Nyaraka mpya za Kagoda zawalipua Rostam, Manji

Nyaraka mpya za Kagoda zawalipua Rostam, Manji

Naona unashindwa kabisa kunielewa. Kesi nyingi sana zinafunguliwa polisi na wao wanzipeleka mbele kusikilizwa, mfano mtu akikuibia na ushahidi wote unao, unaenda mahakamani moja kwa moja? si unaenda kumshitaki kituo chapolisi na hata taarifa za wizi huwa zinapelekwa polisi. Tafadhali sana kwa hilo usitake tubishane. Nakushangaa sana.

Hayo ya msemakweli ndio hayo hayo nnayosema mimi, hana cha kushitaki wala hajui cha kushitaki wala hana ushahidi wa kushitaki na ndio maana kapeleka huo anaouita "ushahidi" kwa DPP na halafu aka leak huo "ushahidi" wake ili aonekane kafanya kitu. Soma posts zangu za mwanzo utanielewa.

My God! Darasani ulipitaje? kama wachangiaji wengine walivyosema, kesi zote za jinai ziko chini ya serikali na DPP ndiye mwenye mamlaka ya mwisho ya kuendesha kesi or otherwise. Individual person hatuna uwezo wa kisheria wa kuendesha kesi za jinai kwani ni wajibu wa serikali kulinda watu na mali zao. hivyo basi katiba imetupa wajibu na haki wa kulinda na kutetea mali za umma. kama alivyofanya msemakweli, amatimiza wajibu wake kama mtanzania mzalendo kuwafichua wezi wa mali za umma.

Kilichobaki ni jamhuri kupita DPP kufungua kesi za watu hao na msemakweli anabaki kama shahidi namba moja. keep in your mind that we have no legal power as individual to institute criminal case...but only director of public prosecution has such power vested to him/her by the law(CPA) to handle and deal with all criminal cases within the United republic of Tanzania. Mama uwe unaelewa basi....
 
Hii taarifa ya msemakweli, wapiga kura wa Igunga haitawaathiri kwa vile wao walifaidika na mapesa ya RA. Kwa Igunga CDM mtumie mbinu nyingine

Ni vizuri pia wananchi wakaelewa wapi walifanya na wanaendelea kufanya makosa wakati wanamchagua mtu. Hii habari inaweza kuwasaidia kuangalia mbali zaidi ya wanavyofikiri e.g. kuepuka kuchagua chama bali waangalie zaidi "mtu".

Naamini candidates wote wanafahamika kwa ukaribu zaidi na watu wa Igunga. Je yupi ana-qualify zaidi kama kiongozi? Mambo ya kuchagua chama ndio unakuta umeuziwa mbuzi kwenye gunia.

Rostam & Co wamejificha chini ya mwamvuli wa CCM for years lakini ukweli ni kwamba hawana sifa yeyote, na hawakustahili uongozi kwenye chama chochote. Ukiwa na candidate sahihi i.e. anayeona mbali, asiyeyumbishwa, asiye-mbinafsi e.t.c is way better than "mlevi wa maji ya bendera na itikadi" Chama hakiletei mtu maendeleo; bali mtu mwenye uongozi dhabiti ataongoza watu wake kwenye njia sahihi kwaajili ya maendeleo yao.
 
Sasa na sisi tusikae kimya tumuunge mkono kwa ujasiri alionao,mtu kama huyo ni muhimu sana kwa nchi hii yenye waoga wa kufa kwa kupigania haki, huku wanakufa kwa njaa,magonjwa na kunyanyaswa na wachache wanaojifanya hii nchi ni yao.
 
Naona mkananganyiko unaendelea!
Mwaka huu kila mtu atasema lake!

