Nyani Ngabu Mjengoni! Interview: Mapenzi, Utajiri&Mali, Marafiki na Maisha ya ugenini.

Nyani Ngabu Mjengoni! Interview: Mapenzi, Utajiri&Mali, Marafiki na Maisha ya ugenini.

NN
I'm interested in knowing your tribe,

My intelligent guess is Pare,
Prove me wrong brother kaka!

I don't need to prove you wrong when you are already dead wrong.

I am a Sukuma. 100% Sukuma.
 
Kumekuwa na hali iliyoanza kujitokeza hivi karibuni kuwa watu wanaodhaniwa na wengine kubainika kuwa wanayoka mkoa mmoja, jamii rafiki na raisi kuanza kutetea kingozi yyte wa kiserikali anayetoka ktk mazingira

Well, sijui kuhusu wengine lakini mimi binafsi sina kabisa mambo ya ukabila.

Sijawahi kumtetea kiongozi yeyote yule kwa sababu tu eti naye ni Msukuma.

Mheshimiwa Paul Makonda nimeshamchana sana humu.

Mheshimiwa rais naye vivyo hivyo.

Wewe hujawahi kuona nikiwachana hao wawili?
 
Kweli uko sahihi ulipo mjibu mkuu swali alilokuuliza kuhusu wazungu kama wanatabia kama zetu za kiswahili,mfano kwenye hiyo video hapo madada wanapigana lakini hizo njemba haziamuulii Bali wana tumia simu zao kuchukua tukio

Tabia hazina kabisa rangi.
 
Aaah trainer!
Now this is you (sneakers and perfumes hahaha)
Mafanikio ni kupata na kuwa na kile ukitakacho na kukifurahia.



1. Kisura wangu. Kumkuza na kumwona naye anafikia ndoto zake [na atazifikia tu maana ana akili sana na ni mjanja hata kunizidi].

2. Uhakika wa kula chakula nikipendacho, kuwa na sehemu nzuri ya kuishi, kuwa na afya njema, na furaha moyoni.

3. Kuendelea kuziongeza ziro kwenye akaunti zangu za benki.



Kwangu mafanikio ni suala endelevu na kwa sababu hiyo halina kikomo.

Na kwa sababu halina kikomo nachoweza kusema tu kwa sasa nafurahia mahali nilipo.

Kwa mfano, hata sasa hivi hapa nikiamua kwenda kununua jozi ya sneakers za Philipp Plein [ PHILIPP PLEIN: La Dernière Boutique en Ligne Mode de Luxe - Site Officiel | Philipp Plein ]naweza bila ya kuwa na wasiwasi wowote ule.

Nikiamua niende St. Thomas huko kupunga upepo naweza kwenda bila ya kuwa na wasiwasi wowote ule.

Nilicho nacho kwa sasa kinanitosha kuyafurahia maisha.
 
Haya sasa zamu yangu mimi..
Braza Nyani Ngabu heshima yako mkuu..

Heshima mbele na ikurudie nawe pia.

Mm napenda unijibu maswali ya ngu kwa kina sio kwa mkato ndio nitaelewa.
Nyani Ngabu.

Haya twende kazi...

Uliifahamu vp JF na ulijiunga lini humu?

Nilijiunga lini humu? Mbona hilo ni rahisi sana kulijua...

Ingia tu kwa profile yangu na utaona nilijiunga lini.

JF niliifahamu kupitia wanachama wenzangu tuliokuwa nao bcstimes.com...

Kwanini ulijiita nyani ngabu na lina maana gani hili jina?

Ilikuwa ni mwaka 2005 huko bcstimes.com..

Kuna jamaa alikuwa anajiita Njabu Ngabu [siku hizi humu anajiita Ndjabu Ngabu au Bucktooth Maftah].

Pia alikuwepo jamaa mmoja hivi alikuwa anajiita Raj Patel.

Raj Patel alikuwa anawachana sana Waafrika.

Sasa siku moja yeye na Ndjabu Ngabu wakawa wanarushiana maneno kwenye moja ya mijadala.

Ndo Raj Patel akamjibu Ndjabu Ngabu kwa kumuita 'Nyani Ngabu' [aliligeuza Ndjabu na kuwa Nyani..yaani kama tusi flani hivi].

Nilipooana Raj kafanya hivyo nikacheka sana. Ndo nami nika sign up kwa hilo jina la Nyani Ngabu.

Basi tokea siku hiyo ndo nikawa Nyani Ngabu.

Ila 'Ngabu' maana yake ni kifaa kama ile patasi ya useremala.

Lakini pia kuna jamaa mmoja huko Congo alikuwa anaitwa Floribert Njabu Ngabu.

Naamini huyo ndo huyu 'Ndjabu Ngabu' alipolitoa hilo jina.

Huyo kwenye avatar ni nani maana hadi Fb umemuweka huyo.

Huyo no Ronnie Coleman. Ni Mr. Olympia wa zamani.

Una hisa (Share) yoyote JF?

Sina kabisa.

Mara ya mwisho kuja TZ lini?

Februari 2017 na nakuja tena September 2017.

Nitaendelea
[HASHTAG]#Mondray2017[/HASHTAG]

Nitakuwepo!
 
Hahahaa sawasawa.



Mimi ni homebody. Napenda sana kukaa nyumbani. Nikitoka labda naenda gym kupasha misuli halafu narudi zangu nyumbani.

Napendelea zaidi kunywa lemonade.

Kwenye vile vinywaji vya watu wazima napendelea Heineken na viroba vile vya Konyagi.

Sivuti kabisa. Si bangi, si sigara, si crack cocaine.

Mambo ya klabu nilishaachana nayo zamani sana. Hata baa siendagi. Napendelea zaidi kunywa nyumbani. Na hata nikinywa si kunywa ile ya kilevi mbwa.

