Nyumba anayodai Polepole imevunjwa siyo makazi yake ya kibunge, analaghai Umma akishirikiana na aliowakuza awamu iliyopita

Nyumba anayodai Polepole imevunjwa siyo makazi yake ya kibunge, analaghai Umma akishirikiana na aliowakuza awamu iliyopita

Utawala dhalimu wa Magufuli umetusaidia kuwatambua watu wa hovyo kabisa, wasio na misimamo, watu wanafiki ambao wapo tayari kufanya chochote kwaajili ya ustawi wa matumbo yao:

Polepole ni rubbish katika siasa za kidemokrasia. Polepole ni uchafu katika uongozi kwa sababu ni kigeugeu. Polepole ni takataka katika siasa za kimaadili kwa sababu anahongeka kwa cheo. Polepole ni mnafiki kwa sababu hakuna anachokisimamia, msimamo wake unategemea yupo wapi, kwenye benchi au ndani ya Serikali.

Hiyo shule anayoiita ya uongozi, atawafundisha vipi watu uongozi wakati yeye mwenyewe hana sifa ya uongozi? Hiyo shule, hakuna chochote anachokilenga, zaidi ya kuwalenga waliopo kwenye Serikali mpya, kuonesha hawafai bali yeye na ile Serikali yake ya utekaji, data za uwongo, uminyaji wa uhuru, haki na demokrasia ndiyo walikuwa wanajuwa kuongoza.
Polepole walau anasimamia anachoamini, wangapi walikuwa karibu na JPM na leo wanamkana waziwazi hao unawaitaje? Mtu kama Nape ambaye alifikia hatua ya kutembea kwa magoti kuomba msamaha huku akimuita baba lakini leo hii anajimwambafai dhidi ya JPM (thanks to technology).

Wapinzani nchi hii ni highly hopeless na hawapaswi kuaminiwa kwa sababu hawana uwezo wa kuisimamia kweli bali maslahi binafsi.
 
Watanzania baadhi ni wavivu wa kufikiri huropoka tu bila kufikiria
 
Ama kweli hii ni JF mpya...nimetafuta like nilichokiona kwenye Heading sijakiona kabisa kwenye COntent!
Halafu kumbe Wabunge Wana Makazi ya Kibunge Dodoma...!?
Anyway huu ni Utopolo tu.
Ukweli unabaki palepale tatizo ni CCM
Sio utopolo ni makolo kabisa.
 
Polepole walau anasimamia anachoamini, wangapi walikuwa karibu na JPM na leo wanamkana waziwazi hao unawaitaje? Mtu kama Nape ambaye alifikia hatua ya kutembea kwa magoti kuomba msamaha huku akimuita baba lakini leo hii anajimwambafai dhidi ya JPM (thanks to technology).

Wapinzani nchi hii ni highly hopeless na hawapaswi kuaminiwa kwa sababu hawana uwezo wa kuisimamia kweli bali maslahi binafsi.
Hivi huyu Polepole umemfahamu juzi baada ya DIKTETA kumpa uKatibu Mwenezi wa CCM? You are not informed kwa kweli.

Je unamkumbuka Polepole wa Bunge la Katiba/ Tume ya Warioba? Kama angekuwa ni mtu wa msimamo asingekubali kufanya kazi na Magufuli. Ila Polepole ni mmoja kati ya wale ambao Nyerere aliwaita "Malaya wa siasa".

Sasa hivi siyo kwamba anamtetea Magufuli bali anatetea tumbo lake
 
Lakini pia kaongea Dar mara kesho yake anadai alikuwa Manyara na anarudi Dodoma ndo anakuta pamevunjwa je Hana majirani? Hawa watu wanapeana michongo ya kututawala Kwa kupanua magoli , tushtuke uhuni huu.[emoji23]

Nakutumia pm inakataa mbona umefunga
 
Hivi huyu Polepole umemfahamu juzi baada ya DIKTETA kumpa uKatibu Mwenezi wa CCM? You are not informed kwa kweli.

Je unamkumbuka Polepole wa Bunge la Katiba/ Tume ya Warioba? Kama angekuwa ni mtu wa msimamo asingekubali kufanya kazi na Magufuli. Ila Polepole ni mmoja kati ya wale ambao Nyerere aliwaita "Malaya wa siasa".

