Njombe: Mfanyabiashara aliyevamiwa na kujeruhiwa afariki dunia

Njombe: Mfanyabiashara aliyevamiwa na kujeruhiwa afariki dunia

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Mfanyabiashara Maarufu mjini Njombe bwana Godfrey Ndambo amevamiwa na kujeruhiwa vibaya na watu Wasiojulikana usiku wakati akirenea nyumbani kwake ambapo baadae alifariki kutokana na majeraha hayo,Polisi wamethibitisha.

Baada ya kuvamiwa walimpora pesa kiasai Cha Milioni 47 na kutokea kusikojulikana.Polisi wanaendelea na uchungywa.msako.
---
Mfanyabiashara maarufu katika mji wa Njombe, Godfrey Ndambo (45) aliyevamiwa na majambazi maeneo ya nyumbani kwake wakati akitokea kwenye biasharab zake na kupigwa na kitu kizito kichwani kilichosababisha majeraha, amefariki dunia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Mahamoud Banga akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Julai 22, 2024 amesema tukio hilo lilitokea Julai 20, 2024, saa 2:30 usiku katika eneo la Uzunguni, Kata ya Ramadhani, Halmashauri ya mji wa Njombe.

Banga amesema wahusika wa tukio hilo ambao idadi yao haijafahamika, walimpiga mfanyabiashara huyo na kutoweka na fedha zinazokadiriwa kuwa ni Sh47 milioni.

"Baada ya kujeruhiwa alitibiwa katika Hospitali ya Kibena na baadaye alihamishiwa mkoani Mbeya wakati matibabu yakiendelea akafariki dunia," amesema Banga.

Amesema jeshi hilo linaendelea kufanya uchunguzi wa kina na baadaye watatoa taarifa ya watu watakaoshikiliwa kuhusika na tukio hilo.

Kamanda huyo amewataka wafanyabiashara mkoani Njombe kufunga kamera maeneo wanayoishi na ziwe wazi muda wote, kwani linapotokea tukio ni rahisi kwa polisi kuanza kufanya uchunguzi kupitia kamera hizo.

My Take
Ni very risk kutembea na pesa nyingi kiasi hicho, unakwepa TRA huku unahatarisha maisha yako.

R.I.P mpambanaji Ndambo sijui kama ndio yule wa Ndambo Construction au ni ukoo tuu.
 
Mfanyabiashara Maarufu mjini Njombe bwana Godfrey Ndambo amevamiwa na kujeruhiwa vibaya na watu Wasiojulikana usiku wakati akirenea nyumbani kwake ambapo baadae alifariki kutokana na majeraha hayo,Polisi wamethibitisha.

Baada ya kuvamiwa walimpora pesa kiasai Cha Milioni 47 na kutokea kusikojulikana.Polisi wanaendelea na uchungywa.msako.

View: https://www.instagram.com/p/C9uimIstI2D/?igsh=MTcyb3F5d3hyancydQ==

My Take
Ni very risk kutembea na pesa nyingi kiasia hicho,unakwepa TRA huku unahatarisha maisha Yako.

R.I.P mpambanaji Ndambo sijui kama ndio yule wa Ndambo Construction au ni ukoo tuu.

Inside job. Halafu waliomvamia utakuta wako zaidi ya 10 na waliochora. Kwa iyo watagawana million mbili mbili. Baada ya kumdhulumu nafsi.
 
Pesa bana unatafuta kwa shiiida
kumbe ndo kifo chako!!

Unajibana wee unanunua gari linabinuka linakuua

Unajibaana wee majambazi yanakuua

Unajibana wee ukizipata unaanza kula freshi sasa kumbe unatengeneza presha na sukari unakufa😂😂

Unajibaana wee ukiomba Mungu uzipate, ukizipata unajisahau na kusema hakuna mungu, unakufa 😂

Pesa hazieleweki toka enzi za kaka Yuda
 
Inside job. Halafu waliomvamia utakuta wako zaidi ya 10 na waliochora. Kwa iyo watagawana million mbili mbili. Baada ya kumdhulumu nafsi.
Mkaldayo kuna mikoa ambayo kuuwawa ni rahisi sana yani watu ni kama wana roho za kishetani. Mikoa kama Geita hivi huwezi pita mwezi hujasikia mtu kachinjwa
 
Back
Top Bottom