Uchaguzi 2020 Nyehunge: Dkt. Magufuli amuamrisha Mfugale atangaze ujenzi barabara ya Sengerema-Nyehunge (KM 46) kisha amuulize hela za kujengea

Uchaguzi 2020 Nyehunge: Dkt. Magufuli amuamrisha Mfugale atangaze ujenzi barabara ya Sengerema-Nyehunge (KM 46) kisha amuulize hela za kujengea

Hahahahahahahaah navuta picha kuku aliekatwa shingo anakuwaje hahahaha oYa anaruka ruka huYo mpaka sio vizuri
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] anakwambia "Mimi sindio Rais?"
 


DKT. Magufuli akiwa anaendelea na kampeni za uchaguzi 2020, amepita kijiji cha Nyehunge akiwa anaelekea Geita ambapo kutoka Sengerema mpaka Nyehunge ni kilomita 46. Alisimama kuongea na wananchi waliokuwa wakimsubiri barabarani, wakati anaielezea barabara hiyo ghafla aliomba simu yake na kumpigia mtu ambae baadae alijulikana ni mkurugenzi mkuu wa TANROADS, Injinia Mfugale na mazungumzo yao yalikuwa hivi.

Magufuli: Hallo, Chief executive

Mfugale: Naam mheshimiwa Rais

Magufuli: Hujambo

Mfugale: Sijambo mheshimiwa

Magufuli: Uko wapi?

Mfugale: Niko Dar es Salaam TANESCO tunazungumzia habari ya Nyerere dam.

Magufuli: Haya, sasa mimi niko Nyehunge, kutoka Sengerema mpaka Nyehunge ni kilomita 46, hii barabara tumeshaifanyizia feasibility study na detail design, nimesimama hapa na wananchi, nataka hii barabara, mimi si ndio Rais?

Mfugale: Ndio mheshimiwa(Wananchi kicheko cha furaha)

Magufuli: Nyehunge Oyee, Unanielewa Chief? Basi hii barabara uitangaze kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Huu ni mwezi wa ngapi? (Mfugale: Mwezi wa tisa). Haya uandae document zote kabla ya mwezi wa 12 haujafika na kandarasi apatikane, niulize hela nitazitoa wapi. Sawa Mfugale?

Mfugale: Nimekuelewa mheshimiwa Rais

Magufuli: Umenielewa, mueleze na Waziri kwamba hayo ni maagizo yangu wala yasibadilike, Asante sana.

MWISHO WA MAONGEZI
Hii serikali mfugale anakuwa promoted kweli sijui sababu ni ipi?
 
Miradi ni maendeleo, kama hutaki miradi hamia ughaibuni.

Lakini jambo la msingi ili kupambana na Magu ilibidi kujipanga kisawasawa kama 2015.

Usione vinaelea vimeundwa, Chadema ya leo siyo ile ya 2015.
Kuna muda inabidi ukae kimya ili watu wasijue kichwani kwako pako wazi kiasi gani
 
Bado tu barabara ya kwenda mbinguni nadhani siku akiwakusanya maaskofu na Mashehe hii ndiyo itakuwa amri. Nawasilisha, huu mwaka jamani Lissu utatuumizia
 
Hiyo ni rushwa kama rushwa nyingine zilivyo!Hata mzee wa ubwabwa aliona tatizo wananchi wana njaa,akaamua kukitatua hapo hapo kwa kuwapa ubwabwa ila akaambiwa hiyo ni rushwa!

Kama ameona kuna hitaji la barabara,kwanini asifanye mawasiliano na huyo mfugale ili mkakati ufanyike na kazi ifanyike?Kwanini atumie jukwaa la kampeni?Hiyo ni rushwa, muiname muinuke hiyo ni rushwa!
Ameongea kama Rais, hata Trump yuko kwenye kampeni na bado anatoa executive order hiyo ndiyo dunia ya kisasa.chadema toeni sera mbadala za kuonyesha ubora wenu, lakini kama sera zenu anazotoa Lissu za kuvunja Muungano na kudanganya eti karume alilazimishwa ni ujuha ulipitiliza.Mtasubiri sana
Kweli maana kunakipindi maji ya ziwa yarivuka nakuja eneo la barabara hali ikawa mbaya sana usafiri ukawa kuunga paka upande mtubwi sehem ya kilomita 46
 
Nimegundua watu wengi wanauhafifu wa uelewa,Rais nikiongozi wa serikalI na shughuli za serikali zinaendelea,kama barabara hiko kwenye mpango wa kujengwa kwanini isijengwe??Watu wameona barabara tu,mbona hamsemi mishahara kwamba silipwe mpaka kampeni ziishe.
 
