Njoo tusimualiane Mambo ya kutisha/kuogopesha uliyowahi kushuhudia hapa Duniani

Njoo tusimualiane Mambo ya kutisha/kuogopesha uliyowahi kushuhudia hapa Duniani

Ilikuwa mwaka 2009,Kuna siku nimelala nikawa naota kuwa nimepanda daladala kituo cha mwenge naelekea posta basi nikawa nimekaa siti ya nyuma ya Costa. Basi kufika kituo cha Victoria akapanda mdada mmoja akaja kukaaa karibu yangu siti ya nyuma,tukaendelea na Safari kufika kituo cha mbuyuni yule dada wa ndotoni akaniachia kikaratasi kina namba za simu akashukia kituo cha mbuyuni,baada ya mda nikastuka kutoka ndotoni kucheki saa ya simu mda huo ni saa tisa za usiku. Basi nimestuka kila kitu kwenye ndoto nilikuwa nakumbuka mpka namba za siku,kesho yake nawahadithia ndugu zangu nilichoota ndotoni na mpka namba za siku zilizokuwa kwenye karatasi nazikumbuka,wakaniambia tujaribu kuzipiga. Baada ya kupiga anapokea msichana ana lafudhi ya kiarabu anaitwa Nasrat na anaishi sinza,nilichofanya ni kuvunja laini na kutafuta line nyingine mpka leo sielew ile ndoto na coincidence zake
Fanya mpango wa namba hizo mzee

Mngoni%
 
Acha nami nishee story yangu japo si mzuri sana katka uandishi.
Ilikua 2010 Dar es salam enzi hizo nikiwa mwanafunzi wa chuo kimoja hapo. Ukweli sikukutana nakiumbe cha kutisha bali ni binaadam alienifanya nibaki na sintofaham na maono tofauti ktk maisha.
Sikubahatika kupata chumba ktk hostel za chuo ikanibidi nipange kitaa flan uswahilini karibu na mwenge hapo. Maisha yalikua fresh tu fadha house alikua na wake wawili na watoto kadhaa hapo kijana mkubwa wa mwenye nyumba alitokea kua mwanangu sana story za hapa na pale, jamaa alikua mstaalabu sana na anasura ya upole by that time alikua kama ana 30 yrs nakuendelea.
Tukio lilotokea lilinifanya nibaki mdomo wazi ni siku moja mida ya saa tisa kasoro huyo bro aliniamsha kwa kugonga mlango nlisita kuitika lkn mwisho nilifunua nakumkuta amemkamata kijana mmoja wa makamo. Jamaa akanambia kwamba huyu ni mwizi na huwa anaibia watu hapo mtaani. Nikamuuliza vp ushahidi unao akadai hana ila amemkuta na kisu mfukoni. Nilitaka kuacha kumpa ushirikiano ila nikaona nimsaidie huyo kijana asijedhurika kwani hakukua na ushahidi wowote. Nilimshauri jamaa kua tuamshe majirani au ndg zake jamaa akawa mbogo. Ilibidi nimfate kwanyuma akiwa amemkamata yule kijana shingoni tukielekea nyumba iliokua opposite na hii tunayokaa. Nilipata bahati ya kumuuliza jamaa akakubali ni kweli hapo aliwahi iba shati na sendoz. Nilijua itakua kesi ndogo lkn tulipofika kwa huyu jirani aligonga mlango mara mbili tatu huyo mzee akafungua na kuelezwa dhumuni la sie kuwepo hapo. Alimtazama yule kijana kwa macho ya dharau na kuulizia mimi kwani hakuwahi niona maeneo hayo ndo jamaa akanitambulisha kama mpangaji wao. Yule mzee haraka bila uoga alitupa jukumu tumuue huyo dogo then tukimaliza tumchome moto hapo hapo. Nilihisi kuogopa nikaona ni kama mzaha vile kwani tulikua wawili tunaopewa jukum hilo. Alipomaliza kufunga mlango wake mzee yule nilimwambia huyu mshkaj kwanini tusimteme tu dogo coz vitu alivyoiba nividogo sana. Msela alinifokea sana na kunipolomoshea matusi makali. Ilibidi niwe mtazamaji asikwambie mtu kifo ni kitu rahisi sana, dogo alishushiwa kipigo hevy ngumi na mateke mpaka akazimia ndipo jamaa alipoanza kutumia mawe yaliyokua pembeni . Ilifika muda dogo alipiga mayowe maskini it was too late, jamaa alihitaji kuua siku hiyo. Baada yakama dakika saba dogo alivuta nikimshuhudia alimsihi yule jamaa akimtaja kwa jina kua unaniua bure bro mimi ni mdogo wako, haikusaidia kitu dogo alipigwa taili mbili na kumwagiwa mafuta ya taa. Aliwaka mpaka mwisho. Niliogopa sana na usiku huo sikulala tena taswira ya kile kipigo ilikua ikinijia kichwani. Niliogopa sababu dogo alouwawa na huyu jamaa ni wa pale mtaani vp mimi mgeni. Nakwanini jamaa hakutaka watu waamshwe na dogo mbona hakua amemuibia huyu jamaa kitu.
Ilibidi iwe siri yangu mpaka nilpokuja kufahamishwa na majirani wengine juu ya kuokotwa mara kwa mara maiti zisizo julikana mtaani. Ilibidi nihame kimya kmya na kujiapiza kua sintokuja kupanga uswahilini tena na hawa binadam wenye sura nzuri za upole niishinao kwa tahadhari kubwa.



Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu nyamatongo hiki kisa kinasisimua sana.

Labda niulize tu, baada ya hilo tukio uhusiano wako na huyo jamaa ulikuaje?

Pili, huyu jamaa yako alikua mwanausalama in any way? Kama sio..kama hutojali unaweza sema alikua akijishughulisha na nini?

Pia, huyo mzee mliyemuamsha usiku; baada ya hapo uliwahi kuonana nae tena? If so, mliongea nini?

Mwisho, unadhani wazazi wa huyu jamaa yako walijua hilo tukio in any way?

Nisamehe kwa maswali mengi....ila hili tukio linafikirisha sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
99
Boya Sana wewe uliogopa nini..?
Ungechukua toto hilo nyie kila kitu mnaonaga negative tu kwanini usiseme bwana kakuonyesha kimwana wa kuoa!
Mkuu Kama unaikumbuka namba yake nitumie halafu ntakupa mrejesho nimemfanya nini!
😂😂😂 Ni miaka zaidi ya 11 Sasa siwez kukumbuka namba
 
Hili lina ukweli na pia lina ukakasi kidogo. Hapo kuna mambo mawili huenda huyo dada akawa ni miongoni mwa majini wale wanaopendaga kuishi na binaadam.
Pia huenda ikawa ni mdada ambae ameenda kwa mganga kutafuta mchumba labda there fore ndo wachumba wanapatikana kishirikina kwa njia hiyo ya kuwaotesha wachumba wakiwa ndotoni😀

Nimejaribu kudadavua tu.. Jamaa kaogopa bure aisee mi nikipata bingo kama hilo silazi damu.. 😀😀
Mabaharia katika ubora wao 😂😂 Ila wanawake wnapatikana tu kwa njia ambazo hazina ukakasi
 
Hahahaaa Mimi ilikuwa siyo kukimbia,
nilikuwa nakatiza uwanjani mida ya saa sits hivi,
Ila nikitembea nasikia kabisa maisha yanaendelea kama mchana,napishana na watu na wanaongea,
nilikuja kushtuka alfajiri natembea palepale uwanjan
Kweli hii Dunia Ina Mambo. Viumbe Vyote eti vya Mungu, Kweli?
 
TUKIO LINGINE LILITUTOKEA UDOGONI UDOGONI.......
Nakumbuka udogoni nili kua na kipaji Cha ufugaji wa sungura
Nakumbuka ilikua mwezi wa kumi na mbili siku Kama mbili ili iwe Xmas
Tulikua tunatoka shambani kwetu Ni mbali kidogo nje ya mji.
Tulikua Mimi mdogo angu anae nifuata kuzaliwa tuliambatana na mtoto wa shangazi yangu na marafiki zetu wengine wa 3 jumla tulikua watu 6
AKATI
Tunarudi nyumbani tulipita njia tofauti na iliyo zoeleka...
TULIONA SHAMBA MOJA KWENYE SHAMBA HILO LILILOKUA NA MWEMBE MKUBWA NA UZIO WA KATANI KUBWA KUZUNGUKA SHAMBA LOTE...
SHAMBA LILIKUA NA MAJANI YA MCHUNGA MAZURI KWA SUNGURA
NA
MAJANI MENGINE MENGINE MAZURI KWA SUNGURA....
TUKASHAURIANA
TUKA INGIA SHAMBANI NA KUANZA KUCHUMA MAJANI
WOTE TULI INAMA KUCHUMA MAJANI
"Gafla mtoto wa shangazi angu AKAANZA kutuambia ANASIKIA harufu ya JINI"
MM NIKA M CRASH tuka endelea kuchuma MAJANI kwa Mara ya pili akasema Tena
ANASIKIA HARUFU YA JINI...
Wote tukambeza na kumshangaa...
Tunaendelea
Kuchuma MAJANI kwa Mara nyingine akasema ANASIKIA HARUFU YA JINI
Gafla
Tukasikia sauti ikisema vijana mnafanya Nini hapa...
HATUKUJUA MZEE ALITOKEA WAP?
Akauliza mnafanya Nini hapa?
Mm nikajibu tunachuma majani ya sungura!
Mzee aka Tu uliza aki sema MMEOMBA
KABLA HATUJAJIB AKASEMA MNAJUA KWENY HILI SHAMBA KUNA NINI?
TUKAKUMBUKA KAULI YA HAMAD ALIYOSEMA ANASIKIA HARUFU YA JINI
TUKASEMA MZEE TUSAMEHE...
HUKU TUKIWA TUNATETEMEKA...
MZEE AKASEMA
NIWASAMEHE KWANI MMEKOSEA NINI....
AKAULIZA MMEOMBA HAPANA....
MZEE AKATUULIZA MNAJUA KWENYE HILI SHAMBA KUNA NINI?
SISI
TUKAKAZANA MZEE TUSAMEHE.....
MWISHO
MZEE AKASEMA TUPENI KILA KITU ALAFU HARAKA ONDOKENI MSIGEUKE NYUMA....
NJIA ILIKUA NYEMBAMBA TULITOKA NDUKI.....
USIKU SIKUPATA USINGIZI....
TANGU SIKU HIYO MTOTO WA SHANGAZI ALIKUA AKINAMBIA KITU SIBISHI....
Duhh hapo kimbembe kinakuja ukijikwaa ukianguka.. Aisee unaweza kuzimia kwa Plesha😀
 
