NYUMA YA PAZIA: CHADEMA ilivyosalitiwa 2015 - Dkt. Slaa

NYUMA YA PAZIA: CHADEMA ilivyosalitiwa 2015 - Dkt. Slaa

Japo Dr.Slaa alizingua lakini bado anabaki kuwa mwanasiasa makini kwa Tanzania..Binafsi nitakwenda nunua hiki kitabu...MENGINE NAJUA ILIKUWA MIPANGO YA KATOLIKI Kuweka pandikizi lao,CHADEMA walichemka sana kumpa nafasi Lowassa yakupeperusha bendera 2015 dhidi ya MKATOLIKI Magufuli.Hapo ilitakiwa asimame Dr.Slaa na hakika Leo kusingekuwa na Ccm....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna kiongozi Tz aliyenivutia kushabikia siasa za upinzani kama dr W. Slaa.
Lakini tangu 'walivyomnywa' mafisadi kihuni, sina hamu tena Cdm.

Sasa huku ninakoishi mkoani Kgm ntakipataje, japo umetoa namba za simu?
Wasifu uliompatia kwenye thread hii unamstahili.
Wasiomuelewa vizuri dr.Slaa hawatakuelewa
 
(Pichani kitabu kikianza kupatikana kwa Wabunge, Dodoma)

Na. M. M. Mwanakijiji

Umpende au umchukie, umkatae au umkubali, umpinge au umuunge mkono Dkt. Wilbrod Slaa Dr Willibrod Slaa anabakia kuwa miongoni mwa wanasiasa wachache Tanzania ambao alama zao katika zama na nyakati za kisiasa ni vigumu kufutika. Unaweza kumuita majina mengi na ya rangi mbalimbali ya kejeli lakini ni vigumu kupuuzia, kudharau au kutupilia mbali mchango wake katika siasa za Tanzania kwa karibu miaka ishirini na mitano. Mchango wake katika kuimarisha siasa za Tanzania akiwa miongoni mwa wabunge wa kwanza kabisa wa upinzani umeacha historia kubwa kuanzia Karatu hadi Dar, toka Tunduru hadi Tarime.

Hata hivyo, matukio ya kisiasa ya mwaka 2015 yanabakia katika historia yetu kama mafundisho makubwa kabisa ya siasa zinavyoweza kuwafanya ndugu wawe maadui, marafiki wake mahasimu, na kutengeneza kile ambacho wenzetu Wamarekani wanasema ni “strange bed fellows” yaani kuwaona watu usiowadhania wamelala kitanda kimoja. Matukio haya yalitokea taifa likiwa katika mwamko mkubwa wa uchaguzi mkuu wa Rais na Wabunge.

Dkt. Slaa akiwa Katibu Mkuu wa chama Kikuu cha upinzani cha CHADEMA, alitarajiwa na alipitishwa na chama chake kuwa mgombea wa Urais huku mtifuano mkubwa ukitarajiwa na hatimaye ulitokea ndani ya Chama cha Mapinduzi. Kwa baadhi ya wachunguzi wa siasa mtifuano au mnyukano uliokuwa unatokea CCM ulifanya kazi ya mgombea wa upinzani uliounganika kuwa ya afueni zaidi.

Hata hivyo, kinyume na matarajio ya watu wengi na kinyume na mantiki zilizozoeleka za kisiasa Edward Lowassa aliyekatwa jina lake ndani ya CCM ambako alikuwa anaongoza kwa mashabiki na kura za maoni alikimbilia CHADEMA na kusababisha chama hicho cha upinzani kulala kitanda kimoja na mtu ambaye walitumia muda mwingi kumhusisha na ufisadi nchini. Ilisemwa “yeyote” isipokuwa CCM. Dkt. Slaa akafyekelewa mbali na chama chake na kusababisha mpasuko wa aina yake ndani ya CCM na CHADEMA.

Dkt. Slaa akaamua kuachana na siasa za vyama na yeye na familia yake wakahamia Canada. Miezi michache baadaye Rais John Magufuli alimteua Dkt. Slaa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Sweden kitu ambacho kilitafsiriwa na baadhi ya watu kwa namna mbalimbali.