Kweli maana kunakipindi maji ya ziwa yarivuka nakuja eneo la barabara hali ikawa mbaya sana usafiri ukawa kuunga paka upande mtubwi sehem ya kilomita 46
Hiyo ni rushwa ya uchaguzi!Kama pameshafanyiwa feasibility study basi tayari barabara iko kwenye mpango!Na kama ina uharaka angeweza kumwelekeza tu Mfugale kwa utaratibu rasmi wa kiofisi!Lakini hii ya kusimama jukwaa la kampeni na kupiga simu kisha kuagiza barabara ijengwe ni rushwa,"rushwa"!!!!!!!!
 
Unayefikiri kuna usawa pole sana, Lissu mwenyewe anajua usawa hakuna kikatiba, na kwa hiyo kampeni za Lissu ni za kutimiza mkakati wa kivuli cha demokrasia nchini na kwa kujua hilo Lissu anapungua gharama za kampeni kwa kuwachangisha michango wananchi!

Siasa ni maisha ya watu, siasa ni biashara za watu na usipojua mchezo huo utaumia sana na huenda ukapoteza maisha halafu wanasiasa wakaendelea kula bata pamoja!
Ni Africa tu tunaona hayo,ndio maana ikifika wananchi wakachoka basi kinanuka kweli kweli na walio madarakani wanatamani ardhi ipasuke waingie!
Haki ni neno dogo,ila limebeba dhamana kubwa sana!Unaweza usione leo au hata maisha yako yote,ila ukibahatika kukutana na madhara ya kupuuzwa kwake basi utatamani usage meno!
Tanzania sio kisiwa!
 
Hiyo ni rushwa alitakiwa awe ameijenga siku nyingi, hata kutoa ajira 13000 na kutoa bima ya afya wakati wa kampeni ni rushwa pia.
Watu wanakusanya tu hizo taarifa kwa ajili ya kuja kuzifanyia kazi baada ya uchaguzi
 
Mhh mkuu mwananchi yeye anataka barabara, hajalishi ni uchaguzi au hapana.
Sisi wananchi tunataka haki ya kuwa na barabara na sio sheria ya kuwa na barabara wakati usio wa uchaguzi.Afterall yanini kutumia hesabu mbovu wakati fika yule Magu ataendelea,tunamdanya nani.
Alafu shughuri zake za ujenzi zinaanza Dec, 2020.


aaaaaaaaaaaaaaaaaaaah, tuache dharau wazeeeeeee
 
Nonsense. Kwani hiyo barabara tu ndio mbovu Tanzania hii. Tume ya uchaguzi haina maana ni vibaraka wake ndio wamejazana hapo.
 
Safi sana muheshimiwa Rais,JPM apendagi ulugwalugwa na tit for tat.
 
Anaendelea kwa mujibu wa nani?Sanduku la kura ndio mwamuzi!
Tunachosema hapa,hilo hitaji la barabara alishaliona ndio maana wakati anaongea akasema wameshafanya feasibility study na vitu kama hivyo!Sasa hiyo kufanya jukwaani ni rushwa,inamaana anawaambia msiponichagua barabara haitajengwa maana pesa najua mimi nitakapozitoa!
Hii ni rushwa ya wazi wazi na haikubaliki kwenye jamii ya wastaarabu!Hatukuwahi kuona mambi haya kipindi cha Mkapa wala kikwete!
Tokea Nyerere, Mwinyi na Mkapa,Kikwete na sasa Magufuli ulishasikia au kuona Kiongozi tokea upinzani anakabidhiwa nchi?
Katika picha halisi, ni chama kimmoja,hadi katiba mpya iliopendekezwa na tume ya Warioba.
Uchaguzi kwa sasa ni kiini macho,heri Magufuli akaendeleza kazi zake.
 
Tokea Nyerere, Mwinyi na Mkapa,Kikwete na sasa Magufuli ulishasikia au kuona Kiongozi tokea upinzani anakabidhiwa nchi?
Katika picha halisi, ni chama kimmoja,hadi katiba mpya iliopendekezwa na tume ya Warioba.
Uchaguzi kwa sasa ni kiini macho,heri Magufuli akaendeleza kazi zake.
Hapa unajaribu kusemaje?Kuwa huwa mnashindwa uchaguzi ila mabavu yanawabakiza madarakani?
Tambua kuwa haki huinua taifa na kustawisha amani na utulivu!Unaweza usiwe mkomavu wa kutosha kuelewa haya,ila ikifika wakati wananchi wakadai haki yao kwa namna nyingine,ndio hapo majuta huwa mjukuu!Mifano ipo mingi na hai!Wale wanaodhulumiwa haki yao wakichoka huwa ni suala la muda tu,na ndio hapo hata maadui inakuwa rahisi kupenyeza mambo yao!Mtu akifikia breaking point,ukampa silaha unategemea nini?Uasi hujengwa taratibu,pigieni chapuo uovu ila tambueni kuwa wanaodhulumiwa nao wana kipimo cha uvumilivu!
 
Back
Top Bottom