Ni pale wakuu wa nchi waliposema wananchi Wasiogope Gonjwa la Dunia, linalo Ua watu/wataalamu kwa Maelfu, eti mjitibu kwa kutumia Nyungu! ili hali wanakufa! lkn watu waka amini wasio wataalamu.

Hili linatisha, sintosahau aisee!!!!!
 
Shukuru Mungu kama hujawahi kutana na hayo mambo,
Mambo hayo husababishwa na Kama kuna Ndugu wana michezo hiyo, Majirani au watu wanaokuzunguka maeneo unayoishi na husababishwa na Husda,michezo,mazoea
Hayo Mambo bwana mkubwa yapo sana sana tu, kama hayajakukuta utayadharau na kupuuza, Kuna muda unakutana na majaribu mpaka unajiuliza hivi kweli mm huwa nasali, kama nasali mbona bado siko imara huyu Mungu ninae miomba ni wa wapi,mbona wengine hawakumbani na hizi zahama..
Mfn: Sumbawanga unaweza sikia vitimbi vingi sana ila wewe ukapangiwa kazi huko ukaishi vzr na ukakataa kuhama kabisa, ila mwinhine anaweza pangiwa huko mwezi mmoja tu akakutana na vitimbi vya hatari haya mambo yanaendana na Ukoo sometimes
mkuu nakubaliana na ww, ninapokaa kuna mtoto wa mzee mwenye nyumba ni mwanamke wa makamo kuna nyepesi kua na yeye ni fundi, siku moja asubuh anamwambia mke wng eti usiku ameota pale kwangu kuna sherehe yuko yeye na mwanangu wanacheza mziki,wife alivyonambia vile nilimind sana maana kuna kitu nilihisi ila nikamwambia wife hamna tatzo kama kuna lolote baya litawarudia,

kesho yake asubuh mwanae wa mwisho kaenda kucheza kavunjika mkono mpaka hospital mpaka kufungwa POP, nikamwambia wife si alitaka sherehe bas hiyo hapo aruke nayo
 
Mshawishi aunt yako siku moja mkamtembelee hapo dukani...
Nawapa story ilimtokea Aunt yangu kabisaa ni member wa jf pia, (i'm sorry Aunt nashare story yako, usinachambe, lol)

Siku moja yupo mitaa ya kariakoo anashangaa shangaa madukani ghafla akatokea mzee mmoja wa makamo akamsabahi kwa bashasha sana, akamuita jina lake na ubin wake, Aunt alijaribu kuvuta kumbu kumbu ni nani huyu kabla hajapata jibu yule mzee akajitambulisha majina yake yote matatu, mmh Aunt akakumbuka mbona huyu niliambiwa alishafariki ila akashindwa kumwambia hilo, kwa hiyo na yeye akamchangamkia na kukumbushana mawili matatu ya watu waliowafahamu,

Yule mzee akamwambia Aunt yeye anafanya kazi duka la muhindi akamuonesha duka lilipo halikua mbali na pale, akamwambia akiwa anahitaji chochote kariakoo afike pale dukani amuulizie kwa jina X (akamtajia a.k.a yake) atampata na kumpa msaada, basi Aunt akashukuru na kuondoka zake.

Lakini alikua bado ana wasiwasi, akampigia simu dada yake (mama yangu), hivi fulani bin fulani unafahamu habari zake? Dada yake akamwambia looh mbona alifariki miaka mingi sanaaaa, tushaanza na kumsahau,

Aunt alitetemeka, alishindwa kwenda kwake akaenda kwa dada yake, akamuhadithia alichokiona, dada yake akampigia simu ndugu wa karibu kabisa na yule mzee akauuliza habari zake jibu ni lile lile ushasahau kama fulani alifariki na tukazika miaka takribani 10 sasa, aliugua kichwa tu akafariki, na alizikwa mkoa wa mbali na pale Aunt alipomuona,

Waliogopa kumwambia yule ndugu aliyoyaona Aunt, lakini shoga angu mimi alishikwa na homa kali wiki nzima, alibaki mdogo akajuta ile safari yake ya kariakoo, hahaha

Uchawi upo kama ambavyo Corona ipo.

