Nje ya mawazo ya Mwanadamu Mungu hayupo, hajawahi kuwepo, na hatakuwepo

Naamini hawa wana tekeleza ahadi ya ibilis yani wanafanya kazi moja kutoa watu katika haki.
Wanajitahidi mnoo yani mtu aamini bingbang dah
Kipimo cha uzwa uzwa ni mtu kuamini "The Bigbang" kuna watu wajinga hapa duniani,ila hawa wakana mungu ndiyo viongozi wao.

Kuna mmoja huku aliongelea kuhusu energy,sasa unamuuliza energy ina maarifa ? Ina sanifu ? Ina malengo ? Ina hekima ? Anakujibu nenda kasome,yaani wao wanaamini ya kuwa kinachoendesha dunia ni energy ukimwambia atueleze hiyo energy inaendesha vipi mambo ? Hajibu mwisho wa siku anakwambia "Mara hujii kuhoji" mara ooh,yaani hawana hoja zaidi ya dhana tu.
 
Wajifanya hawaamini uwepo wa shetani bila kujua wanayo fanya ndo ushetani wenyewe.

Yani wao kina Neton sawa upande mwingine hapana wesha kaririswa
 
Nafikiri mambo ya Mungu yanawezekana kuprove kabisa
Mfano ni kwangu mwenyewe.
Mwaka jana 2020 nilipata kuambiwa na Mungu kuhusiana na huduma ambayo aliniambia ninatakiwa kuifanya lakini nikawa namuuliza maswali. Na Kati ya maswali ambayo nilikuwa namuuliza alinijibu ya kuwa nitatumia vitu Vilivyopo physically katika kuwafundisha watu.

1. Nilimuuliza nitawezaje kumleta mtoto kwenye ili nimfundishe neno lake?
Alinijibu kwa kuniuliza swali ya kuwa mtoto anapenda nini? Nikamjibu, Naye akaniambia ya kuwa katika hicho kitu ambacho mtoto anakipenda Mungu atathibitisha neno lake kupitia hicho kitu.

2. Nikamuuliza ninawezaje kumleta mtu mzima katika kipindi Cha MAFUNDISHO?
Alinijibu kwa kuniuliza swali ya kuwa mtu mzima anapenda nini? Nikamjibu, Naye akaniambia ya kuwa katika hicho kitu ambacho mtu mzima anakipenda Mungu atathibitisha neno lake kupitia hicho kitu.

Kweli nilipoanza kufundisha kumekuwa na maajabu mengi na watu tofauti tofauti ninaowafundisha wameshuhudia wenyewe kwa macho yao.
Kuna wakati hata nilipokuwa nawafundisha watoto katika masomo ya kawaida ambayo si ya neno la Mungu, Mungu alidhihilisha uwepo wake. Mfano zaidi ya utumishi wa Mungu niliopewa Mimi Ni mwalimu wa somo la jeografia. Mfano siku moja nilikuwa nikifundisha kidato Cha kwanza, na nilikuwa naelezea kuhusu mchora ramani ghafla Kuna watoto kadha wakaniambia tumeona Jambo Fulani ulipokuwa unaelezea.

Kwa maneno mengine naweza sema Mungu anajithibitisha mwenyewe kwa kazi zake na maajabu yake ambayo kwa akili za kibinadamu huwezi kuelezea mfano.
1. Kuna watu walikufa na wakafufuliwa katika ulimwengu huu ( je wanasayansi wanaweza wakatuelezea kisayansi ni mechanism gani inatumika kufua wafu) mtu amekufa vipimo vimethibitisha kwa siku tatu lakini mtu akafufuliwa. Rejea kitabu kimoja kinaitwa (raised from the dead reinhard bonnke) pia Kuna ushahidi wa video mbalimbali kuhusu hilo

2. Vipofu waliozaliwa wakiwa vipofu wakaona

3. Wagonjwa waliothibitishwa na vipimo kuwa wagonjwa. Mfano uvimbe, HIV, kansa, kupooza, na mengine mengi yakaponywa bila dawa kwa sekunde chache tu. Hayo yamethibitishwa pia na madaktari baada ya uponyanyi kwa vipimo vya kisayansi.

Ningeweza kuandika mengi lakini si rahisi kuandika yote maana ni mengi
 
Mungu hayupo na shetani hayupo bali ni imagination actors walikuwa invented na binadamu.Nikosoe
 
Mungu hayupo na shetani hayupo bali ni imagination actors walikuwa invented na binadamu.Nikosoe
Unapokanusha jambo unatakiwa uwe ns uthibitisho. Hii ni kanuni ya msingi sana katika mijadala na utafiti. Hapa siwajibiki kukukosoa mpaka pale unakapo jibu maswa au swali hili.

