NYUMA YA PAZIA: CHADEMA ilivyosalitiwa 2015 - Dkt. Slaa

NYUMA YA PAZIA: CHADEMA ilivyosalitiwa 2015 - Dkt. Slaa

Usikubali kufungwa mawazo wako na hisia. Ukisoma vitu vinavyokufurahisha kihisia tu utajikuta kuwa mawazo yako yanatawaliwa na hisia. Hatusomi au kujifunza kwa watu tunaokubaliana nao tu bali hata tusiokubaliana nao au wale ambao hatuwajui kabisa kiasi cha kuweza kuchagua upande. Kuna watu humu nawasoma inaonekana na wao waliumia sana kwa Dkt. Slaa kufanya maamuzi aliyoyafanya na hivyo hisia zao na labda akili zimeumizwa mno kiasi kwamba ukitaka "Dkt. Slaa" wanakuwa kama Manchurian Candidate. Mtu aliyekomaa kihisia, kiakili na kisiasa haogopi au hajidhanii kuwa hafai kujisomea mambo kutoka kwa mtu asiyekubaliana naye. NI suala la ukomavu tu.

Kwa wale ambao wanapanga kusoma au tayari wamesoma nina uhakika watamaliza wakiwa na ufahamu mkubwa sana kuhusu maisha na siasa za Dkt. Slaa na kwa kiasi kikubwa wataweka mitazamo yao katika mitazamo sahihi na labda hata kubadilisha mawazo yao au kuyathibitisha waliyokuwa nayo awali
Binafsi sikuumizwa na alichofanya Slaa, bali NILISIKITISHWA. ni mtu aliyejitoa kutumiwa na "maadui" zake ili "kummaliza" yule waliyetofautiana naye. Hapo tu ndio namwona SLAA HANA MAANA. Slaa alituthibitishia kwamba yeye ni mtu mwenye hekima na busara, anafanya mambo baada ya kufikiri sana. na ANA MSIMAMO. lakini baada ya kutofautiana tu na chama chake, akasusa kila kitu na kuacha misimamo yake yote ya mwanzo. sasa mtu wa aina hiyo anaweza kuja na jipya lipi, zaidi ya kuuthibitisha tu huo UNAFIKI wake?

Narudia tena, Kama Slaa angeendelea na misimamo yake ya kupigani HAKI, na kubaki nje ya mfumo na kuachana na vyama. hapo ningemuelewa. au hata kama angebaki kimya tu, pia ningemuelewa kwamba hapa kuna GREAT MAN ametofautiana na wenzake, ameamua kuachana nao na kukaa kando. lakini kujaribu kuwamaliza? huo kwanza ni ubinafsi na ni kuwasaliti watanzania mamilioni ambao wana imani na siasa za upinzani, hata kama hawakubaliani na CHADEMA. lakini wana imani na upinzani kwa ujumla.
 
(Pichani kitabu kikianza kupatikana kwa Wabunge, Dodoma)

Na. M. M. Mwanakijiji

Umpende au umchukie, umkatae au umkubali, umpinge au umuunge mkono Dkt. Wilbrod Slaa Dr Willibrod Slaa anabakia kuwa miongoni mwa wanasiasa wachache Tanzania ambao alama zao katika zama na nyakati za kisiasa ni vigumu kufutika........

Hata hivyo, kinyume na matarajio ya watu wengi na kinyume na mantiki zilizozoeleka za kisiasa Edward Lowassa aliyekatwa jina lake ndani ya CCM ambako alikuwa anaongoza kwa mashabiki na kura za maoni alikimbilia CHADEMA na kusababisha chama hicho cha upinzani kulala kitanda kimoja na mtu ambaye walitumia muda mwingi kumhusisha na ufisadi nchini. Ilisemwa “yeyote” isipokuwa CCM. Dkt. Slaa akafyekelewa mbali na chama chake na kusababisha mpasuko wa aina yake ndani ya CCM na CHADEMA.

Dkt. Slaa akaamua kuachana na siasa za vyama na yeye na familia yake wakahamia Canada. Miezi michache baadaye Rais John Magufuli alimteua Dkt. Slaa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Sweden kitu ambacho kilitafsiriwa na baadhi ya watu kwa namna mbalimbali.



