Njoo tusimualiane Mambo ya kutisha/kuogopesha uliyowahi kushuhudia hapa Duniani

Jitahidi. Kabla kulala umtaje mwenyezimguu kwa imani yako. Na uachane usitumie vilevi punde unaenda kulala
 
Kuna mwaka 2010 hivi ujana wetu tulikuwa tunataka kuona wachawi usiku kuna Mzee mmoja jirani yetu akatuambia mna moyo pia mna Siri tukamjibu tuna moyo na tuna Siri akatuambia mkitangaza mtakayoyaona mtakufa sie tukajibu atuwezi basi baada ya siku mbili akatuita njooni tupige story ili muone wachawi tukaenda kama mida ya saa kumi tukaoga dawa dawa nyingine tukanawa usoni tukakaanae barazani akatuambia subirin ilipofika kama saa Saba usiku hivi tukasikia jogoo wanawiki ss Mzee akasema ss hiyo ndio muito wao mara tukaona kundi kubwa la watu sio wengi kivile halafu kuna wengine tunawajuwa wangeni wafanyabiashara wanatuuzia vitafunwa wengine wafanyakazi tunawajua vizuri halafu kuna wazee watatu wakaja Hadi karibu yetu wakamwambia unataka tuwauwe hawa vijana akawaambia musiwauwe basi Yule Mzee akatuambia msitangaze Kwa mtu yyte kitendo cha kutangaza mnaweza mkafa bure Kwan wachawi hawependi wajupikane tangu siku hiyo kutaka kuona vitu visivyoonekana mwanza na mwisho
 
Ungekubali kutoka nje ingekuwaje?
 
walikuwa uchi?
 
Zamani mtu akifariki nayemfahamu ama ndugu bc ujue siku hio hakulaliki
 
Nikiwahi kuhadithiwa na mzee wangu aliyekua anafanya kazi katika shule moja mkoani Tabora kwamba kuna mwanafunzi alipewa adhabu achimbe shimo lenye kimo kama chake na akimaliza aripoti kwa mwalimu aliyempa adhabu.

Shimo lilivyokamilika mwanafunzi hakuonekana tena shuleni tokea siku hiyo na lile shimo iliamriwa lifukiwe. Baada ya miezi kaza pakaota mti wa mwembe ukawa unazaa maembe mazuri sana lakini kila yakianguaka kwa kuiva au kutunguliwa ndani huwa linakuwa na damu.
 
Duh kwahiyo watu walikuwa wanakula hayo maembe?
 
imepungua sasa hivi
Ulishafanyia kazi ushauri baadhi ya wadau waliokupa humu Kama vile wakuwaona viongozi wa dini yako na kupata ushauri toka kwao? Au kuipractice nguvu uliyokuwa nayo kwaajili ya manufaa yako?
 
Ulishafanyia kazi ushauri baadhi ya wadau waliokupa humu Kama vile wakuwaona viongozi wa dini yako na kupata ushauri toka kwao? Au kuipractice nguvu uliyokuwa nayo kwaajili ya manufaa yako?
Hapana na kusahau nishasahau labda nisome upya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…