Nyumba ya KUB Mbowe ina CCTV, zinaweza kutoa ushahidi kama alianguka au alivamiwa

Nyumba ya KUB Mbowe ina CCTV, zinaweza kutoa ushahidi kama alianguka au alivamiwa

saidi kindole

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2012
Posts
310
Reaction score
792
Ni aibu kwa bunge badala ya kujadili bajeti ya nchi, linatumia siku mbili kujadili tukio la kuvamiwa Mbowe. Cha kusikitisha hawajadili namna ya kumsaidia mbunge mwenzao bali wanapiga majungu.

Jana Msukuma kasema Mbowe alikuwa anakunywa Konyagi Kubwa (Faru John) na ndio iliyopelekea kuanguka na kuvunjika. Ndugai kasema madaktari wake walimjulisha kuwa Mbowe alikua amelewa chakari.

Kibajaj akasema alianguka akiwa na mwanamke na mwanamke huyo alikimbia. Waitara amemtaja mwanamke huyo kwa jina bungeni. Yani majungu majungu tu.

Kama kuna utata kuhusu kuvamiwa kwa Mbowe, utata huo unapaswa kumalizwa na mambo mawili tu.
#Mosi; Mbowe ana walinzi wa aina mbili. Wa serikali (TISS) na wa chama (Red Brigade). Serikali ilimuondolea Mbowe walinzi mwezi uliopita kwa sababu ya issue ya Covid19 walipotoka bungeni.

Lakini hata baada ya kurudi bungeni hakurudishiwa ulinzi. Hapa kuna kitu hakiko sawa. Kwanini viongozi wengine walibaki na walinzi kama issue ni Covid19? Na kwanini Mbowe hakurudishiwa ulinzi hata baada ya kurudi bungeni?

Wanaohoji kuhusu ulinzi wa Mbowe wanapaswa kuhoji mambo mawili. Kwanini serikali haikumrudishia ulinzi baada ya kurudi bungeni kisha wahoji walinzi binafsi wa Mbowe (red brigade) walikua wapi wakati anavamiwa.

#Pili; Nyumba anayoishi Mbowe ina CCTV 24hrs. Kwnn picha za CCTV zisiwekwe hadharani? Kama alianguka ataonekana na kama alivamiwa ataonekana pia. Kwanini tunapoteza muda kusigana kwenye jambo ambalo ukweli wake ni rahisi tu kupatikana?

Nyumba anayoishi akiwa Dodoma (kama KUB) ni ya serikali with CCTV system. Hata wanaoaccess "control room" ni maafisa wa serikali. Kwanini serikali isitoe hizo picha zinazoonesha Mbowe akianguka?

Kwa ninavyoijua serikali ya CCM ingekua kweli Mbowe kaanguka usiku akiwa na mwanamke na "Faru John" mkononi, nina uhakika wangeprint hizo picha na kuzisambaza kuanzia Lupiro kule Ulanga hadi Yombo Buza kwa Abiola.

Lakini ukiona serikali inakomaa kuwa Mbowe alianguka, lakini haitaki kutoa picha za CCTV, halafu serikali hiyohiyo ilimuondolea ulinzi mwezi mmoja tu uliopita, lazima uhisi kuna kitu. WaTZ wa leo sio wajinga.!
 
#Pili; Nyumba anayoishi Mbowe ina CCTV 24hrs. Kwnn picha za CCTV zisiwekwe hadharani? Kama alianguka ataonekana na kama alivamiwa ataonekana pia. Kwanini tunapoteza muda kusigana kwenye jambo ambalo ukweli wake ni rahisi tu kupatikana?