Boost your Immune System to fight a Covid-19.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwaka 2012 nilienda wilaya ya rungwe kukusanya data, sasa katika harakati za kuzunguka nikafika kijiji fulani kinaitwa malalika sijui kama nimeandika sahihi, kipo 15km kutoka kiwila na 7km kutoka hospitali ya igogwe, nyumba niliyofikia ilijengwa mlimani hivi katikati ya shamba la chai, ilikua na vyumba viwili vya kulala nikapewa chumba kimoja kingine alilala mhudumu wa lile shamba, nyumba ilijengwa kwa tofali za tope ila ndani wamebandika magazeti chumba kizima ndio plasta na juu wameweka shuka ndio ceiling board, usiku nilipokua nimelala nilianza kusikia kishindo kikubwa juu ya bati kama mtu anatembea kutoka upande mmoja wa nyumba kwenda mwingine, mwanzoni nilihisi kama ndoto ila niliposhtuka usingizini niloendelea kusikia kama mtu anatembea juu ya bati, ile hali iliendelea kwa muda mrefu, niliinua kichwa kuchungulia dilishani nje sikuona kitu palikua na ukungu mkali ikabidi nirudi kujifubika branket langu huku moyo ukienda mbio sana nikajua leo kazi ninayo,

baada ya muda ile sauti iliacha ghafla kikaja kitu kama kimbunga mle chumbani upepo mkali ukabandua yale magazeti yote ukutani mavumbi ya tofali yakawa yananiangukia kitandi mimi nimejifunika hadi kichwa nimekaza miguu shuka lisitoke, ule upepo ulipoisha nikaita alexxxx kwa sauti kubwa ambaye ni yule mwenyej wangu aliyelala chumba kingine alipoitika sikujua nimefikaje chumbani kwake, maana niliruka kitandani nikapiga teke kile kimlango cha chumbani nikavamia na mlango wake hadi chumbani kwake, nikamuuliza kama amesikia ivo vitu licha ya kuwa na baridi ila jasho lilikua linanitoka,

jamaa alichonijibu ni tulia acha papara. Nikawa nimekaa kwenye kistuli pembeni ya kitanda chake huku tumewasha kibatali, jamaa akaniambia pametulia rudi ukalale nikakataa nikamwambia silali nakaa hapa hapa wewe lala, nilikaa pale hadi alfajiri nilipoona nje pameanza kupambazuka nikaenda mle chumbani palikua hovyo sana vumbi kila mahali nikachukua kibegi changu nikamwambia yule jamaa mimi nasepa badae njoo kiwira tuongee, nikatoka nikadandia magari yanayobeba ndizi na maparachichi kwenda mnandani, saa nne yule jamaa akikuja kiwira nikampa elfu ishirini nikamwambia ikitokea siku mabosi wangu wakija kijijini kuuliza kama nilifika awambie kuwa nilikuja na nikafanya kazi ila kiukweli nilikimbia huwa sisahau lilie tukio

kuna lingine nililiona wilaya ya mbogwe mkoa wa simiyu, ni vijijini huko ndani kabisa hata barabara hakuna mnapaki gari mnatembea 4km huko tulizinguana na mwenyekiti wa kijiji akatutumia kundi la fisi tukakimbilia kwenye nyumba ya mwanakijiji tukapiga simu kwa mtendaji akaja kutuokoa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii ilitokea miaka ya mwanzoni ya 80. Huko kamsamba kando ya mto Momba (ambalo ndo jina ya wilaya ya Momba). Hicho kijiji na vijiji jirani vilikuwa na matukio acha. Watu walikuwa wanga ile mbaya.

1. Tukio la kwanza baba alikuwa Mwalimu Mkuu wa shule ile. Sasa alikuwa na kawaida ya kuhesabisha namba saa Tisa. Siku moja wanafunzi wakaja kugonga kengele ya namba saa tisa kasoro hivi. Wakakuta kuna kundi la watu wapo shuleni wamejaa kwenye madarasa yote. Wengine wanafundisha, wengine wana pewa adhabu kama shule kabisa mchana. Wale wanafunzi wakaja wakagonga nyumbani ambapo baba akatoka na mdogo wake kwenda kuhakikisha. Baba akawaambia wagonge kengele, vilitoka vidudu mtu urefu havizidi kama mita moja na nusu. Waliwakimbiza mbaya. Bahati nzuri nyumba ilikuwa karibu na shule so wakawahi kuingia ndani. Sauti ikasikika ikisema ole wenu mtusumbue usiku tena. Ile ndo ilikuwa mwisho, kuanzia kesho yake wanafunzi wakaanza kuja kukiwa kumekucha kabisa.

2. Tukio la pili ilikuwa miaka hiyohiyo mida ya saa 12 jioni tukiwa tunaenda kuteka maji kwenye huo mto. Tukaona vyungu vingiii, vizuri vimepangwa pembeni ya mto. Mama akasema dah, vyungu vizuri sijui muuzaji yupo wapi ili aniuzie. Akaanza kuita kama kuna mtu karibu. Kwa mshangao mkuu vyungu vileserereka machoni petu na kukimbilia mtu... Ilikuwa kama nyoka anavyoteleza... Aisee, tulitoka mbio tukajikuta tupo ndani bila tumefikaje.

