MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 14,588
- 32,361
Nimekuwa nikijiuliza sana kwanini muziki nikiusikilizia Bar huwa ni mtamu zaidi ya kusikilizia nyumbani? Nyumbani nina Home Theatre nzuri ya Sony niliyonunua Dirham 1200 kule Deira, Dubai lakini huwa naona haitoi muziki mtamu kama ule wa Bar. Hata kinywaji cha Bar nadhani huwa ni kitamu kuliko nyumbani. Inabidi watafiti waingie chimbo kutuletea majibu ya hili swali.
Katika kuhudhuria Bar mbalimbali hapa Tanzania kwa miaka kadhaa nimegundua kuna nyimbo mbili pendwa sana kwenye mabaa. Ikumbukwe mimi ni miongoni mwa watu wachache waliofika karibu maeneo yote ya nchi hii. Ukimtoa mgombe urais kwa tiketi ya CCM na kiongozi wa mbio za mwenge basi huenda mimi ndo nafuatia kwa kufika maeneo mengi.
i. 100 Kilos ya Ferre Gola
ii. Ya Jean ya Madilu System
Hizo nyimbo ni kama zina mikataba maalum na wamiliki wa mabaa pamoja na wateja wao. Kwa miaka kadhaa sasa ukiingia karibu kila bar hapa Tanzania utasikia zinapigwa. Zipo zingine pia pendwa ila naona hizo mbili ni zaidi.
Katika kuhudhuria Bar mbalimbali hapa Tanzania kwa miaka kadhaa nimegundua kuna nyimbo mbili pendwa sana kwenye mabaa. Ikumbukwe mimi ni miongoni mwa watu wachache waliofika karibu maeneo yote ya nchi hii. Ukimtoa mgombe urais kwa tiketi ya CCM na kiongozi wa mbio za mwenge basi huenda mimi ndo nafuatia kwa kufika maeneo mengi.
i. 100 Kilos ya Ferre Gola
ii. Ya Jean ya Madilu System
Hizo nyimbo ni kama zina mikataba maalum na wamiliki wa mabaa pamoja na wateja wao. Kwa miaka kadhaa sasa ukiingia karibu kila bar hapa Tanzania utasikia zinapigwa. Zipo zingine pia pendwa ila naona hizo mbili ni zaidi.