Sasa hivi siyo kwamba anamtetea Magufuli bali anatetea tumbo lake
Mnapokuwa pamoja sio lazima mkubaliane kila jambo, na pia sio lazima kila mkitofautiana basi ujiuzulu. Pia kuna uwajibikaji wa pamoja, mnapokuwa kwenye vikao mnatofautiana lakini uamuzi ukipitishwa wote katika kanati ni lazima muusimamie hata kama wewe binafsi ulikuwa huuafiki. Je wewe na mkeo huwa mnakubaliana kila kitu?

Jadili au jibu hoja za sasa za Polepole .
 
Unajua maana ya UNAFIKI? nani manafiki kati ya Polepole na SAMIA
Bora Samia Ana endelea kuishi UNAFIKI WAKE.
Alafu Samia wakati yupo makamu hakuwa na maneno mengi.
Kama huyo muenezi na itikadi mstaafu.huyo alikuwa anatembea na ilani ya chama,wanatekeleza,
Huku watu wanakamatwa,wnafungwa,wanauliwa,wanatekwa n.k
ebu nenda kaangalie post za pole pole instagram.uone alikuwa je
 
jibuni hoja anazouliza polepole!!,achani kurukia vitu ambavyo havina mantiki,kuibiwa nako kwa kujadili.
 
Swala sio ku fake tukio,kununua wapinzani,kuwa kwenye serkali iliyopita..nk,,
Hoja za H.Polepole ni za kujibiwa.
 
Polepole anatafuta namna ya kuwafanya Wananchi wajinga, anatafuta namna ya kutumia kile chumba anachodai kimevunjwa kuonyesha Wananchi kwamba yeye ni mzalendo na hakujilimbikizia Mali, anataka kuonyesha Wananchi kwamba yeye ni fukara na mtu wa kiwango Cha chini kimaisha. Tumpuuze

Kwanini ameyafanya haya? Kwanza anataka kubadili upepo na agenda za kitaifa ikiwemo katiba Mpya na kutamka kurejea kwenye meza ya mazungumzo ndani ya CCM akionekana mwanamikakati. Hii tabia ya miaka mingi inayotumiwa na walafi wa madaraka.

Pili anataka yeye pamoja na vibaraka wake endapo mfumo utaamua kufungua shauri na kuchunguza MATENDO yake ndani ya chama na adhari zake kwenye serikali basi arudi Kwa Wananchi kupitia picha alizotuma apate uungwaji MKONO kwamba anaonewa. Mfano mzuri WA eneo analojua linaweza kumpeleka mahakamani kwa makosa ya Uhujumu uchumi ni pamoja na kununua wapinzani ambapo mfano wa wazi ni kile kitendo Cha yeye kupeleka milioni 30 mahakamani kumnunua Mashinji.

Tatu, kupitia tukio hili anataka kunyamaza atuaminishe amenyamazishwa kumbe maovu yake huko nyuma yalishamnyamazisha Toka mteule wake wa awali alipoondoka.

Polepole amekuwa live kwenye shule yake sijui ya siasa na mandhari aliyokuwa anarushia matangazo ipo wazi, anamzuga Nani? Wabunge Wana nyumba Dodoma yeye alikwenda kupanga chumba Kwa kukosa Kodi au kwa sababu gani? Mbunge Hana viti Wala kitanda, hizi michezo inatuondoaje kwenye reli? Lakini pia kaongea Dar mara kesho yake anadai alikuwa Manyara na anarudi Dodoma ndo anakuta pamevunjwa je Hana majirani? Hawa watu wanapeana michongo ya kututawala Kwa kupanua magoli , tushtuke uhuni huu.
Nakushukuru mkuu. Ubarikiwe sana
 
Swala sio ku fake tukio,kununua wapinzani,kuwa kwenye serkali iliyopita..nk,,
Hoja za H.Polepole ni za kujibiwa.
Mnaamini kwenye kujibu hoja nyie ? Mbona Tundu lisu alipohoji juu ya mkataba ya madini mlimminia risasi kama jambazi?????
 
Pole Pole Ni mmoja wa watu waliokua na nguvu na Ushawishi Mkubwa awamu iliyopita alipanda cheo haraka akawa Mwenezi wa CCM..Maovu na uonevu uliofanyika Yumo anajua anahusika au aliratibu....leo nae analia kwa style ile ile....
Ajitulize mana matendo ya serikali zote ni yale yale na kama hakukemea maovu asitudanganye sasa....

Sio yeye Tu wako watu wengi wameumiza sana watu....
 
Nyumba ya Polepole kuvunjwa haijalishi iwe ya kibunge au ya kiraia huo ni uhalifu na unatakiwa kufanyiwa kazi na jeshi la polisi bila kujali chochote.

