Njia ipi ni njema kidato cha sita au chuo kwa mtoto anayetaka kusomea tiba? Amemaliza kidato cha 4.

Njia ipi ni njema kidato cha sita au chuo kwa mtoto anayetaka kusomea tiba? Amemaliza kidato cha 4.

rakeyescarl

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2007
Posts
481
Reaction score
147
Mtoto wangu alifaulu vizuri sana kidato cha 4 na kwenda shule nzuri sana kidato cha 6 na tukakubaliana kuwa akimaliza kidato cha 6 atakwenda chuo bara lolote anapotaka yeye. Ghafla baada ya muhula wa kwanza akabadirika anasema anataka kwenda kwenye chuo kiko SA. Na amekwishajaza makaratasi na amekubaliwa. Imebidi nivute subira, nimemwambia nitamjibu, ingawa nilikuwa naelekea kumbeba na kwenda kumpeleka shuleni kwake kwa nguvu kwani naona shule yake wana pass kwa 90% au zaidi. Nitashukuru kama nitapata ushauri hapa, natanguliza shukurani.
 
Mwache aende akapate Elimu bora kuliko huku tunakosubirishana miaka dahari kusomea kitu kile kile.
 
Jibu au ushauri wangu una pande mbili za shilingi hivyo utachagua mwenyewe, yaani ni kwamba inategemea na akili ya mtoto mwenyewe, unajua utaratibu wa kidato cha tano na sita wakati mwingine umsaidia mtoto kukomaa kiakili na kumalizia utoto wake. Mwanafunzi wa kidato cha tano na sita bado anakuwa kwenye uangalizi wa karibu wa waalimu kipindi chote ambacho atakuwa shuleni, hivyo ni vigumu kwake kuingia kwenye makundi na mambo ya ajabu, tukumbuke kipindi hicho udadisi wa mtoto uongezeka hivyo akiwa hana uangalizi anaweza kupotea.

Lakini kama unaamini kuwa mwanao amekomaa vilivyo kiakili, akili ninayoiongelea sio ile ya kujibia mitihani na kufaulu bali ile akili ya kujitambua, nasema hivi kwa sababu nimeona watoto wengi wakiharibika pale walipojiunga vyuo moja kwa moja baada ya kumaliza masomo ya kidato cha nne, wengi wao walipofika vyuoni walishindwa kutumia uhuru uliopitiliza ambao waliupata huko, hivyo wengi waliangukia mikononi mwa watu wabaya au kujiingiza kwenye tabia zisizo njema machoni mwa Mungu na wanadamu, hii ni kwa sababu waliruka hatua ya makuzi, kwa miaka ya hivi karibuni tunaona watoto wanamaliza kidato cha nne wakiwa wadogo yaani chini ya miaka kumi na nane(18). kwa mantiki hiyo mtoto huyo akienda chuo moja kwa moja ni hatari kwa ustawi wake.

Mwisho namaliza kwa kusema haina ulazima wa kumrusha mtoto, najua wengine watasema mbona Ughaibuni au Nchi nyingine wanafanya hivyo, jibu ni utamaduni wetu, makuzi na hatua za maendeleo zinatofautiana sana. Pia sio kila kilicho kizuri kwa wenzetu kinaweza kuwa kizuri kwetu.
 
Chuo ni bora zaidi kuliko A level, lakini kwa nini umpeleke huko SA mbali wakati kuna vyuo vizuri vya diploma hapa Tanzania au Kenya?
 
Back
Top Bottom