Njooni tusemezane. Sheria gani inakataza watu kuchangishana? Waziri Mkuu yupo sahihi kumkamata Niffer?

Njooni tusemezane. Sheria gani inakataza watu kuchangishana? Waziri Mkuu yupo sahihi kumkamata Niffer?

Naomba kufahamu, sheria gani imevunjwa ama kukiukwa na Niffer kuchangisha fedha
Punguza mhemko na papara, penda kujifunza na kujielimisha! Pitia hii sheria ukurasa wa 20.
 

Attachments

You belong to the past. Mwaka 2024 unaweza toa hoja kama hii? Dawa hapo weka mechanism ya kuwatumia hao influensa kupata michango ya raia wwa kawaida. Unadhani nifa atapata mchango gani toka kwenye taasisi ama mashirika, yale mashirika yanataka pr ni wazi yataenda serikalini na kwenye vyombo vya habari wakati wanatoa mchango wao. Sasa nifa anakusaidia kuipata pesa ya wadangaji, masista duu na mabrazameni wa buku 2000 na kada kama hizo. Ambazo kiuhalisia hazina interaction na formalities.
Mosi, the past shapes the future, pili serikali haitegemei influensa kusimamia majukumu yake, hao influensa wanaweza kuwepo au wasiwepo lkn matukio yakitokea serikali itafanya wajibu wake..to maintain ORDER..tatu, angalia kwa upana mambo ya michango kijana, dunia ina tatizo la money laundering na michango inatumiwa sana kutakatisha pesa haramu! huwezi achia kila mtu achangishe michango pasina utaratibu..mara zote huwekwa utaratibu na serikali kukusanya michango kwa wanaopenda kusaidia wahanga, km huiamini serikali basi nenda mwenyewe kwa wahanga mahali walipo uwape mchango wako!
 
Nawaamkua nyote

Tarehe 17 Novemba 2024, Waziri Mkuu akiwa eneo la Kariakoo kukagua zoezi linaloeneelea la uokoaji wa waliokwama chini ya kifusi cha ghorofa iliyoanguka. Alitoa maagizo kwa jeshi la polisi kumkamata Mtanzania aitwaye Niffer ambaye kupitia mitabdaoni alitoa taarifa kuwa amechangisha pesa za za kuwahani wahanga wa ajali ya ghorofa. kuna mambo kadhaa ya kuangazia hapa
  1. Niffer ametoa taarifa ya kuchangisha na kuelezea kiwango alichokikusanya
  2. Waziri Mkuu ameipokea taarifa ya Niffer kama vile anapokea briefings za kiuchunguzi
  3. Waziri Mkuu anatoa agizo la kukamatwa na kuhojiwa Niffer ili aeleze nani kamruhusu kuchangisha tarehe 17 Novemba 2024
  4. Tarehe 18 Novemba 2024, waziri Mkuu anaelekeza polisi wamhoji mmiliki wa jengo lililoanguka. Agizo hilo limekuja baada ya wananchi kuhoji alipo mmiliki wa jengo na kama hajakamatwa tangu siku ya jengo kuanguka.
  5. Jengo limeanguka ahsubuhi saa tatu halafu Mkuu wa Mkoa na vikosi vya uokozi wanafika eneo la tukio saa nane mchana. Hilo jambo halijamkera Waziri Mkuu
Naomba kufahamu, sheria gani imevunjwa ama kukiukwa na Niffer kuchangisha fedha ambapo si mara ya kwanza kuchangisha na kuwasilisha kwa walengwa?

Naomba kufahamu. Ni michango gani ya wahanga iliyolusanywa kupitia serikali na ikawasilishwa kwa walengwa? Nakumbuka michango ya tetemeko la ardhi Kagera ilikusanywa na walengwa hawwkuambulia senti. Vivyo hivyo mafuriko Morogoro wahanga waliishia kusikia redioni michango ambayo haikuwafikia.

Waziri Mkuu atueleze. Matumizi ya fedha za dharurq na majanga chini ya ofisi yake zimetumikqje tangu aingie ofisini?

