Nyaraka mpya za Kagoda zawalipua Rostam, Manji

Nyaraka mpya za Kagoda zawalipua Rostam, Manji

Mbona tuliambiwa na seriokali kagoda ni ya jeshi haiguswi, kumbe ni uwongo, my GOD.
 
Mbona watu wengi tu huenda kufunguwa kesi za jinai polisi? kama hana ushahidi wa kutosha hata huy dpp atamshitaki nani? wewe umeona kuna ushahidi hapo wa kumshitaki mtu ukashinda?

Besides, nakubaliana na wewe kuwa kesi za EPA si za jinai kama wengi wanavyotaka ziwe
. EPA ni madeni na kesi zake ni za madai na si za jinai. Ukilielewa hilo hapo ndio utajuwa kuwa Kikwete alipowataka waliochukuwa hizo pesa wazirudishe wenyewe, alifanya jambo la maana sana. Kwani ni wazi kabisa hizo ni kesi za madai na ukizifanyia papara kuzipeleka mahakamani unaweza kujikuta kuwa kesi inakuwa dragged kwa muda mrefu sana kiasi kuwa inakutia hasara zaidi na mwisho wake fedha usizipate na kesi ukashindwa.

Haya ya Kumtafuta RA na YM ni majungu tu, hakuna kesi hapo ni wajanja wachache wanajitafutia umaarufu. Na wajinga wengi wanaamini hapo kuna kesi. Nashangaa sana.

Dada faiza, issue ya EPA si madai kama unavyosema. fedha za EPA zilipatikana kwa udanganyifu (Fraud) na hakuna maelezo ya kujitosheleza kutoka BOT wala makampuni yaliyochota fedha hizo i.e. Kagoda, Deep green etc.

Kwa hivyo basi ni jinai mbele ya macho ya sheria na hiki ndicho kilicho mgharimu marehemu Barali(kama kweli alikufa) kufukuzwa kazi na mzee wa kaya. tumeona wahindi wengine wakishitakiwa kwa makosa ya kula njama, kughushi na kujipatia fedha hizo za EPA kwa njia ya udanganyifu. je hatua hizo zote unazihusisha na kesi ya madai? una ushaidi gani kama yasemwayo ni majungu?

Do you have any social or political interest with RA &YM? lastly, let us appreciate the work of which this guy have shown and it mark the good beginning......
 
Mbona tuliambiwa na seriokali kagoda ni ya jeshi haiguswi, kumbe ni uwongo, my GOD.

Na aliyesema ni Waziri Mkuu Pinda kuwa "tukiyachokonoa haya, nchi haitayawalika"
 
Faiza kesi huwa hazifunguliwi polisi. Kesi zinafunguliwa mahakamani. Unapoenda polisi unaenda kuripoti au kulalamikia tukio ili polisi wafanye uchunguzi na kuchukua hatua zaidi. Wakishamaliza uchunguzi wao na kuona kuna ushahidi wa kumfungulia mtuhumiwa kesi mahakamani then wanapeleka faili kwa DPP ili afanye hivyo. Ukienda polisi kuripoti issue za madai sijui kama watakusaidia.

Umesema kuwa EPA ni madeni na kesi zake ni za madai na si za jinai. Sasa vipi mtu akigundulika kuwa alitumia jina au kampuni bandia kupata hela za EPA, utamfungulia kesi ya mada au ya jinai? Hata kama ingelikuwa tuhuma na kesi za EPA ni za madai, Msemakweli ataenda kushtaki kama nani? Anamdai nani?

Kuhusu swali lako kama naona kuna ushahidi wa kumshitaki mtu na kushinda, mie bado sijafika huko. Besides tumeambiwa kuna ushahidi zaidi ya uliowekwa hapa, so ni vigumu kutoa a definitive answer.


Naona unashindwa kabisa kunielewa. Kesi nyingi sana zinafunguliwa polisi na wao wanzipeleka mbele kusikilizwa, mfano mtu akikuibia na ushahidi wote unao, unaenda mahakamani moja kwa moja? si unaenda kumshitaki kituo chapolisi na hata taarifa za wizi huwa zinapelekwa polisi. Tafadhali sana kwa hilo usitake tubishane. Nakushangaa sana.

Hayo ya msemakweli ndio hayo hayo nnayosema mimi, hana cha kushitaki wala hajui cha kushitaki wala hana ushahidi wa kushitaki na ndio maana kapeleka huo anaouita "ushahidi" kwa DPP na halafu aka leak huo "ushahidi" wake ili aonekane kafanya kitu. Soma posts zangu za mwanzo utanielewa.
 
Huo wote ni ushahidi "circumstantial" na sio "solid" na ndio maana si Msemakweli wala Msemauongo wanaoweza kushitaki wao wenyewe na wanaupeleka kwa DPP, kwani wanajuwa kwa ushahidi kama huo, wakishindwa kesi! wanafilisiwa. Kwani hao watu unao "wapeleka" mahakamani dau lao ni kubwa.