Kule Kamsamba kulikuwa na ushirikina na matukio ya kutisha acha kabisa. Sijui sasa hali ikoje. Kukutana na mtu anatembea upande upande badala ya kwenda mbele anakuwa anaenda kulia au kushoto ilikuwa kawaida. Tukiuliza wakubwa wanasema hao ni misukule. Mara nyingine tumeenda porini tukakuta kiwiliwili, damu bado mbichi, halafu masela hatuogopi tunaendelea na mishe yetu tu. Siku moja tukakutana na hao wajuba wana visu na ndoo, aisee tulikula nao ligi kwa masaa kama mawili hivi bila kutukuta.

Habari za kuchunana ngozi kule ndo ilikuwa chimbuko. Ilikuwa kama serikali haipo. Maana maiti inaokotwa na inazikwa tu. Vyombo vya habari ndo vikaja saidia.
 
Mwaka 2012 nilienda wilaya ya rungwe kukusanya data, sasa katika harakati za kuzunguka nikafika kijiji fulani kinaitwa malalika sijui kama nimeandika sahihi, kipo 15km kutoka kiwila na 7km kutoka hospitali ya igogwe, nyumba niliyofikia ilijengwa mlimani hivi katikati ya shamba la chai, ilikua na vyumba viwili vya kulala nikapewa chumba kimoja kingine alilala mhudumu wa lile shamba, nyumba ilijengwa kwa tofali za tope ila ndani wamebandika magazeti chumba kizima ndio plasta na juu wameweka shuka ndio ceiling board, usiku nilipokua nimelala nilianza kusikia kishindo kikubwa juu ya bati kama mtu anatembea kutoka upande mmoja wa nyumba kwenda mwingine, mwanzoni nilihisi kama ndoto ila niliposhtuka usingizini niloendelea kusikia kama mtu anatembea juu ya bati, ile hali iliendelea kwa muda mrefu, niliinua kichwa kuchungulia dilishani nje sikuona kitu palikua na ukungu mkali ikabidi nirudi kujifubika branket langu huku moyo ukienda mbio sana nikajua leo kazi ninayo, baada ya muda ile sauti iliacha ghafla kikaja kitu kama kimbunga mle chumbani upepo mkali ukabandua yale magazeti yote ukutani mavumbi ya tofali yakawa yananiangukia kitandi mimi nimejifunika hadi kichwa nimekaza miguu shuka lisitoke, ule upepo ulipoisha nikaita alexxxx kwa sauti kubwa ambaye ni yule mwenyej wangu aliyelala chumba kingine alipoitika sikujua nimefikaje chumbani kwake, maana niliruka kitandani nikapiga teke kile kimlango cha chumbani nikavamia na mlango wake hadi chumbani kwake, nikamuuliza kama amesikia ivo vitu licha ya kuwa na baridi ila jasho lilikua linanitoka, jamaa alichonijibu ni tulia acha papara. Nikawa nimekaa kwenye kistuli pembeni ya kitanda chake huku tumewasha kibatali, jamaa akaniambia pametulia rudi ukalale nikakataa nikamwambia silali nakaa hapa hapa wewe lala, nilikaa pale hadi alfajiri nilipoona nje pameanza kupambazuka nikaenda mle chumbani palikua hovyo sana vumbi kila mahali nikachukua kibegi changu nikamwambia yule jamaa mimi nasepa badae njoo kiwira tuongee, nikatoka nikadandia magari yanayobeba ndizi na maparachichi kwenda mnandani, saa nne yule jamaa akikuja kiwira nikampa elfu ishirini nikamwambia ikitokea siku mabosi wangu wakija kijijini kuuliza kama nilifika awambie kuwa nilikuja na nikafanya kazi ila kiukweli nilikimbia huwa sisahau lilie tukio, kuna lingine nililiona wilaya ya mbogwe mkoa wa simiyu, ni vijijini huko ndani kabisa hata barabara hakuna mnapaki gari mnatembea 4km huko tulizinguana na mwenyekiti wa kijiji akatutumia kundi la fisi tukakimbilia kwenye nyumba ya mwanakijiji tukapiga simu kwa mtendaji akaja kutuokoa.

Sent using Jamii Forums mobile app
nmecheka kama mazuri ila dunia jamani
 
Momba ndio wapi mkuu
Hii ilitokea miaka ya mwanzoni ya 80. Huko kamsamba kando ya mto Momba (ambalo ndo jina ya wilaya ya Momba). Hicho kijiji na vijiji jirani vilikuwa na matukio acha. Watu walikuwa wanga ile mbaya.
1. Tukio la kwanza baba alikuwa Mwalimu Mkuu wa shule ile. Sasa alikuwa na kawaida ya kuhesabisha namba saa Tisa. Siku moja wanafunzi wakaja kugonga kengele ya namba saa tisa kasoro hivi. Wakakuta kuna kundi la watu wapo shuleni wamejaa kwenye madarasa yote. Wengine wanafundisha, wengine wana pewa adhabu kama shule kabisa mchana. Wale wanafunzi wakaja wakagonga nyumbani ambapo baba akatoka na mdogo wake kwenda kuhakikisha. Baba akawaambia wagonge kengele, vilitoka vidudu mtu urefu havizidi kama mita moja na nusu. Waliwakimbiza mbaya. Bahati nzuri nyumba ilikuwa karibu na shule so wakawahi kuingia ndani. Sauti ikasikika ikisema ole wenu mtusumbue usiku tena. Ile ndo ilikuwa mwisho, kuanzia kesho yake wanafunzi wakaanza kuja kukiwa kumekucha kabisa.
2. Tukio la pili ilikuwa miaka hiyohiyo mida ya saa 12 jioni tukiwa tunaenda kuteka maji kwenye huo mto. Tukaona vyungu vingiii, vizuri vimepangwa pembeni ya mto. Mama akasema dah, vyungu vizuri sijui muuzaji yupo wapi ili aniuzie. Akaanza kuita kama kuna mtu karibu. Kwa mshangao mkuu vyungu vileserereka machoni petu na kukimbilia mtu... Ilikuwa kama nyoka anavyoteleza... Aisee, tulitoka mbio tukajikuta tupo ndani bila tumefikaje.