Kweli ITATUWEKA HURU
Kama kawaia PM anahemka tu
 
Nawaamkua nyote

Tarehe 17 Novemba 2024, Waziri Mkuu akiwa eneo la Kariakoo kukagua zoezi linaloeneelea la uokoaji wa waliokwama chini ya kifusi cha ghorofa iliyoanguka. Alitoa maagizo kwa jeshi la polisi kumkamata Mtanzania aitwaye Niffer ambaye kupitia mitabdaoni alitoa taarifa kuwa amechangisha pesa za za kuwahani wahanga wa ajali ya ghorofa. kuna mambo kadhaa ya kuangazia hapa
  1. Niffer ametoa taarifa ya kuchangisha na kuelezea kiwango alichokikusanya
  2. Waziri Mkuu ameipokea taarifa ya Niffer kama vile anapokea briefings za kiuchunguzi
  3. Waziri Mkuu anatoa agizo la kukamatwa na kuhojiwa Niffer ili aeleze nani kamruhusu kuchangisha tarehe 17 Novemba 2024
  4. Tarehe 18 Novemba 2024, waziri Mkuu anaelekeza polisi wamhoji mmiliki wa jengo lililoanguka. Agizo hilo limekuja baada ya wananchi kuhoji alipo mmiliki wa jengo na kama hajakamatwa tangu siku ya jengo kuanguka.
  5. Jengo limeanguka ahsubuhi saa tatu halafu Mkuu wa Mkoa na vikosi vya uokozi wanafika eneo la tukio saa nane mchana. Hilo jambo halijamkera Waziri Mkuu
Naomba kufahamu, sheria gani imevunjwa ama kukiukwa na Niffer kuchangisha fedha ambapo si mara ya kwanza kuchangisha na kuwasilisha kwa walengwa?

Naomba kufahamu. Ni michango gani ya wahanga iliyolusanywa kupitia serikali na ikawasilishwa kwa walengwa? Nakumbuka michango ya tetemeko la ardhi Kagera ilikusanywa na walengwa hawwkuambulia senti. Vivyo hivyo mafuriko Morogoro wahanga waliishia kusikia redioni michango ambayo haikuwafikia.

Waziri Mkuu atueleze. Matumizi ya fedha za dharurq na majanga chini ya ofisi yake zimetumikqje tangu aingie ofisini?

Kweli ITATUWEKA HURU
Waziri mkuu hakumkamata yeyote, tusizushe.
 
Sheria ya usimamizi wa maafa ya mwaka 2022, kifungu cha 26(2) inasema jukumu la kuchangisha litafanywa na Kamati ya maafa iliyo chini ya ofisi ya Waziri mkuu, kupitia akaunti maalumu.

Kiufupi ni kwamba Niffer alikuwa anaingiliia majukumu ya ofisi ya waziri mkuu, mbaya zaidi akaanza kujibizana na waziri mkuu mtandaoni huku akijinasibu kwamba ana jeshi kubwa nyuma yake...... Nadhan hilo jeshi alimaanisha watu kama wewe mtoa mada

Embu peleka upumbavu wako huko hiyo sheria haikatazi mtu mwingine kukusanya michango.
Watu wanaweza kukusanya ila wanatakiwa waiwasilishe kwenye kamati ya maafa.
Sasa huyo binti si alikuwa anawasaidia kukusanya halafu awapelekee.
Kimsingi Kasimu Majaliwa kachemsha sana kwenye hiyo ishu kwa kutoa agizo la ajabu na hovyo kabisa AMEKURUPUKA
Unless otherwise wangemsubiri akusanye na asingeziwasilisha kwenye kamati ndio wamkamate.
 

Attachments

  • Screenshot_2024-11-19-15-09-34-72.png
    Screenshot_2024-11-19-15-09-34-72.png
    274.4 KB · Views: 2
  • sw-1675254187-SHERIA YA USIMAMIZI WA MAAFA Na. 6 YA MWAKA, 2022..pdf
    sw-1675254187-SHERIA YA USIMAMIZI WA MAAFA Na. 6 YA MWAKA, 2022..pdf
    460.4 KB · Views: 2
Another marked assassin!!

Mkuu wala huhitaji kunilia radar, njoo tuonane face to face!! Uchawa mpaka kwenye maoni ya michango ya maafa ya Niffer!!

