Njombe: Viongozi wa CHADEMA pamoja na dalali wa mbao wakamatwa kwa kuhusishwa na mauaji ya Kada wa CCM Emmanuel Mlelwa

Njombe: Viongozi wa CHADEMA pamoja na dalali wa mbao wakamatwa kwa kuhusishwa na mauaji ya Kada wa CCM Emmanuel Mlelwa

Kwa Lissu walisema kuwa wanamsubiri aje atoe ushahidi. Huu wa Njombe wameupata kwa maiti au?
 
Hakuna watu ninaowachukia duniani Kama Wana ccm
 
CHADEMA ikichukua nchi oktoba 28 italifuta jeshi la polisi , huu ujinga wa kuwanunua wagombea udiwani ulipangwa na kwamba wakikataa watapewa kesi yoyote , na hii imevuja tangu wiki 2 zilizopita eti leo ndio inatekelezwa ! Poor Polisi
Mkuu inaonekana unajua vizuri undani wa mauaji haya ya kutisha!! , enheee tueleze ndiyo CHADEMA mkaamua kumuua huyo kijana? Halafu TUNDU anaimba 'haki haki' aibu kubwa!! Roho ya marehemu haitamwacha salama.
 
Hii spidi ndio inatakiwa katika kufanya uchunguzi wa mauaji ambayo yanahusishwa na mambo ya kisiasa. Laiti kama yale mauaji ya Geita kwa mfuasi wa Chama kinzani yangechunguzwa kwa spidi hii, wananchi wangeona haki imetendeka. Yaelekea sasa haki, kama yalivyo maendeleo, ni kwa baadhi tu ya watu katika nchi hii.
 
Polisi wataalamu wa kubambikia watu kesi! Mtu aue, halafu abaki na mkanda, ili iweje? Mola atawahukumu na kuwapa stahiki yenu!
 
Option iliyopo sasa hivi ni kuuawa makada kesi kupelekewa wagombea ili kuongeza wanaopita bila kupingwa
 
Mpaka raha yani so smooth...

Polisi wala hawajatumia nguvu kubwa, wamefuatilia mawasiliano ya simu then wakawaokota mmoja baada ya mwingine chap.

Mpaka na mkanda wa marehemu kwenye gari yani kuonyesha jinsi wauaji walivyo malofa.

Kumbe yule aliyekuwa anamtishia ben saanane kwenye sms pia angeweza kupatikans kwa urahisi hivi?

Na ile gari aliyoitajaga lissu kuwa inamfuatilia ingeweza kupelekea watuhumiwa kujulikana ndani ya siku kadhaa?

Labda mikoa inapishana uwezo wa kiuchunguzi. Hongereni Njombe mko fit.
Hapo ndipo usanii wa polisi wetu unapojidhihirisha wazi wazi. Usikute mkanda huo uliwekwa tu kama wanavyobambikiziaga watu wengine madawa ya kulevya. Polisi wetu na akina Diamond et al kazini.
 
Mkanda wa marehemu kwenye gari ya mgombea udiwani wa Chadema!! Ebu Polisi kuweni serious basi msilete isidingo kama ya watekaji wa Mo, kumbukeni Rais aliwaambia watanzania sio wajinga.
Kilichotafutwa ni ushahidi...mkanda ukachomekewa duu
 
Vifo vimekuwepo muda mrefu na waliokufa na kupotea ni wengi but polisi mnaposema mkanda kwenye gari hakika mnaanza kuyumba kwa sehemu semeni vitu ambavyo ni critical jamii isione mnaleta siasa maana hao pia ni wagombea wanaweza kuzuliwa jambo la uongo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona hizi mbinu ni za zamani sana?
Tanzania has a long journey to go kama ni hivi!.
Mbona watu wanasahau kwamba kuna Mungu ambaye kila mtu atasimama mbele zake baada ya kufa ambako ni mara moja tu?

Tutumai elevator gani ili akili za watu wenye dhamana za uongozi wapande kiwango?

Ni nani role model wa fikra duni namna hii?

Ohh My Country Tanzania!. I m Crying for you my Mama land!. God, have mercy on us in Jesus Name!. We need you God. Is only you who can rescue my Country!. We need you Heavenly father.

Mungu naomba Umtume malaika Raguel kwenye nchi ya Tanzania aje kusimama katika haki na kweli juu ya shauri hili. Katika Jina la Yesu Kristo aliye hai nimeomba . Watu wote tuseme Amen.
Mbinu mpya zikoje hebu tufahamishe, lazima mchezee kichapo cha kisheria huu ujinga wenue wa kujifanya mko juu ya sheria. Kisanga kikitokea unavuna mwenyewe, tunawaambia acheni ushabiki wa kijinga wa kujifanya mko juu ya sheria. Leo boss wenu lISSU anafundishwa namna ya kuheshimu sheria za nchi, akitoka huko atakuwa amepata digree ya uaminifu. Jinga kabisa
 
Back
Top Bottom