Kubwa hata hivyo, ni sakata zima la siasa za 2015 na matokeo yake katika upinzani na siasa za Tanzania. Kitabu hiki kinatoa maonyo, mwongozo, na elimu kwa wanasiasa wanaofuatia katika upinzani na chama tawala na wapinzani watarajiwa na watawala watarajia. Mwanasiasa yeyote ni lazima apate nakala ya kitabu hiki, mwanahistoria yeyote ni lazima anunue nakala yake wakati wanafunzi wa shule na vyuo watapata elimu muhimu juu ya uongozi kutoka katika kitabu hiki kilichoandikwa kwa lugha ya Kiswahili.
NAJARIBU TU KUTAFAKARI "YULEYULE ALIYEYAPINGA YALEYALE NA KUMTUKUMU MTU YULEYULE LEO HII KALALA KITANDA KILEKILE CHA WATU WALEWALE HUKU AKITAFUNA KIPANDE CHAKE CHA MKATE PASIPO KELELE WALA MAKEMEO!!!"
UNAFIKI MTUPU!!!
 
Halafu napenda muelewe wala msitake kupotosha, cdm ilivyokuwa iko kwenye damu za wananchi hiyo 2015, ingepata kura nyingi sana iwapo Dr. Slaa angekuwa mgombea, na hata kama asingekuwa rais kutokana na mfumo wa uchaguzi ulivyo, bado cdm ingebaki na haiba yake, kuliko ilivyokuwa baada ya Lowassa kuingia.

Umefafanua vizuri sana; watu hawataki kukubali kuwa wao ndio waliogeuka na hadi hivi sasa hawataki kukubali kuwa walifanya makosa.
 
Ni kweli hayuko ccm, lakini unapokuwa balozi kwa uteuzi wa mwenyekiti wa ccm, hasa mwenyekiti mwenyewe akiwa ni Magufuli, automatically ww ni mwanaccm.

Duh.. hii ni reasoning ya ajabu sana. Huwi mwana CCM kwa vile umekubali kuwa Balozi. Huku ni kutokuelewa mgawanyo wa utendaji serikalini. Hivi kila mtu anayefanya kazi serikalini ni mwana CCM kwa vile tu amekubali kufanya kazi serikalini? au hii ina apply kwa vile tu mtu kateuliwa na Rais? Tutengeneza hoja vizuri. Ili mtu awe mwana CCM kuna masharti yake. Unachotakiwa ni kunionesha kuwa Dkt. Slaa katimiza masharti hayo. Kwa mfano, siyo kila mtu anayepinga CCM ni mpinzani au mwanachama wa CHADEMA. Na siyo kila anayeunga mkono CHADEMA ni "mwanachadema". Katiba zote za vyama vya siasa zina ibara inayoitwa "Masharti ya Uanachama". Pitia hii itakufunulia kidogo kama kweli Dkt. Slaa ni Mwana CCM kwa vile tu ameteuliwa na kushika Ubalozi.
 
Kama ''abstract'' ni hiyo ya MM, nachelea kusema kitabu kitaongelea migogoro zaidi kuliko demokrasia aliyosimamia kwa nguvu. Tuna migogoro ya kutosha! Nahitaji kusoma kitu tofauti.

Kwa kweli uamuzi wa kusoma kitabu hiki ni wa mtu mwenyewe na wala hauitaji ushawishi. Kitabu hiki ni cha maisha ya kisiasa ya Dkt. Slaa; kinaanzia toka kuzaliwa kwake na safari yake ya kitaaluma hadi alipofikia. Kwa ufupi ni kuwa kitabu hiki kiliandikwa kabla ya Dkt. Slaa kuteuliwa kuwa Balozi. Hivyo, hakihusiani na hakideal kwa kiasi kikubwa na yaliyotokea baada ya kuteuliwa Ubalozi.
 
Lowasa ilitumika kama sababu tu, ili aitumie kukisaliti chama,

aliyemteua yeye kuwa balozi ndio huyo huyo aliyemrusisha lowasa ccm, tena kwa kumlazimisha arudi na si kwa hiari yake.

Maana ingekuwa ni mfumo mwingine uliomteua at least hoja yake ingeleta sense,

Lakini pia kubadilika kwa mitazamo yake kuhusu masuala mbalimbali yanayoendelea nchini ni ushahidi mwingine.
 
Duh.. hii ni reasoning ya ajabu sana. Huwi mwana CCM kwa vile umekubali kuwa Balozi. Huku ni kutokuelewa mgawanyo wa utendaji serikalini. Hivi kila mtu anayefanya kazi serikalini ni mwana CCM kwa vile tu amekubali kufanya kazi serikalini? au hii ina apply kwa vile tu mtu kateuliwa na Rais? Tutengeneza hoja vizuri. Ili mtu awe mwana CCM kuna masharti yake. Unachotakiwa ni kunionesha kuwa Dkt. Slaa katimiza masharti hayo. Kwa mfano, siyo kila mtu anayepinga CCM ni mpinzani au mwanachama wa CHADEMA. Na siyo kila anayeunga mkono CHADEMA ni "mwanachadema". Katiba zote za vyama vya siasa zina ibara inayoitwa "Masharti ya Uanachama". Pitia hii itakufunulia kidogo kama kweli Dkt. Slaa ni Mwana CCM kwa vile tu ameteuliwa na kushika Ubalozi.