Katika kitabu cha NYUMA YA PAZIA Dkt. Slaa anaelezea kwa kina matukio mbalimbali ambayo yalitokea hadi kufikia Lowassa kukaribishwa CHADEMA na kwa nini hakuwa tayari kusimama jukwaani kumnadi Lowassa na akabakia na utimamu wa kimaadili na akili. Hata hivyo, kitabu hiki kinaenda zaidi ya nyuma ya pazia la siasa za 2015. Inatufunulia kumuelewa Dkt. Slaa kwani kwa kiasi chake kitabu hiki pia ni bibliografia (historia ya maisha) ya mwanasiasa huyu nguli, mcheshi, na msomi.

Ndani ya kitabu hiki tunaweza kukutana na mtu ambaye anatufundisha mambo mbalimbali kuhusiana na uongozi. Mojawapo ya mambo ambayo msomaji atayafurahia atakapokutana nayo ni jinsi gani Dkt. Slaa ni mtunzaji mzuri sana wa kumbukumbu. Siyo tu katika akili lakini katika nyaraka na vielelezo mbalimbali. Anataja tarehe, mahali na siku kama shahidi katika kesi nzito. Bila utata anataja pia majina mbalimbali ya wahusika mbalimbali katika ujasiri ambao utawakumbusha watu wengi ile hotuba yake ya “Orodha ya Mafisadi” ya pale Mwembe Yanga.

Kitabu hakigusi siasa tu za 2015 lakini pia kinatudokeza safari ya Dkt. Slaa kutoka upadre hadi kuwa mwanasiasa mbobezi. Wengi watashtushwa, kushangazwa na kuburudishwa na masimulizi yake ya mikutano yake na Baba wa Taifa Mwl. Nyerere wakati huo Dkt. Slaa akiwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu. Pia watakutana na jinsi gani Dkt. Slaa alisimamia kupinga ufisadi ndani ya Kanisa Katoliki kiasi cha kumgonganisha yeye na mmojawapo wa maaskofu waandamizi wa wakati huo. Msomaji pia ataburudishwa na masimulizi yake ya kujaribu kuinua hali na maisha ya watu wa Karatu katika kile ambacho kilimsababishia kuwa mbunge mpendwa sana wa wana Karatu na kuthubutu kufanya kitu ambacho hakikuwahi kufanywa Tanzania – Karatu kuwa Halmashauri ya kwanza ya mji kuongozwa na upinzani.

Kubwa hata hivyo, ni sakata zima la siasa za 2015 na matokeo yake katika upinzani na siasa za Tanzania. Kitabu hiki kinatoa maonyo, mwongozo, na elimu kwa wanasiasa wanaofuatia katika upinzani na chama tawala na wapinzani watarajiwa na watawala watarajia. Mwanasiasa yeyote ni lazima apate nakala ya kitabu hiki, mwanahistoria yeyote ni lazima anunue nakala yake wakati wanafunzi wa shule na vyuo watapata elimu muhimu juu ya uongozi kutoka katika kitabu hiki kilichoandikwa kwa lugha ya Kiswahili.

Nyuma ya pazia ni kitabu kinachomfunua mbele yetu na kutujulisha kwa undani juu ya mtu, maisha, zama na nyakati za Dkt. Wilbrod Slaa, Balozi, Baba, Mume na miongoni mwa viongozi maridadi ambao Tanzania imepata nafasi ya kuwa nao na wameacha alama zisizofutika. Umpende au umchukie, umkatae au umkubali, umpinge au umuunge mkono Dkt. Wilbrod Slaa ametupatia hazina ya maarifa ambayo wenye hekima watawahi kuipata katika nakala chache ambazo zimeshaingia nchini.

UNAWEZA KUPATA NAKALA YAKO WAPI?
Unaweza kupata nakala yako kwa bei ya jumla au rejareja. Bei ya reja reja ni shilingi 20,000/- TU na kwa bei ya jumla unaweza kupata punguzo kubwa kufuatana na mahitaji yako.
Maeneo ya posta, mkabala na Jengo la Benjamin Mkapa karibu na Mahali yanapoegeshwa magari yaendayo Sinza yenye michoro ya Rangi Nyekundu.
Mhudumu Genoveva - 0753 059 144
Au wasiliana na Erasto Tumbo kuweza kuagiza nakala zako:
0713 474707/0688 211683
Ujïnga mtupu. Amerudi Lowassa amkimbie tena. Hoja yako ya matangazo ni dhaifu haifikirishi.
 