Kusema Polepole anajikweza kisa nyumba yake haikuwa na mali nao ni ushamba tu, ingekuwa na mali nyingi naamini pia ungesema Polepole fisadi, kuwa na mali nyingi au chache ni life style ya mtu yeyote anajiamulia, sio kigezo cha uzalendo, na sio kila mwenye mali nyingi au chache ni mwizi au mtakatifu, hizi sababu nyepesi ulizo leta hapa hazina mashiko.

Kuhusu majirani sidhani kama Polepole ameajiri majirani zake wawe walinzi wake, nao wanakazi zao, una hakika wakati wa tukio hao majirani walikuwepo nyumbani? na kama walikuwepo hawakuwa na shughuli nyingine wakawa wametega macho na masikio yao kwa Polepole tu?

"Ushuani" ni tofauti na "uswahilini" ambapo kila anaeingia na kutoka huonekana, hata ukila maharage kwako majirani wote wanajua, usikariri maisha yako ukayahamishia kwa mwenzako.

Siku hizi watu wanapanda ndege wanazunguka karibia nchi nzima kwa siku moja, wewe unashangaa umbali kati ya Manyara na Dodoma ambao hata kwa gari mtu anafika? hizi mindset zenu.

Hicho kikao walichokaa Polepole na CCM wenzake ili watuondoe kwenye lengo la msingi [Katiba Mpya] kilifanyika lini na wapi? Kila siku mnalilia mikutano ya kisiasa irudishwe kwa wote, ila Polepole kutoa maoni yake apuuzwe!, hamkumbuki anayemnyima Polepole ndie anaewanyima nyie.

Sio kwasababu Polepole ni mwanasiasa mwenye mawazo tofauti na kambi yake ndio aanze kutengwa na kutafutiwa sababu za kila aina, ajibiwe hoja zake maisha yaendelee, kwasababu ni haki yake kutoa maoni na wanaoulizwa sharti wamjibu wasimtishe, kumkejeli, au vyovyote vingine.

Haiwezekani leo kutaka Polepole apuuzwe kwa kutoa hoja zake, ila nyie "wana demokrasia" mkitoa hoja zenu mtake zijibiwe, hii ni double standard, haki haina mipaka na haichagui sura, kama mnaona Polepole ana makosa nendeni mahakamani na hao wenzenu mliowaunga mkono bila kujitambua, opposition is an art.

Kinachotia moyo ni kuwa mawazo mengi mitandaoni si misimamo rasmi ya vyama.

Ieleweke CDM kama chama hakijawahi kujilaumu kwa kuwa na yeyote aliyekuja au kuondoka katika wakati wowote.

Chama makini kina agenda za kudumu si marafiki wa kudumu.

Kuna tofauti ya hoja za Polepole na Polepole kama mtu.

Kwamba anadai ananyamazishwa? Hata sisi tunanyamazishwa.

Kulitambua hilo halimlazimishi awaye yote kuchukua hatua yoyote. Hata kwenye kulazimishwa kwake, kuyatambua madhila ya kunyamazishana si muhani.
 
Mnapokuwa pamoja sio lazima mkubaliane kila jambo, na pia sio lazima kila mkitofautiana basi ujiuzulu. Pia kuna uwajibikaji wa pamoja, mnapokuwa kwenye vikao mnatofautiana lakini uamuzi ukipitishwa wote katika kanati ni lazima muusimamie hata kama wewe binafsi ulikuwa huuafiki. Je wewe na mkeo huwa mnakubaliana kila kitu?

Jadili au jibu hoja za sasa za Polepole .
Polepole hana hoja yeyote zaidi ya kuwa ni fungu la kukosa. Muache afurahie uhuru wa maoni ambao Rais SSH ameturudishia baada ya Magufuli kutunyima miaka 5
 
Kinachotia moyo ni kuwa mawazo mengi mitandaoni si misimamo rasmi ya vyama.

Ieleweke CDM kama chama hakijawahi kujilaumu kwa kuwa na yeyote aliyekuja au kuondoka katika wakati wowote.

Chama makini kina agenda za kudumu si marafiki wa kudumu.

Kuna tofauti ya hoja za Polepole na Polepole kama mtu.

Kwamba anadai ananyamazishwa? Hata sisi tunanyamazishwa.

