Nyegere wanamaliza kuku bandani, je nitawadhibitije?

Nyegere wanamaliza kuku bandani, je nitawadhibitije?

Ukishindwa vyote ulivyoshauriwa fuga Kanga wachanganye na hao kuku. Aisee Kanga ni wakuda sana kelele yao si ya kawaida wakihisi hatari lazima utaamka wewe na majirani
Ushauri wako unachekesha sn Ila ndy ukweli anaopaswa kuufanyia kazi..kanga wakuda ahahaha
 
Ukijua kazi ya mbwa usinge uliza, tatizo mnafuga mbwa kama wale wa wema sepetu vilamba K, kazi ya mbwa ni kukupa viashiria vya tatizo, na kuzuia hata kupambana ili wewe uamke ukamsaidie
... vilamba K... 😂 😂 😂😂 😂 😂
 
Sawa ila unaweza kuamini Nungu nungu na miba yake yote hadi karibia na kichwa kizima ila anauwawa na viumbe vinavyo kula nyama yake.

Kila kitu kina mbabe wake ila sio nyegere kumvimbia pride ya simba 10, wakat mbwa tu anamuua nyegere ukibisha utakuwa hujawinda sungura, nyani kwa mbwa
Nungu Nungu analika kweli, niliona chatu amekufa sababu ya kumla tu, miba yote ilitoka na kutoboa utumbo wote wa chatu. Wote wawili wakafa... 😂
 
Simba anamwangusha nyati eti sembuse nyegere wa kg 20 hadi 30, sema simba hawezi kukala sbb kana harufu mbaya sana na manyoya mengi
Wanakapa sifa nyingi, sema tu kale kadubwana kana ushujaa fulani, kabishi kukubali, sio eti ndio mbabe kwa simba, waache masihara na simba[emoji23]
 
The honey badger is notorious for its strength, ferocity and toughness. It is known to savagely and fearlessly attack almost any other species when escape is impossible, reportedly even repelling much larger predators such as lion and hyena.
In the Kalahari, honey badgers were also observed to attack domestic sheep and goats, as well as kill and eat black mambas. A honey badger was suspected to have broken up the shells of tent tortoises in the Nama Karoo. In India, honey badgers are said to dig up human corpses. It can devour all parts of its prey, including skin, hair, feathers, flesh and bones, holding its food down with its forepaws.
NB-kuku wameenda na huyu mnyama kweli, weka floor ya simiti na kokoto. 😂 😂 😂 😂 😂
IMG_20210521_170832.jpg
 
Ukishindwa vyote ulivyoshauriwa fuga Kanga wachanganye na hao kuku. Aisee Kanga ni wakuda sana kelele yao si ya kawaida wakihisi hatari lazima utaamka wewe na majirani
Tatizo la kanga janja janja nyingi... unaweza ukawafuga ila hawalali bandani
 
tatizo kama hilo mimi lilinikuta, na anatabia ya kubeba na kwenda kupaki kisha anarudia mpaka asubuhi ifike[emoji41]

kama utaweza weka taa yenye mwanga mkali karibu na banda kwa nje ndio iliyonisaidia mm maana jamaa anagopa sana mwanga

zaidi ya hapo pole sana☻
 
Nyegere /honeybugger huwez kumzuia kwa Mbwa hata siku moja.

Huyo dawa yake ni fanya namna ale Sumu afee
 
Wakuu nina banda la kuku nimelijenga kwa miti na kukandika kwa udongo sasa usiku nikiwa nimelala anakuja mnyama anachimba na kuingia kisha anakamata kuku tena wale wakubwa kabisa anaondoka nao.

Cha kushangaza matukio yote hayo (kuchimba mpaka kuondoka na kuku) anayafanya ndani ya usiku mmoja tu tena bila ya mimi kushtuka yaani asubuhi ndo nakuta uharibifu huo. Amebomoa siku ya kwanza akasepa na mijogoo miwili, baada ya siku kama tatu akaja tena akachomoka na kuku mmoja mwenye watoto, kisha kesho yake akaja tena kwa spidi ya 5G akasepa na kuku watatu wakubwaa! Dah!!

Sasa katika kuuliza uliza wazoefu wanasema huyo ni nyegere na kumdhibiti kwake wanasema ni mapambano ya ana kwa ana tu au ufuge mbwa. Tangu hapo sijachukua hatua yoyote na wala hajaja tena mnyama huyo pamoja na kwamba nilikuwa kama nimemsusia alipovunja kwa mara ya mwisho sikuziba tena mashimo yale.

Sasa leo nikakumbuka kumbe kuna JamiiForums ambapo huwa tunapata suluhisho kwa mambo mbalimbali na ndomana nimeleta hoja hii wadau namdhibiti vipi mnyama huyu?