Mzee tofautisha kufanya kazi serikalini na kuteuliwa na mwenyekiti wa ccm kwa nafasi ya uwakilishi. Nasisitiza tena, unapochaguliwa na Magufuli kwa nafasi ya uwakilishi ww automatically ni mwanaccm, na ndio maana unasikia Slaa anasema yote waliyopiga kelele wapinzani yametekelezwa, huku katiba mpya haijapatikana na demokrasia inayumba vibaya. Nipe tofauti alichoongea Slaa na wanachoongea Makada wa ccm.
 
Mzee tofautisha kufanya kazi serikalini na kuteuliwa na mwenyekiti wa ccm kwa nafasi ya uwakilishi. Nasisitiza tena, unapochaguliwa na Magufuli kwa nafasi ya uwakilishi ww automatically ni mwanaccm, na ndio maana unasikia Slaa anasema yote waliyopiga kelele wapinzani yametekelezwa, huku katiba mpya haijapatikana na demokrasia inayumba vibaya. Nipe tofauti alichoongea Slaa na wanachoongea Makada wa ccm.
Kwa kweli kwa hili siwezi kukusaidia. Inawezekana ama huelewi mfumo wa utendaji kazi na utumishi serikalini au unataka kuendeleza ligi isiyokuwepo. Dkt. Slaa hakuteuliwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi kufanya shughuli za CCM. Lakini pia inawezekana huelewi mgawanyo wa shughuli za chama na shughuli za serikali. Balozi wa nchi yetu haitwi "Balozi wa CCM Italia!"
 
Kwa kweli kwa hili siwezi kukusaidia. Inawezekana ama huelewi mfumo wa utendaji kazi na utumishi serikalini au unataka kuendeleza ligi isiyokuwepo. Dkt. Slaa hakuteuliwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi kufanya shughuli za CCM. Lakini pia inawezekana huelewi mgawanyo wa shughuli za chama na shughuli za serikali. Balozi wa nchi yetu haitwi "Balozi wa CCM Italia!"

Huenda unadhani unaongea na mtu asiyejua lolote hivyo unadhani ninayokuambia nakuambia kwa bahati mbaya, au nina uelewa mdogo wa mambo ya serikali na mipaka ya ccm ndani ya serikali. Kwa taarifa yako Magufuli hajui tofauti kati ya serikali na ccm, na hata kama anajua haheshimu hizo tofauti, hasa kwa watu anaowapa vyeo vya fadhila kama hao mabalozi. Ndio maana nakuambia ukitaka kujua ukichaguliwa na Magufuli unakuwa mwanaccm automatically bila kadi, sikiliza anachoongea sasa hivi baada ya kupewa ubalozi.
 
(Pichani kitabu kikianza kupatikana kwa Wabunge, Dodoma)

Na. M. M. Mwanakijiji

Umpende au umchukie, umkatae au umkubali, umpinge au umuunge mkono Dkt. Wilbrod Slaa Dr Willibrod Slaa anabakia kuwa miongoni mwa wanasiasa wachache Tanzania ambao alama zao katika zama na nyakati za kisiasa ni vigumu kufutika. Unaweza kumuita majina mengi na ya rangi mbalimbali ya kejeli lakini ni vigumu kupuuzia, kudharau au kutupilia mbali mchango wake katika siasa za Tanzania kwa karibu miaka ishirini na mitano. Mchango wake katika kuimarisha siasa za Tanzania akiwa miongoni mwa wabunge wa kwanza kabisa wa upinzani umeacha historia kubwa kuanzia Karatu hadi Dar, toka Tunduru hadi Tarime.

Hata hivyo, matukio ya kisiasa ya mwaka 2015 yanabakia katika historia yetu kama mafundisho makubwa kabisa ya siasa zinavyoweza kuwafanya ndugu wawe maadui, marafiki wake mahasimu, na kutengeneza kile ambacho wenzetu Wamarekani wanasema ni “strange bed fellows” yaani kuwaona watu usiowadhania wamelala kitanda kimoja. Matukio haya yalitokea taifa likiwa katika mwamko mkubwa wa uchaguzi mkuu wa Rais na Wabunge.

Dkt. Slaa akiwa Katibu Mkuu wa chama Kikuu cha upinzani cha CHADEMA, alitarajiwa na alipitishwa na chama chake kuwa mgombea wa Urais huku mtifuano mkubwa ukitarajiwa na hatimaye ulitokea ndani ya Chama cha Mapinduzi. Kwa baadhi ya wachunguzi wa siasa mtifuano au mnyukano uliokuwa unatokea CCM ulifanya kazi ya mgombea wa upinzani uliounganika kuwa ya afueni zaidi.

