Nyegere wanamaliza kuku bandani, je nitawadhibitije?

Nyegere wanamaliza kuku bandani, je nitawadhibitije?

hata mimi

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2017
Posts
1,356
Reaction score
1,442
Wakuu nina banda la kuku nimelijenga kwa miti na kukandika kwa udongo sasa usiku nikiwa nimelala anakuja mnyama anachimba na kuingia kisha anakamata kuku tena wale wakubwa kabisa anaondoka nao.

Cha kushangaza matukio yote hayo (kuchimba mpaka kuondoka na kuku) anayafanya ndani ya usiku mmoja tu tena bila ya mimi kushtuka yaani asubuhi ndo nakuta uharibifu huo. Amebomoa siku ya kwanza akasepa na mijogoo miwili, baada ya siku kama tatu akaja tena akachomoka na kuku mmoja mwenye watoto, kisha kesho yake akaja tena kwa spidi ya 5G akasepa na kuku watatu wakubwaa! Dah!!

Sasa katika kuuliza uliza wazoefu wanasema huyo ni nyegere na kumdhibiti kwake wanasema ni mapambano ya ana kwa ana tu au ufuge mbwa. Tangu hapo sijachukua hatua yoyote na wala hajaja tena mnyama huyo pamoja na kwamba nilikuwa kama nimemsusia alipovunja kwa mara ya mwisho sikuziba tena mashimo yale.

Sasa leo nikakumbuka kumbe kuna JamiiForums ambapo huwa tunapata suluhisho kwa mambo mbalimbali na ndomana nimeleta hoja hii wadau namdhibiti vipi mnyama huyu?

1621590164818.png

 
Dawa ni hiyo ya kuacha hilo shimo lake wazi. Kikawaida, wanyama huogopa mashimo waliyoyachimba wenyewe wakiamini kuwa huenda kuna mtego umewekwa. Suluhisho lingine ni kuwa na mbwa wakali ambao watapiga kelele na kupambana naye atakapokuja wakati wowote.
 
Nachofahamu hakuna mnyama kama kicheche na wengine wanaofanana na jamii hio anaweza kuwabeba kuku zaidi ya mmoja, Chunguza hapo zaidi unaweza kuta ni mtu anakuibia halafu wewe unasema ni Nyegere, kama ni nyegere mbona hawafurukuti kiasi mtu alieko karibu asikie vishindo?

Mkuu kama kuku wako wote wamepotea namna hio na hujawai sikia kelele za kuku usiku Jua huyo ni mtu anawaiba, kwangu vibaka waliingia katika banda usiku wakachukua kuku wote 13 waliokuwepo na sikuskia kelele, kumbe kibaka akiingia anamkamata kuku koromeo kama ananyoga, huku ameshikilia mbawa.
 
Mmmmmmhmn hapo mbona imekaa kama ni kazi ya mwizi binadamu na sio mwizi mnyama?

Kama vipi jenga banda la matofali. Unaweka msingi kama kawa, na ndani unasakafia.
 
Huyo si mtu mkuu? 😂 Nyumbani kuna kuku kule, nikiwa likizo, mida ya usiku, hata kuingie paka kwa compound, nakwambia nitajua sababu kuku hawanyamazi kwa fujo tu hadi niamke kumfukuza paka ndio fujo liishe. 😂
 
Back
Top Bottom