Nyani Ngabu Mjengoni! Interview: Mapenzi, Utajiri&Mali, Marafiki na Maisha ya ugenini.

interview nzuri sana
 
Shukrani STUNTER, naiman maswali mengi yameulizwa wacha tusubirie majibu!

nami ntauliza nkitulia.
 
Shukrani STUNTER, naiman maswali mengi yameulizwa wacha tusubirie majibu!

nami ntauliza nkitulia.
Nashukuru sana kwa time yako, jitahidi uulize swali mkuu, tunalisubiria
 
Nyani Ngabu hongera sana kumpata kisura pamoja na kuyafurahia maisha,

Ahsante sana.

Yupo hapa pembeni yangu na anawapa Hi nyote.

Washafunga shule hivyo hana la kufanya zaidi ya kuniganda tu.

Je unaweza kutuambia japo kidogo siri ya mafanikio yako?

Wala hakuna siri ambayo wengine hamuijui.

Ila kwa manufaa ya mjadala naweza kusema ni mambo yafuatayo.

1. Bidii na nidhamu. Hapo kwenye nidhamu namaanisha kujizuia kufuja au kutumia vibaya hela zako. Ubahiri wa kibusara unahusika.

2. You become who you surround yourself with. Watu wanaokuzunguka kama hawana mbele wala nyuma basi nawe utaishia kuwa kama wao tu. Mimi napenda kuji surround na watu wachapa kazi, wenye nidhamu, na wenye maadili ninayoyapenda na yanayoendaa na yangu. Epuka sana kujihusisha na watu wenye 'crabs in the bucket mentality'.

3. A can-do attitude. Huwa sikubali kushindwa kirahisi kama jambo nikilivalia njuga. Huwa naamini naweza kufanya chochote kama nikizielekezea nguvu na akili zangu kwenye kitu.

4. Siogopi sana kukosea. Kukosea ni mwalimu mzuri sana kama una nia ya kujifunza toka kwenye makosa.

5. Nipo jasiri...huwa najisemea kimoyomoyo...kama flani kaweza kwa nini mimi nishindwe?

Na unahisi vijana wengine labda wanakosea wapi hasa ambapo panawakwamisha?

Nadhani wengi wanakosea sana hapo kwenye nidhamu. Huwa wanashindwa vita dhidi ya vishawishi na mwishowe wengine huishia hata kula hela ya mtaji.

Na katika harakati za kiutafutaji ni vitu gani umejifunza ambavyo unaweza kushea nasi japo kidogo?

Usiwe mwepesi wa kuamini watu na usiwe mwepesi wa kufanya maamuzi bila ya kufikiria kwa kina, mapana, na marefu.
 
Unatumia aina gani ya Passport, "Student, Visiting, Working au Personal Business ?

Cc Nyani Ngabu
 
Ndiyo, nimeshawahi.

Kuhusu nilifikia wapi au tulifikia wapi, hayo ni yetu binafsi.

Ahsante kwa swali lako [la kimtego 😀].
Vizuri,
Mwisho unaichukuliaje JF ya sasa hivi na ya kipindi cha nyuma? Kuna mapungufu kwenye michango ya wanachama au imeboreka zaidi?

Kama kawaida comment either yes or no kulingana na jibu lako.
 
Ngoja nijipange nije nikuletee ng'ombe ili nimuoe kisura.... Inabidi niwe mkweo tu, au hauozeshi wala vumbi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…