Hata hivyo, kinyume na matarajio ya watu wengi na kinyume na mantiki zilizozoeleka za kisiasa Edward Lowassa aliyekatwa jina lake ndani ya CCM ambako alikuwa anaongoza kwa mashabiki na kura za maoni alikimbilia CHADEMA na kusababisha chama hicho cha upinzani kulala kitanda kimoja na mtu ambaye walitumia muda mwingi kumhusisha na ufisadi nchini. Ilisemwa “yeyote” isipokuwa CCM. Dkt. Slaa akafyekelewa mbali na chama chake na kusababisha mpasuko wa aina yake ndani ya CCM na CHADEMA.

Dkt. Slaa akaamua kuachana na siasa za vyama na yeye na familia yake wakahamia Canada. Miezi michache baadaye Rais John Magufuli alimteua Dkt. Slaa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Sweden kitu ambacho kilitafsiriwa na baadhi ya watu kwa namna mbalimbali.

Katika kitabu cha NYUMA YA PAZIA Dkt. Slaa anaelezea kwa kina matukio mbalimbali ambayo yalitokea hadi kufikia Lowassa kukaribishwa CHADEMA na kwa nini hakuwa tayari kusimama jukwaani kumnadi Lowassa na akabakia na utimamu wa kimaadili na akili. Hata hivyo, kitabu hiki kinaenda zaidi ya nyuma ya pazia la siasa za 2015. Inatufunulia kumuelewa Dkt. Slaa kwani kwa kiasi chake kitabu hiki pia ni bibliografia (historia ya maisha) ya mwanasiasa huyu nguli, mcheshi, na msomi.

Ndani ya kitabu hiki tunaweza kukutana na mtu ambaye anatufundisha mambo mbalimbali kuhusiana na uongozi. Mojawapo ya mambo ambayo msomaji atayafurahia atakapokutana nayo ni jinsi gani Dkt. Slaa ni mtunzaji mzuri sana wa kumbukumbu. Siyo tu katika akili lakini katika nyaraka na vielelezo mbalimbali. Anataja tarehe, mahali na siku kama shahidi katika kesi nzito. Bila utata anataja pia majina mbalimbali ya wahusika mbalimbali katika ujasiri ambao utawakumbusha watu wengi ile hotuba yake ya “Orodha ya Mafisadi” ya pale Mwembe Yanga.

Kitabu hakigusi siasa tu za 2015 lakini pia kinatudokeza safari ya Dkt. Slaa kutoka upadre hadi kuwa mwanasiasa mbobezi. Wengi watashtushwa, kushangazwa na kuburudishwa na masimulizi yake ya mikutano yake na Baba wa Taifa Mwl. Nyerere wakati huo Dkt. Slaa akiwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu. Pia watakutana na jinsi gani Dkt. Slaa alisimamia kupinga ufisadi ndani ya Kanisa Katoliki kiasi cha kumgonganisha yeye na mmojawapo wa maaskofu waandamizi wa wakati huo. Msomaji pia ataburudishwa na masimulizi yake ya kujaribu kuinua hali na maisha ya watu wa Karatu katika kile ambacho kilimsababishia kuwa mbunge mpendwa sana wa wana Karatu na kuthubutu kufanya kitu ambacho hakikuwahi kufanywa Tanzania – Karatu kuwa Halmashauri ya kwanza ya mji kuongozwa na upinzani.

Kubwa hata hivyo, ni sakata zima la siasa za 2015 na matokeo yake katika upinzani na siasa za Tanzania. Kitabu hiki kinatoa maonyo, mwongozo, na elimu kwa wanasiasa wanaofuatia katika upinzani na chama tawala na wapinzani watarajiwa na watawala watarajia. Mwanasiasa yeyote ni lazima apate nakala ya kitabu hiki, mwanahistoria yeyote ni lazima anunue nakala yake wakati wanafunzi wa shule na vyuo watapata elimu muhimu juu ya uongozi kutoka katika kitabu hiki kilichoandikwa kwa lugha ya Kiswahili.

Nyuma ya pazia ni kitabu kinachomfunua mbele yetu na kutujulisha kwa undani juu ya mtu, maisha, zama na nyakati za Dkt. Wilbrod Slaa, Balozi, Baba, Mume na miongoni mwa viongozi maridadi ambao Tanzania imepata nafasi ya kuwa nao na wameacha alama zisizofutika. Umpende au umchukie, umkatae au umkubali, umpinge au umuunge mkono Dkt. Wilbrod Slaa ametupatia hazina ya maarifa ambayo wenye hekima watawahi kuipata katika nakala chache ambazo zimeshaingia nchini.

