Nyerere alituuza na kuzalisha umasikini


Ulitaka waishitaki serikali iliyowapora mali zao kwenye mahakama hizi hizi za serikali? Kesi ya nyani apelekewe ngedere siyo?

Viwanda, biashara, na mali za watu zilitaifishwa kwa sababu za sera za Ujamaa. Hakuna cha wahindi kudaiwa madeni wala nini. Kasome kitabu (Ujamaa essays on socialism) alichoandika Nyerere mwenyewe utaelewa. Kasome Azimio la Arusha utaelewa. Na Ujamaa haukuwa Tanzania peke, ulikuwepo kwenye nchi zingine za Afrika ambako ulifeli kama ulivyofeli hapa.

Kenya ilitupiga ovateki kiuchumi zamani sana. Na mpaka leo hatujaikamata. Unaposema kuna Wakenya wanakuja kutafuta fursa bongo ni sawa na kusema kuna Waturuki na Wachina waliojaa Dar kutafuta fursa hawataki kuondoka. Kwa mantiki hiyo Tanzania ina uchumi bora kuliko Uturuki na China. Lakini siyo kweli.
 
Hivyo viwanda vilikua marehemu anayetembea wakati anang'atuka,kiwanda hakifi siku moja
 
Kwanza hakukuwa na raia Milioni 60 kipindi Nyerere anatawala.

Hivyo uchambuzi wako ni bogus, void na null ukitumia dhana ya wakati wa sasa
 
Hivyo viwanda vilikua marehemu anayetembea wakati anang'atuka,kiwanda hakifi siku moja
Mpaka Mzee Ruksa anaingia viwanda vyote vya nguo vilikuwa vinafanya kazi.
Viwanda vya sukari alivyoviacha JKN, mpaka leo vinafanya kazi.

General tyre wakenya wamechukua machine wanatengenezea YANA tyres;

Tatizo hakuwa Nyerere, tatizo hapakuwa na watu wenye weledi na uzoefu wa management ya viwanda.
Hao wanaolaumu initiatives za Nyerere, ilitakiwa watuonesha Kenya au Mozambique au Zambia kawa bora kwa ukubwa kiasi gani tofauti na sisi ili ku-justify facts.
 
Pumbavu!
 
MWALIMU NYERERE ni kati ya viongozi wachache waliofanya vizuri katika uongozi wa nchi. Sababu ya uchumi kuwa mbaya ulitokana na athari ya vita vya KAGERA na production of agricultural goods instead of manufactured goods na hii ilipelekea unequal balance of trade.
Tatizo hilo halipo Tanzania tu, lipo katika nchi karibu zote za Ulimwengu wa tatu.
Hoja yako ingekuwa sahihi, kama tatizo lingekuwa Tanzania tu.
Kwa issue ya Zanzibar pia ilikuwa sahihi, Kwasababu hawakuungana kwa kila kitu isipokuwa ni baadhi ya mambo na hivyo si vibaya kusimamia masuala yao ambayo siyo ya muungano. Kwa suala la watu milioni 2 kuongoza watu million 60, ni suala la kubadili katiba tu, kwa kuweka kipengele kitachosema kuwa kama rais atafariki uchaguzi ufanyike baada ya miezi 3 au vinginevyo.
Hatahivyo, sioni tatizo nchi kuongozwa na wazanzibari watupu kama wako vizuri kuliko watanzania wengine katika nafasi hiyo.
NB
NYERERE Sasa hivi hayupo hivyo jaribu kutoa mtazamo wa jinsi ya kutatua tatizo lililopo badala ya kulaumu.
Kwasababu, hatakama angeweka mfumo mzuri bado angeweza kujitokeza rais fulani na akaubadilisha na akatawala anavyotaka yeye( Mfano: Museveni, Kagame, Paulo Biya, nk) . Sisi tuna uafadhali Kwasababu, baada ya miaka 10, tunapata sura mpya.
 
Kama viwanda vilikua vikifanya kazi, kwa nini palikua na ukosefu wa bidhaa muhimu zikiwepo nguo Hadi kupelekea watu kutembea uchi kule kusini na suala hili kukoma ruksa alipoweka biashara huria na kufungua mipaka!?..general tyre kiwanda Cha kupewa Cha kizamani kilikua na uzalishaji mdogo kikizidiwa oda,ukosefu wa bidhaa muhimu ulipelekea kuzaliwa 'ulanguzi'
 
Naunga mkono hoja, huyu sijui hata hizo sifa huwa anapewa na nani, aliharibu nchi vibaya sn
 
Naunga mkono hoja, huyu sijui hata hizo sifa huwa anapewa na nani, aliharibu nchi vibaya sn
Kuna watu hawawezi kuelewa madhara ya kila kitu kutoka ikulu.ubunifu unakufa watu wanafanya kazi kwa matakwa ya aliyewateua ata kama yanaleta madhara kwa Taifa.Nyerere angejenga misingi ya kuongoza Taifa kwa pamoja na uwazi wa malengo ya Taifa.Yaani kila mwananchiiii ajue malengo ya taifa.
 
