Ni ubora gani unauona ktk awamu ya tano tofauti na awamu zote zilizo pita za uongozi wa juu wa nchi yetu ya Tanzania?
Awamu ya tano hata miaka miaka miwili haijafikisha bado.
Itakuwa si haki kuilinganisha na awamu zingine za uongozi wa nchi yetu.
So for me the jury is still out.
Walau ikikaribia kufikisha miaka mitano ikiwa madarakani ndo nitaweza kutoa a more balanced verdict.
Ngoja niwape muda kidogo....
Angali bado ni raia halali mwenye uraia wa nchi moja Tz( kama kweli). Unashirikije ktk prosperity ya nchi yako Tz?
Nalipa kodi.
Pia nasaidia watu wengi sana hususan ndugu wa karibu na hata wa mbali.
Ni taasisi ipi ya kiserikali au mfumo gani was kiserikali unaamini unatakiwa reform ya lazima na haraka hapa Tz?
Duh!
Sehemu na nyanja za kiserikali zinazohitaji mabadiliko ni nyingi sana.
Kuna mfumo wa elimu, afya, utoaji haki, uchukuzi, makusanyo ya mapato, na mengineyo mengi tu.
Nchi nzima inahitaji mageuzi.
Ila kama ni kuchagua moja basi naweza kusema ni mfumo wa utoaji haki.
Watu wenye kipato cha chini hususan kwenye mahakama za mwanzo huko huwa wanataabika sana.
Nalijua hilo, nimeshuhudia kwa macho yangu jinsi wanavyotaabika. Ningependa kuona mabadiliko ya kweli ili watu wapate haki zao wanazostahili.
Kulazimishwa au kuona kama unalazimika kuinunua haki iliyo yako ni jambo baya sana.
Haki siyo bidhaa. Haki ni haki. Haipaswi kununuliwa.
Ulisema ulisoma secondary, kama ulisoma Tz unaionaje elimu ya public schools kipindi unasoma na kipindi cha sasa?
Siwezi kulinganisha wakati wangu na sasa hivi kwa sababu sasa hivi sisomi tena.
Lakini nachoona sasa hivi ni rahisi zaidi kusoma/ kujifunza kuliko ilivyokuwa enzi nasoma.
Sasa hivi mtu huhitaji hata kwenda maktaba.
Mambo yote yapo kiganjani.
Sasa hivi hakuna kabisa sababu ya mtu kufeli [kama mambo mengine yako sawa].
Ni jambo gani la lazima ambalo ukikutana ungependa umshauri/ kumuomba raisi kuhusu nchi na ujumla wake?
Ningemwomba awe mfano mzuri wa uwazi katika matumizi ya pesa za walipa kodi na kutuambia tunamlipa mshahara kiasi gani.
Pia nitamwomba awashauri wabunge watunge sheria ya uwazi kuhusu malipo ya viongozi wote, sheria itakayolazimisha malipo ya viongozi wa umma yanakuwa ni public information.
Umekuwa big fan wa lugha ya kingereza hasa unakiandika kwa ufasaha.
Hata kuongea naongea kwa ufasaha sana. Juzi nilikuwa naongea na jamaa mmoja kutoka Ireland na nilipomwambia natoka Tanzania akashangaa sana kwa sababu naongea Kiingereza vizuri mno. Kwa hiyo siyo kuandika tu.
Je unahisi ni kusoma kama somo, au lugha ya kusomea na kusomeshwa au kutokana na matumizi ya kila siku ughaibuni?
Ni mchanganyiko wa mambo mengi.
Nikiwa mdogo kabisa, yaani nilipoanza kuongea, nyumbani wazazi walikuwa wananiongelesha kwa lugha mbili. Kiingereza na Kisukuma.
Walitaka nizijue hizo lugha tokea utotoni kabisa ili kurahisisha kuzimudu huku ukubwani. Na matokeo yake ndo hayo sasa. Najua Kiswahili, Kiingereza, na Kisukuma.
Unawezaje kuzungumzia brain drainage inayofanyika ktk nchi yetu kupitia shule binafsi hasa za kimataifa. Ambazo haziwaandai next generation kufit ktk mazingira ya Tz bali yale ya ughaibuni?
Brain drainage ndo nini? Sijawahi kabisa kuisikia hiyo. Hivyo kabla sijajibu naomba nifahamishe ni kitu gani ili hata nikijibu nijue ulichoniuliza ni nini.
Ahlan wa sahlan.