1. Umejuaje kama Shetani hayupo na Mungu hayupo ?

2. Shetani ni nani na Mungu ni nani ?

Ukishajibu maswali haya ndiyo nitakuja kukukosoa.

Shukrani.
 
We mbona mwepes wa kusahau
Hii ni jana leo umesahau kama nlikwambia mim seeker
ukilala unasahau?
Sio nimesahau ila unaji contradict mwenyewe, hapa umedai kua una amini mungu yupo tena umemchambua kwa kumtofautisha na Miungu ya dini zingine, kusema upo katika kumtafiti at the same unasema yupo hiyo ni contradiction otherwise ukiri kua haujui mpaka pale utapo malizia utafiti wako uje na jibu la hitimisho

 
Maswali yako unaweza kujibu yakiangukia kwenye logic ulizo kalil
kazi ya hizo logic ni kukusaidia kuja na mawazo yako halisi sio kumeza
logic zipo kuuona uhalisia sio kumeza terminologies
wewe ni nan?
Muulize mungu wako, au sio mjuzi wa yote?
 
Hili nimeshlifanya zaidi ya mara kumi humu.

Na hakuna aliye weza kuzikosoa hoja zangu na ithibati zangu na hatotokea wala hajawahi kutokea.
Ebu thibitisha, kwani ni mara ngapi mijadala kama hii inajadiliwa humu? Kwanini unashiriki tena wakati ulishawahi kushiriki mada kama hizi mara nyingi?

I can bet hata hilo jibu lako la kusema "Hili nimeshlifanya zaidi ya mara kumi humu" sio mara ya kwanza unalitoa kwenye uzi huu, ulishawahi fanya before sa kwanini umelirudia?

Jikite kwenye mada, huu ni uzi mwingine kama umeingia kwenye mjadala kuna watu wengi wanafatilia ambao hizo nyuzi zingine ambazo unadai ulishawahi kutoa majibu hawajawahi kuzisoma. Na pengine hilo unalodai kua ni jibu ni some sort of rhetorical tu. Ni eidha uweke link ya hilo jibu kwenye huo uzi ambao unadai ulilijibu swali hilo au ukubali kua huwezi

Thibitisha mungu yupo
 
Ni logical fallacy inayo fanya attempt kubadilisha mada ambayo inajadiliwa
Shida ni kuw umesoma angle moja tu ya philosophy ambayo ni logic tena kwa terminology tu.
Philosophy ni pana jarbu kuielewa kwa mapana yake
 
Allah na Mungu wanashare gan huko mbinguni?
 
Huyo Muhamad aliyeoteshwa anatofauti gan na babu wa loliondo?
 
Ebu thibitisha, kwani ni mara ngapi mijadala kama hii inajadiliwa humu? Kwanini unashiriki tena wakati ulishawahi kushiriki mada kama hizi mara nyingi?
Nashiriki katika mijadala ambayo siulizwi swali hilo. Ndiyo maana ulipouliza swali nimekujibu kwamba kazi hiyo nimeshaimaliza zamani.

Kwahiyo rejea katika hiyo mijadala ya nyuma.
I can bet hata hilo jibu lako la kusema "Hili nimeshlifanya zaidi ya mara kumi humu" sio mara ya kwanza unalitoa kwenye uzi huu, ulishawahi fanya before sa kwanini umelirudia?
Maana yake mlango huo nimeshaufunga na hakuna wakupinga nilicho kiandika. Kwahiyo haijalishi idadi za hapo nyuma lakini kwa sasa kazi hiyo nimeshaimaliza ndiyo maana hata katika mjadala huu tunamkosoa mtoa mada kwa uvivu wake wa kufikiri.
Unaposema nijikite kwenye mada wapi nimetoka nje ya mda kijana ?

Nakupa kazi hiyo warejeshe katika nyuzi ambazo tulijadiliana kuhusu ithibati ya uwepo wa Mola. Maana unaweza kukataa pia kama hatujawahi kujadili hili.

Sasa mboma unaleta dhana kijana ? Au umesahau kama hatujawahi kujadiliana kuhusu hili ? Kama ni hivyo unavyo sema,sisi tunasema hivi kilicho andikwa kimeandikwa,rejea hiyo mijadala ya nyuma kisha kosoa nilicho kithibitisha.
Thibitisha mungu yupo
Hii kazi nimeshaifanya zaidi ya mara kumi humu na hakuna aliyeweza kukosoa ithibati wala hakuna aliye weza kuthibitisha ya kuwa Mola hayupo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…