Njombe: Askari 3 wafariki na wengine 9 kujeruhiwa katika ajali

Njombe: Askari 3 wafariki na wengine 9 kujeruhiwa katika ajali

The Sheriff

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2019
Posts
747
Reaction score
2,112
sharon.jpg

Askari 3 wa Jeshi la Polisi mkoani Njombe wamefariki dunia na wengine 9 kujeruhiwa baada ya gari la polisi kugongana na basi la abiria la Sharon linalofanya safari zake Njombe-Arusha.

Tukio hilo limetokea leo Februari 3, saa 12 asubuhi.
1580730963970.png

Njombe. Polisi watatu wamekufa na wengine tisa kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wamepanda kugongana na basi na kampuni ya Sharon linalofanya safari zake kati ya Njombe na Arusha.

Akizungumza leo Jumatatu Februari 3, 2020 mganga mfawidhi wa Hospitali ya Kibena-Njombe, Dk Anord Mtega Maganga amethibitisha kupokea miili ya askari polisi hao, kwamba wengine tisa ni majeruhi.

Ajali hiyo imetokea leo alfajiri eneo la kituo cha Polisi cha Mkoa wa Njombe.
1580730927129.png
 
Askari watatu wafariki dunia na wengine kujeruhiwa baada ya kupata ajali



Tweet





Askari watatu wa Jeshi la Polisi Mkoani Njombe wamefariki dunia na wengine 9 kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha magari matatu ikiwemo gari la polisi ambalo lilikuwa likipeleka askari Lindoni.

RPC Njombe Hamis Issa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

 
Too sad,inasikitisha sana,Pumzikeni kwa amani wapendwa,maisha ya binadamu siku zote Mungu ndo anayajua.Nawapa pole familia za marehemu,ndugu,jamaa na marafiki na watanzania wote kwa ujumla.
 
Hahahahaah hii Kali! Nilikua hapo kituoni Njombe miezi mitatu iliyopita aieee yule binti pale mapokezi alikua anajibu watu vibaya sana! Nikaishia kucheka tu. Kikaja kiaskari kingine kimeshupaa utadhani komamanga LA kiangazi, kikajifanya kunipiga mkwara nikatabasamu tu nikatoka nje nikamwambia sawa boss.

Asante kwa Taarifa.
Natumaini Raia wenzetu kwenye Basi hawajapata madhara.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom