Njia pekee ya kuzuia CORONA Tanzania Ni kuzuia watu kuingia na kutoka nchini

mwanamabadiliko

JF-Expert Member
Joined
Oct 30, 2010
Posts
938
Reaction score
1,540
Ethiopia waligoma kuzuia safari China, Kuna cases 104 mwafrica 1 amekufa, Congo pia.
Marekani wameshazuia, sisi haya mambo ya urafiki tuacheni, naiomba serikali nipo chini ya miguu yake wazuie safari zote, huu ugonjwa Ni mbaya.

Corona ikija kutuua au kuua ndugu zetu CCM haitapona, nasema haitapona, chukueni hatua tuokoe kizazi chetu.

---
 
Acha ku panick Tutaenda kukanyaga mafuta kawe
 
Ahahahaaaa [emoji3][emoji23][emoji1787]. Intelligencia ingekuwa ni Cdm wangeshazuiliwa. Lakini kwa waChina ni rafiki zetu tangu enzi za Mao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanavyojenga hizi hospital zao za wilaya zinawapa kiburi kuwa wako imara kuzuia corona, urafiki una mipaka, watu wana magonjwa wewe unasema Rafiki wakati huo uwezo wa kuzuia ugonjwa huo huna, better precautions than cure.

Europe kwa sas corona imefika na hospitals zao ni imara kushinda Tanzania, USA pamoja na kuwa imara bado wamezuia walau kwa mwezi mmoja wageni kutoka Eu kuingia nchini kwao sisi tuancheka cheka tu kama kitu cha kufurahia.
 
SueIsmael,
Basi labda wakubwa watashituka ikifika Kenya kwa sasa tuko salama. Au hiikitu haipendi joto.
 
Serikali sikivu ya awamu ya tano haijawasikia bado??
 
Hujanisoma tu mkuu. Mzaha mkubwa wanafanya wenye maamuzi. Hapa nilipo naenda mjini kwa mahesabu sana. Mwezi mzima nimetimba posta mara 1 tu na daladala la Goms linavyojaza jioni na asubui ni hatari.
Kwani vitengo vya intelijensia vinasemaje?? Acha kujitisha tuko salama.
 
Akili ya watu tulio nao TZ wanaweza kufanya kama kimbilio la wageni wakati huko nje kukiwaka moto! Nje nyingi sasa zinazuia safari zisizo za lazima, Kama Italy nchi nzima hakuna safari kati ya mji na mji kuzuia maambukizi zaidi

Watanzania wazidi kupewa elimu kuhusu huu ugonjwa
 
Utaifanya nini CCM, kama korona imeingia? , Kama umekosa la kufanya pale inapo embrace viongozi na watumishi wanao wateka na kuwauwa obviously kwenye Corona hutawafanya chochote!.


 
Basi labda wakubwa watashituka ikifika Kenya kwa sasa tuko salama. Au hiikitu haipendi joto.

Joto linaathiri muda wa kuishi wa kirusi hichi kikiwa nje ya mwili wabinadamu lakini siyo kwa kiasi kikubwa sana. Kibaya zaidi mtu unaweza kuwa navyo lakini asionyeshe dalili na akavisambaza pia.

Kwa kifupi, nimeelewa kuna aina mbili ya hivi virusi. Aina ya kwanza ikikupata unapata dalili za mafua na homa, koo kuuma lakini ukatibu kama mafua mengine ukapona. Aina ya pili ndio mbaya sana ambayo ina develop pneumonia, mapafu yanajaa maji inabidi mtu awekewe vifaa vya kupumua na kutoa maji mpaka apone. Hivyo vifaa mara nyingi vinapatikana hopitali kubwa, hasa vyumba vya ICU. Tanzania tunavyo vya kutosha kuhudumia mlipuko ukitokea?

Maji masafi na sabuni ndio wawe rafiki zetu wa kudumu kwa sasa.

Laiti serikali ingehakikisha stendi zote za vyombo vya usafiri, malango ya kuingilia sokoni, maeneo ya mikusanyiko yote, nk. kuwe na maji na sabuni. Watu walazimishwe kunawa mikono kabla ya kuingia na baada ya kutoka kwenye maeneo haya na vyombo vyote vya usafiri.

Kuna uzi humu unatoa updates za Virusi na maambukizi ya Corona au COVID-19:
Fahamu kinachojiri kuhusiana na kirusi cha Corona (Coronavirus)
 
Nina hakika corona ikiingia nchini CCM watatumia kama fursa ya kuonyesha inavyowajali wananchi kwa kuanzisha vituo vya kuwahifadhi waathirika!
 
Corona ni ugonjwa wa kupita.. Sisiemu itaondolewa madarakani kutokana na matendo yake na KARMA

Jr[emoji769]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…