Polepole walau anasimamia anachoamini, wangapi walikuwa karibu na JPM na leo wanamkana waziwazi hao unawaitaje? Mtu kama Nape ambaye alifikia hatua ya kutembea kwa magoti kuomba msamaha huku akimuita baba lakini leo hii anajimwambafai dhidi ya JPM (thanks to technology).Utawala dhalimu wa Magufuli umetusaidia kuwatambua watu wa hovyo kabisa, wasio na misimamo, watu wanafiki ambao wapo tayari kufanya chochote kwaajili ya ustawi wa matumbo yao:
Polepole ni rubbish katika siasa za kidemokrasia. Polepole ni uchafu katika uongozi kwa sababu ni kigeugeu. Polepole ni takataka katika siasa za kimaadili kwa sababu anahongeka kwa cheo. Polepole ni mnafiki kwa sababu hakuna anachokisimamia, msimamo wake unategemea yupo wapi, kwenye benchi au ndani ya Serikali.
Hiyo shule anayoiita ya uongozi, atawafundisha vipi watu uongozi wakati yeye mwenyewe hana sifa ya uongozi? Hiyo shule, hakuna chochote anachokilenga, zaidi ya kuwalenga waliopo kwenye Serikali mpya, kuonesha hawafai bali yeye na ile Serikali yake ya utekaji, data za uwongo, uminyaji wa uhuru, haki na demokrasia ndiyo walikuwa wanajuwa kuongoza.
Wapinzani nchi hii ni highly hopeless na hawapaswi kuaminiwa kwa sababu hawana uwezo wa kuisimamia kweli bali maslahi binafsi.