NYON, USWIZI: Droo ya Ligi ya UEFA; Bayern v R.Madrid, Liverpool v Roma! Droo ya EUROPA League; Arsenal apewa Atletico

NYON, USWIZI: Droo ya Ligi ya UEFA; Bayern v R.Madrid, Liverpool v Roma! Droo ya EUROPA League; Arsenal apewa Atletico

Ukiambiwa kuwa wao Liver hawakutangaza ila 'walijua' utakubali??

umeisoma hiyo "story"?
7d861ed2-4bd7-48ce-9c59-42e7dc0697e9.png

umeona imeandikwa lini?
 
watu mnawadharau sana AS ROMA, kumbukeni ndo kamtoa mfalme wenu Messi .
 
!
!
Madrid atapita kiulaini sana. Bayern ya miaka mitatu nyuma ilikuwa balaa sana. Hii ya sasa Haina makali sana.
Roma ni timu ya kuiogopa kwa sasa. Sina uhakika kama Liverpool itatoboa.
Nadhani Madrid atabeba ndoo kwa Mara ya tatu
 
Leo kunafanyika droo ya michuano ya klabu bigwa Ulaya na Michuano ya Europa league. Droo hii kufanyika Nyon, Uswizi
Droo ya Europa League inatarajiwa kufanyia saa 13:00 mchana wa leo kwa muda wa Tanzania(12:00 CAT) na (10:00 GMT)

Droo ya UEFA inatarajiwa kuanza saa 14:00 mchana wa leo kwa saa za Tanzania(13:00 CAT) na (11:00 GMT)

Timu zilizopo UEFA zinazosubiri kujua zitacheza na nani ni Liverpool(Uingereza), AS Roma(Italia), Real Madrid(Uhispani) na Bayern Munich(Ujerumani)


Matokeo ya droo ya nusu fainali ya UEFA ligi
  • Bayern Munich(Ujerumani) Vs Real Madrid(Uhispani)
  • Liverpool(Uingereza) Vs S Roma(Italia)
Michezo hii ya nusu fainali itafanyika mnamo Aprili 24/25 na Mei 1/2. Fainali itafanyika Mei 26 katika uwanja wa NSC Olimpiyskyi, Kyiv
==

Timu zilizofika hatua ya nusu fainali ya EUROPA league ni Salzburg(Austria), Marseille(Ufaransa), Atlético de Madrid(Uhispania) na Arsenal(Uingereza)


Matokeo ya droo ya nusu fainali ya Europa ligi
  • Marseille(Ufaransa) Vs Salzburg(Austria)
  • Arsenal(Uingereza) Vs Atlético de Madrid(Uhispania)
Michezo hii ya nusu fainali itafanyika mnamo Aprili 26 na Mei 03. Fainali itafanyika Mei 16 katika uwanja wa Stade de Lyon, Lyon-Ufaransa


My take
:
Natamani Liverpool akutane na Real Madrid, Arsenal apewe Atletico
Nami napenda Liver awavae Madrid
 
Waingereza na mashabiki wa liver wanaamini Mancity ni timu bora kabisa duniani kwa sasa hivyo kuitoa kwa goli za kutosha basi kunawapa wao uwezo wa kumfunga yeyote ila hawajui kuwa mancity haijawahi hata fika nusu fainali ya uefa champions league.
Hivi hata mchezaji mmoja mmoja, unawezaje walinganisha na kina Ronaldo, Modric, Casemiro, Marcelo, Verane, etc na kina Salah, Mane, Firmino, etc ambao hata hawajashinda vitu.

Napenda wakutane na Real fainali wapewe somo, tena inaweza kuwa fainali moja ya one sided sana!!
Nitajie waliofika nusu fainali msimu uliopita wa club bingwa.
 

My take
:
Natamani Liverpool akutane na Real Madrid, Arsenal apewe Atletico

Ni Liverpool vs Bayern Munchen ktk fainali za Mei, 26/2018 ....

Kuna uwezekano mkubwa kuwa, mwisho wa Real Madrid ni pale Allianz Arena na Santiago Bernabou itakuwa ni ku sign - off tu

Kwa AS Roma dhidi ya Liverpool FC, ni wazi Liverpool atapasua kwa kuangalia historia na viwango vya ubora vya timu. Liverpool wako vizuri zaidi ya AS Roma!!
 
Real Madrid Vs Atletico Madrid
Juventus Vs Monaco
Ok uko sawa, nilisahau kidogo. Ila msimu wa 2015/16 semi final man city aliingia na alipangwa na real madrid, akatolewa kwa gili moja.
Sasa unaposema kuwa man city hawajawai fika nusu fainali ya ucl huwa napata mashaka sana na statement yako
 
Ok uko sawa, nilisahau kidogo. Ila msimu wa 2015/16 semi final man city aliingia na alipangwa na real madrid, akatolewa kwa gili moja.
Sasa unaposema kuwa man city hawajawai fika nusu fainali ya ucl huwa napata mashaka sana na statement yako
Ok.
Yawezekana nilisahau hilo kutokana na rekodi yao mbovu ulaya ila hiyo pekee haliifanyi Mancity kuwa kigogo wa ulaya.
 
Back
Top Bottom