Kule Kamsamba kulikuwa na ushirikina na matukio ya kutisha acha kabisa. Sijui sasa hali ikoje. Kukutana na mtu anatembea upande upande badala ya kwenda mbele anakuwa anaenda kulia au kushoto ilikuwa kawaida. Tukiuliza wakubwa wanasema hao ni misukule. Mara nyingine tumeenda porini tukakuta kiwiliwili, damu bado mbichi, halafu masela hatuogopi tunaendelea na mishe yetu tu. Siku moja tukakutana na hao wajuba wana visu na ndoo, aisee tulikula nao ligi kwa masaa kama mawili hivi bila kutukuta. Habari za kuchunana ngozi kule ndo ilikuwa chimbuko. Ilikuwa kama serikali haipo. Maana maiti inaokotwa na inazikwa tu. Vyombo vya habari ndo vikaja saidia.
 
Mimi kuna kisa kilinitokea nilikua kama darasa la 5. Wazee wameenda kulala na mimi nilikua na chumba changu tofauti na madogo zangu nikaenda zangu kulala,nakumbuka mlango nilifunga vizur kabisa dogo nikajipigia zangu mbonji usingizi mwororo! Asubuh kuamka LAHULA LAKWATA pembeni ya kitanda kwa chini kuna kimba moja la kinyesi,kuangalia mlango umefungwa vilevile,na udogo wangu nikaanza kutetemeka nikaenda kuwaamsha wazee,mshua kuja pale akacheka akasema hamna lolote huyu kashindwa akayamwagia majivu picha likaisha hivyo.

lakin ile nyumba ikifika mida ya saa mbili usiku kuna vitu vinatembea juu ya bati afu kama vinateleza af unasikia kishindo kama vimedondoka mkienda mliposikia kishindo hamna kitu.
Nakumbuka nilishawah kumwamsha dogo saa 9 usiku nikidhan kumepambazuka twende shule tukawah namba,fresh tumejiandaa tukaenda kuwaaga wazee tukaanza safari,hapa ndo hua naamin mungu yupo maana baada ya kufika mtaani maana inabdi tukatze mtaani afu tuvuke eneo la makaburi ndo tufike shule,ila ule utulivu wa mtaani nikamwambia dogo turudi home hii sio kawaida kama tukichelewa leo namba basi,tukarudi zetu home na kuingia vyumbani kwetu bila kuwataarifu wazee,kumbe huku room kwa wazee bi mkubwa akashtuka akasema hawa wametuaga wanaenda shule kwan saa ngapi?

kuangalia muda ni saa 9 na dakika kadhaa ebana ee dingi alikurupuka na pensi flan ya kulalia kifua wazi akaelekea shule kutufata,kufika pale anaita mlinzi haonekani ikabdi arudi huku anasema kesho nasafiri naenda nyumbani naona watu hatuheshimiani,bi mkubwa akasema hebu tuwaangalie vyumbani mwao,kuja kuangalia bi mkubwa akasema SI HAWA HAPA!

Wale mabibi jirani ***** zao lakin walikuja kuuelewa mziki
 
Tukio LINGINE LILINITOKEA MIAKA kumi iliyopita Nakumbuka yalikua maafali ya WASABATO...
NILIPEWA KADI ZAIDI YA MBILI KWA KUA MWENYEKITI ALIKUA NI RAFIKI ANGU....
STORY ILIKUA IVI....
ILIKUA SAA SITA KAMA NA DAKIKA 50 MCHANA..
NIKAPATA WAZO NIKAMPITIE RAFIK ANGU THABIT
RAFIKI ANGU THABIT ALIKUA ANAKAA JIRANI NA SHULE YA MSINGI....
ILI NIFIKE KWAO ILINIBIDI NIKATIZE KATIKATI YA UWANJA WA MPIRA....
ILE
ILE NAKATIZA KANDO KANDO YA UWANJA KUNA MTI MMOJA MKUBWA SANAA
MAJIRA HAYO YA MCHANA HAKUKUA NA MTU YEYOTE BARABARANI
NILIFIKA MITA CHACHE KARIBU NA MTI MKUBWA HAPO UWANJANI...
GAFLA
NIKAONA MDADA WA KIISLAMU ALIE VALIA HIJABU NYEUSI....
NILIPO
TUPA JICHO KWA MARA YA PILI TULIKUTANA USO KWA USO....
BINTI ALIKUA NA UZURI USIO WA KAWAIDA....
SURA ILIYO MELEMETA AKIWA AMESHIKILIA ULE MTI MKUBWA HUKU AKINITAZAMA
MPK NIKAOGOPA...
NIKA ANGALIA PEMBENI NIKARUDIA KUMUANGALIA TENA YULE DADA ALIENDELEA KUNITAZAMA MIMI NILIANGALIA MBELE SIKUGEUKA TENA NYUMA...
YULE DADA ALIKUA AMEVALIA HIJABU NYEUSI NDEFU MPKA CHINI MIGUU HAIONEKANI WALA MIKONO....
ALIKUA MWARABU SI MWARABU SHOMBE SIO SHOMBE
HAKUA MWEUPE WALA MWEUSI
UZURI WAKE ULIKUA KAMA WAHABESHI TOKA ETHIOPIA