Hakika ukungu unaanza kutoweka!!
Ahahah nakujok
 
Mosi, the past shapes the future, pili serikali haitegemei influensa kusimamia majukumu yake, hao influensa wanaweza kuwepo au wasiwepo lkn matukio yakitokea serikali itafanya wajibu wake..to maintain ORDER..tatu, angalia kwa upana mambo ya michango kijana, dunia ina tatizo la money laundering na michango inatumiwa sana kutakatisha pesa haramu! huwezi achia kila mtu achangishe michango pasina utaratibu..mara zote huwekwa utaratibu na serikali kukusanya michango kwa wanaopenda kusaidia wahanga, km huiamini serikali basi nenda mwenyewe kwa wahanga mahali walipo uwape mchango wako!
Why are you obsessed with ORDER, have you seen any signs of anarchy?
Kwanza only future of progressive thinkers can be shaped by their past, this doesn't benefit society of sticklers for rules like what you're.
Pili yote ulosema including money laundering ndio tumesema weka control mechanism au auditing.
Tatu uongo serikali sio self sufficient ni mara nyingi tu inaalika michango toka kwa wadau mbalimbali, hata kariakoo kwenyewe kuna wadau wengi tu wasiotoka serikalini PM aliwataja na kuwashukuru, mv Bukoba wadau binafsi walishiriki nk
Unataka kusemaje tena?
 
This Man should not be trusted Again. Hupaswi kumwamini mwuongo hata kama akiongea Ukweli.
 
Msilete ushabiki kwenye mambo ya kisheria! Huyo Nifer hajaenda kuuawa bali anahojiwa na mamlaka zitaona nia yake ilikuwa nini. Mamlaka hazina bifu na huyo dada naamini ni ishu ya yeye kutoa ushirikiano tu ishu yake inaisha.

Sema kwa akili zake za mitandaoni ndo utaskia anapost kuwa ana strong arm hayo ndo yanaweza kumkost. Nadhan hajui serikali inavyofanya kazi yeye anajua kuuza bidhaa kutoka China basi. Anafikiri serikali ni kama konteina la bidhaa
Kumuhoji mtu ni mpaka pawe na jambo linalokiuka utaratibu au sheria fulani. Sasa tunachotaka kujua, huyo Niffer kafanya kosa gani au kakiuka utaratibu upi uliosababisha aitwe kuhojiwa??
 
K
Sheria irekebishwe. Inaua moyo wa kujitolea. Iangalie namna ya kujumuisha wenye ushawishi na ambao kwa kweli hufanya harambee za namna hiyo kwa matukio ndani ya jamii, kama malisa, nifa na mwl yusuf. Wapo wengi ambao huwiwa kufanya mchango wao kupitia ushawishi wao. Ofisi ya waziri mkuu sidhani kama ina ushawishi wa kuwafikia wafuasi wa mitandao ya kijamii wa watu kama nisha, sasa unatap vipi michango yao hao ambao ni "jeshi kubwa" ili nao wajisikie wamefanya kitu kwenye maafa yoyote. Ni kwa kuwatumia influensa, watu wanaowafutilia mitandaoni kama nifa.
Kwa Nini huo ushawishi wao wasiutumie kwenye utaratibu uliowekwa?!
 
Nawaamkua nyote

Tarehe 17 Novemba 2024, Waziri Mkuu akiwa eneo la Kariakoo kukagua zoezi linaloeneelea la uokoaji wa waliokwama chini ya kifusi cha ghorofa iliyoanguka. Alitoa maagizo kwa jeshi la polisi kumkamata Mtanzania aitwaye Niffer ambaye kupitia mitabdaoni alitoa taarifa kuwa amechangisha pesa za za kuwahani wahanga wa ajali ya ghorofa. kuna mambo kadhaa ya kuangazia hapa
  1. Niffer ametoa taarifa ya kuchangisha na kuelezea kiwango alichokikusanya
  2. Waziri Mkuu ameipokea taarifa ya Niffer kama vile anapokea briefings za kiuchunguzi
  3. Waziri Mkuu anatoa agizo la kukamatwa na kuhojiwa Niffer ili aeleze nani kamruhusu kuchangisha tarehe 17 Novemba 2024
  4. Tarehe 18 Novemba 2024, waziri Mkuu anaelekeza polisi wamhoji mmiliki wa jengo lililoanguka. Agizo hilo limekuja baada ya wananchi kuhoji alipo mmiliki wa jengo na kama hajakamatwa tangu siku ya jengo kuanguka.
  5. Jengo limeanguka ahsubuhi saa tatu halafu Mkuu wa Mkoa na vikosi vya uokozi wanafika eneo la tukio saa nane mchana. Hilo jambo halijamkera Waziri Mkuu
Naomba kufahamu, sheria gani imevunjwa ama kukiukwa na Niffer kuchangisha fedha ambapo si mara ya kwanza kuchangisha na kuwasilisha kwa walengwa?

