Niwaaminishe vipi watu kuwa mimi sijawahi na sivuti Bangi?

Niwaaminishe vipi watu kuwa mimi sijawahi na sivuti Bangi?

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963
Jamani hili jambo linanisikitisha na linaninyima raha hadi sasa.

Ni hivi miaka ya nyuma kidogo wakati nasoma nilianza kufuga Rasta hadi namaliza chuo nipo na Rasta zangu ndefu tu.

Nipo Nimeingia kitaa baada tu ya kutoka chuo nikaamua nipunguze wingi wa zile Rasta, yaani niwe na Rasta tano tu kichwani kwa hiyo ikabidi niunge unge zile Rasta kichwani ili zitoke tano, lengo la kufanya hivyo ni kupunguza wingi wa kuwa na rasta nyingi maana nilikuwa na Msitu haswa wa rasta.

Kwa hiyo nikawa na mikonga mitano ya nywele.

Miaka imepita nikaja kunyoa zile nywele kutokana sababu flani flani hivi. Basi baada ya hapo nakuja kutana na watu tofauti tofauti wa mtaani na wa familia wananipongeza kwa kukata nywele maana wanaambiwa nilikuwa mvutaji hodari wa bangi🤔🤔.

Leo kuna mtu tuliwahi fanya nae kazi enzi hizo nimekutana nae akaniambia hongera Bushmamy naamini sasa hivi huvuti mibangi yako kama zamani, nikamuuliza ushawahi niona navuta hiyo mibangi akasema ameambiwa hivyo ila yeye hajawahi niona.

Japo niliapa pale Kuwa ukweli wa Mungu sijawahi vuta Bangi lakini naona hakuamini na wala sikuhangaika naye maana silali na sili kwake ili nilitaka ajue kuwa watu wanajua kusema uongo.

Hata wazazi wangu hadi leo wanaamini hadi sasa napuliza.

Jamani kweli hiyo kitu. Sijawahi fanya kabisa nivip naweza waaminisha kuwa sijawahi hata shika hiyo kitu na mkono wangu, au niwapotezee?
 
Sasa bangi inahalalishwa na inatajwa kama dawa ..na ishaanza kuwa kama sigara au better kuliko sigara.

Wewe why unaogopa kuonekana unavuta?

Advantage yake watu wakikuhisi unavuta hawakuletei upuuzi ovyo ovyo

Wanajua utawavutia uwakomeshe
 
1.Hakuna haja ya kutumia nguvu mkuu. Mtu akikuambia unavuta mwambie sawa. Huvuti jibu ni sawa. Ksbb hakuna unachopoteza kama una maisha yako

2. Hata hivyo bangi mbona fresh tu kuna shida gani kwenye bangi?. Bangi sawa na bia tu. Vipi ukiambiwa unakunywa bia nyingi,haitajisikia vibaya kama ya bangi si ndio?. Lakini wale vijana unaowaona wamechakaa sababu ya bangi ni ksbb tu wanavuta wakiwa hawana kitu,lazima ikuchakaze,ni sawa na wangekunywa bia nyingi huku hawana hela ya kula watachakaa tu. Wapo wengi tu wenye uwezo wanapiga huo mmea wako,wala huwezi kujua.

3. Ukilichukulia ni fahari sasa ukiambiwa hivyo halitakusumbua. Hii kitu hukijui wanapiga watu wazito ni vile tu hawaweki wazi.
 
Daaah pole Sana....

Hao hawawajui wavuta BANGE....wanaongea hisia...wanaongea YANAYOWAJIA VICHWANI....

Bange haijifichi....iko PEUPEE...

1.Midomo Myeusi tofauti na kipindi Cha nyuma..we unayo?
2.Viganja na vidole vyeusi(kwa Moshi na moto wa vyaukucha)..uko hivyo?!!!
3.Macho mekundu baada ya BLAZE...we uko hivyo?!!!
4."kusizi" Sana na maongezi machache baada ya BLAZE...we uko hivyo?!!!

Rasta ni STYLE tu ya nywele.....

Wala si kila MNYOA KIPARA huwa havuti KIJITI....

Peace
 
Sasa bangi inahalalishwa na inatajwa kama dawa ..na ishaanza kuwa kama sigara au better kuliko sigara..

Wewe why unaogopa kuonekana unavuta?

Advantage yake watu wakikuhisi unavuta
Hawakuletei upuuzi ovyo ovyo
Wanajua utawavutia uwakomeshe
🤣🤣
 
Hebu weka kapicha ukiwa na rasta na sisi tuone kwanini wanakusingizia hivyo
 
Back
Top Bottom