UNAWEZA KUPATA NAKALA YAKO WAPI?
Unaweza kupata nakala yako kwa bei ya jumla au rejareja. Bei ya reja reja ni shilingi 20,000/- TU na kwa bei ya jumla unaweza kupata punguzo kubwa kufuatana na mahitaji yako.
Maeneo ya posta, mkabala na Jengo la Benjamin Mkapa karibu na Mahali yanapoegeshwa magari yaendayo Sinza yenye michoro ya Rangi Nyekundu.
Mhudumu Genoveva - 0753 059 144
Au wasiliana na Erasto Tumbo kuweza kuagiza nakala zako:
0713 474707/0688 211683
Siyo lazima kununua kitabu hicho kwani maisha yataenda tu bila ya kijitabu hicho!
Pia kukimbia kwake "choo" sebuleni" na leo analala pamoja na kinyesi chenyewe kunaondoa hadhi na umaarufu walau kidogo alioupata. Na kuwa kumsikiliza Delila wake na kumbu kumbu ya ulaji mihogo vitamtesa sana kwani wenye KUTAFAKARI,KUKUMBUKA NA KUCHAMBUA mambo na watukio watahitimisha kuwa Slaa ni binadamu kama wengine na usaliti ni sehemu ya maisha.Yeye si wa kwanza na hatakuwa wa mwisho. "GODS BITS OF WOOD" -O.SEMBENE na kina SOUNKARE wataendelea kujidhihirisha.
 
Kuna mambo mengi mno KWENYE SIASA yanayohitaji utulivu wa kutosha kuyaelewa
Dk Slaa katika hatua za awali alikubaliana na wazo la LOWASA kujiunga na CHADEMA
Tulipomuuliza kwenye kamati kuu kwanini alikubali kujiunga kwa Lowasa kwenye chama, akatujibu kwamba Lowasa alisema atakuja na mtaji ambao kwa wakati ule Dk alisema hakuuona
Pili alisema alidhani Lowasa atakuwa mwanachama tu lakini hatakuwa mgombea urais
Tatu ,alisema Lowasa atoke hadhani kwa watanzania ajisafishe kwanza kuhusu tuhuma za ufusadi ambazo yeye(Dk slaa)ana ushahidi nazo.
Sisi tulimuita Lowasa mbele ya Dk slaa( katibu mkuu) wetu kipindi hicho na Lowasa akatolea ufafanuzi kila jambo kwa ufasa.
Katika hatua hiyo Dk Slaa akaridhika lakini baadaye hatukumuona bali tulichoona ni barua ya kumkaimisha Salum Mwalimu nafasi yake.
Maoni yangu ya ujumla ni kwamba Dk Slaa alikuwa sahihi kusimamia kile alichokiamini lakini alichoghafilika kidogo ni kuharibu kazi kubwa aliyoipigania kwa miongo miwili mizima yaani robo ya umri wake kwa kukwazwa tu kwa mara moja.
Lazima katika haya mapambano tupime baina ya masilahi mslapana ya jamii na taasisi tunazozisimamia ukilinganisha na masilahi yetu. Nadhani Dk amesimamia masilahi yake zaidi kuliko masilahi mapana ya jamii ya wapenda mageuzi makububwa ya mfumo wa kiutawala.
Kitabu cha Dk mambo mengi ameyasema kwa ukweli kufurahisha watu fulani wa makundi fulani na ndio maana nasema ni wakati wa watanzani kupima wanasisa vizuri bila kujali vyama vyao.
Dk Slaa hawezi kuwaona viongozi wa CHADEMA kama viongozi waliodalalia chama chao. Mwanzoni
kiongozi kama Mbowe,Tindu Lisu,Mnyika walikuwa hawkubaliani kabisa na swala la LOWASA kujiunga na CHADEMA lakini sisi wajumbe wa Kamati kuu ndio tuliowalazimisha baada ya kuona uwezo na nafasi ya Lowasa kukiletea chama ushindi
Hatukukjbsliana kirahisi ila tulipata nguvu ya kuwashawishi baada yakuona kwamba katika hatua za awali Dk Slaa aliunga wazo hilo mkono.
Kwahiyo Dk kushutumu vio gozi wenzake ni kujitetea kusiko na mashiko yoyote.
Lakini mwisho wa siku yote ni historia CHADEMA ipo na itaendelea kuwepo bila kujali mawimbi yanayoikumba,
tukumbuke dr Slaa anatumiwa na chama chake kipya, ccm kuiua CHADEMA.
uchaguzi mwakani atarudishwa kukitetea chama cha ccm,