KILICHO NIOKOA NI KIMOJA TUU HUWA SINAGA TABIA ZA KUSHOBOKEA WADADA....
TULI TAZAMANA ZAIDI YA MARA 3 NA YULE MDADA NA SIKUMSEMESHA KITU...
ALINITAZAMA SANA...ILA NILIJIKAZA KIUME NIKAKATIZA KAMA SIJAONA KITU....
NILIPO FIKA KWAO NA RAFIK ANGU MITA MIA 200 TOKA ENEO LA TUKIO FASTA NIKAMWAMBIA
TUKARUDI UWANJANI HATUKUKUTA MTU...
NILIOGOPA SANA TULIENDA KWENY SHEREHE YA WASABATO NILIPO MALIZA KULA TUMBO LILIANZA KUUMA NA NILI HARISHA SANAA
NILIOGOPA SANA TANGU SIKU IYO NILI ANZA KULALA NA BIBLIA KITANDANI.....
 
Mwaka 2012 nilienda wilaya ya rungwe kukusanya data, sasa katika harakati za kuzunguka nikafika kijiji fulani kinaitwa malalika sijui kama nimeandika sahihi, kipo 15km kutoka kiwila na 7km kutoka hospitali ya igogwe, nyumba niliyofikia ilijengwa mlimani hivi katikati ya shamba la chai, ilikua na vyumba viwili vya kulala nikapewa chumba kimoja kingine alilala mhudumu wa lile shamba, nyumba ilijengwa kwa tofali za tope ila ndani wamebandika magazeti chumba kizima ndio plasta na juu wameweka shuka ndio ceiling board, usiku nilipokua nimelala nilianza kusikia kishindo kikubwa juu ya bati kama mtu anatembea kutoka upande mmoja wa nyumba kwenda mwingine, mwanzoni nilihisi kama ndoto ila niliposhtuka usingizini niloendelea kusikia kama mtu anatembea juu ya bati, ile hali iliendelea kwa muda mrefu, niliinua kichwa kuchungulia dilishani nje sikuona kitu palikua na ukungu mkali ikabidi nirudi kujifubika branket langu huku moyo ukienda mbio sana nikajua leo kazi ninayo, baada ya muda ile sauti iliacha ghafla kikaja kitu kama kimbunga mle chumbani upepo mkali ukabandua yale magazeti yote ukutani mavumbi ya tofali yakawa yananiangukia kitandi mimi nimejifunika hadi kichwa nimekaza miguu shuka lisitoke, ule upepo ulipoisha nikaita alexxxx kwa sauti kubwa ambaye ni yule mwenyej wangu aliyelala chumba kingine alipoitika sikujua nimefikaje chumbani kwake, maana niliruka kitandani nikapiga teke kile kimlango cha chumbani nikavamia na mlango wake hadi chumbani kwake, nikamuuliza kama amesikia ivo vitu licha ya kuwa na baridi ila jasho lilikua linanitoka, jamaa alichonijibu ni tulia acha papara. Nikawa nimekaa kwenye kistuli pembeni ya kitanda chake huku tumewasha kibatali, jamaa akaniambia pametulia rudi ukalale nikakataa nikamwambia silali nakaa hapa hapa wewe lala, nilikaa pale hadi alfajiri nilipoona nje pameanza kupambazuka nikaenda mle chumbani palikua hovyo sana vumbi kila mahali nikachukua kibegi changu nikamwambia yule jamaa mimi nasepa badae njoo kiwira tuongee, nikatoka nikadandia magari yanayobeba ndizi na maparachichi kwenda mnandani, saa nne yule jamaa akikuja kiwira nikampa elfu ishirini nikamwambia ikitokea siku mabosi wangu wakija kijijini kuuliza kama nilifika awambie kuwa nilikuja na nikafanya kazi ila kiukweli nilikimbia huwa sisahau lilie tukio, kuna lingine nililiona wilaya ya mbogwe mkoa wa simiyu, ni vijijini huko ndani kabisa hata barabara hakuna mnapaki gari mnatembea 4km huko tulizinguana na mwenyekiti wa kijiji akatutumia kundi la fisi tukakimbilia kwenye nyumba ya mwanakijiji tukapiga simu kwa mtendaji akaja kutuokoa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Wilaya ya mbogwe simiyu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii ilitokea miaka ya mwanzoni ya 80. Huko kamsamba kando ya mto Momba (ambalo ndo jina ya wilaya ya Momba). Hicho kijiji na vijiji jirani vilikuwa na matukio acha. Watu walikuwa wanga ile mbaya.
1. Tukio la kwanza baba alikuwa Mwalimu Mkuu wa shule ile. Sasa alikuwa na kawaida ya kuhesabisha namba saa Tisa. Siku moja wanafunzi wakaja kugonga kengele ya namba saa tisa kasoro hivi. Wakakuta kuna kundi la watu wapo shuleni wamejaa kwenye madarasa yote. Wengine wanafundisha, wengine wana pewa adhabu kama shule kabisa mchana. Wale wanafunzi wakaja wakagonga nyumbani ambapo baba akatoka na mdogo wake kwenda kuhakikisha. Baba akawaambia wagonge kengele, vilitoka vidudu mtu urefu havizidi kama mita moja na nusu. Waliwakimbiza mbaya. Bahati nzuri nyumba ilikuwa karibu na shule so wakawahi kuingia ndani. Sauti ikasikika ikisema ole wenu mtusumbue usiku tena. Ile ndo ilikuwa mwisho, kuanzia kesho yake wanafunzi wakaanza kuja kukiwa kumekucha kabisa.
2. Tukio la pili ilikuwa miaka hiyohiyo mida ya saa 12 jioni tukiwa tunaenda kuteka maji kwenye huo mto. Tukaona vyungu vingiii, vizuri vimepangwa pembeni ya mto. Mama akasema dah, vyungu vizuri sijui muuzaji yupo wapi ili aniuzie. Akaanza kuita kama kuna mtu karibu. Kwa mshangao mkuu vyungu vileserereka machoni petu na kukimbilia mtu... Ilikuwa kama nyoka anavyoteleza... Aisee, tulitoka mbio tukajikuta tupo ndani bila tumefikaje.

