dr namugari
JF-Expert Member
- Nov 19, 2022
- 10,466
- 18,206
2014 nilikuwa afsa katka bank hiyo huko tabora
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Huenda na mhimili wa mahakama ungeongozwa na mwanamke, na yeye ungemtaja; uwongo?View attachment 2805767
MS Ruth Zaipuna Mkurugenzi Mkuu NMB.
======
Wasalaam Jf team,
Waswahili tunasema " Mnyonge Mnyongeni lakini haki yake Mpeni "
Sote tunakumbuka baada ya NBC Bank kuvunjwa Mwaka 1997 na baadae kuanzishwa kwa Benki mpya ya Makabwera ya NMB na baadae Benki hiyo kubinafsishwa kwa Rabobank ya Uholanzi iliyomiliki hisa asilimia 49 na Rabo baadae kumuuzia baadhi ya Shea Arise,
Wakati wote NMB PLC imekuwa ikiongozwa na watu kutoka nje ya nchi tu isipokuwa huyu Mkurugenzi wa Sasa Bi Ruth Zaipuna aliyekabidhiwa nafasi hiyo ya Ukurugenzi Mkuu rasmi mwaka 2020.
Kumbukumbu zinaonesha wakati mama huyu anaingia madarakani NMB bank ilikuwa na matawi yapatayo 100 tu nchi nzima na ATMs zipatazo 500 nchi nzima.
Leo NMB bank imefikisha matawi zaidi ya 230 na ATMs zaidi ya ATMs 1,000 na mawakala zaidi 12,000 nchi nzima hii ni sawa na kusema mama huyu ameikuza bank hii ya Makabwera kwa zaidi ya marambili, yaani ukuaji wa 100% au kwa lugha rahisi ni sawa na kusema NMB bank PLC imefika katika Kila Jimbo la Uchaguzi la kiserikali haba bara.
Kutoka katika tovuti ya NMB taarifa zinaonesha NMB bank ilikuwa na wateja wasiozidi 600,000 miaka kumi iliyopita na wakati huu wa Ruth Zaipuna banki hii imefikia wateja zaidi ya 6M nchi nzima,karibu mara kumi zaidi.
Kuhusu Uzalendo & Uzawa Kunajambo la kujifunza kwa hawa wanawake watatu yaani Rais Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan, Spika wa bunge la JMT na IPU Mhe Dkt Tulia Aksoni na Mkurugenzi Ruth Zaipuna kwa namna wanavyoleta mabadiliko ya kasi kwenye taasisi wanazoziongoza,
Hebu tazama orodha hii ya faida kwa mabenki kumi ya Tanzania yaliyofanya vizuri katika robo ya tatu tu ya mwaka huu wa 2023 ndio utaelewa vizuri nachosema kuhusu huyu Mkurugenzi.
1. NMB Bank: TZS 398 billion
2. CRDB Bank: TZS 280 billion
3. Stanbic Bank: TZS 95 billion
4. StanChart: TZS 64 billion
5. NBC Bank: TZS 62 billion
6. Citibank TZS 44 billion
7. PBZ TZS 41 billion
8. Exim Bank TZS 40 billion
9. Absa Bank TZS 37 billion
10. KCB Bank TZS 35 billion
Taarifa zinaonesha faida ya Jumla kwa mabenki yote Tanzania ni shilingi trilioni moja katika robo hii ya tatu, Hii ni sawa na kusema NMB PLC pekee anamiliki 40% ya faida yote huku ikimpiku kwa mbali mshindani wake wa karibu CRDB bank kwa zaidi ya TZS 118 BL sawa na 70% ya faida yake.
Wakati Ruth Zaipuna anakuwa Mkurugenzi Mkuu Benki hii ilikuwa na wastani wa faida ya TZS 200BL baada ya kodi wakati Leo faida imekuwa na kufikia wastani wa karibu TZS 400BL kwa mwaka yaani sawa na marambili zaidi.
Pia, taarifa zinaonesha Benki ya NMB inashika nafasi ya sita kwa Ukubwa katika nchi zote Kusini mwa jangwa la Sahara na ndio Benki pekee toka Tanzania inayoshindana kimataifa katika ukubwa wa Biashara.