Moja ya Mjumbe wa kamati kuu aliyekwenda na ujumbe wa kamati ndogo ya kamati kuu kwenda kuongea na Dk Slaa kuhusu uamuzi wake huo.
Jambo kubwa alilolalamika ni kwamba hamkubali LOWASA lakini tatizo kubwa lilokuwa dhahiri ni kwamba alishafanyiwa maandalizi yote ya kuwa mgombea Urais kwanini ghfla tu Kamati kuu inafanya mabadiko ya mgombea.
Tulimpa facts zote lakini hakutaka kutuelewa.
Katika kikao Cha kamati kuu alipewa facts zote kwanini ni muhimu kumkubali Lowasa licha ya upungufu ambao uitajwa kwa LOWASA na kwamba yeye hawezi kukipa chama ushindi au upinzani ambao ungefanana na wa LOWASA pamoja na upungufu ambao LOWASA alisemekana anao.
Kamati kuu ilimuambia Demokrasu ni kuhusu watu na watu wanasema nini kwa wakati huo.
Mwaka 2015 LOWASA alikuwa ni mwanasiasa anayekubalika kwa jamii ya makundi yote kuliko mwanasiasa yoyote kwa kipindi kile hususani kwa wagombea Urais waliokuwa wametia nia.
Tulimueleza Dk kuanza kutafakarifu udhaifu wa Lowasa ambao kwa maeneo mengine umeongezewa chumvi ilihali wananchi wanampenda hakutusaidii kupata ushindi au kutoa upinzani wa kutosha kwa mgombea wa CCM.
Na mimi binafsi nilimuambia Dk Slaa hata kama LOWASA hatashinda Urais lakini atakuwa Katibu mkuu wa Chama kikibwa sana nchini.
Naamini uwezo wa Dk Slaa ni Mkubwa sana kwahiyo angesimama kwenye nafasi ya ukatibu mkuu kipindi kile cha uchaguzi tungepata idadi kubwa ya wabunge na madiwani kuliko tuliopata sasa
Lakuni hata kura za uais huenda zingekuwa nyingi kuliko zilizopatikana kwa matangazo ya Tume ya Uchaguzi
Kwahiyo nadhani kitabu chake anataka tu kuwaaminisha wananchi kuhusu uhalali wa uamuzi wake lakini kama hakuwa na mbegu ya ubinafsi hakupaswa kufanya uamuzi ule aliofanya.
Yote yamepita ,
CHADEMA tunapaswa kusonga mbele kwani haya tunayopitia ndio kanuni za mchakato wa safari tunayotaka kwenda
Kwavyovyote vile safari lazima ifike mwisho

Kuna mambo mengi mno KWENYE SIASA yanayohitaji utulivu wa kutosha kuyaelewa
Dk Slaa katika hatua za awali alikubaliana na wazo la LOWASA kujiunga na CHADEMA
Tulipomuuliza kwenye kamati kuu kwanini alikubali kujiunga kwa Lowasa kwenye chama, akatujibu kwamba Lowasa alisema atakuja na mtaji ambao kwa wakati ule Dk alisema hakuuona
Pili alisema alidhani Lowasa atakuwa mwanachama tu lakini hatakuwa mgombea urais
Tatu ,alisema Lowasa atoke hadhani kwa watanzania ajisafishe kwanza kuhusu tuhuma za ufusadi ambazo yeye(Dk slaa)ana ushahidi nazo.
Sisi tulimuita Lowasa mbele ya Dk slaa( katibu mkuu) wetu kipindi hicho na Lowasa akatolea ufafanuzi kila jambo kwa ufasa.
Katika hatua hiyo Dk Slaa akaridhika lakini baadaye hatukumuona bali tulichoona ni barua ya kumkaimisha Salum Mwalimu nafasi yake.
Maoni yangu ya ujumla ni kwamba Dk Slaa alikuwa sahihi kusimamia kile alichokiamini lakini alichoghafilika kidogo ni kuharibu kazi kubwa aliyoipigania kwa miongo miwili mizima yaani robo ya umri wake kwa kukwazwa tu kwa mara moja.
Lazima katika haya mapambano tupime baina ya masilahi mslapana ya jamii na taasisi tunazozisimamia ukilinganisha na masilahi yetu. Nadhani Dk amesimamia masilahi yake zaidi kuliko masilahi mapana ya jamii ya wapenda mageuzi makububwa ya mfumo wa kiutawala.
Kitabu cha Dk mambo mengi ameyasema kwa ukweli kufurahisha watu fulani wa makundi fulani na ndio maana nasema ni wakati wa watanzani kupima wanasisa vizuri bila kujali vyama vyao.
Dk Slaa hawezi kuwaona viongozi wa CHADEMA kama viongozi waliodalalia chama chao. .

