera, Maembe na matunda mwitu kama nsungwi, ntarali na zambarao nk
Kipanga na lukula ni vijiji vilivyosifika kwa kuwa na maembe mengi sana,
Bila kusahau matunda ya mfulu.
 
Wanyamwezi pia wamegawanyika katika makabila madogomadogo kwa mfano Wakonongo, wapimbwe nk,
Hii ni wilaya kubwa pengine kubwa kuliko zote Tanzania kwa ukubwa wa takribani 27,873 kilometre za mraba, ni wilaya iliyosahaulika kabisa kimaendeleo tangu miaka ya Uhuru, wananchi wake wengi wao wanaishi katika dimbwi la umaskini mkubwa, Wilaya hii ilikuwa inajulikana kama Wilaya ya Tabora vijijini hadi miaka ya 2000 ndipo ikapewa hadhi ya kuwa wilaya kamili.
Ni kubwa ila ni ndogo sana kwa wilaya ya simanjiro
 
Unajua mamba mpaka ukishiriki ndiyo uatayajua ninachojua akina mama wa kinyamwezi ni wataratibu sana na hasa wale waliokulia kijijini na wanauwezo wa kupika vizuri na hasa kwa kutumia kiongo cha Karanga mambo haya hupelekea muoji akazama na watu wa pembeni wakadai ni limbwata
Kuhusu Limbwata rudi upya mkuu.
 
Back
Top Bottom