Bila Shaka na prof lipumba naye yupo chimbo kutuletea hadithi Kama hii hasa 2015 kilichotokea niwaambie tu hiki kimetoka kimkakati zaidiii hasa ukizingatia uchaguzi upo jirani LENGO NI KUTUGAWA TU WATANZANIA
 
Usikubali kufungwa mawazo wako na hisia. Ukisoma vitu vinavyokufurahisha kihisia tu utajikuta kuwa mawazo yako yanatawaliwa na hisia. Hatusomi au kujifunza kwa watu tunaokubaliana nao tu bali hata tusiokubaliana nao au wale ambao hatuwajui kabisa kiasi cha kuweza kuchagua upande. Kuna watu humu nawasoma inaonekana na wao waliumia sana kwa Dkt. Slaa kufanya maamuzi aliyoyafanya na hivyo hisia zao na labda akili zimeumizwa mno kiasi kwamba ukitaka "Dkt. Slaa" wanakuwa kama Manchurian Candidate. Mtu aliyekomaa kihisia, kiakili na kisiasa haogopi au hajidhanii kuwa hafai kujisomea mambo kutoka kwa mtu asiyekubaliana naye. NI suala la ukomavu tu.

Kwa wale ambao wanapanga kusoma au tayari wamesoma nina uhakika watamaliza wakiwa na ufahamu mkubwa sana kuhusu maisha na siasa za Dkt. Slaa na kwa kiasi kikubwa wataweka mitazamo yao katika mitazamo sahihi na labda hata kubadilisha mawazo yao au kuyathibitisha waliyokuwa nayo awali
 
Haya uliyoyasema ndio ukweli Wenyewe, sijui shetani gani alimpitia huyu Dr Slaa, alipambana miaka mingi kuleta mabadiliko yenye tija ktk nchi hii lakini alishindwa maamuzi ya muda mfupi tu 2015 na kupotexa mwelekeo mazima.
Mweh..Sasa kitabu kinajaribu kujibu swali hili kwa kina.
 
Ngoja nipitie copy yangu hapo
(Pichani kitabu kikianza kupatikana kwa Wabunge, Dodoma)

Na. M. M. Mwanakijiji

Umpende au umchukie, umkatae au umkubali, umpinge au umuunge mkono Dkt. Wilbrod Slaa Dr Willibrod Slaa anabakia kuwa miongoni mwa wanasiasa wachache Tanzania ambao alama zao katika zama na nyakati za kisiasa ni vigumu kufutika. Unaweza kumuita majina mengi na ya rangi mbalimbali ya kejeli lakini ni vigumu kupuuzia, kudharau au kutupilia mbali mchango wake katika siasa za Tanzania kwa karibu miaka ishirini na mitano. Mchango wake katika kuimarisha siasa za Tanzania akiwa miongoni mwa wabunge wa kwanza kabisa wa upinzani umeacha historia kubwa kuanzia Karatu hadi Dar, toka Tunduru hadi Tarime.

Hata hivyo, matukio ya kisiasa ya mwaka 2015 yanabakia katika historia yetu kama mafundisho makubwa kabisa ya siasa zinavyoweza kuwafanya ndugu wawe maadui, marafiki wake mahasimu, na kutengeneza kile ambacho wenzetu Wamarekani wanasema ni “strange bed fellows” yaani kuwaona watu usiowadhania wamelala kitanda kimoja. Matukio haya yalitokea taifa likiwa katika mwamko mkubwa wa uchaguzi mkuu wa Rais na Wabunge.

Dkt. Slaa akiwa Katibu Mkuu wa chama Kikuu cha upinzani cha CHADEMA, alitarajiwa na alipitishwa na chama chake kuwa mgombea wa Urais huku mtifuano mkubwa ukitarajiwa na hatimaye ulitokea ndani ya Chama cha Mapinduzi. Kwa baadhi ya wachunguzi wa siasa mtifuano au mnyukano uliokuwa unatokea CCM ulifanya kazi ya mgombea wa upinzani uliounganika kuwa ya afueni zaidi.

Hata hivyo, kinyume na matarajio ya watu wengi na kinyume na mantiki zilizozoeleka za kisiasa Edward Lowassa aliyekatwa jina lake ndani ya CCM ambako alikuwa anaongoza kwa mashabiki na kura za maoni alikimbilia CHADEMA na kusababisha chama hicho cha upinzani kulala kitanda kimoja na mtu ambaye walitumia muda mwingi kumhusisha na ufisadi nchini. Ilisemwa “yeyote” isipokuwa CCM. Dkt. Slaa akafyekelewa mbali na chama chake na kusababisha mpasuko wa aina yake ndani ya CCM na CHADEMA.