Hadithiii ndeefuuu.. Ujinga mtupu!

Nyie ni matapeli wa kisiasa tu kama walivyo matapeli wengine!
 
Kinyesi kimemfuata chumbani sebuleni backyard?
Mama junior hujambo habari za sweeden, sisi huku bado tunasubiri ahadi ya shule yetu uliyotuahidi kabla ya kukimbilia ughaibuni.

Huku kwetu Ibwera umasikini umezidi maisha ni magumu kuliko wakati wa JK, tunashindia mihogo ukipata tutumie angalau kidogo.

Mpao obashule bona okwo omumahanga
 
(Pichani kitabu kikianza kupatikana kwa Wabunge, Dodoma)

Na. M. M. Mwanakijiji

Umpende au umchukie, umkatae au umkubali, umpinge au umuunge mkono Dkt. Wilbrod Slaa Dr Willibrod Slaa anabakia kuwa miongoni mwa wanasiasa wachache Tanzania ambao alama zao katika zama na nyakati za kisiasa ni vigumu kufutika. Unaweza kumuita majina mengi na ya rangi mbalimbali ya kejeli lakini ni vigumu kupuuzia, kudharau au kutupilia mbali mchango wake katika siasa za Tanzania kwa karibu miaka ishirini na mitano. Mchango wake katika kuimarisha siasa za Tanzania akiwa miongoni mwa wabunge wa kwanza kabisa wa upinzani umeacha historia kubwa kuanzia Karatu hadi Dar, toka Tunduru hadi Tarime.

Hata hivyo, matukio ya kisiasa ya mwaka 2015 yanabakia katika historia yetu kama mafundisho makubwa kabisa ya siasa zinavyoweza kuwafanya ndugu wawe maadui, marafiki wake mahasimu, na kutengeneza kile ambacho wenzetu Wamarekani wanasema ni “strange bed fellows” yaani kuwaona watu usiowadhania wamelala kitanda kimoja. Matukio haya yalitokea taifa likiwa katika mwamko mkubwa wa uchaguzi mkuu wa Rais na Wabunge.

Dkt. Slaa akiwa Katibu Mkuu wa chama Kikuu cha upinzani cha CHADEMA, alitarajiwa na alipitishwa na chama chake kuwa mgombea wa Urais huku mtifuano mkubwa ukitarajiwa na hatimaye ulitokea ndani ya Chama cha Mapinduzi. Kwa baadhi ya wachunguzi wa siasa mtifuano au mnyukano uliokuwa unatokea CCM ulifanya kazi ya mgombea wa upinzani uliounganika kuwa ya afueni zaidi.

Hata hivyo, kinyume na matarajio ya watu wengi na kinyume na mantiki zilizozoeleka za kisiasa Edward Lowassa aliyekatwa jina lake ndani ya CCM ambako alikuwa anaongoza kwa mashabiki na kura za maoni alikimbilia CHADEMA na kusababisha chama hicho cha upinzani kulala kitanda kimoja na mtu ambaye walitumia muda mwingi kumhusisha na ufisadi nchini. Ilisemwa “yeyote” isipokuwa CCM. Dkt. Slaa akafyekelewa mbali na chama chake na kusababisha mpasuko wa aina yake ndani ya CCM na CHADEMA.

Dkt. Slaa akaamua kuachana na siasa za vyama na yeye na familia yake wakahamia Canada. Miezi michache baadaye Rais John Magufuli alimteua Dkt. Slaa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Sweden kitu ambacho kilitafsiriwa na baadhi ya watu kwa namna mbalimbali.

Katika kitabu cha NYUMA YA PAZIA Dkt. Slaa anaelezea kwa kina matukio mbalimbali ambayo yalitokea hadi kufikia Lowassa kukaribishwa CHADEMA na kwa nini hakuwa tayari kusimama jukwaani kumnadi Lowassa na akabakia na utimamu wa kimaadili na akili. Hata hivyo, kitabu hiki kinaenda zaidi ya nyuma ya pazia la siasa za 2015. Inatufunulia kumuelewa Dkt. Slaa kwani kwa kiasi chake kitabu hiki pia ni bibliografia (historia ya maisha) ya mwanasiasa huyu nguli, mcheshi, na msomi.