Watanzania tuna la kujivunia toka kwa Mkurugenzi huyu mzawa akisaidiwa na management nzima ya NMB PLC pamoja na Bodi ya Wakurugenzi wa NMB PLC chini ya Dkt Edwin Mhede, Hakika Mmestahili Heshima.
Kwa msiofahamu Mwaka 2021, Benki ya NMB chini ya Ruth Zaipuna ilitambuliwa na kutunukiwa tuzo saba za kimataifa
ikiwemo tuzo ya Euromoney ya Ubora, ikiitambua benki ya NMB kama Benki
bora Tanzania (kwa miaka tisa mfululizo) na tuzo kutoka Jarida la Global
Finance ikiitambua benki ya NMB kama benki salama zaidi Tanzania.
Pia mwaka 2021, benki ya NMB ilitambuliwa na kupewa tuzo na Mamlaka ya
Mapato Tanzania (TRA) ikiitambua kama mlipa kodi mkubwa zaidi kwenye
sekta ya fedha na pia mlipa kodi mkubwa namba tatu kwa ujumla nchini hii ni chini ya Ruth Zaipuna.
Kwa matokeo haya, Huenda Ukimwacha Rais Dkt Samia na Spika Dkt Tulia mwingine ni huyu Ruth Zaipuna wa NMB PLC deserves better.
Hizi benki Nmb na Crdb zinaongoza sio kwa sababu ya akili za mtu bali ndio zinazoongoza kumpokea mishahara ya wafanyakazi wa umma na binafsi hii ndio sababu kuu.View attachment 2805767
MS Ruth Zaipuna Mkurugenzi Mkuu NMB.
======
Wasalaam Jf team,
Waswahili tunasema " Mnyonge Mnyongeni lakini haki yake Mpeni "
Sote tunakumbuka baada ya NBC Bank kuvunjwa Mwaka 1997 na baadae kuanzishwa kwa Benki mpya ya Makabwera ya NMB na baadae Benki hiyo kubinafsishwa kwa Rabobank ya Uholanzi iliyomiliki hisa asilimia 49 na Rabo baadae kumuuzia baadhi ya Shea Arise,
Wakati wote NMB PLC imekuwa ikiongozwa na watu kutoka nje ya nchi tu isipokuwa huyu Mkurugenzi wa Sasa Bi Ruth Zaipuna aliyekabidhiwa nafasi hiyo ya Ukurugenzi Mkuu rasmi mwaka 2020.
Kumbukumbu zinaonesha wakati mama huyu anaingia madarakani NMB bank ilikuwa na matawi yapatayo 100 tu nchi nzima na ATMs zipatazo 500 nchi nzima.
Leo NMB bank imefikisha matawi zaidi ya 230 na ATMs zaidi ya ATMs 1,000 na mawakala zaidi 12,000 nchi nzima hii ni sawa na kusema mama huyu ameikuza bank hii ya Makabwera kwa zaidi ya marambili, yaani ukuaji wa 100% au kwa lugha rahisi ni sawa na kusema NMB bank PLC imefika katika Kila Jimbo la Uchaguzi la kiserikali haba bara.
Kutoka katika tovuti ya NMB taarifa zinaonesha NMB bank ilikuwa na wateja wasiozidi 600,000 miaka kumi iliyopita na wakati huu wa Ruth Zaipuna banki hii imefikia wateja zaidi ya 6M nchi nzima,karibu mara kumi zaidi.
Kuhusu Uzalendo & Uzawa Kunajambo la kujifunza kwa hawa wanawake watatu yaani Rais Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan, Spika wa bunge la JMT na IPU Mhe Dkt Tulia Aksoni na Mkurugenzi Ruth Zaipuna kwa namna wanavyoleta mabadiliko ya kasi kwenye taasisi wanazoziongoza,
Hebu tazama orodha hii ya faida kwa mabenki kumi ya Tanzania yaliyofanya vizuri katika robo ya tatu tu ya mwaka huu wa 2023 ndio utaelewa vizuri nachosema kuhusu huyu Mkurugenzi.