Dkt. Slaa akaamua kuachana na siasa za vyama na yeye na familia yake wakahamia Canada. Miezi michache baadaye Rais John Magufuli alimteua Dkt. Slaa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Sweden kitu ambacho kilitafsiriwa na baadhi ya watu kwa namna mbalimbali.

Katika kitabu cha NYUMA YA PAZIA Dkt. Slaa anaelezea kwa kina matukio mbalimbali ambayo yalitokea hadi kufikia Lowassa kukaribishwa CHADEMA na kwa nini hakuwa tayari kusimama jukwaani kumnadi Lowassa na akabakia na utimamu wa kimaadili na akili. Hata hivyo, kitabu hiki kinaenda zaidi ya nyuma ya pazia la siasa za 2015. Inatufunulia kumuelewa Dkt. Slaa kwani kwa kiasi chake kitabu hiki pia ni bibliografia (historia ya maisha) ya mwanasiasa huyu nguli, mcheshi, na msomi.

Ndani ya kitabu hiki tunaweza kukutana na mtu ambaye anatufundisha mambo mbalimbali kuhusiana na uongozi. Mojawapo ya mambo ambayo msomaji atayafurahia atakapokutana nayo ni jinsi gani Dkt. Slaa ni mtunzaji mzuri sana wa kumbukumbu. Siyo tu katika akili lakini katika nyaraka na vielelezo mbalimbali. Anataja tarehe, mahali na siku kama shahidi katika kesi nzito. Bila utata anataja pia majina mbalimbali ya wahusika mbalimbali katika ujasiri ambao utawakumbusha watu wengi ile hotuba yake ya “Orodha ya Mafisadi” ya pale Mwembe Yanga.

Kitabu hakigusi siasa tu za 2015 lakini pia kinatudokeza safari ya Dkt. Slaa kutoka upadre hadi kuwa mwanasiasa mbobezi. Wengi watashtushwa, kushangazwa na kuburudishwa na masimulizi yake ya mikutano yake na Baba wa Taifa Mwl. Nyerere wakati huo Dkt. Slaa akiwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu. Pia watakutana na jinsi gani Dkt. Slaa alisimamia kupinga ufisadi ndani ya Kanisa Katoliki kiasi cha kumgonganisha yeye na mmojawapo wa maaskofu waandamizi wa wakati huo. Msomaji pia ataburudishwa na masimulizi yake ya kujaribu kuinua hali na maisha ya watu wa Karatu katika kile ambacho kilimsababishia kuwa mbunge mpendwa sana wa wana Karatu na kuthubutu kufanya kitu ambacho hakikuwahi kufanywa Tanzania – Karatu kuwa Halmashauri ya kwanza ya mji kuongozwa na upinzani.

Kubwa hata hivyo, ni sakata zima la siasa za 2015 na matokeo yake katika upinzani na siasa za Tanzania. Kitabu hiki kinatoa maonyo, mwongozo, na elimu kwa wanasiasa wanaofuatia katika upinzani na chama tawala na wapinzani watarajiwa na watawala watarajia. Mwanasiasa yeyote ni lazima apate nakala ya kitabu hiki, mwanahistoria yeyote ni lazima anunue nakala yake wakati wanafunzi wa shule na vyuo watapata elimu muhimu juu ya uongozi kutoka katika kitabu hiki kilichoandikwa kwa lugha ya Kiswahili.

Nyuma ya pazia ni kitabu kinachomfunua mbele yetu na kutujulisha kwa undani juu ya mtu, maisha, zama na nyakati za Dkt. Wilbrod Slaa, Balozi, Baba, Mume na miongoni mwa viongozi maridadi ambao Tanzania imepata nafasi ya kuwa nao na wameacha alama zisizofutika. Umpende au umchukie, umkatae au umkubali, umpinge au umuunge mkono Dkt. Wilbrod Slaa ametupatia hazina ya maarifa ambayo wenye hekima watawahi kuipata katika nakala chache ambazo zimeshaingia nchini.