Ndani ya kitabu hiki tunaweza kukutana na mtu ambaye anatufundisha mambo mbalimbali kuhusiana na uongozi. Mojawapo ya mambo ambayo msomaji atayafurahia atakapokutana nayo ni jinsi gani Dkt. Slaa ni mtunzaji mzuri sana wa kumbukumbu. Siyo tu katika akili lakini katika nyaraka na vielelezo mbalimbali. Anataja tarehe, mahali na siku kama shahidi katika kesi nzito. Bila utata anataja pia majina mbalimbali ya wahusika mbalimbali katika ujasiri ambao utawakumbusha watu wengi ile hotuba yake ya “Orodha ya Mafisadi” ya pale Mwembe Yanga.

Kitabu hakigusi siasa tu za 2015 lakini pia kinatudokeza safari ya Dkt. Slaa kutoka upadre hadi kuwa mwanasiasa mbobezi. Wengi watashtushwa, kushangazwa na kuburudishwa na masimulizi yake ya mikutano yake na Baba wa Taifa Mwl. Nyerere wakati huo Dkt. Slaa akiwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu. Pia watakutana na jinsi gani Dkt. Slaa alisimamia kupinga ufisadi ndani ya Kanisa Katoliki kiasi cha kumgonganisha yeye na mmojawapo wa maaskofu waandamizi wa wakati huo. Msomaji pia ataburudishwa na masimulizi yake ya kujaribu kuinua hali na maisha ya watu wa Karatu katika kile ambacho kilimsababishia kuwa mbunge mpendwa sana wa wana Karatu na kuthubutu kufanya kitu ambacho hakikuwahi kufanywa Tanzania – Karatu kuwa Halmashauri ya kwanza ya mji kuongozwa na upinzani.

Kubwa hata hivyo, ni sakata zima la siasa za 2015 na matokeo yake katika upinzani na siasa za Tanzania. Kitabu hiki kinatoa maonyo, mwongozo, na elimu kwa wanasiasa wanaofuatia katika upinzani na chama tawala na wapinzani watarajiwa na watawala watarajia. Mwanasiasa yeyote ni lazima apate nakala ya kitabu hiki, mwanahistoria yeyote ni lazima anunue nakala yake wakati wanafunzi wa shule na vyuo watapata elimu muhimu juu ya uongozi kutoka katika kitabu hiki kilichoandikwa kwa lugha ya Kiswahili.

Nyuma ya pazia ni kitabu kinachomfunua mbele yetu na kutujulisha kwa undani juu ya mtu, maisha, zama na nyakati za Dkt. Wilbrod Slaa, Balozi, Baba, Mume na miongoni mwa viongozi maridadi ambao Tanzania imepata nafasi ya kuwa nao na wameacha alama zisizofutika. Umpende au umchukie, umkatae au umkubali, umpinge au umuunge mkono Dkt. Wilbrod Slaa ametupatia hazina ya maarifa ambayo wenye hekima watawahi kuipata katika nakala chache ambazo zimeshaingia nchini.

UNAWEZA KUPATA NAKALA YAKO WAPI?
Unaweza kupata nakala yako kwa bei ya jumla au rejareja. Bei ya reja reja ni shilingi 20,000/- TU na kwa bei ya jumla unaweza kupata punguzo kubwa kufuatana na mahitaji yako.
Maeneo ya posta, mkabala na Jengo la Benjamin Mkapa karibu na Mahali yanapoegeshwa magari yaendayo Sinza yenye michoro ya Rangi Nyekundu.
Mhudumu Genoveva - 0753 059 144
Au wasiliana na Erasto Tumbo kuweza kuagiza nakala zako:
0713 474707/0688 211683
Ujinga tu. watu wenye akili tupo tunawekeza kwenye viwanda na biashara kubwa, we upo busy unawekeza kwenye majungu tu.

We mzee bado una mentality za kimasikini
 
Katika kitabu cha NYUMA YA PAZIA Dkt. Slaa anaelezea kwa kina matukio mbalimbali ambayo yalitokea hadi kufikia Lowassa kukaribishwa CHADEMA na kwa nini hakuwa tayari kusimama jukwaani kumnadi Lowassa na akabakia na utimamu wa kimaadili na akili.
Huyu bwana ni muongo sasa Lowasa amesharudi na yuko CCM tayari unafikiri zile siri kama zipo za alichokifanya lowasa atakizungumzia tena humo, sijui kama watakutana uso kwa uso
 
All in all tutai- miss sana CDM ya Dr. Slaa, jiwe mjanja sana aliona atumie kila namna kumtoa Dr. kutoka CDM,
 
Laana ya tamaa; kweli wazee achaneni kuoa uzeeni. Bado anaamini kua Lowasa ndo kilimuondoa CDM? Mwezie Lipumba alisharudi na yeye pia atarudi. Yaani Dr Slaa anadhani kua kilichokua kinatendeka alikijua yeye na Fina pekee?
 
Back
Top Bottom