1. NMB Bank: TZS 398 billion
2. CRDB Bank: TZS 280 billion
3. Stanbic Bank: TZS 95 billion
4. StanChart: TZS 64 billion
5. NBC Bank: TZS 62 billion
6. Citibank TZS 44 billion
7. PBZ TZS 41 billion
8. Exim Bank TZS 40 billion
9. Absa Bank TZS 37 billion
10. KCB Bank TZS 35 billion
Taarifa zinaonesha faida ya Jumla kwa mabenki yote Tanzania ni shilingi trilioni moja katika robo hii ya tatu, Hii ni sawa na kusema NMB PLC pekee anamiliki 40% ya faida yote huku ikimpiku kwa mbali mshindani wake wa karibu CRDB bank kwa zaidi ya TZS 118 BL sawa na 70% ya faida yake.
Wakati Ruth Zaipuna anakuwa Mkurugenzi Mkuu Benki hii ilikuwa na wastani wa faida ya TZS 200BL baada ya kodi wakati Leo faida imekuwa na kufikia wastani wa karibu TZS 400BL kwa mwaka yaani sawa na marambili zaidi.
Pia, taarifa zinaonesha Benki ya NMB inashika nafasi ya sita kwa Ukubwa katika nchi zote Kusini mwa jangwa la Sahara na ndio Benki pekee toka Tanzania inayoshindana kimataifa katika ukubwa wa Biashara.
Watanzania tuna la kujivunia toka kwa Mkurugenzi huyu mzawa akisaidiwa na management nzima ya NMB PLC pamoja na Bodi ya Wakurugenzi wa NMB PLC chini ya Dkt Edwin Mhede, Hakika Mmestahili Heshima.
Kwa msiofahamu Mwaka 2021, Benki ya NMB chini ya Ruth Zaipuna ilitambuliwa na kutunukiwa tuzo saba za kimataifa
ikiwemo tuzo ya Euromoney ya Ubora, ikiitambua benki ya NMB kama Benki
bora Tanzania (kwa miaka tisa mfululizo) na tuzo kutoka Jarida la Global
Finance ikiitambua benki ya NMB kama benki salama zaidi Tanzania.
Pia mwaka 2021, benki ya NMB ilitambuliwa na kupewa tuzo na Mamlaka ya
Mapato Tanzania (TRA) ikiitambua kama mlipa kodi mkubwa zaidi kwenye
sekta ya fedha na pia mlipa kodi mkubwa namba tatu kwa ujumla nchini hii ni chini ya Ruth Zaipuna.
Kwa matokeo haya, Huenda Ukimwacha Rais Dkt Samia na Spika Dkt Tulia mwingine ni huyu Ruth Zaipuna wa NMB PLC deserves better.
Ha ha ha!Wewe Jidu La Mabambasi Sio Kila sehemu ni Siasa tu kaka jaribu kuwa na adabu na watu serious kama hawa. Truest me ,In a Bank you can't temper even with a single coin.
Duuh,Ha ha ha!
Mgejua tu, Banks in Tz are the riskiest kuweka amana yako.
Wafanyakazi wa mabenki wanapiga deal zisizo na kawaida.
Bahati yao ni kwamba since wana deal na cash isiyo yao, wana a big margin ya faida, wanaweza ku cover wizi wote unaoendelea ndani ya benki.
Mfumo wetu wa kifisadi utawaangusha, wabaki tu na taaluma na kazi zao huko walipo, nidhamu serikalini inapaswa kurejea kwa kiwango cha juu sana ndo unaweza kuwatumia wataalamu hawa, wanaoibua madudu kama prof assad ndio wanatengenezewa zengwe na kuondolewa, nchi ya ajabu sana hiiKuna vichwa pale NMB ni balaa ukiacha ZAIPUNA Kuna kichwa kinaitwa MPONZI Jamaa mmoja hivi ana upara ni hatari. Kuna DONATUS Richard mkuu wao wa biashara yaani wapo creative balaa I wish hivi vichwa vije vimsaidie mama kwenye uchumi pia vipewe uhuru wa kufanya kazi aiseee tutatoboa
Akichaguliwa kuwa mbunge wa viti maalum na kisha kupewa huo uwaziri wa fedha akatae?Hongera sana Mama Ruth, ila sije ukathubutu kuingia kwenye siasa utaharibu profession yako, naona wengine humu wanatamani uwe waziri wa fedha
Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
Akatae tu, hamjayaona yaliyowatokea wakina prof assad na wengineAkichaguliwa kuwa mbunge wa viti maalum na kisha kupewa huo uwaziri wa fedha akatae?