UNAWEZA KUPATA NAKALA YAKO WAPI?
Unaweza kupata nakala yako kwa bei ya jumla au rejareja. Bei ya reja reja ni shilingi 20,000/- TU na kwa bei ya jumla unaweza kupata punguzo kubwa kufuatana na mahitaji yako.
Maeneo ya posta, mkabala na Jengo la Benjamin Mkapa karibu na Mahali yanapoegeshwa magari yaendayo Sinza yenye michoro ya Rangi Nyekundu.
Mhudumu Genoveva - 0753 059 144
Au wasiliana na Erasto Tumbo kuweza kuagiza nakala zako:
0713 474707/0688 211683
 
Mzee Mwanakijiji Gulwa na Laface77 wanadai Dr. Slaa ni mzinzi toka akiwa Padri na baada ya kuacha Upadri, ni kweli? Na je kwenye hicho kitabu chake kaelezea ilikuwaje aliacha Upadri. Jee Suala la Uzinzi ni sababu mojawapo ya kuacha Upadri?
Mweh Sasa sasa usome kitabu...na hata hapo juu hujasoma nilichosema? Ni uvivu wa aina gani huu??!!
 
(Pichani kitabu kikianza kupatikana kwa Wabunge, Dodoma)

Na. M. M. Mwanakijiji

Umpende au umchukie, umkatae au umkubali, umpinge au umuunge mkono Dkt. Wilbrod Slaa Dr Willibrod Slaa anabakia kuwa miongoni mwa wanasiasa wachache Tanzania ambao alama zao katika zama na nyakati za kisiasa ni vigumu kufutika. Unaweza kumuita majina mengi na ya rangi mbalimbali ya kejeli lakini ni vigumu kupuuzia, kudharau au kutupilia mbali mchango wake katika siasa za Tanzania kwa karibu miaka ishirini na mitano. Mchango wake katika kuimarisha siasa za Tanzania akiwa miongoni mwa wabunge wa kwanza kabisa wa upinzani umeacha historia kubwa kuanzia Karatu hadi Dar, toka Tunduru hadi Tarime.

Hata hivyo, matukio ya kisiasa ya mwaka 2015 yanabakia katika historia yetu kama mafundisho makubwa kabisa ya siasa zinavyoweza kuwafanya ndugu wawe maadui, marafiki wake mahasimu, na kutengeneza kile ambacho wenzetu Wamarekani wanasema ni “strange bed fellows” yaani kuwaona watu usiowadhania wamelala kitanda kimoja. Matukio haya yalitokea taifa likiwa katika mwamko mkubwa wa uchaguzi mkuu wa Rais na Wabunge.

Dkt. Slaa akiwa Katibu Mkuu wa chama Kikuu cha upinzani cha CHADEMA, alitarajiwa na alipitishwa na chama chake kuwa mgombea wa Urais huku mtifuano mkubwa ukitarajiwa na hatimaye ulitokea ndani ya Chama cha Mapinduzi. Kwa baadhi ya wachunguzi wa siasa mtifuano au mnyukano uliokuwa unatokea CCM ulifanya kazi ya mgombea wa upinzani uliounganika kuwa ya afueni zaidi.

Hata hivyo, kinyume na matarajio ya watu wengi na kinyume na mantiki zilizozoeleka za kisiasa Edward Lowassa aliyekatwa jina lake ndani ya CCM ambako alikuwa anaongoza kwa mashabiki na kura za maoni alikimbilia CHADEMA na kusababisha chama hicho cha upinzani kulala kitanda kimoja na mtu ambaye walitumia muda mwingi kumhusisha na ufisadi nchini. Ilisemwa “yeyote” isipokuwa CCM. Dkt. Slaa akafyekelewa mbali na chama chake na kusababisha mpasuko wa aina yake ndani ya CCM na CHADEMA.

Dkt. Slaa akaamua kuachana na siasa za vyama na yeye na familia yake wakahamia Canada. Miezi michache baadaye Rais John Magufuli alimteua Dkt. Slaa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Sweden kitu ambacho kilitafsiriwa na baadhi ya watu kwa namna mbalimbali.

Katika kitabu cha NYUMA YA PAZIA Dkt. Slaa anaelezea kwa kina matukio mbalimbali ambayo yalitokea hadi kufikia Lowassa kukaribishwa CHADEMA na kwa nini hakuwa tayari kusimama jukwaani kumnadi Lowassa na akabakia na utimamu wa kimaadili na akili. Hata hivyo, kitabu hiki kinaenda zaidi ya nyuma ya pazia la siasa za 2015. Inatufunulia kumuelewa Dkt. Slaa kwani kwa kiasi chake kitabu hiki pia ni bibliografia (historia ya maisha) ya mwanasiasa huyu nguli, mcheshi, na msomi.