Assume wewe ni DPP aliyejivua gamba na assume anayosema msemaweli yanauwa proved na edvidence kuwa ni kweli. Nitajie washstakiwa utaowaweka kwenye orodha ya kushtakwa ukiunganisha na wale wengine. teh teh teh
 
huyu mwanaharakati ni jasiri sana kwani anajua wazi ni vigumu kutoa ushahd mzito km huo na ukabakizwa hai. MI NIMESHAANZA KUMPA USHIRIKIANO KWA KUMUOMBEA KWA MWENYEZ MUNGU AMLINDE NA MAKILLER WA MAGAMBA wewe je utampa ushirikiano gani
 
Faisa nimekuelewa vizuri kabisa. Mantiki yako ni kwamba kesi huwa zinafunguliwa polisi. Mantiki yangu ni kuwa kesi huwa zinafunguliwa mahakamani. Polisi wanachunguza tukio wakiridhika na ushahidi wanapeleka faili kwa DPP ili atumie mamlakaka yake ya kufungua kesi. Hakuna mahakama kwenye vituo vya polisi. Nafikiri tatizo hapa lipo kwenye matumizi ya neno "kesi". Zamani wakati tukiwa na wanasheria wachache, DPP ali delegate mamlaka fulani kwa polisi kuendesha kesi mahakani. Sidhani kama bado ndivyo ilivyo. Kuhusu mtu akikuibia na ushahidi wote unao, unaenda mahakamani moja kwa moja? Simply, huwezi kwenda mahakamani mwenyewe kwa sababu wewe sio Jamhuri. Katika makosa ya jinai Jamhuri ndio yenye mamlaka ya kumshitaki mtuhumiwa. Wewe utakuwa shahidi tuu. Unapoenda kulalamika polisi, wao wanachunguza kama tuhuma zako ni za kweli. Wakikuta ni za kweli wanapeleka malalamiko yako kwa DPP ili Jamhuri ifungue kezi dhidi ya mtuhumiwa.
EMT Very Interesting ... !Ukiangalia swala zima la jinsi kesi zinavyofunguliwa kwa mtizamo wa haraka haraka ... Mtu unaweza kufikiri ..ni swala linaloeleweka na kama liko wazi na moja kwa moja. Mambo mengine madogo madogo ... Utafikiri ... Haya nayajua ... lakini Looh!!!!Maelezo yamekuwa very elaborative and educating!!
 
Faisa inawezekana kweli ukawa ni "circumstantial" rather than "direct" evidence lakini circumstantial evidence unakubalika mahakamani. Kama shahidi akisema alimwona mtuhumiwa akimchoma kisu marehemu, then huo utakuwa ni ushahidi wa moja kwa moja. Lakini akisema alimwona mtuhumiwa akiingia kwenye nyumba ya marehemu, akasikia merehemu akipiga kelele halafu alimwona mtuhumiwa akitoka ndani ya nyumba ya marehemu na kisu chenye damu, then huo ni circumstantial evidence.

Kwa mfano forensic evidence ni circumstantial. Expert evidence ni circumstantial. Na zote zinakubaliwa mahakamani. Ukweli ni kwamba, kwenye kesi nyingine ni vigumu kupata ushahidi wa moja kwa moja. Faiza, it is the necessity for inference, and not the obviousness of a conclusion, that determines whether or not evidence is circumstantial.

EMT, Hakuna evidence isiyokubaliwa mahakamani. Lakini kumbuka, kesi zinajengwa na strong "evidences" and not strong assumptions. The so called evidence provided by Msemakweli is neither forensic nor can it stand in a "product liability" case. Remember, EPA is a product liability case, the product being servicing of loans. You are mixing circumstantial evidence za criminal cases na civil law suits. In civil cases you have cases which can easily be decided using circumstantial forensic evidence but when it comes to intangible product like servicing of loans, if the circumstantial evidence suggests a possibility of innocence, the prosecution has the burden of disproving that possibility.

In our case here Mr. Msemakweli never ever would he agree to be the the prosecutor of the so called case as his "evidence" without doubt suggests a possibility of innocence from the word go. That is why he throws it to DPP, simply to avoid counter suits and considering all the hours he has put to look for the so called evidence to be wasted for nothing? No. Throw it to DPP and leak it to the media, and many would be fooled to praise him as he did something useful. Its simply bogus and he knows it.

Believe me or not, if the so called evidence was solid evidence, without any possibility of doubt, he wouldn't have missed the chance to open the case himself. Who wouldn't want to be his countries hero?
 
kama ni mwanaharakati wa ukweli,hatutakubai wamtishie maisha.
 
Senema ya sarakasi inaendelea. Ngoja tuone episode itakayofuata.
 