Faisa inawezekana kweli ukawa ni "circumstantial" rather than "direct" evidence lakini circumstantial evidence unakubalika mahakamani. Kama shahidi akisema alimwona mtuhumiwa akimchoma kisu marehemu, then huo utakuwa ni ushahidi wa moja kwa moja. Lakini akisema alimwona mtuhumiwa akiingia kwenye nyumba ya marehemu, akasikia merehemu akipiga kelele halafu alimwona mtuhumiwa akitoka ndani ya nyumba ya marehemu na kisu chenye damu, then huo ni circumstantial evidence.

Kwa mfano forensic evidence ni circumstantial. Expert evidence ni circumstantial. Na zote zinakubaliwa mahakamani. Ukweli ni kwamba, kwenye kesi nyingine ni vigumu kupata ushahidi wa moja kwa moja. Faiza, it is the necessity for inference, and not the obviousness of a conclusion, that determines whether or not evidence is circumstantial.
 
Niko hom nachek taarifa ya habari ya ITV kuna mdau mmoja amejitokeza na ametaja wezi waliousika kwenye ile skendo ya Epa na Kagoda. Kama mmemuona mtagundua kwamba ni wa2 wachache sana wenye uwezo huo. Je watamuacha hai hata akatoe huo ushahidi mahakamani,? Maana jamaa yupo tayari kutoa ushahidi mahakamani. Amesema ana mpaka videos na sauti ambazo ni ushahidi unaotosha kabisa.
Wanajf 2muungeni mkono huyu mwanaharakati kwa sababu pesa hizo ni za watanzania.
 
mkuu amewataja kina nani? manake nimeona image tu bila sauti,hujuma za eid.
 
Naona unashindwa kabisa kunielewa. Kesi nyingi sana zinafunguliwa polisi na wao wanzipeleka mbele kusikilizwa, mfano mtu akikuibia na ushahidi wote unao, unaenda mahakamani moja kwa moja? si unaenda kumshitaki kituo chapolisi na hata taarifa za wizi huwa zinapelekwa polisi. Tafadhali sana kwa hilo usitake tubishane. Nakushangaa sana.

Hayo ya msemakweli ndio hayo hayo nnayosema mimi, hana cha kushitaki wala hajui cha kushitaki wala hana ushahidi wa kushitaki na ndio maana kapeleka huo anaouita "ushahidi" kwa DPP na halafu aka leak huo "ushahidi" wake ili aonekane kafanya kitu. Soma posts zangu za mwanzo utanielewa.

Faisa nimekuelewa vizuri kabisa. Mantiki yako ni kwamba kesi huwa zinafunguliwa polisi. Mantiki yangu ni kuwa kesi huwa zinafunguliwa mahakamani. Polisi wanachunguza tukio wakiridhika na ushahidi wanapeleka faili kwa DPP ili atumie mamlakaka yake ya kufungua kesi. Hakuna mahakama kwenye vituo vya polisi. Nafikiri tatizo hapa lipo kwenye matumizi ya neno "kesi". Zamani wakati tukiwa na wanasheria wachache, DPP ali delegate mamlaka fulani kwa polisi kuendesha kesi mahakani. Sidhani kama bado ndivyo ilivyo.

Kuhusu mtu akikuibia na ushahidi wote unao, unaenda mahakamani moja kwa moja? Simply, huwezi kwenda mahakamani mwenyewe kwa sababu wewe sio Jamhuri. Katika makosa ya jinai Jamhuri ndio yenye mamlaka ya kumshitaki mtuhumiwa. Wewe utakuwa shahidi tuu. Unapoenda kulalamika polisi, wao wanachunguza kama tuhuma zako ni za kweli. Wakikuta ni za kweli wanapeleka malalamiko yako kwa DPP ili Jamhuri ifungue kezi dhidi ya mtuhumiwa.
 
Naona unashindwa kabisa kunielewa. Kesi nyingi sana zinafunguliwa polisi na wao wanzipeleka mbele kusikilizwa, mfano mtu akikuibia na ushahidi wote unao, unaenda mahakamani moja kwa moja? si unaenda kumshitaki kituo chapolisi na hata taarifa za wizi huwa zinapelekwa polisi. Tafadhali sana kwa hilo usitake tubishane. Nakushangaa sana.

Hayo ya msemakweli ndio hayo hayo nnayosema mimi, hana cha kushitaki wala hajui cha kushitaki wala hana ushahidi wa kushitaki na ndio maana kapeleka huo anaouita "ushahidi" kwa DPP na halafu aka leak huo "ushahidi" wake ili aonekane kafanya kitu. Soma posts zangu za mwanzo utanielewa.