1. Mheshimu Mwalimu kwa kujengea taifa moja ambalo mtu kutoka Kakonko anaongea na Mpemba Wete, kwa lugha moja bila mkarimani.

2. Mheshimu Mwalimu kwa uzalendo na uadilifu wake; aliacha karibu urithi wote wa madini na wanyama na hakuwahi hata kumiliki Kitalu cha kuwinda wala futi moja ya mgodi wa madini.

3. Mheshimu Mwalimu kwa kuifanya Tanzania kuheshimika duniani.

4. Mheshimu Mwalimu kwa kuasisi Muungano wa kipekee duniani, hivyo Tanzania kuwa dola imara.

NOTE: Usirudie tena kumjadili Mwalimu Nyerere kirahisi. Umasikini au utajiri unaanzia kwako. Wewe umefanya nini kujikwamua ktk umasikini?πŸ™πŸ™πŸ™
 
Tuna mfumo wa hovyo sn huu
 
Zaidi ya asilimia 50 ya watanzania walizaliwa wakati Nyerere hayupo duniani. Na ni Marais wanne walipita baada ya Nyerere. Sasa iweje lawama ziende kwa Nyerere kwa umaskini uliopo. Chukulia tu mfano Diamond kafanikiwa kimaisha kwa kiasi chake na alizaliwa wakati raisi ni Mwinyi
 
Wote mnao lalamika umasikini wa Tanzania ni kwa sababu ya Mwalimu.

Swali: Je Mwalimu alikufa na akili zenu ?
 
Yaani nchi ya watu Mill 60 sasa hivi inaongozwa na mkoa wenye watu laki mbili
Hii inafikirisha sana.
Lakini tambua Kuwa Zanzibar si Mkoa , ni Moja ya nchi mbili zilizounda Jamuhuri ya Muungano.
Zanzibar nzima ina watu milioni 1.8 hivi, pamoja na hao wamo wahamiaji toka Tanganyika wliofurika kuja kuisaidia CCM ili ishinde kiubwete 2025.
Nyerere alizifisidi Nchi zote mbili kwa kuziacha zikiwa Fukara, huku watu wake wakiwa katika kiwango cha juu cha Ujinga, wakijigamba kufuta ujinga wa kujua kusoma na kuandika tuu.
 
Unapoona viwanda au miradi inakufa baada ya uongozi fulani kutoka madarakani, jibu ni rahisi tuu.
'' hawakuunda mifumo ,waliunda umaarufu wao na wafuasi tuu''
Kama Nchi imeweka mifumo isiyotetereka , hata serikali ikiwa haipo kwa mwaka mzima , maisha yanaendelea bila kutegemea wanasiasa.

Mpaka Mzee Ruksa anaingia viwanda vyote vya nguo vilikuwa vinafanya kazi.
Viwanda vya sukari alivyoviacha JKN, mpaka leo vinafanya kaz
 
Kuna msemo mmoja niweke nukuu toka kwa John Maxwell, everything raise and falls because of leadership.

Tuweke swali rahisi la kujiuliza, Nyerere kaondoka 1985, mpaka miaka ya 90 (term ya pili ya Mzee Ruksa) ginnery nyingi na textile industry bado zilikuwa operational.

Suala, je waliofuatia walifikiria component ya ukarabati wa machinery na kununua technology ili kuendeleza uzalishaji?
Kuna watu wanamlaumu alietoka akiacha vitu vinafanya kazi, mpaka Mkapa anaingia mfumo wa viwanda ulikuwa umekufa.

Bado kuna maswali ya msingi, kama mahitaji ya soko yanahitaji leather, mashuka, pamba za hospitali, kwanini tununue nje ya Tanzania badala ya kuzalishia hapa kukidhi soko la ndani then tuuze nje kilichobakia?

Fate ya kesho inabaki wa uongozi; Mathalani, JPM alimshawishi Bakhresa kuzalisha sukari kwa kumpatia shamba kubwa Bagamoyo na soon Bagamoyo sugar imeanza kuzalisha sukari.

Tunawezaje kuwa taifa ambalo kila km chaku inaibuka petro station badala ya kuweka incentive hao wenye hela za kujenga petrol station, kwanini wasiwekewe sera rafiki ya kuzalisha vitu vyenye tija kukidhi mahitaji ya ndani na nje?

Bahati mbaya, nchi hii hatuma stable investment financing na inakuwa ngumu kumshawishi mtu aweke hela yake kwenye nini.
Tunabaki kuwa wachuuzi wa mafuta toka uarabuni, wachuuzi wa miswaki, wachuuzi wa dawa za mswaki, wachuuzi wa dawa za kusafishia choo, wachuuzi wa toothpick, wachuuzi wa cotton buds, wachuuzi wa mifagio ya ndani (soft brooms)

Unawaza, wizara ya viwanda na biashara na wizara ya fedha, wanawaza nini; wana mikakati gani?
 
Ukiuliza mtanzania juu ya matatizo yanayowasumbua, badala akupee jibu ataanza kuji compare na wakenya alafu aseme afadhali sisi.


Washenzi sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…