My God! Darasani ulipitaje? kama wachangiaji wengine walivyosema, kesi zote za jinai ziko chini ya serikali na DPP ndiye mwenye mamlaka ya mwisho ya kuendesha kesi or otherwise. individual person hatuna uwezo wa kisheria wa kuendesha kesi za jinai kwani ni wajibu wa serikali kulinda watu na mali zao. hivyo basi katiba imetupa wajibu na haki wa kulinda na kutetea mali za umma. kama alivyofanya msemakweli, amatimiza wajibu wake kama mtanzania mzalendo kuwafichua wezi wa mali za umma. kilichobaki ni jamhuri kupita DPP kufungua kesi za watu hao na msemakweli anabaki kama shahidi namba moja. keep in your mind that we have no legal power as individual to institute criminal case...but only director of public prosecution has such power vested to him/her by the law(CPA) to handle and deal with all criminal cases within the United republic of Tanzania. mama uwe unaelewa basi....

Hapo ndipo mtajuwa kuwa darasa ni kitu kizuri sana. Kesi za EPA hazijawa "criminal" cases, EPA ni servicing of loans na aliyepewa hiyo kazi kama hajatimiza wajib wake ana mawili, kulipa kiasi cha fedha alichopewa au kama hana cha kulipa kufilisiwa mali yake kama ataonekana kafanya makosa yaku breach contract yake.

Msemakeli hana kesi hapo, wala hana ushahidi wa kesi. Kama ana kesi angeifunguwa zamani. Anampelekea ushahidi DPP, DPP ndio auchambuwe huo ushahidi kama ana kesi inayohusu hao waliotajwa, cha kujiuiza jee DPP ana kesi ya Kigoda? au unapelekwa ushahidi ili aweze kuupima kama unafaa kufunguwa kesi? Jibu wala huna haja ya kunipa mimi, kama unalo jibu weka moyoni mwako likusaidie fikra zako.
 
Msemakweli amesema yale anayofikiri ni kweli na tumeyaona hapa! Na inawezekana anamengine ya kushindilia ukweli anoamini unaweza kumtia mtuhumiwa/watuhumiwa hatiani.Hiyo ni hatua ya kwanza. Tusubiri upande wa pili nao utakuja vipi.

Si mara ya kwanza kuwepo kwa vielelezo vya namna hii, vielelezo vyenyekuonekana vinashawishi na pengine sio kushawishi tu ..lakini vilivyo vya kweli ...lakini bado ...huo ni upande mmoja...Tusubiri upande wa pili utakuja vipi!Upande wa pili kwenye hoja hii umetajwa kama Rostam na Manji na wengine mbalimbali ... Haki itatendeka?

Tanzania tumeona kesi nyingi zenye mwuonekana kama huu ... hii ni ya karibuni zaidi ...

Tusubiri tuione ....Itachukua mkondo uleule tuliouzoea au? ..NDIO.. Au hii inajipya?
 
So msemakweli ndo invisible kumbe...!! Nimekuona ITV news leo ingawa TBC1 hawajataka kabisa kuonesha mabos wao wakuu Manji na Rostam wanaanikwa live. Good move CHADEMA.
 
Msemakweli amesema yale anayofikiri ni kweli na tumeyaona hapa! Na inawezekana anamengine ya kushindilia ukweli anoamini unaweza kumtia mtuhumiwa/watuhumiwa hatiani.Hiyo ni hatua ya kwanza. Tusubiri upande wa pili nao utakuja vipi.

Si mara ya kwanza kuwepo kwa vielelezo vya namna hii, vielelezo vyenyekuonekana vinashawishi na pengine sio kushawishi tu ..lakini vilivyo vya kweli ...lakini bado ...huo ni upande mmoja...Tusubiri upande wa pili utakuja vipi!Upande wa pili kwenye hoja hii umetajwa kama Rostam na Manji na wengine mbalimbali ... Haki itatendeka?

Tanzania tumeona kesi nyingi zenye mwuonekana kama huu ... hii ni ya karibuni zaidi ...

Tusubiri tuione ....Itachukua mkondo uleule tuliouzoea au? ..NDIO.. Au hii inajipya?
Kwa haya yaliotolewa JF usitegemee upande wa pili kuwa utakuja hapa. Ukimtuhumu mtu unatakiwa wewe ndio upeleke ushahidi kamili na si unaemtuhumu aje kutoa ushahidi.
 
Back
Top Bottom