Dawa hapa ni kuchimba floo ya banda kisha unapanga mawe makubwa au tofali za simenti ambayo hawezi kuyasukuma kisha unapiga floo hatarudi tena.
Alitembelea kwangu siku ya kuamkia pasaka mwaka huu akabebeba kuku mmoja, nikapanga tofali kwenye kitako cha banda, usiku uliofuata akaja akachimba na kila alipojaribu kuibukia ndani ya banda anashindwa anaendelea kuchimba kwa mlalo matokeo yake akajikuta yuko nje ya usawa wa banda ndo akabuka na kukosa kuku. Akachimba upande mwingine napo akajikuta ametokea nje. Tangu hapo hajawahi rudi na kuku wangu wako salama Salmin bin seif (safe).
Pia unaweza kujenga banda lako kwa juu maana yeye (nyegere) huwa hapandi juu ya banda la kuku
images (2).jpeg
 
Huyu nyegere mnampaisha mnoo.. Simba huwa anakaona kama kadubwasha kaajabu kadogo kanajidai kudindisha.. Ila simba aamue lake nyegere jeuri anaipatia wapi.. [emoji23]
Huyo nyegere jeuri yake kwa nyoka tuu,Seema huwa ananifurahisha Sana anavyowabalasa hata koboko akimuona nyegere anakimbia 😃😃acha kabisa
 
Huyu mdudu sielewagi kwa nini hushambulia eneo hilo tu.....!/nadhani hujua lina maumivu makali.
Au sababu ya wivu wake,😃,huwa nasikia hyu mdudu anawivu kupindukia ikitokea umemuona Yuko na mpenz wake huwa ataki shobo kabisa
 
Dawa hapa ni kuchimba floo ya banda kisha unapanga mawe makubwa au tofali za simenti ambayo hawezi kuyasukuma kisha unapiga floo hatarudi tena.
Alitembelea kwangu siku ya kuamkia pasaka mwaka huu akabebeba kuku mmoja, nikapanga tofali kwenye kitako cha banda, usiku uliofuata akaja akachimba na kila alipojaribu kuibukia ndani ya banda anashindwa anaendelea kuchimba kwa mlalo matokeo yake akajikuta yuko nje ya usawa wa banda ndo akabuka na kukosa kuku. Akachimba upande mwingine napo akajikuta ametokea nje. Tangu hapo hajawahi rudi na kuku wangu wako salama Salmin bin seif (safe).
Pia unaweza kujenga banda lako kwa juu maana yeye (nyegere) huwa hapandi juu ya banda la kukuView attachment 1798151
Kumbe hawezi kuparamia juu mshenzi huyu
 
Kumbe hawezi kuparamia juu mshenzi huyu
Hawezi kabisa, yeye ni kuchimba na kutokea chini. Mwezi uliopita nilijenga banda jipya nikapanga tofali za simenti chini akaja tena akafukua kidogo akatembea bila shaka baada ya kukuta pagumu na hajarudi tena.
 
Wakuu nina banda la kuku nimelijenga kwa miti na kukandika kwa udongo sasa usiku nikiwa nimelala anakuja mnyama anachimba na kuingia kisha anakamata kuku tena wale wakubwa kabisa anaondoka nao.

Cha kushangaza matukio yote hayo (kuchimba mpaka kuondoka na kuku) anayafanya ndani ya usiku mmoja tu tena bila ya mimi kushtuka yaani asubuhi ndo nakuta uharibifu huo. Amebomoa siku ya kwanza akasepa na mijogoo miwili, baada ya siku kama tatu akaja tena akachomoka na kuku mmoja mwenye watoto, kisha kesho yake akaja tena kwa spidi ya 5G akasepa na kuku watatu wakubwaa! Dah!!

Sasa katika kuuliza uliza wazoefu wanasema huyo ni nyegere na kumdhibiti kwake wanasema ni mapambano ya ana kwa ana tu au ufuge mbwa. Tangu hapo sijachukua hatua yoyote na wala hajaja tena mnyama huyo pamoja na kwamba nilikuwa kama nimemsusia alipovunja kwa mara ya mwisho sikuziba tena mashimo yale.

Sasa leo nikakumbuka kumbe kuna JamiiForums ambapo huwa tunapata suluhisho kwa mambo mbalimbali na ndomana nimeleta hoja hii wadau namdhibiti vipi mnyama huyu?

mapambano ya ana kwa ana wanakupoteza, nyegere haogopi kabisa mwanadamu, akiamua hata ukikaa hapo pembeni ya banda atapita mbele yako na kweanda kukamata kuku. ukileta za kuleta fujo zake utazipenda, anao uwezo hata kukuua, na kama mwanaume, linda sana sehemu zako za siri, atazing'ofoa. ule mgongo wake hata ukipiga mkuki huwa hauingii, ila kama kuna mwanga, na wewe ni hodari, mvizie na fimbo kubwa na imara mpige maeneo ya puani pale ndio huwa anakufa, ila ukipiga maeneo mengine unapoteza muda hafi na haumii, ndivyo alivyoumbwa, ndo ulinzi wake Mungu alimuumba nao. ni ushauri tu, sisi tuliozaliwa maporini tunawajua wadudu hao, bora ukutane na simba ila sio hao, akiamua kukufuata anaweza kukufuata hadi chumbani kwa kukunusa.
 
Back
Top Bottom