Ndani ya kitabu hiki tunaweza kukutana na mtu ambaye anatufundisha mambo mbalimbali kuhusiana na uongozi. Mojawapo ya mambo ambayo msomaji atayafurahia atakapokutana nayo ni jinsi gani Dkt. Slaa ni mtunzaji mzuri sana wa kumbukumbu. Siyo tu katika akili lakini katika nyaraka na vielelezo mbalimbali. Anataja tarehe, mahali na siku kama shahidi katika kesi nzito. Bila utata anataja pia majina mbalimbali ya wahusika mbalimbali katika ujasiri ambao utawakumbusha watu wengi ile hotuba yake ya “Orodha ya Mafisadi” ya pale Mwembe Yanga.

Kitabu hakigusi siasa tu za 2015 lakini pia kinatudokeza safari ya Dkt. Slaa kutoka upadre hadi kuwa mwanasiasa mbobezi. Wengi watashtushwa, kushangazwa na kuburudishwa na masimulizi yake ya mikutano yake na Baba wa Taifa Mwl. Nyerere wakati huo Dkt. Slaa akiwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu. Pia watakutana na jinsi gani Dkt. Slaa alisimamia kupinga ufisadi ndani ya Kanisa Katoliki kiasi cha kumgonganisha yeye na mmojawapo wa maaskofu waandamizi wa wakati huo. Msomaji pia ataburudishwa na masimulizi yake ya kujaribu kuinua hali na maisha ya watu wa Karatu katika kile ambacho kilimsababishia kuwa mbunge mpendwa sana wa wana Karatu na kuthubutu kufanya kitu ambacho hakikuwahi kufanywa Tanzania – Karatu kuwa Halmashauri ya kwanza ya mji kuongozwa na upinzani.

Kubwa hata hivyo, ni sakata zima la siasa za 2015 na matokeo yake katika upinzani na siasa za Tanzania. Kitabu hiki kinatoa maonyo, mwongozo, na elimu kwa wanasiasa wanaofuatia katika upinzani na chama tawala na wapinzani watarajiwa na watawala watarajia. Mwanasiasa yeyote ni lazima apate nakala ya kitabu hiki, mwanahistoria yeyote ni lazima anunue nakala yake wakati wanafunzi wa shule na vyuo watapata elimu muhimu juu ya uongozi kutoka katika kitabu hiki kilichoandikwa kwa lugha ya Kiswahili.

Nyuma ya pazia ni kitabu kinachomfunua mbele yetu na kutujulisha kwa undani juu ya mtu, maisha, zama na nyakati za Dkt. Wilbrod Slaa, Balozi, Baba, Mume na miongoni mwa viongozi maridadi ambao Tanzania imepata nafasi ya kuwa nao na wameacha alama zisizofutika. Umpende au umchukie, umkatae au umkubali, umpinge au umuunge mkono Dkt. Wilbrod Slaa ametupatia hazina ya maarifa ambayo wenye hekima watawahi kuipata katika nakala chache ambazo zimeshaingia nchini.

UNAWEZA KUPATA NAKALA YAKO WAPI?
Unaweza kupata nakala yako kwa bei ya jumla au rejareja. Bei ya reja reja ni shilingi 20,000/- TU na kwa bei ya jumla unaweza kupata punguzo kubwa kufuatana na mahitaji yako.
Maeneo ya posta, mkabala na Jengo la Benjamin Mkapa karibu na Mahali yanapoegeshwa magari yaendayo Sinza yenye michoro ya Rangi Nyekundu.
Mhudumu Genoveva - 0753 059 144
Au wasiliana na Erasto Tumbo kuweza kuagiza nakala zako:
0713 474707/0688 211683
Huko nyuma tulikuwa pamoja na Padre Slaa vizuri tu. Lakini alipoingia Lowasa CHADEMA, sikumwelewa kabisa Slaa. Ningeelewa kama angekaa pembeni na kuachana na siasa, akatulia. Lakini kuiunga mkono serikali ya CCM? hapo sitakaa nimuelewe kabisa - eti hana chama!! thubutu yake!! anaganga njaa tu kama wengine. Slaa amekuwa mwepesi sana.
 
Dr Slaa hawezi kuwa mwalimu mzuri wa siasa kwa sasa.