Nyumba anayoishi akiwa Dodoma (kama KUB) ni ya serikali with CCTV system. Hata wanaoaccess "control room" ni maafisa wa serikali. Kwanini serikali isitoe hizo picha zinazoonesha Mbowe akianguka?
It's true nyumba ya KUB ina CCTV, ila Mhe. Mbowe aligoma kuitumia, hivyo ndio ile iliyokuwa ikitumiwa na Lissu!. Kitu ambacho mimi sikijui ni labda kama baada ya Lissu kufutwa ubunge, Mhe. Mbowe hatimaye alikubali kuhamia kwenye hiyo nyumba rasmi ya KUB ambayo ni ya serikali, ina CCTV, ulinzi na wafanyakazi wote wakilipwa na serikali ikiwemo gari, dereva na msaidizi.
P
 
Tena Kuna wanaotoa maelezo bila aibu unafikiri walikuwa naye,Mbowe hajaanza kunywa pombe Jana Wala juzi.
 
It's true nyumba ya KUB ina CCTV, ila Mhe. Mbowe aligoma kuitumia, hivyo ndio ile iliyokuwa ikitumiwa na Lissu!. Kitu ambacho mimi sikijui ni labda kama baada ya Lissu kufutwa ubunge, Mhe. Mbowe hatimaye alikubali kuhamia kwenye hiyo nyumba rasmi ya KUB ambayo ni ya serikali, ina CCTV, ulinzi na wafanyakazi wote wakilipwa na serikali ikiwemo gari, dereva na msaidizi.
P
Umeanza kuuma na kupuliza.
 
CCM hawana hoja...wamebakia kutumia mabavu kutisha viongozi na kubadilisha sheria za uchaguzi dk za majeruhi ili walau watoe mlisi.

Hii itawacost...dunia ya leo si ya miaka ya 80s'..huwezi kutawala nchi yako utakavyo wewe!!

Weka uchunguzi huru ili ujisafishe vinginevyo tuhuma zote zinakuangukia weye kwamba muhusika katika tukio zima.
 
"Kila uchwao kitokacho Africa ni kituko kingine"

Kwa hiyo pamoja na kujifaragua kote kule juu ya vyombo vya ulinzi kutumiwa na watawala dhidi ya wapinzani,bado haohao ndo wanamlinda?

Watu wanahoji Red B kwa sababu hawatarajii kusikia Mbowe bado anategemea ulinzi wa serikali kwa kilichompata Lisu.

Hivi kwa tukio lile la Lisu,ni kipi hasa ambacho anasubiri hata kuhama kwenye hizo nyumba za serikali ambazo ulinzi kwao ni 0?

Kwa nini asitafute nyumba ambayo atakuwa na control kamili ya ulinzi wake ikiwepo hizo CCTV camera badala ya kuleta ngonjera zilezile kila tukio?

Kama aliweza kulikataa shangingi,anashindwaje kuikataa hiyo nyumba na ulinzi asiouamini?

Haya mambo ndo yanawafanya wenye AKILI TIMAMU waone haya matukio yote ni sanaa zaidi kuliko uhalisia.
 
Uko sawa kabisa kwa hoja za Walinzi wa serkali na cctv camera.
Je la mlinzi wake nalo haliwezi pia kutumika mpaka walinzi wa serkali itolewe sababu kwanini waliondolewa.
Covid 19 na kujitenga wa wabunge wa chadema inaweza kuwa sababu.
Huenda hadi apimwe baada ya siku 14. Tangu arejee bungeni
 
It's true nyumba ya KUB ina CCTV, ila Mhe. Mbowe aligoma kuitumia, hivyo ndio ile iliyokuwa ikitumiwa na Lissu!. Kitu ambacho mimi sikijui ni labda kama baada ya Lissu kufutwa ubunge, Mhe. Mbowe hatimaye alikubali kuhamia kwenye hiyo nyumba rasmi ya KUB ambayo ni ya serikali, ina CCTV, ulinzi na wafanyakazi wote wakilipwa na serikali ikiwemo gari, dereva na msaidizi.
P
Kuna mbunge jana kasema yeye ni jirani yake, labda kama huyo mbunge pia anakaa mtaani, otherwise ,Mbowe anaishi kwenye nyumba hizo za serikali
 
Back
Top Bottom