Nalala muda wowote tu ule. Hata mchana huwa nalala. Siku zingine nalala asubuhi. Ndo raha ya kuishi kwako hiyo. Kwa mama na baba huwezi kulala na kuamka muda wowote utakao wewe. Ukipitiliza wanakuja kukugongea uamke😀.

Ndo maana napenda kuishi kwangu.

Taste yangu ya muziki ni eclectic. Napenda muziki wa aina nyingi ili mradi masikioni mwangu uwe unasikika vizuri.

Napenda nyimbo za Marvin Gaye, Mariah Carey, Jokha Kassim, Mariam Khamis, Ali Kiba, Future, Gucci Mane, Justin Bieber, Shania Twain, Remmy Ongala, na kadhalika.



Napenda kuwa na watu wa aina zote. Wabongo, Waghana, Wanaija, Wajamaica, Wazungu, Wahindi, Waarabu, Wakorea, Walatino...sina kabisa ubaguzi.

Ili mradi mtu awe poa tu [na msafi...sipendi harufu za vikwapa]...sina tatizo naye kabisa.



Hapana kwa kweli.

Nina muda sana sijahudhuria shughuli za Watanzania.

Ninaotembeleana nao ni wachache sana. Hawazidi wawili.



Najua kupika vyakula vingi. Kwa mfano leo nimepika rice noodles zenye binzari. Ngoja baadaye ntaweka picha uone.

Huwa napika wali, maharage ya nazi, makande, mbuzi choma, kuku choma, maini rosti, mchicha, biryani la kuku, mayai ya kukaanga kama jicho la ng'ombe, omelette, maandazi, vitumbua, na vinginevyo.



Ugali siupendi [ajabu kwa sababu mimi ni ngosha] na kwa sababu siupendi hata kujifunza sijataka.

Uji nilikuwa najua lakini sijaupika siku nyingi sana hadi nadhani nitakuwa nishasahau.

Oooh supa na unajibu vizuri sana, nimenogewa kusoma utafikiri nimeshika autobio yako. Labda utakuja kuiandika ya Nyani Ngabu na yote ya humu tangu ujiunge, si ndio?
 
Kuna siku nilikuwa sister office nchini kwa watu. Nikaingia chooni nikipishana na cleaner kwenye corridor. You know those people who would leave traces of Grey matter chooni na hawatumii brush kusafisha? Nikakuta hapo. I had to clean so that the cleaner wouldn't think it was me iwe legacy niliyowaachia.

Well, this is living and other stories.
Imagine unaingia chooni huku watu wanakuona unaingia chooni.....

Hapana aisee...sipendi kabisa.
 
Ustaadh asante kwa shout out, ila we jamaa ni mtata sana, ngoja nicheki na Hance Mtanashati tukuripoti unyanganywe kabisa uplatnumz.

Hahaa...wewe nakukubali sana.

Unanielewa vizuri mno.

Na ndo maana sikumbuki hata kuwahi kukwazana na wewe humu.

Nadhani huwa unajua ninapokuwa serious na ninapokuwa nazingua tu.

I tip my hat off to you ma dude!!

Massive respect.
 
Hahaa...wewe nakukubali sana.

Unanielewa vizuri mno.

Na ndo maana sikumbuki hata kuwahi kukwazana na wewe humu.

Nadhani huwa unajua ninapokuwa serious na ninapokuwa nazingua tu.

I tip my hat off to you ma dude!!

Massive respect.

Am humbled man.

JF watu wengi tukisoma kitu tunakichukulia hivyo hivyo kilivyoandikwa, bila hata kufanya tafakari ya nini mwandishi alichokusudia, ndo pale unakimbilia kutoa hitimisho la uongo.

Ila tungekuwa tunajipa muda wa kuwaza nini mhusika anakusudia, tungeelewa kwamba wakati mwingine ni uchokozi tu.
 
Oooh supa na unajibu vizuri sana, nimenogewa kusoma utafikiri nimeshika autobio yako. Labda utakuja kuiandika ya Nyani Ngabu na yote ya humu tangu ujiunge, si ndio?

Ebana eeh...unaona sasa...

Umenipa wazo zuri sana kwa kweli na nitalifanyia kazi.

Nitaiandika hiyo autobiography ya NN humu...

Shukraaaan nyiiiiiingi sana Coco.
 
huyu nyani ngabu bure kabisa majigambo lakini kichwani mweupe hebu tuletee mama yetu Faizafox uone moto wake.
 
Ebana eeh...unaona sasa...

Umenipa wazo zuri sana kwa kweli na nitalifanyia kazi.

Nitaiandika hiyo autobiography ya NN humu...

Shukraaaan nyiiiiiingi sana Coco.

Karibu sana Ngabu, nimefurahi umeipokea... hiyo itabidi iwe kwenye pdf document pia tuisome hata tukiwa nje ya mitandao. Kila la kheri
 
Mimi naomba kuuliza,

Jina lako (nyani ngabu) linamaana gani?
 
Namna uwezavyo kusimamia na kusemea jambo bila kuacha,
(Mf. Kudai mshahara wa rais ujulikane), ni kitu adimu sana katika nchi hii.
Wengi wetu hatuna huo utashi au uwezo wa hilo. Na hili lina athari za wazi katika jamii yetu.

Je kuna kitu katika mazingira uliyoishi kimekujengea uwezo huo? Tushirikishe.

2. Mimi ni mmoja wa member wa humu ambao husoma vingi na hutoa comment au hoja mara chache. Nafurahia sana kukusoma. Asante kwa muda wako.
 
Kuna Maswali mawili yameulizwa zaidi ya mara 2 unayapotezea, kuhusu maana ya Nyani Ngabu na Avatar yako
 
Back
Top Bottom