CHADEMA ni center party kinachofuata ideology ya social democracy na kwa miaka yake yote katika siasa amehubiri ideology alipohama CDM hakutangaza kuwa ideology hiyo ilikuwa haifai je kuhamia Kwake ccm amekubaliana na ideology ya ujamaa ya ccm ?

Kwangu mimi Dr Slaa ameshapoteza moral authority ya kuwa mwalimu wa siasa ije mvua like mvua hana ideology anayoiamini zaidi ya useless activism tu.
Dkt. Slaa alihamia lini na Wapi CCM? Nina uhakika wa asilimia mia moja hutarudi na jibu la tarehe wala mahali.
 
i will buy and read this book as intellectual ila credibility ya Dr Slaa kwangu ishaondoka kabisa. Ila najua ni mtu mwenye fikra na historia kwa hilo kitabu chake ni muhimu kwa sie tunaopenda kujifunza.
 
Mimi nilidhani kwenye hicho kitabu chake cha nyuma ya pazia atatuambia kile alichofanyiwa na anachofanyiwa sasa na mkewe (Josephine Mshumbuzi), kumbe ni zile zile blah blah zake za kiCCM.

Afahamu tu kuwa kisiasa, watanzania walishamchoka na kumdharau sana toka awasaliti mwaka 2015. Hana jipya tena la kuwasemea. Kama Yuda alivyomsalitia Yesu Kristo dakika za mwisho kwa kupewa pesa, ndiyo hivyo hivyo Dr.Slaa alivyofanya 2015 kwa maslahi ya CCM, maana aliahidiwa pesa nyingi na kazi nzuri, akapewa ulinzi maalum kutoka ikulu huku akilindwa masaa 24, akahamia hoteli ya kifahari katikati ya jiji la Dar, akapewa hifadhi maalum ya kimaisha nchini Canada, kisha akazawadiwa ubalozi nchini Sweden na sasa anakaribia kurejeshwa nchini ili kupewa kazi maalum ya kisiasa (hili nina uhakika nalo kwa 100% soon linakuja kufanywa).

Yote kwa yote, msalimie sana Dr.Slaa, na mwambie watanzania tulio wengi bado tuko timamu, hatuipenda na hatuitaki CCM, huku bado tunashindia mihogo.

Mwisho kabisa mwambie Edward Lowassa alisharudi zake CCM, kama kile kisa cha yeye Slaa kuikacha Chadema na kuikumbatia CCM ilikuwa ni Edward Lowassa kuhamia CHADEMA, sasa Lowassa wapo naye CCM, atunge hadithi mpya.

Poor Slaa!

Ila ni kweli kuwa, kama anaendelea kumtaja Edward Lowassa katika kitabu chake kama sababu ya yeye kuachana na "siasa za vyama" katika mtazamo uleule aliokuwa nao mwaka 2015 alipohama na kurudi nyuma.....

Basi, hakika mantiki na maudhui yote ya kitabu hicho yanakuwa "invalid" na yanakosa maana yoyote kwa sababu, tayari tena MTU huyohuyo (his nightmare) "wanalala naye kitanda kimoja hukohuko CCM!!"

Sijui atawaambia nini watu ktk hili....

Anyway, kwangu mimi kwa kulielewa hili i.e Edward Lowassa vs yeye Dr Slaa, siwezi kununua kitabu hicho unless nipewe bure labda naweza kujitahidi kukisoma hivyohivyo....
 
Watu wengi wenye hekima na busara huwa wanaacha kazi ya fasihi andishi, hasa kupitia utunzi wa vitabu ili kutambulisha yale wanayoyaamini na kutambulisha misimamo yao ktk maisha waliyoyapitia. Ndivyo ambavyo Dr. Slaa amefanya.

Naam! Tunaweza kutofautiana naye kimawazo ama kumuhukumu kwa aina ya maamuzi aliyowahi kuyafanya sehemu fulani ya maisha yake, na pengine hatukuyapenda ikijumuisha; kuacha ukasisi, kutengana na mwandani wake wa awali, kuoa mke mwingine, kutengana na mambo ya kisiasa, kukubali "offer" ya ubalozi ambayo anaihudumu mpaka sasa.

Yote hayo ni mapito ktk maisha yake, na kuendana na umri alioufikia, ndipo hasa ni wakati stahiki wa kuja na "Bibliography" yake. Na sehemu ya nukuu ktk uzi huu ni kwamba; "Umpende, usimpende,....." Yeye ameshafanya jambo muhimu sana ktk fasihi.
 
Back
Top Bottom