Naomba kufahamu. Ni michango gani ya wahanga iliyolusanywa kupitia serikali na ikawasilishwa kwa walengwa? Nakumbuka michango ya tetemeko la ardhi Kagera ilikusanywa na walengwa hawwkuambulia senti. Vivyo hivyo mafuriko Morogoro wahanga waliishia kusikia redioni michango ambayo haikuwafikia.

Waziri Mkuu atueleze. Matumizi ya fedha za dharurq na majanga chini ya ofisi yake zimetumikqje tangu aingie ofisini?

Kweli ITATUWEKA HURU
Mkuu hoja zako zinapangana zenyewe kwa zenyewe na umechanganya mambo mengi sana kwenye kitu unachohoji. Kwa Tanzania sijui lakini nachojua ni kwamba kwenye nchi nyingi, kukusanya fedha katika mazingira ya janga kama hili ni lazima uwe na kibali. Nadhani hata Tanzania lazima kuwe na utaratibu maalum. Unaweza kutumia common sense tu na kuona kuwa kwenya majanga yanayohusisha public kama hili, ukiruhusu uchashangishaji wa fedha bila utaratibu maalum unakaribisha ufisadi na utapeli. Waziri mkuu yuko sahihi kabisa.
 
Why are you obsessed with ORDER, have you seen any signs of anarchy?
Kwanza only future of progressive thinkers can be shaped by their past, this doesn't benefit society of sticklers for rules like what you're.
Pili yote ulosema including money laundering ndio tumesema weka control mechanism au auditing.
Tatu uongo serikali sio self sufficient ni mara nyingi tu inaalika michango toka kwa wadau mbalimbali, hata kariakoo kwenyewe kuna wadau wengi tu wasiotoka serikalini PM aliwataja na kuwashukuru, mv Bukoba wadau binafsi walishiriki nk
Unataka kusemaje tena?
Freedom without order is chaos..in everything there must be orders with no regard of anything..provided peace n harmony prevails! control imewekwa, mambo yote ya michango yanaratibiwa chini ya ofisi ya waziri mkuu ili ku-counter check issues zote, utapeli, money laundering nk...utakuwa ni ujinga kudai namna nyingine kuratibu michango kwa wahanga pasina kusema utaratibu uliopo una kasoro gani??? wachangiaji wawepo au wasiwepo serikali itafanya wajibu wake, haimtegemei niffer kuisaidia wala sisi hatumhitaji niffer kukusanya michango..kwa hiyo niffer asipokuwepo..? na niffer asipokusanya michango wewe unakosa nini? tunakataa niffer kukusanya michango kwa sababu tayari upo utaratibu wa kufanya hicho anachokifanya, yeye hahitajiki! pili akiachiwa watatokea wengine kufanya kile kile anachofanya na si lazima wafanye kwa nia njema..ndio maana njia rahisi ni yeye kufahamu haruhusiwi kukusanya michango..labda ya harusi lkn si ya majanga! hope umeelewa, kasome na hiyo sheria..!
 

Attachments

  • SHERIA YA USIMAMIZI WA MAAFA Na. 6 YA MWAKA 2022..pdf.png
    SHERIA YA USIMAMIZI WA MAAFA Na. 6 YA MWAKA 2022..pdf.png
    72.6 KB · Views: 3
Kumuhoji mtu ni mpaka pawe na jambo linalokiuka utaratibu au sheria. Sasa tunachotaka kujua, huyo Niffer kafanya kosa gan au kakiuka utaratibu upi??
Hivi inaingia akilini kuwa janga kama hili mtu binafsi ajitokeze na kuanza kuchangisha fedha bila kibali? Huoni kuna uwezekano mkubwa wa fedha kutumika vibaya au hata kupigwa? Vitu vingine tuwe tunatumia common sense. Huoni kuwa watu watatumia loophole kama hizi kutapeli?
 