Aende ili kulisaidia TaifaAkichaguliwa kuwa mbunge wa viti maalum na kisha kupewa huo uwaziri wa fedha akatae?
Huenda Jemedari ameliona hili!Aende ili kulisaidia Taifa
Imeenda hii😆😆Huenda Jemedari ameliona hili!
ATM na branches bado ni muhimu Kuna watu hawawataki kabisa mawakala na branch kwaajili ya deposit na withdraw kubwa kubwa na opinng ya akauntKuna vitu nimeviona
1. She is competent, NO QUESTION
2. Idadi ya matawi na ATMs zilizofunguliwa haziko sawa kama ulivyozitaja taking into consideration that huduma nyingi sana kwa sasa zinaweza kufanywa na agents kwa gharama nafuu Banks zinapigania kupunguza gharama Kwa ku push huduma za kawaida za kibenki kumalizwa na Agents. Hivyo sio fahari tena kwa Banks kujinasibu kwa kufungua matawi mengi na ATM
ukichunguza sana kwa Jiji kama Dsm utaona baadhi ya maeneo ATM za Nmb hazipo Tena
3.Ukiangalia qualifications za Board Members 80% ni watu wenye background za IT ukijumlisha na umaridadi wa Banking Software za Nmb vinambeba CEO
Kuna uwezekano mkubwa kutokana na software nzuri end of day's work inakuwa observed mpaka Rabobank/Netherland
4. Tatizo la Crdb kuwa na ONLY ONE MAN SHOW (Kimei) limeinyanyua Nmb baada tu ya Kimei kustaafu ndio Nmb ilianza kufurukuta. Alikuwa hodari sana kufanya lobbying kwa Government institutions na mashirika makubwa
5. Magu na Hisia za Uchaga
Inasemekana Magu alikuwa amenuwia kuvunja Chaga group zilizotamalaki TRA, Bandari na CRDB
ambayo ilianza na Kimei, hii kwa kiasi fulani hata wateja wakubwa nao kuhama hama
CRDB bado sana kwa hawa NMB kwasababu NMB imejengwa kwenye msingi wa MicrocleintsKuna vitu nimeviona
1. She is competent, NO QUESTION
2. Idadi ya matawi na ATMs zilizofunguliwa haziko sawa kama ulivyozitaja taking into consideration that huduma nyingi sana kwa sasa zinaweza kufanywa na agents kwa gharama nafuu Banks zinapigania kupunguza gharama Kwa ku push huduma za kawaida za kibenki kumalizwa na Agents. Hivyo sio fahari tena kwa Banks kujinasibu kwa kufungua matawi mengi na ATM
ukichunguza sana kwa Jiji kama Dsm utaona baadhi ya maeneo ATM za Nmb hazipo Tena
3.Ukiangalia qualifications za Board Members 80% ni watu wenye background za IT ukijumlisha na umaridadi wa Banking Software za Nmb vinambeba CEO
Kuna uwezekano mkubwa kutokana na software nzuri end of day's work inakuwa observed mpaka Rabobank/Netherland
4. Tatizo la Crdb kuwa na ONLY ONE MAN SHOW (Kimei) limeinyanyua Nmb baada tu ya Kimei kustaafu ndio Nmb ilianza kufurukuta. Alikuwa hodari sana kufanya lobbying kwa Government institutions na mashirika makubwa
5. Magu na Hisia za Uchaga
Inasemekana Magu alikuwa amenuwia kuvunja Chaga group zilizotamalaki TRA, Bandari na CRDB
ambayo ilianza na Kimei, hii kwa kiasi fulani hata wateja wakubwa nao kuhama hama
Nadhani kama Taifa lazima tuitumie zaidi resources yetu ya ndaniTunamtaka Ruth Serikalini haraka tukuze uchumi wetu
Wasiwasi wangu huyu hawezi kukubali kwenda Serikalini.Nadhani kama Taifa lazima tuitumie zaidi resources yetu ya ndani
But kwa uwezo wake Serikalini atasaidia watu wengi zaidi kuliko bankWasiwasi wangu huyu hawezi kukubali kwenda Serikalini.