Kulitambua hilo halimlazimishi awaye yote kuchukua hatua yoyote. Hata kwenye kulazimishwa kwake, kuyatambua madhila ya kunyamazishana si muhani.
Justice is a two way traffic, kama vile ambavyo unaruhusiwa kupita wewe wakati wa kwenda, basi ndivyo inavyotakiwa upishane na mwenzako apite anaporudi, lakini sio umkatalie kupita kwasababu ya sura yake! this is immaturity.
 
Polepole anatafuta namna ya kuwafanya Wananchi wajinga, anatafuta namna ya kutumia kile chumba anachodai kimevunjwa kuonyesha Wananchi kwamba yeye ni mzalendo na hakujilimbikizia Mali, anataka kuonyesha Wananchi kwamba yeye ni fukara na mtu wa kiwango Cha chini kimaisha. Tumpuuze

Kwanini ameyafanya haya? Kwanza anataka kubadili upepo na agenda za kitaifa ikiwemo katiba Mpya na kutamka kurejea kwenye meza ya mazungumzo ndani ya CCM akionekana mwanamikakati. Hii tabia ya miaka mingi inayotumiwa na walafi wa madaraka.

Pili anataka yeye pamoja na vibaraka wake endapo mfumo utaamua kufungua shauri na kuchunguza MATENDO yake ndani ya chama na adhari zake kwenye serikali basi arudi Kwa Wananchi kupitia picha alizotuma apate uungwaji MKONO kwamba anaonewa. Mfano mzuri WA eneo analojua linaweza kumpeleka mahakamani kwa makosa ya Uhujumu uchumi ni pamoja na kununua wapinzani ambapo mfano wa wazi ni kile kitendo Cha yeye kupeleka milioni 30 mahakamani kumnunua Mashinji.

Tatu, kupitia tukio hili anataka kunyamaza atuaminishe amenyamazishwa kumbe maovu yake huko nyuma yalishamnyamazisha Toka mteule wake wa awali alipoondoka.

Polepole amekuwa live kwenye shule yake sijui ya siasa na mandhari aliyokuwa anarushia matangazo ipo wazi, anamzuga Nani? Wabunge Wana nyumba Dodoma yeye alikwenda kupanga chumba Kwa kukosa Kodi au kwa sababu gani? Mbunge Hana viti Wala kitanda, hizi michezo inatuondoaje kwenye reli? Lakini pia kaongea Dar mara kesho yake anadai alikuwa Manyara na anarudi Dodoma ndo anakuta pamevunjwa je Hana majirani? Hawa watu wanapeana michongo ya kututawala Kwa kupanua magoli , tushtuke uhuni huu.
Hilo la Katiba mpya kuwa "ajenda ya kitaifa" si kweli. Inapaswa kuwa ajenda ya kitaifa lakini hadi sasa imebaki kuwa ajenda ya kundi flani tu. La muhimu ni kujibidiidha ili iwe hivyo ie ajenda ya kitaifa, japo najua "wasiopenda kushaurika" watakemea.
 
Justice is a two way traffic, kama vile ambavyo unaruhusiwa kupita wewe wakati wa kwenda, basi ndivyo inavyotakiwa umuache mwenzako apite wakati wa kurudi, lakini sio umkatalie kupita kwasababu ya sura yake! this is immaturity.

Ifahamike kuwa pana watu wasiotutakia mema katikati ya urojo rojo kama hizi:

Tuwatambue wanaohaha kutusambaratisha kama Taifa

(Hiyo ikiwa kabla zile ya siku 100)
 
Ifahamike kuwa pana watu wasiotutakia mema katikati ya urojo rojo kama hizi:

Tuwatambue wanaohaha kutusambaratisha kama Taifa

(Hiyo ikiwa kabla zile ya siku 100)
Naona bado unaendelea kutazama sura za watu, unakosea brazaj.

Haki za nchi hii hazimilikiwi na kikundi fulani cha watu, ni za watanzania wote bila kuwabagua kwa namna yoyote, au kuwahukumu bila kuwafikisha mahakamani. Yeyote anayenyimwa haki yake lazima tumpiganie kwa umoja wetu ili siku tukidai haki zetu, wawepo wakutusikiliza.

Vinginevyo ukiendelea kuleta hii segregation ya kuwatenga baadhi, na hii mentallity yako ndio inayofanya ionekane madai ya Katiba Mpya ni kikundi fulani cha watu, sio watz wote, tubadilike, nadhani utakuwa hujui hata maana ya haki tunayoipigania kila siku.
 
Back
Top Bottom