Nyumba yetu inazidi. Rais onyesha uwepo wako, Uwezo Wako Anza na Wale Marrionates Wote Wawili Pale Wapumzishe. The Drama King wa Pinga Chanjo Apuuzwe

Tafadhali rekebisha kichwa cha mada isomeke Onesha na sio onyesha.

Onesha- Ona
Onyesha- Onya

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Kwingine kote nimekuunga mkono, Ila hapa umejionyesha kwa dhahiri chuki zako jinsi zilivyo kwa huyo mjamaa!

Ukiacha chuki yako utauona ukweli mzuri wa huyo mjamaa
 
Serikali inatakiwa kummaliza huyo taperi kwa risasi nyingi za kichwa, haiwezekani hailetee dharau serikali,Ni wakati Sasa azimwe kabisa, ana chuki binafsi na Rais aliyepo Sasa, na ana ukabila wa Hali ya juu na udini pia
 
Wakipumzika wengine atawatoa wapi?

Wabunge wetu ndio hawa akina babu Tale Kinanasi, Kigwangalla, Tabasamu, Kibajaj yaani wote ni full comedy!
Wewe lazima uitwe kwenye kamati ya maadili ya chama chetu, huwezi kuwadhalilisha wabunge namna hii!
 
Kwanini huyo Drama King apuuzwe? nae anatakiwa kushughulikiwa ili iwe fundisho kwa wengine wanaopingana na maamuzi ya chama chao kwa public.
Huwa naheshimugi sana mawazo yako mkuu, hapa ninatofautiana na wewe kistarabu kabisa,

Ni lazima kwa sasa kama taifa tufikie kwenye kiwango cha juu kabisa kwa kutumia uhuru wetu kuwaacha watu wafikiri zaidi hasa kunapotokea sintofahmu na mambo makubwa yanayohitaji akili kibwa zitumike ili kupata ukweli, hii ni kwa ajiri yetu sisi wenyewe na kwa faida yetu

Wapiga kelele kuhusu chanjo hizi, kwanza hawapo Tanzania pekee, hadi huko zinakotengenezwa wapo kina Askofu Gwajima wengi tu, kwa nini inapotokea Tz iwe ni kosa kubwa tena la kijinai?

Kwani kelele za Gwajima lengo lake ni nini? Je, ni kuzitaka mamlaka ziboresha Baadhi ya mambo ili wananchi wakubali kiulaini kupata chanjo? ama ni anataka na kuwahimiza wananchi kwamba,hata watalaamu wakiboresha na kuwahakikishia zaidi usalama wa chanjo waendelee kuzikataa chanjo?

Ni wapi Gwajima amekataa katakata chanjo kwamba hazifai na hataki watu wachanje? Anachokifanya Gwajima, ni sehemu ya kuikumbusha wizara husika kuwa kuna hiki na kile fanyeni!

Mamlaka inasema, Chanjo ni salama, Lakini kwa nini mamlaka hiyo hiyo inakataa kuingia gharama pindi mwananchi akipata madhara ya chanjo?

Kosa la huyo unayedhani anakosa ni lipi? Kwa nini uhuru wetu kama nchi hatutaki tuutumie kwa ajiri yetu sisi wenyewe, Kwa nini mnadhani kila anayetaka jambo fulani litolewe maelezo ya kina anakiuka uhuru wake?

Tuacheni ujinga, Tukifanya mambo yetu kwa faida yetu tunakosa nini
 
Huyo taperi ni wakati sasa serikali immalize mazima, Ni hatari kwa usalama wa Taifa
 
Pascal, unarudi taratibu kutoka ulikokuwa na kwenda kwenye u-great thinker. Nenda hivyo hivyo, baadaye unaweza kuwa kwenye full level, kabla ya kuitwa kwenye kamati.

Ulichoongea ni logic. Rais kuendelea kuwa na wasaidizi waliosema chanjo haifai wakati tunaposema kuwa chanjo ni muhimu, kwanza ni kuwadhalilisha hao wasaidizi mbele ya wananchi. Anataka wale matapishi yao.

Hii ni sawa na alivyofanyiwa bwana mmoja ambaye alisema nafasi ya ukuu wa Wilaya haina maana, ifutwe, halafu yeye huyo huyo akateuliwa kuwa mkuu wa Wilaya, akaanza kupuyunga na kuonesha DC alivyo na kazi nyingi. Hatimaye akadhalilishwa zaidi kwa kupewa nafasi ya kuwa katibu mwenezi wa chama ilihali kabla yake alitamka kuwa CCM haiwezi kushinda kwenye uchaguzi ulio huru na wa haki. Sasa akaanza kupiga kelele kama taahira kuwa CCM itashinda uchaguzi wowote ule kwenye mazingira yoyote yale. Mpaka leo huyu bwana yupo, ni binadamu, lakini ambaye hawezi kuaminika kwa lolote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…