Kule Kamsamba kulikuwa na ushirikina na matukio ya kutisha acha kabisa. Sijui sasa hali ikoje. Kukutana na mtu anatembea upande upande badala ya kwenda mbele anakuwa anaenda kulia au kushoto ilikuwa kawaida. Tukiuliza wakubwa wanasema hao ni misukule. Mara nyingine tumeenda porini tukakuta kiwiliwili, damu bado mbichi, halafu masela hatuogopi tunaendelea na mishe yetu tu. Siku moja tukakutana na hao wajuba wana visu na ndoo, aisee tulikula nao ligi kwa masaa kama mawili hivi bila kutukuta. Habari za kuchunana ngozi kule ndo ilikuwa chimbuko. Ilikuwa kama serikali haipo. Maana maiti inaokotwa na inazikwa tu. Vyombo vya habari ndo vikaja saidia.
Hilo tukio lako la kukuta watu saa tisa wapo darasani wanasoma liliwahi kunikuta hata mimi, ila mimi haikuwa darasani....ilikuwa mida hiyo hiyo mibovu, nikiwa kikosi fulani huko Nachingwea mwaka 2013. Siku hiyo nipo zamu, kiongozi wa eneo nililopaswa kulifanyia ungalizi siku hiyo. Na niliwajibika kwa sehemu mbili zote zikiwa karibu: sehemu A, na ambapo zamu ilinisoma sehebu B, lakini nikiangalia sehemu zote mbili.

Jioni katika kushusha bendera nikawapanga watu wa kituo A ndo washushe, halafu sisi wa kituo B tutapandisha asubuhi. Na mimi nilikuwa wa mwisho kulinda siku ile, ina maana baada ya kuzurura zurura mpaka saa 6 nkaamua nilale ili saa kumi nishike zamu yangu. Sasa ilipofika saa kumi kasoro nikaamka, pako salama nikawapumzisha waliopo nasi wa zamu ya saa kumi tukaamka... Nikamwambia mwenzangu hebu baki hapo mi nifike kituo A nikacheki nako kuko poa, sasa nikiwa naenda kituo A nkapita sehemu ambapo kuna milingoti ya bendera... wacha kabisa, nikakuta watu wawili wafupi mno kwa kipimo cha kawaida wananifika kiunoni, wapo kwenye milingoti ya bendera wanashusha bendera, wamevaa kombati, wana silaha kama kawaida, na nyuma yao kuna watu nane wapo kwenye paredi ya kushusha bendera! Nikatulia nikawacheki, baadaye wakamaliza, wakageuka nyuma, wakaungana na paredi hao wakasepa kuelekea kwenye misufi... na wakapotea.

Nilishangaa sana maana sisi bendera tukishusha huipeleka kituo A, wao wakapeleka kwenye misufi na wakapotelea huko. Siku za baadae nilipowauliza wakongwe wakasema hiyo ni kawaida, yaani sisi tunaposhusha hao hupandisha, na sisi tunapopandisha wao huwa washashushandio , ila shukuru hawajakuona... wakasema hivyo vituo unaweza ukashangaa hata usiku magari yanawashwa hafu humuoni anayeyawasha, mabovu hutengenezwa na usimuone anayeyatengeneza pia... nikastaajabu sana!!!
 
Back
Top Bottom