Nyie mnaopenda kuiga biashara za watu hebu jaribuni kuweni wabunifu, mnaleta chuki ipo siku tutakuja kuonana wabaya

Nyie mnaopenda kuiga biashara za watu hebu jaribuni kuweni wabunifu, mnaleta chuki ipo siku tutakuja kuonana wabaya

Maduka ya kariakoo ni tofauti na maduka tulipo sisi huku mtaani, kule wanawateja wengi na mwingiliano wa watu ni mkubwa tofauti na huku mtaani ambapo watu wakipita unawahesabu kabisa.

Alafu isitoshe mimi sijakataa kuwe na biashara ya aina moja sehemu moja, lakini mimi hofu ni kwamba biashara za aina moja zinapokuwa nyingi sehemu moja kwenye maeneo ambayo hayana mwingiliano mkubwa wa watu unafikiri nini kitatokea kwa wafanyabiashara wa maeneo hayo??

Hapa nilipo mimi kuna stationary kama nne mimi pia nikiwemo, anakuja mtu anafungua stationary apo apo mwisho wa siku wauzaji tunakuwa wengi kuliko wanunuzi na hapo biashara lazima iwe ngumu.

Kingine ni kuhusu hawa wamiliki wa fremu. Unampangisha mtu afanye biashara the same ambayo mpangaji wa awali anaifanya! Howcome?? Apo si nikuleta uchonganishi na kugombanisha watu bila sababu za msingi??

Mwisho wa siku tunaanza kuitana wachawi, yaani acha tu ndugu yangu.
As long as kodi ya fremu ya miezi 6 amenilipa haina shida. We jiongeze waganga hawatoi majini tu😀
 
Upangaji wa biashara ni jukumu la serikali kwa baadhi ya nchi na nchi na sio kiholela kama kwetu

Kuna watu povu limewatoka bila kutembea na kuona Dunia huwezi kujua mambo mengi na ndio maana wengi hawana uelewa

Kwa mfano UK biashara zina namba kuanzia A1,A2,A3,A4, na A5 zote hizo ni biashara tofauti tofauti
Unakuta duka linakodishwa kwa mfano A1 hiyo ni biashara ya posta, au retail goods na huwezi kufungua chakula kama mgahawa

Biashara zinadhibitiwa na serikali na sio kiholela kama sisi

Zipo biashara zinazofanana mtaa mmoja labda kwa sababu ya demand lakini sio kuweka vinyozi 5 mtaa mmoja
Tanzania idadi kubwa ya watu ni wafanyabihashara, wafanyakazi ni asilimia chache. Asa anataka bihashara moja afanye peke yake?, Hiyo haitotokea abadani. Bali bihashara ni ushindani, na katika ushindani anatakiwa aongeze ubunifu na njia za kufanya bihashara yake ionekane Ina huduma Bora zaidi yake, bila kukosa maombi. Na kama si muombaji basi ndo hivyo ageukie upande wa pili, lakini hivi hivi hatoboi. Narudia Tena bila maombi hatoboi [emoji1][emoji1]
 
Aisee!! Nimecheka Sana.

Mkuu, yaani unaelezea as if unatoa mashtaka Kwa Baba yako. Hii ni dunia huru, wanasemaga ni uwanja wa fujo.

Hao wenzio hakuna baya Wala kosa walilofanya machoni pa Mungu. Wao pia wanapambania ridhiki ya halali.

Nafikiri ni wakati wako ww sasa kutafuta changamoto kwengine.
 
Neno Ubunifu linatumika ndivyo sivyo; Biashara hizi unless wewe ni UBER, Ebay, Amazon et-al; au teknolojia fulani ikitoka kutumia teknolojia hio kurahisisha mambo huenda huo ndio ukaita Ubunifu...

Ukiona watu wanafanya hicho unachofanya, una genge la nyanya na yeye analeta ni kwamba barrier of entry huenda ni ndogo - Hakuna mtu hajui nini Kilimanjaro / Uhai au maji yoyote anachofanya ila ni investment needed ni kubwa basi watu wanabaki kuangalia tu.... na hata wakiingia ile first to market na branding bado huenda ikawazuia

Pili kama vipi hao watu wengi wamekuja kuiga hio Biashara na wewe ni Gwiji la kunusa Fursa basi watumie hao wengi kama wateja - kuwa supplier wao bidhaa wanazotaka....

Sema issue kubwa watanzania wote ni madalali katika level tofauti na ni wachuuzi wa kutoa hapa kupeleka pale ama sivyo haya mambo yasingetokea...., Mbona hawajaenda Kumuiga Diamond au watoke kabisa Tanzania wakamuige Messi; na kina Ronaldo....
 
Mbongo Aisee ni mtu mwenye kichwa kigumu sana. Imagine mtu unaona kabisa sehemu fulani kuna biashara kama nne zinazofanana we unaenda kuanzisha biashara hiyo hiyo, hivi hii inaingia akili kweli au mnataka watu tuanze kuitana wachawi??

Mtu unaona kabisa sehemu fulani kuna stationary na studio kama tano na wewe pia unataka unazishe stationary kisa tu umemuona fulani ana wateja wengi kwenye stationary na wewe umeamua kuleta biashara yako tuanze kugombania wateja mwisho wa siku watu tunaanza kuitana wachawi

Halafu isitoshe nyinyi mnaopangisha fremu utamruhusu vipi mtu afanye biashara the same kama wapangaji wengine wanafanya hiyo biashara, huko ni kuleta uchonganishi. Kugombanisha pasipo na sababu za msingi.

Hii kuigana igana biashara inatia hasira sana. Basi tu watu tunaamua kuishi hivo hivyo. Siku ya pili sasa wateja wamepungua sana ofisini kwangu. Itoshe kusema wabongo mnamauzi sana.

Ongeza ubunifu, Customer care na punguza Bei
 
[emoji1][emoji1][emoji1] hii ndiyo bongo. Hakuna kulaumiana ndo tushazaliwa umo.
Hahahah iko hivyo yani. Ukija mtaa nnaoishi utacheka. Yani kila mtu anayefungua biashara ni duka la mangi, butcher, pharmacy🤣 sema maduka ya mangi ndio yamezidi 🤣🤣🤣!

Kwa haraka tu yapo kama 14 pamoja na la jumla moja ni 15 shops.
 
Acha ujinga.

Biashara ni ubunifu, sio aina ya biashara ama bidhaa.

Wewe kuwa mbunifu tu na huduma nzuri kwa wateja. Usihofu mtu kufungua biashara kama yako. Kitu pekee unaweza kua nacho peke yako hapa Duniani ni kyuma ama mboo tu.
Na hta mbo#ro kila mtu anayo kasoro kina dada nasema hivii pambaneni na hali zenu msitupangie nq fremu zetu nna fremu kumi na zote hta mje kupangisha wote muuze madaftari furesh tuu
 
Wewe sio mfanyabiashara km ni hivyo, sasa ungekua kkoo si ungenuna na duka ungefunga!!!

Kuwa mbunifu usiwe mwepesi kukata tamaa
Ebu jaribu kutofautisha maduka ya kariakoo na huku uswazi. Kule kuna mwingiliano mkubwa wa watu tofauti na uku mtaani ambapo watu wakipita unawahesabu kabisa.

Unakuta wauzaji ni wengi kuliko wanunuzi shida ndio inapoanza apo
 
Back
Top Bottom