Tatizo la kung'ag'aia Madrasa na kusahau elimu ya Dunia unakuwa huelewi kila ukipewa somo, Labda ukija kwa Marehemu Mama yangu mkubwa Bi Halima pale Mtaa wa Amani kuna Madrasa nilikuwa nasoma nitaomba muda uje nilkueleweshe vizuri jinsi Wa-JF wanavyokuelewesha na wewe bado hujutambui wala kuelewa. Labda tukiwa kwenye Madrasa utaelewa na unaweza kushikwa na hasira na kuamua kwenda Magogoni kumtimua yule Fisadi Papa anayewaleya Mafisadi wenzake.
 
Mwanaharakati Kaneirugaba Msemakweli leo ameibua majina ya watu anaodai kuwa ndio wamiliki wa kampuni ya Kagoda iliyoshiriki kukwapua pesa za madeni ya nje katika BoT. Kaneirugaba akiongea katika televisheni ya ITV ametaja viranja wa Kagoda kuwa ni Rostam Aziz, Yusuph Manji na washiriki wanne akiwemo mwanamke mmoja. Akiongea kwa kujiamini Msemakweli amesema anaushahidi wa maandishi, video na sauti yake. Ameitaka serikali kuwafungulia mashataka haraka. Source: ITV.
 
Kawataja kina Rostam Azizi, Yusuph Manji, na majina mengine ya kihindi.
 
Bwana invisible embu fafanua hapo kwenye form za kufungulia account holland house na kuomba VISA card mbona majina tofauti na yaliyotajwa?
TUNAOMBA URUDISHE KWANZA ILE DISCUSSION YA BWANA SHIMBO NA KAMA MLIMSINGIZIA TUNAOMBA MUOMBE RADHI KABLA HATUAJAENDELEA NA HII......samahanini sana ila mi nimepoteza imani kidogo tangu mambo ya shimbo yalipowekwa kapuni
 
Jamaa ni jasiri, Mungu ampe ujasiri na amlinde ili hao wahusika waweze kushughulikiwa na Mahakama ipasavyo, manake wasije wakamfanyizia kabla .....
 
Naomba Msemakweli apewe Ulinzi wasije wakamkolimba

Huyo msema kweli ni wanamtumia tu . Serikali yetu maboss wote wamewekwa mfukoni. Wakizidiwa iabidi wawatumie undercover kusawazisha mambo. Hii issue wala haikuhitaji msema kweli. Anayosema msema kweli Serikali na taasisis zake za uchunguzi zinauwezo wa kuyajua na kuyafanyia kazi.

Sasa kama mabosi wa taaaisi za ulinzi na usalama waliogopa kusema nini wanafahamu wanaaamua kumtumia Msemakweli ionekana yeye ndo kaibua na najua zaidi ya kile ambacho DPP, UWT hawajui basi tujue na tuelewe kuna hatari zaidi

Hii nchi inaonyesha kuna watu hata wakivunja sheria kuna taraibu tofauti za kuwashtaki . Hayao anayosema msemakweli yalitaiwa kutangazwa siku nyingi na DPP au Polisi.kwa maana nyingine vyombo hivyo viko mfukoni mwa wajanja wachache.

DPP ile P ya kati kati sio Public bali ni Private. sababu historia na so far anaonekana yuko upande wa wachache. na hata kesi nyingi zenye maslahi ya umma Vs ididividual seriali inashindwa sababu ya poor competence na masalahi binafsi ya DPP.
 
Faisa nimekuelewa vizuri kabisa. Mantiki yako ni kwamba kesi huwa zinafunguliwa polisi. Mantiki yangu ni kuwa kesi huwa zinafunguliwa mahakamani. Polisi wanachunguza tukio wakiridhika na ushahidi wanapeleka faili kwa DPP ili atumie mamlakaka yake ya kufungua kesi. Hakuna mahakama kwenye vituo vya polisi. Nafikiri tatizo hapa lipo kwenye matumizi ya neno "kesi". Zamani wakati tukiwa na wanasheria wachache, DPP ali delegate mamlaka fulani kwa polisi kuendesha kesi mahakani. Sidhani kama bado ndivyo ilivyo.

Kuhusu mtu akikuibia na ushahidi wote unao, unaenda mahakamani moja kwa moja? Simply, huwezi kwenda mahakamani mwenyewe kwa sababu wewe sio Jamhuri. Katika makosa ya jinai Jamhuri ndio yenye mamlaka ya kumshitaki mtuhumiwa. Wewe utakuwa shahidi tuu. Unapoenda kulalamika polisi, wao wanachunguza kama tuhuma zako ni za kweli. Wakikuta ni za kweli wanapeleka malalamiko yako kwa DPP ili Jamhuri ifungue kezi dhidi ya mtuhumiwa.
Mbona unateseka sana kumuelekeza mtu ambaye hujionea fahari kubisha hata vitu asivyo vijua? Hata hivyo nakusifu kwa uvumilivu na busara zako.
 
Back
Top Bottom