Freedom without order is chaos..in everything there must be orders with no regard of anything..provided peace n harmony prevails! control imewekwa, mambo yote ya michango yanaratibiwa chini ya ofisi ya waziri mkuu ili ku-counter check issues zote, utapeli, money laundering nk...utakuwa ni ujinga kudai namna nyingine kuratibu michango kwa wahanga pasina kusema utaratibu uliopo una kasoro gani??? wachangiaji wawepo au wasiwepo serikali itafanya wajibu wake, haimtegemei niffer kuisaidia wala sisi hatumhitaji niffer kukusanya michango..kwa hiyo niffer asipokuwepo..? na niffer asipokusanya michango wewe unakosa nini? tunakataa niffer kukusanya michango kwa sababu tayari upo utaratibu wa kufanya hicho anachokifanya, yeye hahitajiki! pili akiachiwa watatokea wengine kufanya kile kile anachofanya na si lazima wafanye kwa nia njema..ndio maana njia rahisi ni yeye kufahamu haruhusiwi kukusanya michango..labda ya harusi lkn si ya majanga! hope umeelewa.
I can't consume your word salads, no but thanks. You wrote A whole lot paragraph without saying anything of substance, rather than repeating yourself.
 
1. Kukitokea maafa/janga la kitaifa, usichangishe fedha. Sheria ya usimamizi wa maafa ya mwaka 2022, kifungu cha 26(2) inasema jukumu la kuchangisha litafanywa na Kamati ya maafa iliyo chini ya ofisi ya Waziri mkuu, kupitia akaunti maalumu.

2. Ukichangisha fedha kwa matatizo mengine ambayo si maafa (eg matibabu, elimu, yatima) usitumie namba/akaunti binafsi. Ni kosa kisheria. Tumia taasisi (NGO) iliyosajiliwa.

Kwa mujibu wa Sheria ya NGO namba 24 ya mwaka 2002, kifungu cha 32, michango ya kibinadamu (charitable initiatives) inaratibiwa na mashirika yaliyosajiliwa na sio mtu binafsi. Lengo la sheria ni kuweka "Check & Balance" ili kudhibiti ubadhirifu kwa sababu NGO inafanyiwa auditing angalau mara 2 kwa mwaka (internal & external).

3. Kama unataka kumsaidia mtu na huna NGO, tumia namba za mhusika mwenyewe, lakini kwanza upate kibali kutoka ofisi ya Mkuu wa wilaya. Kifungu cha 122 cha sheria ya serikali za mitaa ya mwaka 1982 inataka michango inayokusanywa na mtu binafsi kwa ajili ya "charity" ipate kibali kwa DC.

#Swali: Je watu wanafahamu haya?

#Jibu: Hapana. Kuna watu wanachangisha pesa kwa nia njema kabisa (utmost good faith) lakini hawajui utaratibu wa kisheria ulivyo.

#Swali: Je nini kifanyike?

#Jibu: Wapewe elimu. Hawapaswi kutishwa, kubezwa au kukatishwa tamaa. Kama mtu amechangisha fedha kupitia akaunti yake binafsi ili aokoe maisha ya mgonjwa kwanini umshtaki? Ni kweli hajafuata utaratibu lakini kafanya jambo jema. Kwahiyo kunaweza kuwa na "actus reus" lakini kusiwe na "mens rea" na hivyo ikawa ngumu kuestablish jinai.

#Points3ZaKukariri;
1. Michango ya maafa/majanga inakusanywa na serikali tu.

2. ⁠Michango ya "charity" inakusanywa na taasisi/NGO iliyosajiliwa na inayowasilisha auditing report wizarani.

3. ⁠Ukitaka kuchangisha na huna NGO tumia namba/akauti za mhitaji mwenyewe kwa kibali cha DC.

#UshauriKwaSerikali: Watanzania wanapendana sana, lakini wengi hawana imani na serikali kuhusu michango. Wanakumbuka kuchangia wahanga Kagera pesa zikabadilishwa matumizi. Kwahiyo tumieni watu wenye ushawishi kuhamasisha (eg wasanii, viongozi wa dini, wanamichezo, wanahabari etc).!

copy and pasted kutoka kwa ukurasa wa instagram wa Malisa GJ
Umecopy na kupaste, Lakini somo limeingia! Hongera mkuu.
 
Back
Top Bottom